Wasomi jifunzeni kwa dada Mwasu, dereva wa bajaji msomi mwenye shahada mbili

Wasomi jifunzeni kwa dada Mwasu, dereva wa bajaji msomi mwenye shahada mbili

Je ! Ni wasomi wangapi wana vyeti vizuri vya elimu juu, lakini wanapata taabu sana baada ya kukosa ajira na hata pesa ya kununua wembe nk ?
Na ndiyo point yangu mkuu. Tunahimiza kundi kubwa lichukue taaluma fulani wakati mahitaji ya wenye taaluma hiyo ni madogo.
Mwisho wa siku una miaka 24 na cheti chako, af unaambiwa start small, wakati ungeanza small ukiwa na miaka 13 sa hivi ungekuwa sugu wa kitaa.
 
View attachment 1660302

Tofauti na mawazo ya wengi kuwa ukisoma hadi chuo kikuu lazima uajiriwe, Mwasu Mavere ameonyesha upande mwingine wa shilingi, kwamba unaweza kujiajiri na kufanikiwa zaidi. Licha ya kuwa na shahada ya uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), yeye ameamua kuwa dereva wa pikipiki ya miguu mitatu (bajaji) akisafirisha abiria katikati ya makao makuu ya nchi, Dodoma.

Dada Mwasu anasema wasomi wengi wanatembea na bahasha miaka hadi mitatu bila kupata kazi, kumbe wangeuza hata karanga zingewaingizia kipato badala ya kuzunguka na vyeti. Hata hivyo, anasema mfanyabiashara msomi ni tofauti na asiyesoma, kwa kuwa ile elimu aliyonayo msomi anaitumia kufanya vizuri kwenye biashara zake. “Kuna wasomi wengi wanaendesha bajaji na bodaboda na wapo wengine wengi mtaani wanatafuta kazi, hawajajua kuwa kuna kazi ya kuendesha bajaji na kujipatia fedha kama walioajiriwa, hivyo niwatake waache kuchagua kazi,” alisema Mwasu alipozungumza na Mwananchi.

Mwasu alianza shughuli za usafirishaji abiria Desemba 2018 katika eneo la eneo la Royal Village, Dodoma lakini baada ya muda alihamia katikati ya mji ili kupata abiria wa pande zote. Anasema wasomi wengi wanatembea na bahasha miaka hadi mitatu bila kupata kazi, kumbe wangeuza hata karanga zingewaingizia kipato badala ya kuzunguka na vyeti.

Hata hivyo, anasema mfanyabiashara msomi ni tofauti na asiyesoma, kwa kuwa ile elimu aliyonayo msomi anaitumia kufanya vizuri kwenye biashara zake. “Kuna wasomi wengi wanaendesha bajaji na bodaboda na wapo wengine wengi mtaani wanatafuta kazi, hawajajua kuwa kuna kazi ya kuendesha bajaji na kujipatia fedha kama walioajiriwa, hivyo niwatake waache kuchagua kazi,” alisema Mwasu alipozungumza na Mwananchi.

Mwasu alianza shughuli za usafirishaji abiria Desemba 2018 katika eneo la eneo la Royal Village, Dodoma lakini baada ya muda alihamia katikati ya mji ili kupata abiria wa pande zote. “Elimu yangu ni masters, lakini mshahara mdogo niliokuwa nalipwa ndio uliosababisha nikaamua kuacha kazi na kujishughulisha na biashara mbalimbali ikiwemo kuuza nguo na hatimaye nikaanza kuendesha bajaji,” anasema.

Mwasu, mama wa watoto wawili anasema mshahara aliokuwa analipwa ambao haukukidhi mahitaji yake wala kuendana na kiwango chake cha elimu, ulisababisha akaichukia ajira akaamua kujiajiri mwenyewe.Alisema mwaka 2009 alihitimu shahada ya sociology and political science nchini Kenya na baada ya hapo alirudi nchini na kufanya kazi katika NGOs mbalimbali.

