Wasomi jifunzeni kwa dada Mwasu, dereva wa bajaji msomi mwenye shahada mbili

Wasomi jifunzeni kwa dada Mwasu, dereva wa bajaji msomi mwenye shahada mbili

Si akafungue hta tuition basi hapo kitaa!!
Can you tell kipi bora kati ya kufungua tuition na kumiliki company ya bajaj mfano wa uber?

Unadhani how much atatengeza kutoka kwenye company hiyo ambayo itakuwa inafanya kazi Tanzania nzima?

6 million per day or 50 million per day tsh?

Now kati ya yeye na wewe nani ungemuona yupo sahihi?
 
Mkuu unadhani kila binadamu ana mipango sawa na mwingine kwenye maisha yao?
Unajuaje kwamba hana idea kubwa ya kufanya kitu kikubwa baada ya kuwekeza?

Mkuu unajua kuhusu chimbuko la Facebook?

Mkuu hakuna kitu simple yaani unaibuka tu tayari una company.

That's why nikakuuliza unadhani kila binadamu ana mipango au ndoto sawa na mwingine?

Unajuaje kama anataka kufungua company mfano wa uber ile yeye anatumia bajaj instead sababu bajaj inatumika zaidi maeneo ya mitaani.
Unajuaje hana hiyo idea?

Ungemuona sahihi kumiliki company ya bajaj ila chimbuko lake hulijui na akikwambia chimbuko lake utakataa?
Mkuu tusitafute justification.... Wote waliotoboa walifanya vitu vilivyopo kwa namna tofauti.

Mfano angeingia dili say na wasafi ili waziite ''Wasafi Xpress'' so bajaji zake zinakua na brand kubwa na zingesafirisha mpka A list.

Ssa kuona mtu ana masters alafu anaendesha biashara kwa style ile ile iliopo na doubt elimu yake.

Huyo kma ana M.A basi ni zile za kubebwa ila content hana kichwani. Anatudhalilisha wasomi
 
"UDOM ni chuo cha vilaza"....in Magu's voice.
Kwa kweli mkulu hakukosea kuwaita vilaza Kama output za chuo hicho ndo type hii ya kina Mwasu
 
Can you tell kipi bora kati ya kufungua tuition na kumiliki company ya bajaj mfano wa uber?

Unadhani how much atatengeza kutoka kwenye company hiyo ambayo itakuwa inafanya kazi Tanzania nzima?

6 million per day or 50 million per day tsh?

Now kati ya yeye na wewe nani ungemuona yupo sahihi?
Afungue UBER wakati bajaj anayotumia hta rangi tu no kma zilizopo mtaani? Ameshindwa hta customization na product differentiation ndio aweze franchising kma UBER?

Mimi niliwahi fungua biashara huko nyuma ila kwakuwa sikua na mtaji nkaongea na superstar mmoja yye akawa ndio kma mmiliki ila mwisho wa siku alikua kivuli tu. So yye akawa kma ananiletea wateja mie naingiza pesa. Hapo ndio unaona elimu ilifanya kazi sio upuuzi wa kuendesha bajaji!!

Hvi tunaelewa Masters ni nini? Ada tu million 6-8 alafu ukaendeshe bajaj? Matatizo ya taaluma yake yote yana ufumbuzi?

NB: Kina zuckeberg unaowatolea mfano walijiajiri kupitia Taaluma zao. Sio zuckeberg alisomea IT alafu akaendeshe malori ni upuuzi
 
Mkuu tusitafute justification.... Wote waliotoboa walifanya vitu vilivyopo kwa namna tofauti.
Sitafuti justification bali ni ukweli.

Kwamba kama mtu ni masikini basi huwezi kufika popote bila kuanzia chini.

That's why kuna wapenda shortcut au wote wanakimbilia ajira.
Ssa kuona mtu ana masters alafu anaendesha biashara kwa style ile ile iliopo na doubt elimu yake.
Unaweza ukaniambia kuna wasomi wangapi Tanzania walio apply elimu zao ukiondoa waliopata ajira.

If hujui wangapi mention majina yao then uangalie chimbuko lao.
 
Naomba namba yake awe anakuja kunichukua huku Koromije na kunipeleka Dom wakati wa mikutano ya bunge.
 
Sitafuti justification bali ni ukweli.

Kwamba kama mtu ni masikini basi huwezi kufika popote bila kuanzia chini.

That's why kuna wapenda shortcut au wote wanakimbilia ajira.

Unaweza ukaniambia kuna wasomi wangapi Tanzania walio apply elimu zao ukiondoa waliopata ajira.

