Washauri wa Rais Magufuli, mshaurini aache kutumia Kiingereza kwenye hadhara

Washauri wa Rais Magufuli, mshaurini aache kutumia Kiingereza kwenye hadhara

Mmekosa hoja....Nyie hata kiswahili hamjui sembuse kingereza....!!Upinzani wengi ni vijana mpechempeche marioo wa mjini wapenda vya bure,kingereza wamekijulia Kwenye movie na nyimbo za kina Cellin Dione...Wanaume wa kweli hawezi ongea hoja za kijinga kama hizi...!!
Ni hoja za werevu. Ukisoma kiingereza toka darasa la tatu hadi juu unatakiwa kukijua vizuri sana.
 
julaibibi

Hoja hapa ni kuwa umesoma form one hadi six kwa kiingereza, degree ya kwanza hadi phd kwa Kiingereza, ukaenda kuchukua Masters UK lakini bado Kiingereza kinakupa tabu. Kuna jambo na ninavyomuona mkuu wetu angejua hii lugha angeongea hiyo hiyo hata Manzese kwa mfuga mbwa.
 
Hivi huyu mtu hiyo "thesis" ya PhD yake aliandika kwa lugha gani hasa wakati inaeleweka kuwa lugha ya kufundishia kwenye Higher Learning Institutions zetu ni Kiingereza?

Hilo jopo la walimu lililomkagua na kumpa hiyo "doctorate degree" nao lazima elimu na uelewa wao uwe questioned.

Ufahamu na uelewa wa John Pombe Magufuli katika nyanja zote una kasoro na elimu yake hii inatia shaka mno. Huyu mtu ni mwizi wa mitihani. Hakusoma na kufaulu huyu. Huyu mtu ni mfano halisi wa zao la mfumo wetu wa hovyo wa elimu chini ya Sera na mipango ya CCM kwa miaka zaidi za 60 sasa.

Haiwezekani mtu mwenye elimu ya kiwango cha "udaktari wa sayansi ya kemia" awe hana uwezo wa kujieleza kwa ufasaha si kwa Kiingereza tu bali hata kwa Kiswahili.

Huyu mtu brain yake ni almost zero. Huyu mtu anachoweza kila anapopata nafasi ya kuongea ni kurusha kejeli na kashfa kwa kina mama na watu wake anaowaongoza, baaasi.

Na hii ndiyo sababu nchi yetu iko kwenye hali mbaya kwa sababu tumempa NGUVU na MAMLAKA makubwa ya kiuongozi wa nchi mtu ambaye akili zake zinatakiwa ziwe scrutinized kuhakiki ubora wake.
 
Rais Magufuli ni mtu huru, ni fikra huru. Na hiki ndicho kinachomfanya awe rais bora miongoni mwa marais tuliowahi kuwa nao Tanzania. Anawaza kivyake, anasema anavyotaka iwe kingreza, kiswahili au kisukuma. Akosee au asikosee.

Rais wetu si mtumwa wa mtu yeyote, akili zake hajashikiwa na mtu yeyote. Anafanya anavyoona inafaa popote pale na muda wowote ule.

Ogopa kiongozi anayesema kwa staili ya ajili kuwaridhisha watu fulani au eti aendane na fikra fulani. Political correctness. Ni wabaya maana hawana ubunifu, hawawezi fanya maamuzi magumu, yaani wapo wapo tu kama maroboti ya kikundi fulani cha watu au fikra. Tulipopata uhuru kutoka kwa mkoloni maana yake ilikuwa ni uhuru kamili -- kimwili, kifikra na kimaamuzi.
Kwa mtazamo wangu, huyu si mtu huru kama unavyosema. Mfano ni ishu hii ya 'kizungu'. Angekuwa huru na mwenye kujiamini asingelazimisha kuongea kiingereza wakati tayari mfumo wa ukalimani/tafsiri ulikuwepo (utaona wageni walikuwa na zile interpretation headsets). Ilikuwa ni katika kujaribu kuwathibitishia wanaomnanga kuhusu 'kizungu' kuwa naye yumo! Hiyo siyo attitude ya mtu aliye huru kifikra.
 
Mkuu usitake kutudanganya wakati wote tulisikia alivyokuwa akiongea. Hii ni version yako ya kiufipa ufipa.
 
Mmekosa hoja....Nyie hata kiswahili hamjui sembuse kingereza....!!Upinzani wengi ni vijana mpechempeche marioo wa mjini wapenda vya bure,kingereza wamekijulia Kwenye movie na nyimbo za kina Cellin Dione...Wanaume wa kweli hawezi ongea hoja za kijinga kama hizi...!!