Ilifopika mwaka 2011 aliamua kujiendeleza katika Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) huku akiendelea kufanya kazi. Alihitimu mwaka 2013 shahada ya uzamili katika utawa (Masters of public adminstration). Alisema wakati anafanya kazi kwenye shirika lisilo la kiserikali la Afnet alikuwa programme officer na field officer baada ya muda akahamia katika shirika jingine la Ngonedo ambapo alikuwa monitoring and evaluation officer (ufuatiliaji na tathmini).

Mwasu alisema katika kipindi alichofanya kazi hakuwa na mshahara uliokuwa unazidi Sh390,000 kwa mwezi, ambao amesema haukuwa unakidhi mahitaji yake. Alisema kipindi hicho anafanya kazi alikuwa na mtoto mdogo, hivyo kutokana na mahitaji yake kuwa mengi na mshahara mdogo alipomaliza shahada ya uzamili aliamua kuacha kazi na kuanzisha biashara mbalimbali ikiwemo kuuza nguo. “Hela hiyo haikuwa inakidhi mahitaji yangu, mwisho wa siku nikaona ili nisiingie kwenye vishawishi vya kuiba fedha ofisini ili kukidhi mahitaji, bora niache kazi, niliona ni bora kujiajiri mwenyewe kuliko kuajiriwa kwani nilichokuwa ninalipwa hakilingani na elimu yangu.

“Wakati huo nafanya kazi, nilikuwa nakusanya hela kidogo kidogo na kuna siku nilienda field, pesa niliyolipwa na zile akiba zangu nikaamua kuanzisha biashara kwa mtaji wa Sh400,000. Nilikwenda Kariakoo (Dar es Salaam na kuchukua mzigo wa nguo na kuja kuuza Dodoma.” Alisema Mwasu, biashara yake ilikuwa vizuri na alikuwa anaingiza fedha kuliko zile alizokuwa analipwa wakati ameajiriwa.

Biashara hiyo aliifanya kwa muda mrefu hadi akawa anasafiri kwenda China pamoja na wafanyabiashara wengine kuchukua mzingo wa nguo na kuuza nchini. “Katika biashara kuna kuinuka, lakini pia unaweza kushuka. Biashara yangu ilikuja kuwa mbovu nikawa napata hasara, si kila siku ni kupata faida, hasara kwa mfanyabiashara haikwepeki nawakati huo tayari nilikuwa nishapata mtoto wa pili. “Licha ya hasara hiyo, sikukata tamaa badala yake nikaamua kubadilisha kazi ya kufanya. Niliamua kuachana na biashara kabisa na kuwa dereva bajaj,” alisema.

Endelea kufahamu Kilichomfanya aendeshe bajaji na Manufaa yake pamoja na Changamoto aipatayo kupitia link >>> Mwasu, dereva wa bajaj mwenye shahada mbili

View attachment 1660415

Elimu ya Tanzania kwa sasa imebadilika.
Yaani kwa sasa ni kusoma kuongeza elimu tu(Kua na vyeti vingi).
Kuhusu swala la ajira kwa sasa ni kujikita kwenye fani tu.
Yaa inatakiwa ukisoma ualimu jiandae kuwa muuza mafuta sheli.
 
Na hili gazeti la mwananchi wanafeli sana, badala ya kutuletea emerging youth billionaires watu wawe inspired, tunarudishana kwenye udereva wa bajaji
Au kutuletea emerging innovations in Tz..! Magazeti yetu ya bongo yanatuangusha sana!!
 
Huyo kaamua kuwa kioja kwenye jamii.

Aingie kwenye fani ya vioja na vituko huko bongo movie atapiga hela
 
Haikuwa na maana kupoteza muda na fedha kugharamia elimu mpk shahada mbili af uishie kuwa dereva Bajaji,sbb ata bila elimu hyo angeweza kuendesha. Nafikir kaz hyo sio ndoto yke ila anafanya 2 ili kukidh mahtaji,Hvo si mfano wa kuigwa coz ukimuiga huyu unaiga hasara kwa familia.
 