If hujui wangapi mention majina yao then uangalie chimbuko lao.
Mie nawafahamu wawili ni wasomi wa M.A mmoja Godwin mwingine Winnie. Hawajaajiriwa ila wame design products mwingine App mpya kabisa sokoni. Na wana progress nzuri.

Hao ndio ilipaswa mwananchi iwahoji maana wamejiajiri kusolve matatizo ya sekta zao sio kuendesha bajaji. Ni kudhalilisha elimu ya Masters

UDOM wamfutie hyo award.... Haiwezekani shida za sociology na administration hazijaisha alafu anaendesha bajaji!!!
 
Huu upumbavu inabidi tuuache mwaka huu 2020 huko tuendako tutaanza kuwazaba makofi mtu yoyote anaewaambia wasomi kuwa wakajiajiri.

Hivi mtu asome miaka yote zaidi ya 15 halafu uje umletee upuuzi wa kuwa ajiajiri, hiyo taaluma alisomea ya kazi gani?!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Afungue UBER wakati bajaj anayotumia hta rangi tu no kma zilizopo mtaani? Ameshindwa hta customization na product differentiation ndio aweze franchising kma UBER
Unadhani kwanini asiweze?
Mimi niliwahi fungua biashara huko nyuma ila kwakuwa sikua na mtaji nkaongea na superstar mmoja yye akawa ndio kma mmiliki ila mwisho wa siku alikua kivuli tu. So yye akawa kma ananiletea wateja mie naingiza pesa. Hapo ndio unaona elimu ilifanya kazi sio upuuzi wa kuendesha bajaji!!
Mkuu wewe hautoshi kujitolea mfano ndani ya graduates karibu mill 6 hauwezi fika hata asilimia .05.

Still narudia hamuwezi kufanana mipango na mwingine hata kama muwe na elimu sawa au elimu ya shule ilifundisha kuongea na superstars kama hauna mtaji?
Kina zuckeberg unaowatolea mfano walijiajiri kupitia Taaluma zao. Sio zuckeberg alisomea IT alafu akaendeshe malori ni upuuzi
Yeah ila Zuckerberg hakuibuka tu na company from nowhere.

And nani amekwambia Zuckerberg amesomea IT
Wakati hata chuo hakumaliza?
 
Mie nawafahamu wawili ni wasomi wa M.A mmoja Godwin mwingine Winnie. Hawajaajiriwa ila wame design products mwingine App mpya kabisa sokoni. Na wana progress nzuri.
Would you tell me walianzaje bila mtaji?

Let me ask you a question.

Imagine wewe ni mtoto wa masikini au ni masikini as huyo dada pia umemaliza chuo na elimu yako let say una economics degree na una plans za kumiliki company kubwa ya usafiri.

Wewe ungefanya nini kwenye situation kama hiyo?
 
View attachment 1660302

Tofauti na mawazo ya wengi kuwa ukisoma hadi chuo kikuu lazima uajiriwe, Mwasu Mavere ameonyesha upande mwingine wa shilingi, kwamba unaweza kujiajiri na kufanikiwa zaidi. Licha ya kuwa na shahada ya uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), yeye ameamua kuwa dereva wa pikipiki ya miguu mitatu (bajaji) akisafirisha abiria katikati ya makao makuu ya nchi, Dodoma.

Dada Mwasu anasema wasomi wengi wanatembea na bahasha miaka hadi mitatu bila kupata kazi, kumbe wangeuza hata karanga zingewaingizia kipato badala ya kuzunguka na vyeti. Hata hivyo, anasema mfanyabiashara msomi ni tofauti na asiyesoma, kwa kuwa ile elimu aliyonayo msomi anaitumia kufanya vizuri kwenye biashara zake. “Kuna wasomi wengi wanaendesha bajaji na bodaboda na wapo wengine wengi mtaani wanatafuta kazi, hawajajua kuwa kuna kazi ya kuendesha bajaji na kujipatia fedha kama walioajiriwa, hivyo niwatake waache kuchagua kazi,” alisema Mwasu alipozungumza na Mwananchi.

Mwasu alianza shughuli za usafirishaji abiria Desemba 2018 katika eneo la eneo la Royal Village, Dodoma lakini baada ya muda alihamia katikati ya mji ili kupata abiria wa pande zote. Anasema wasomi wengi wanatembea na bahasha miaka hadi mitatu bila kupata kazi, kumbe wangeuza hata karanga zingewaingizia kipato badala ya kuzunguka na vyeti.

Hata hivyo, anasema mfanyabiashara msomi ni tofauti na asiyesoma, kwa kuwa ile elimu aliyonayo msomi anaitumia kufanya vizuri kwenye biashara zake. “Kuna wasomi wengi wanaendesha bajaji na bodaboda na wapo wengine wengi mtaani wanatafuta kazi, hawajajua kuwa kuna kazi ya kuendesha bajaji na kujipatia fedha kama walioajiriwa, hivyo niwatake waache kuchagua kazi,” alisema Mwasu alipozungumza na Mwananchi.

