Tetesi: Wasio na Vitambulisho vya Utaifa Kutopata Mshahara?

Tetesi: Wasio na Vitambulisho vya Utaifa Kutopata Mshahara?

Jamaa anatia huruma... na vile mwezi huu salary imeongezwa.. patamu hapo!!
Mie mwenyewe hapa nina mashaka kama nitapa au la! maana mie nimezaliwa 11/5 na ndio tarehe ambayo iko kwenye kitambulisho changu cha NIDA na cheti cha kuzaliwa lakini kwenye Lawson inasomeka nimezaliwa 10/5.
 
Mie mwenyewe hapa nina mashaka kama nitapa au la! maana mie nimezaliwa 11/5 na ndio tarehe ambayo iko kwenye kitambulisho changu cha NIDA na cheti cha kuzaliwa lakini kwenye Lawson inasomeka nimezaliwa 10/5.
hahaha imekula kwako hiyo!! Hadi taarifa zifanane... kwa nini hukurekebisha mapema ulivyoona salary slip ina makosa ya tarehe?
 
Hizo taarifa si za kweli.
Huu sio uhakiki huu ni mpango wa kuunganisha taarifa za watumishi ambazo zimetawanyika sehemu mbalimbali(nida, utumishi na hazina) ili zifanane kuepuka mrundikano wa taarifa nyingi zinazojirudiarudia.

Na ni zoezi endelevu hivyo halihusiani na usitishwaji wa mishahara.

Mshahara utasitishwa kama itabainika taarifa zako zilizoko utumishi ni tofauti na za nida na hazifanani na za hazina na pia umeshindwa kuthibitisha taarifa sahihi ni zipi.
Hapo tayari unakuwa ni mtumishi hewa.
 
Mbona pengine sijaskia hizo mambo za uhakiki kupitia ID sijui za kazi mara salary au ni zoezi jipya

Sent from my TECNO Camon CX using JamiiForums mobile app
Ni kwa watumishi wa umma wote! hata kama uko "SU"
 
Zoezi likoje Mkuu kama kwenu lishaanza maana wengine tupo likizo na ofisi bado haijatupa taarifa

Sent from my TECNO Camon CX using JamiiForums mobile app
Hili zoezi linashughulikiwa na ofisi ya Utumishi kwenye ofisi yako (HR office kama wanalivyozoea kujiita). Kuna ofisi ambazo zina matawi sehemu mbalimbali na kule walipo hakuna mtu wa kuwahakiki hivyo wanakwenda ofisi za Halmashauri za miji, manispaa au jiji walipo au wanakwenda ofisi ya Mkuu wa mkoa.

Unatakiwa kwenda kwenye uhakiki na vitu vitatu: salary slip, kitambulisho cha kazini na kitambulisho cha taifa alimaarufu NIDA. kama uko likizo jitahidi uwasiliane na ofisi yako idara ya utumishi wakupe utaratibu. usidharau hii serikali ya awamu hii kukutoa kwenye system ni dakika!
 
Hili zoezi linashughulikiwa na ofisi ya Utumishi kwenye ofisi yako (HR office kama wanalivyozoea kujiita). Kuna ofisi ambazo zina matawi sehemu mbalimbali na kule walipo hakuna mtu wa kuwahakiki hivyo wanakwenda ofisi za Halmashauri za miji, manispaa au jiji walipo au wanakwenda ofisi ya Mkuu wa mkoa.

Unatakiwa kwenda kwenye uhakiki na vitu vitatu: salary slip, kitambulisho cha kazini na kitambulisho cha taifa alimaarufu NIDA. kama uko likizo jitahidi uwasiliane na ofisi yako idara ya utumishi wakupe utaratibu. usidharau hii serikali ya awamu hii kukutoa kwenye system ni dakika!
Nimekuelewa Mkuu.

Sent from my TECNO Camon CX using JamiiForums mobile app
 
kwani bado kuna ugumu wa kukipata maana nakumbuka changu niliambiwa ntapigiwa simu hadi leo zaidi ya mwaka kama sio miaka. NIDA nao wawe aggressive kwenye kazi zao nimejua kilipo baada ya kwenda kukifuatilia sasa hivi angalau najua hata namba yangu.
kazi kwenu watumishi wa umma.
Kama hukupigiwa simu jua kuna tatizo mahali, unatakiwa kukifuata baada ya mwezi mmoja... Hata kama hujapigiwa simu... Kwa hiyo nenda Kachukue kama hakipo basi taarifa zako hazikwenda kwa hiyo Itabidi urudie tena kujaza fomu na sasa utaratibu umebadilika mkuu...

Lazima fomu yako ipite uhamiaji wa ndani kwa ajili ya mhuri na utapewa maelekezo huko kabla ya kupata huo mhuri....

Omba Mungu kiwepo tuu...
 
kuisoma nambaaa

Sent from my Samsung galaxy- S7 edge using Jamiiforum mobile App
 
Kama hukupigiwa simu jua kuna tatizo mahali, unatakiwa kukifuata baada ya mwezi mmoja... Hata kama hujapigiwa simu... Kwa hiyo nenda Kachukue kama hakipo basi taarifa zako hazikwenda kwa hiyo Itabidi urudie tena kujaza fomu na sasa utaratibu umebadilika mkuu...

Lazima fomu yako ipite uhamiaji wa ndani kwa ajili ya mhuri na utapewa maelekezo huko kabla ya kupata huo mhuri....

Omba Mungu kiwepo tuu...
asante. walikichungulia kwenye system pale 7/7 kipo . ngoja siku niliyoambiwa ikifika nikakione kama kipo kweli. ingawa nilipewa namba ya hicho kitambulisho.
asante kwa maelezo mkuu
 
Wakuu, kwahiyo mshahara hatutopata au?
 
Hata mie hapa kibaruani kwangu tumesisitizwa kuhakikisha tunafanyiwa uhakiki huo wa kuonesha kitambulisho cha kazi, salary slip na kitambulisho cha taifa, wanasema ukizembea kuna hatari ya kukosa "mtonyo" wa mwezi wa saba.


Mie ofisini kwangu tarehe ya mwisho ya uhakiki ni tarehe 25 unadhani nitakosa mshahara Wa July hapo?, kwanza cjawahi kuwa na kitambulisho cha Taifa.
 
Back
Top Bottom