Na ndiyo point yangu mkuu. Tunahimiza kundi kubwa lichukue taaluma fulani wakati mahitaji ya wenye taaluma hiyo ni madogo.
Mwisho wa siku una miaka 24 na cheti chako, af unaambiwa start small, wakati ungeanza small ukiwa na miaka 13 sa hivi ungekuwa sugu wa kitaa.j
Kuajiriwa Tanzania ni sawa na kupata mkopo 100% wa chuo kutoka bodi ya mikopo helsb
 
Haikuwa na maana kupoteza muda na fedha kugharamia elimu mpk shahada mbili af uishie kuwa dereva Bajaji,sbb ata bila elimu hyo angeweza kuendesha. Nafikir kaz hyo sio ndoto yke ila anafanya 2 ili kukidh mahtaji,Hvo si mfano wa kuigwa coz ukimuiga huyu unaiga hasara kwa familia.
Maoni tumeyasoma. Asante !
 
Wewe kama kweli elimu uliyosoma imekuelimisha basi jibu hilo swali.

Imagine wewe ni mtoto wa masikini then umemaliza chuo.
But una ndoto za kumiliki company kubwa itakayo tatua changamoto za kijamii.

Hapo wewe utafanyaje as mtoto wa masikini ili utimize hizo plans?
Ujiajiri kupitia taaluma yako mbona changamoto ni nyingi?

Si akafungue hta tuition basi hapo kitaa!!

Mie nlipomaliza chuo nilijiajiri ila kupitia taaluma yangu nikawa nafundisha wanachuo wapya, naandika tafiti, naandaa business plans, docx za negotiation n.k so bado nilikua eneo langu nililosomea.

Sasa imagine mimi na Msc ya Uchumi niendeshe bajaj, Y nilienda shule?
 
Hivi katika dunia ya utandawazi unalaumu mfumo wa elimu huku utandawazi unakupa chance ya kujifunza chochote kilicho kosekana kwetu? .
Good sababu siongei as an individual bali kwa ajili ya majority.

Nadhani unapoongelea utandawazi unaamanisha internet ambayo yote yaliyokesana kwenye elimu yetu yapo huko.
Mimi ninayo access.

Question: now can you tell wanafunzi wangapi wa kitanzania wana access ya internet?
Namaanisha wanafunzi wote Tanzania haijarishi ni primary, secondary ngazi za juu kabisa.

Ukiacha wasio na access wenye access hawatumii huo utandawazi kujifunza bali kujiharibu bila kujua.


halafu to a mbadala elimu iboreshwe nini sio lawama tu.
Lawama ni dalili ya kushindwa.
Mkuu mbadala wa elimu nishatoa sana.


Pia nina imani hiyo serikali inajua inachokifanya kama itaamua kubadilisha mfumo.
Hivi umetafiti kuwa mfumo wa elimu yetu haufanani na nchi zingine?
Unadhani mfumo tunaoutumia sisi unafanana na nchi zote?
 
Aisee ni naona sio kitu cha kujivunia ila ni ufinyu wa upana wa elimu yetu.
Masters then unaendesha bajaj ni sawa kwa ajili ya kipato ila sio kujivunia na kuwa front page.
 
Si akafungue hta tuition basi hapo kitaa!!
Mkuu unadhani kila binadamu ana mipango sawa na mwingine kwenye maisha yao?
Unajuaje kwamba hana idea kubwa ya kufanya kitu kikubwa baada ya kuwekeza?
Sasa imagine mimi na Msc ya Uchumi niendeshe bajaj, Y nilienda shule
Mkuu unajua kuhusu chimbuko la Facebook?

Mkuu hakuna kitu simple yaani unaibuka tu tayari una company.
Mie nlipomaliza chuo nilijiajiri ila kupitia taaluma yangu nikawa nafundisha wanachuo wapya, naandika tafiti, naandaa business plans, docx za negotiation n.k so bado nilikua eneo langu nililosomea.
That's why nikakuuliza unadhani kila binadamu ana mipango au ndoto sawa na mwingine?

Unajuaje kama anataka kufungua company mfano wa uber ile yeye anatumia bajaj instead sababu bajaj inatumika zaidi maeneo ya mitaani.
Unajuaje hana hiyo idea?

Ungemuona sahihi kumiliki company ya bajaj ila chimbuko lake hulijui na akikwambia chimbuko lake utakataa?
 
Hata Rais John Magufuli wakati anasoma, hakuwa na ndoto ya urais kama wengine ... ! Alichukua PhD kuongeza elimu si kipato.
 
Back
Top Bottom