Mwasu alianza shughuli za usafirishaji abiria Desemba 2018 katika eneo la eneo la Royal Village, Dodoma lakini baada ya muda alihamia katikati ya mji ili kupata abiria wa pande zote. “Elimu yangu ni masters, lakini mshahara mdogo niliokuwa nalipwa ndio uliosababisha nikaamua kuacha kazi na kujishughulisha na biashara mbalimbali ikiwemo kuuza nguo na hatimaye nikaanza kuendesha bajaji,” anasema.

Mwasu, mama wa watoto wawili anasema mshahara aliokuwa analipwa ambao haukukidhi mahitaji yake wala kuendana na kiwango chake cha elimu, ulisababisha akaichukia ajira akaamua kujiajiri mwenyewe.Alisema mwaka 2009 alihitimu shahada ya sociology and political science nchini Kenya na baada ya hapo alirudi nchini na kufanya kazi katika NGOs mbalimbali.

Ilifopika mwaka 2011 aliamua kujiendeleza katika Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) huku akiendelea kufanya kazi. Alihitimu mwaka 2013 shahada ya uzamili katika utawa (Masters of public adminstration). Alisema wakati anafanya kazi kwenye shirika lisilo la kiserikali la Afnet alikuwa programme officer na field officer baada ya muda akahamia katika shirika jingine la Ngonedo ambapo alikuwa monitoring and evaluation officer (ufuatiliaji na tathmini).

Mwasu alisema katika kipindi alichofanya kazi hakuwa na mshahara uliokuwa unazidi Sh390,000 kwa mwezi, ambao amesema haukuwa unakidhi mahitaji yake. Alisema kipindi hicho anafanya kazi alikuwa na mtoto mdogo, hivyo kutokana na mahitaji yake kuwa mengi na mshahara mdogo alipomaliza shahada ya uzamili aliamua kuacha kazi na kuanzisha biashara mbalimbali ikiwemo kuuza nguo. “Hela hiyo haikuwa inakidhi mahitaji yangu, mwisho wa siku nikaona ili nisiingie kwenye vishawishi vya kuiba fedha ofisini ili kukidhi mahitaji, bora niache kazi, niliona ni bora kujiajiri mwenyewe kuliko kuajiriwa kwani nilichokuwa ninalipwa hakilingani na elimu yangu.

“Wakati huo nafanya kazi, nilikuwa nakusanya hela kidogo kidogo na kuna siku nilienda field, pesa niliyolipwa na zile akiba zangu nikaamua kuanzisha biashara kwa mtaji wa Sh400,000. Nilikwenda Kariakoo (Dar es Salaam na kuchukua mzigo wa nguo na kuja kuuza Dodoma.” Alisema Mwasu, biashara yake ilikuwa vizuri na alikuwa anaingiza fedha kuliko zile alizokuwa analipwa wakati ameajiriwa.

Biashara hiyo aliifanya kwa muda mrefu hadi akawa anasafiri kwenda China pamoja na wafanyabiashara wengine kuchukua mzingo wa nguo na kuuza nchini. “Katika biashara kuna kuinuka, lakini pia unaweza kushuka. Biashara yangu ilikuja kuwa mbovu nikawa napata hasara, si kila siku ni kupata faida, hasara kwa mfanyabiashara haikwepeki nawakati huo tayari nilikuwa nishapata mtoto wa pili. “Licha ya hasara hiyo, sikukata tamaa badala yake nikaamua kubadilisha kazi ya kufanya. Niliamua kuachana na biashara kabisa na kuwa dereva bajaj,” alisema.

Endelea kufahamu Kilichomfanya aendeshe bajaji na Manufaa yake pamoja na Changamoto aipatayo kupitia link >>> Mwasu, dereva wa bajaj mwenye shahada mbili

View attachment 1660415
Mawazo ya kijinga kabisa, hivi hiyo bajaji ndicho alichosomea??? Kwa nini anaingilia kazi za watu???? Hivi tofauti ya aliyesoma na asiyesoma ni kitu gani??? Kwa nini asingetafuta namna ya kutatua changamoto za jamii kulingana na alichosomea???? Idiot kabisa huyu msomi. Vyuo vinahitaji kujitransform toka kutoa digrii za makaratasi mpaka problem solver kuliko hawa wanaokariri eti kuuza karanga ni kujiajiri.
 
Tujifunze nini sasa? Toa ujinga hapa.
Hatukusomea kuendesha bajaji sisi.
Yeah Hukusomea kufungua company.

Like mwenye uber hakusomea udereva taksi just like you.

