Wasichana na wanawake tafuteni waume siyo wafanyakazi

Wasichana na wanawake tafuteni waume siyo wafanyakazi

Sasa nyote musifanye kazi ndio kusudio lako au??
Sikuhizi swala la kazi ni mtihani, wanawake wengi wanataka mtu mwenye kazi rasmi. Ukiwa huna mishe au mbangaizaji ni ngumu sana ku engage nao sababu wengi ni walengaji unless awe amefikia kwenye dead-end (30 yrs and older).

Wanatafuta chimbo la kujichimbia ili walie kivulini bila kuhaso. Akute una kila kitu ili aanze kutambia mashosti zake kuwa baasha wake una hela na ndinga kali apartment kali.
 
Wanawake, mabinti wa sasa hawataki ugumu wa maisha, wanaogopa kuteseka.
😂😂😂 hahah ukiwasema hivyo watakwambia unataka waishi kama bibi zao wa mwaka 47?

Ila wanaume tuna kazi sana zama hizi! Ndio wengine wamejiamulia nao kuwa walengaji, anaangalia mwanamke anayejiweza ndio anaongeza nguvu. Matokeo yake ndio ile kauli yao wanawake "sikuhizi kuna waowaj basi"
 
Pole mkuu. Vijana wa hovyo humu JF hawapendi uhuru wa mwanamke. Hawapendi mwanamke ajieleze kile takacho bali kile watakacho,uzi wako umewachoma na kuwauma sana.

Tuvijana tuvivu tuvivu tunaona kama umetusimanga kwa vile unaishi london walitegemea utakua tiketi ya kuwavuta huko ulipo.

Tukikubali kupeana uhuru humu hizi judgements za ajabu ajabu zitapungua na kuisha. Anatokea mburura mmoja na kutoa mifano ya wazazi wake mara nyenyenyee eti yeye alilelewa na mke kabla hajapata kazi.


Maisha ya saiv ni kusaidiana na sio kutegemeana na kupunjana. Wakaka,wababa,wababu wanalalamika kuchunwa pesa kila leo ila hawapendi mwanamke mwenye pesa awe na uhuru wa pesa zake
kusaidiana mwaliongea humu tu ila wengi wenu mmejiwekea kuwa mwanaume lazma akuhudumie while unacho offer ni mbunye tu. Yani as long as unampa mbunye yeye ndio akufanyie kila kitu, alipe kodi, akufungulie biashara, akupe pocket money, akukojoze, akutoe outing n.k. wakati huo wewe ni jobless.

Ila ikitokea kinyume wewe ndio una kazi kuyafanya hayo kwa umpendaye huwezi. Yet mnazungumzia kusaidiana kupi huko? Nyie mkiwa jobless tunawabeba ila sisi tukiwa jobless utaskia siwezi kulea mwanaume 😂😂😂
 
Mfano huyo mwanaume akipoteza kazi, ndoa itaendelea kuwepo?
Akipoteza kazi ni divorce tu maana mwanamke hawezi vumilia zaidi ya mwezi awe anatoa yeye hela tu 😂! Utasimangwa hadi utaiona dunia chungu. Kazi zenyewe ngumu labda kama una mtaji uanze kuendesha boda boda which is hard. Ulikuwa manager Boa bank ghafla uanze kuwa boda boda ni ngumu.

Kipaji hicho tumeumbiwa sisi tu mkuu, unamlisha mtu na kumvisha for 40 yrs bila kulalamika.
 
Nimekuelewa mdogo wangu, unamtizama na mwanaume husika. Kuwa haya ni maisha, muhimu tu asiwe mvivu atatafuta kazi nyengine. Tatizo mdogo wangu akiwa mvivu.
kwa huko London kazi inawezekana ikawa rahisi kuipata ila bongo ni shughuli ni rahisi kuhisi mtu ni mvivu ila fursa ya kazi hamna. Tulioko bongo ndio tunaelewa namna kazi ilivyo kazi kuipata. Ila ukiwa nayo mambo yanakuwa mukide mbaya wanawake utawakimbia wewe.
 
Punguza munkari na kujishuku, hamna mtu ametukana mtu hapa, ni mawazo huru na maoni huru, maoni ya mtu yakiwa ni tofauti na uliyonayo kichwani usitafsiri kama tusi au kusakamwa.

Mfungua uzi kaleta mada yake huru, hajashinikizwa na mtu au hajaja kujibu uzi wa mtu mwingine,

Uzi za wanaotaka wenza ni nyingi hivyo basi huna haja ya kuhofia kila usomacho.

Naona sehemu nyingi unaandika watu wanatukana na kukashifu binafsi sijaona matusi wala kashfa sijui unatafsiri namna gani, inaonekana hujiamini kwa namna fulani, mtu asiyejiamini siku zote hudhani ni yeye tu anaonewa na kutukanwa na kusemwa, badili mtazamo wako sasa.
Mtoto wa watu anajishtukia aisee 😂😂😂
 
Sikuhizi swala la kazi ni mtihani, wanawake wengi wanataka mtu mwenye kazi rasmi. Ukiwa huna mishe au mbangaizaji ni ngumu sana ku engage nao sababu wengi ni walengaji unless awe amefikia kwenye dead-end (30 yrs and older).

Wanatafuta chimbo la kujichimbia ili walie kivulini bila kuhaso. Akute una kila kitu ili aanze kutambia mashosti zake kuwa baasha wake una hela na ndinga kali apartment kali.
Mimi sio mwanamke ninaetegemea cha mtu na wala sitaki mume mvivu, sote tuwe na kazi.
 
Kizazi hiki Cha kudanga ni hatari Sana kwenye mustakabali wa ndoa..wanawake waelewa ktk hili wachache Sana..Sio Kila mwanaume anakuwa tayari amejikamilisha ndio aingie kuoa..Mwanaume akiwa na vision ya Nini anataka kufanya na anajibidisha inatosha.Mengine Mungu atafungua mbele ya safari .

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Hayo ni maoni yako
 
Sidhani kama umemuelewa mtoa mada, hajamaanisha uolewe na marioo au kibenten hapana, alichomaanisha ni kuwa uolewe au kuoa kwa sababu ya upendo, mengine ni nyongeza.
Nilikuja muelewane baadae nikajibu tena, ahsante saaana.
 
Back
Top Bottom