Hiyo siyo hoja ya kijinga hatuwezi kukaa kimya mtu mwenye Phd na mwalimu akiongea kingereza kama hicho hata mtu ukisikiliza huelewi alikuwa anaongea nini kwanini tusiseme. Hilo ni tatizo huyo ni kiongozi wa nchi kwanini asitumie kiswahili tu
 
Mmekosa hoja....Nyie hata kiswahili hamjui sembuse kingereza....!!Upinzani wengi ni vijana mpechempeche marioo wa mjini wapenda vya bure,kingereza wamekijulia Kwenye movie na nyimbo za kina Cellin Dione...Wanaume wa kweli hawezi ongea hoja za kijinga kama hizi...!!

Unatetea nini we we?

Unajifanya huoni tatizo?

Huyu ni mwalimu by profession. Amefundisha miaka mingi shule mbalimbali Tanzania.

Alikuwa anafundishaje vijana wetu kama Kiingereza ambayo ndiyo lugha ya kufundishia shule za sekondari iwapo anashindwa kukiongea na kuandika kwa ufasaha ingalau kwa 75% tu?

Ufasaha wa lugha ni muhimu sana tunapokuwa tunaongea ama kuandika. Ukikosea tu kidogo, unakuwa umepotosha na ujumbe kwa wanaopaswa kuupata.

Ndiyo mnataka tuulee ujinga huu? NO WAY. HAPANA.

Aliipataje PhD yake huyu? Huyu ndiyo maana anaua watu kwa sababu hapendi huu udhaifu wake ulioko nyuma ya pazia uhojiwe!

Tatizo liko wazi kabisa, makosa yana na yanendelea kufanyika mchana kweupe halafu wewe unahusianisha na "vijana wa upinzani?"

Kama nyie wenyewe hamkosiani huko. Hamuoni matatizo.

Basi, kama nchi, we have a really big problem!!

Maana yake kama walioko serikalini hawaoni kuwa hili ni tatizo, basi watabaki kuwa wajinga na wapumbavu hivyo hivyo mpaka pale watakapokuwa wamenyang'anywa madaraka, wawe nje ya mfumo wa utawala ndipo watakapogundua na kusema;

"...alaaa, kumbe tulikuwa wapunbavu na wajinga hivi?"
 
Nakubali mkuu hapo kwenye kuelewa tu maswali mara kadhaa amekua akipuyanga sasa kama tu kuelea swali ni tatizo basi kujibu ndio zaidi, kwakweli akiwa kama raia number one anatutia aibu sana kama taifa

Sent from my TECNO L8 Lite using JamiiForums mobile app

JIWE ni tatizo kwasababu hakubali mapungufu yake; ili kuweza kumsaidia mtu mwenye tatizo lolote lile ni lazima kwanza muhusika akubali kuwa ana tatizo ndio ataweza kupata msaada!!!
 
Ungeleta uzi kwa kilugha kilicho kuja na ngalawa ingependeza zaidi
 
Ni aibu kwa rais wa nchi kama Tanzania, ambaye amesoma mpaka chuo kikuu kwa kiingereza, akaishi ulaya, akafanya Phd kwa kiingereza halafu hajui kuongea kiingereza fasaha.

Rais wa nchi ndio kioo cha nchi, kiingereza kibovu cha rais wetu ni aibu kwetu sisi sote. Wasaidizi wa rais wako wapi kumsaidia kumfundisha kiingereza kizuri.
Wasaidizi wenyewe kajaza Vilaza watupu Mkuu watamshauri nini, Msigwa na Buhohela? Vilaza 100%
 
Kwani Amekosea Wapi Jameni

Sisi tuangalie Kazi. Haya ya Viingereza sio mhimu sana kwani Urusi wanaongea Kiingereza? Leteni Hoja mfano zile za maslahi ya wafanyakazi sio hii.
 
Huyu asingekuwa katili Mimi ningekuwa miongoni mwa watanzania wanaompenda na kumhurumia na kumtetea ila tatizo ni ukatili wake na visasi vya ajabu na kujifikiria kwamba yeye ndio alfa na omega na mjua kila kitu na mzalendo kuliko aliowaumba watz na msifiwa kuliko yesu na mkweli kuliko ukweli wenyewe anayefaa kukosoa wengine ila si kukosolewa

NINAJUTA SANA KUMFAHAMU JIWE amenifanya niishangae tz na watz hivi ni kweli tunaridhika na mfumo unaomfanya mwadamu mwenzetu mwenye mapungufu mengi kama sisi kuwa kama Mungu? Pole sana magufuli kwa kupewa mzigo mkubwa wa kiuungu na katiba yetu. Ila tutendee haki (yaani tuletee maji 😂😂😂😂)watanzania wote hata ambao hatutakuchagua
 
Yani nimecheka sana hata sijui nani atanisaidia kutafsiri mana hata sielewi maana yake kwa kiswahili, nitamlipa sh 15,000 atakaye nitafsiria ili nielewe
 
Back
Top Bottom