Now unajua yuko wapi?
No you don't yeye aliona miaka kadhaa mbele.

Bila shaka wakati anaanza ungekuwa una mmock just like this.
 
Mawazo ya kijinga kabisa, hivi hiyo bajaji ndicho alichosomea??? Kwa nini anaingilia kazi za watu???? Hivi tofauti ya aliyesoma na asiyesoma ni kitu gani??? Kwa nini asingetafuta namna ya kutatua changamoto za jamii kulingana na alichosomea???? Idiot kabisa huyu msomi. Vyuo vinahitaji kujitransform toka kutoa digrii za makaratasi mpaka problem solver kuliko hawa wanaokariri eti kuuza karanga ni kujiajiri.
Mkuu unadhani mmiliki halali wa uber alisomea udereva taksi?
 
Yule mzee hajaenda shule kihistoria so kastruggle kwelikweli miaka yote Hadi kawa bilionea,ila huyu bi mdada kapoteza muda class halafu anakuja kutamba eti ana masters anaendesha bajaji,angeishia la 7 na kuanza kuendesha bajaji then akaja mitandaoni na kusema niliishia la 7 nikajiajiri kuendesha bajaji na sasa nina miliki bajaji 10 ange-motivate vijana na wasomi wengine ,ila huyu dada ni kama anatumika kipropaganda na kuishusha hadhi elimu yetu
Mwisho wa siku Ni kuwa na pesa haijalishi background yako Ni ipi

Kama unaingiza pesa kwangu Mimi is okey sijali unaingizia juani au kwenye AC
 
Mkuu unadhani mmiliki halali wa uber alisomea udereva taksi?
Yeye alileta suluhisho la upatikanaji wa usafiri kwa bei nafuu na pahala popote, na huo ndiyo usomi, na usomi wa kuelewa namna ya kutatua changamoto haijalishi umesomea kitu gani. Hivyo huyu mdada na li bajaji lake hajatatua tatizo la jamii zaidi ya kuwa sawa na wale hawajaenda shule, afikirie mara nyingi contribution ya elimu yake kwa jamii.
 
Jambo la aibu sana!

Jitu na madigrii yake linaendesha bajaji- ati na serikali nayo inajivunia!!

Serikali inatumia mabilioni ya fedha kusomesha watu ambao wanaishia kuwa bodaboda!! NA WANAFIKIRI WAKO SAWA?

Propaganda za ajabu sana! Ujanja ujanja wa kisiasa tu huu hakuna la kujifunza hapo!

Wameshindwa kuwasaidia vijana, badala yake wameamua kuja na propaganda uchwara!

AIBU! AIBU! AIBU! AIBU! AIBU! AIBU!
Wewe unafanya kazi ?

Serikali inaweza kukusomesha lakini haikupi guarantee ya kazi

Kama ndio unafanya kazi ukifukuzwa hapo unaweza survive hata mwaka mzima ?

kumtukana mtu anayeingiza Senti zake kihalali Ni ujuha

Ukitaka aende kudanga? na kujidhalilisha ?

Mpe moyo anaweza kua kiuchumi na kesho na kesho anaanzisha big business

'started from the bottom"-drake

[emoji123][emoji123][emoji123]
 
Yeye alileta suluhisho la upatikanaji wa usafiri kwa bei nafuu na pahala popote, na huo ndiyo usomi, na usomi wa kuelewa namna ya kutatua changamoto haijalishi umesomea kitu gani. Hivyo huyu mdada na li bajaji lake hajatatua tatizo la jamii zaidi ya kuwa sawa na wale hawajaenda shule, afikirie mara nyingi contribution ya elimu yake kwa jamii.
So unadhani aliibuka tu from nowhere na company kubwa namna vile?

Unajua company ya uber ilipoanzia?
usomi wa kuelewa namna ya kutatua changamoto haijalishi umesomea kitu gani
Mkuu dk chache nyuma uliandika hivi
Mawazo ya kijinga kabisa, hivi hiyo bajaji ndicho alichosomea??? Kwa nini anaingilia kazi za watu???? Hivi tofauti ya aliyesoma na asiyesoma ni kitu gani??? Kwa nini asingetafuta namna ya kutatua changamoto za jamii kulingana na alichosomea????
Kwamba anafanya kitu ambacho hakusomea now unajicontradict mwenyewe kwamba kutatua changamoto za jamii haijarishi umesomea nini.

Ina maana huna uhakika na unachokiandika?

That's why nimekuuliza kwani mmiliki wa uber alisomea udereva taksi?

Na je huyo mmiliki wa uber aliibuka tu na hiyo huge company from nowhere?

Je unajua uber ilivyoanza?
 
Back
Top Bottom