Warere Beach Resort: Zainab Oladehinde alikubaliana na mlinzi kufanya mapenzi. Alitaka tumlipe fidia USD 10,000

Warere Beach Resort: Zainab Oladehinde alikubaliana na mlinzi kufanya mapenzi. Alitaka tumlipe fidia USD 10,000

Mkuu nchi yetu ina matatizo mengi sana, NA Polisi kwa kweli wanachangia sana hayo matatizo, Binafsi nimeshuhudia mengi Zanzibar kwenye maeneo ya utalii yanayowakuta watalii kama Ukabaji, uchomoaji, utapeli.

Lakini huyu dada anatia shaka sana, Wa Nigeria ni watu wa matukio, Kesi kama hizo wameshafanya maeneo mengi sana.
Nakubaliana na maoni yako kiongozi, tatizo kuu hapa ni utendaji kazi wa polisi na serikali kwa ujumla.

Na kesi ya huyu dada serikali isibaki tu kwenye mazoea kwamba wanigeria tabia zao ni mbaya, bali ije na majibu ya kiuchunguzi wa haki.
 
Na kwa kuwa wanajua Hotel ingeogopa kuchafuliwa so walidhani ni rahisi watalipwa.

Kwa uchumi huu amekwama na hotel itaendelea na kazi zake.
Analeta utani na uchumi wa Kati huyu!watu tunapumulia gas ye anataka hela
 
Tumia akili ndgo tu,ukienda bank au geast House mlinzi akakupga kofi then unaenda kwa meneja kulalamika juu ya hilo then eti meneja anakujibu "Huyu sio mfanyakazi wetu".nenda kwenye kampun yao ukashitaki..is it possible?ikiwa ndo hivyo basi itakua ni upumbavu wa kiwango cha lami..binafsi hata mimi siwez kubal..nitakomaa na meneja..mana mlinzi nimemkuta kwenye property la meneja,ndo mana nasema Zainab hakutendewa haki..hata defence ya Warere ni za hovyo..sijui hata kama hao staff wao wanajua issue zozote za customer care..
Kiingereza ni kigumu kidogo. Mlinzi alifikishwa polisi. Baada ya yeye kusema kuwa alikaribishwa na Zainabu, Zainabu alishauriwa amshitaki yeye, kampuni iliyomwajiri na hata hoteli yenyewe. Zainabu alikataa kufanya hivyo kutokana na ushauri wa mawakili wake. Yeye akasema alipwe fidia ya dola 10000, lakini hoteli ikamwambia kuwa hawawezi kumlipa bila Mahakama kumkuta mlinzi ana hatia. Hoteli isingeweza kumshitaki mlinzi kwa sababu wao sio injured party. Na wangemshitaki halafu akathibitisha kuwa kweli Zainabu alimkaribisha, angeweza kuishtaki hoteli kwa kumharibia jina. Kitu kingine ni hofu ya kuset precedence. Watu wakijua kuwa hoteli iko tayari kutoa pesa ili kuepuka kuchafuliwa wengine wangemuiga Zainabu. Na itathibitisha kuwa huo ndio mchezo wa hiyo hoteli.

Inawezekana kuwa yalimpata kweli Zainabu lakini kukataa kwake kwenda mahakamani kumemharibia. Na hata kama ni PTSD, kukaa mwaka mzima kabla ya kuweka wazi yaliyomkuta yanafanya asionekane mwaminifu. Kingine ni simulizi zake kuhusu kunuka kwa jamaa, kumuita "baby", kukubali kwenda kuchukua kondom, kota kunanukia kutia chumvi.

Zainabu hapo mwanzo hakuzungumzia msaada na ushirikiano alioupata kutoka kwa wanasheria wa kizanzibari bali alikazania kuwa si hoteli wala polisi walimsaidia! Hii ni kujenga hoja kuwa wazanzibari ni watu ovyo sana.

Zainabu angeaminiwa zaidi kama angetumia huo mwaka aliokaa kimya kukusanya ushahidi kuwa kile kitendo hakikuwa isolated na kuna wengine yaliwakuta hayo hayo. Wengi wetu hatuna imani na polisi wetu na tunajua kuna watu waovu ambao wako tayari kuwatenda vibaya wanawake waliokuwa peke yao. Ila kwenye hili, Zainabu kawaangusha wenzake. Bahati mbaya kwake tunajua pia kuwa kuna wanawake ambao wanatembea na wafanyakazi wa hotelini, beach boys n.k. Kuna wanaume pia wanaofanya hivyo hivyo.

Amandla...
 
Sijasema ubakaji rudia utizame vizuri, nimesema ukabaji, Wale vijana wanaovamia watu na mapanga, Nimeshuhudia mzungu akivuja damu baada ya kurambwa panga na kunyang'nywa Camera yake pamoja na simu.
Kwa matukio kama hayo kwa ufupi tu tuseme Kwaheri Utalii, KIla siku zinavyokwenda NUngwi na KIwengwa hali zinazidi kuwa mbaya Na serekali haishuhuliki kabisa.
Hata ubakaji unaweza kuwepo. Kuna vijana wa ovyo sana. Mwanamke mgeni akiwachekea kidogo basi wanajua wameisha pata tiketi ya kwenda ulaya. Hawajui wengine wanafanya hivyo kwa kuhofia kuonekana wabaguzi.

Amandla...
 
Tuliza tako dogo subiri Mamlaka ifanye kazi yake haukuwa eneo la tukio tulia
Kuwashwa siyo lazima uwe na kipele hama hisia za kupeleka mkono shm ili ujikune.

Njia nyingine huwa tunatumia watu wazima, ningeona jambo zuri umuulize huo mkuno wa pili aliyekuachisha kunyonya ila maswali utakayoulizwa dunia ni msongamano.

Kaa kwa kutulia yankee!.
 
Alafu kuna watu nawafuatilia ni wanaheshimika wanaandika eti "kaeni na huyo binti mzungumze naye" nimecheka aseee.
Eti alisikia anashikwa shikwa maziwa akidhani anaota. Au alikuwa kalewa chakali pombe zimemjaa anaota.

Mazingira ya hitel ni ngumu sana ku attemp rape.

Highly secured environment.
 
Na nchi inavyofunguliwa huyo mlinzi asubiri ghadhabu na hasira plus kutolewa mfano, this has happened in the worse time for him..., huenda Madam President wakati ana-launch her premier ashapiga simu na kuuliza huyo kiumbe kama yupo mtaani...

Na huyu binti nadhani ameona the timing wouldn't have been more perfect than this time...

Instead ya kuongelea "This is a Female Lion" tunaongelea Security ya watalii..., na wakikumbushia na issue zile za tindikali this issue needs to be handled delicately...
Ila kama ni script basi wenzetu wapo juu na kama ni real happened basi ni jambo lingine.

Ila ninachojiuliza, kwenye hatari ya kubakwa badala ya kupiga ukunga unabagain na mbakaji wako real, na mpaka anatoka kwenda kuchukua kondomu.
 
Back
Top Bottom