Wataalam wa kuchambua Biblia, nini maana ya hiki kifungu?

Wataalam wa kuchambua Biblia, nini maana ya hiki kifungu?

Down To Earth

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2011
Posts
21,940
Reaction score
16,643
Mungu aliye mkamilifu, asiye fananishwa na kitu, Alfa na Omega; hapa anatamkwa namna hii?

Ama kuna namna ilimaanishwa na Mwandishi wa Wakorinto?
Screenshot_20231226-113307.jpg
 
si kila mstari kwenye bible unaweza kuuelewa wenyewe kama wenyewe anzia juu kidogo at least mstari wa 15 au 16 utapata kuelewa paulo alimaanisha nini

unless uwe na lingine ulilolikusudia
Pia hivyo...coz anakuwa hajaelewa context kacherry pick
 
Mungu aliye mkamilifu, asiye fananishwa na kitu, Alfa na Omega; hapa anatamkwa namna hii?

Ama kuna namna ilimaanishwa na Mwandishi wa Wakorinto?
View attachment 2853435
Sorry ,,,tushike lipi?

Ujinga wa Mungu au Upumbavu wa Mungu?

1 Kor 1:25
Kwa sababu upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu
 
Tengeneza biblia yako ! Weka kifungu kama hicho badili kama ifuatavyo -

" kwa sababu upumbavu wa EXCEL una hekima zaidi kuliko mtu yoyote humu jamii forum na udhaifu wa EXCEL una nguvu zaidi wa ya yeyote humu jamii forum.

Mwandishi anawafikishia ujumbe watu ambao WANAMDHARAU EXCEL na je ? Ujumbe huu .

EXCEL binafsi atauchukuliaje? Mwandishi ni adui yake?

Wengine nao watajisikiaje?
 
Mungu aliye mkamilifu, asiye fananishwa na kitu, Alfa na Omega; hapa anatamkwa namna hii?

Ama kuna namna ilimaanishwa na Mwandishi wa Wakorinto?
View attachment 2853435
Excel, hapa tatizo lipo katika udhaifu wa kutafsiri kwenda Kiswahili, na pia kuelewa maana ya andiko. Mungu hana upumbavu wala ujinga, na ni hatari sana kumfikiria Mungu katika muktadha huo kwa sababu unaweza ukafanya kufuru au dhambi isiyosameheka kwa sababu ya utakatifu wake.

Maneno yaha ya Paulo katika andiko hili katika lugha sanifu ya Kiswahili yanapaswa kusomeka hivi, "Kwa sababu kitu kipumbavu cha Mungu ni chenye hekima kuliko wanadamu, na kitu dhaifu cha Mungu ni chenye nguvu kuliko wanadamu."

Sasa nini maana ya andiko hili? Ni wazi Mungu aliumba vitu vyenye complexity tofauti tofauti, na kama ni katika suala la design, basi utasema kuna uumbaji wa Mungu ni wa design iliyotumia akili ya juu sana. Kwa mfano, fikiria alivyoumba ubongo wa mwanadamu, ambao ni wa kipekee kuliko compyuta zenye nguvu sana. Lakini pia fikiria kiumbe rahisi sana alichoumba Mungu, kama earthworm. Katika macho ya kibinadamu, unaweza kuona kiumbe kama earthworm ni cha kipumbavu, au mwingine akaona Mungu kuumba vitu kama nzi halikuwa jambo la hekima.

Lakini sasa, ndio Paulo anawakumbusha watu, kwamba katika mtazamo wa kibinadamu, kile tunachoona kuwa cha " kipumbavu au kitu dhaifu" ni chenye hekima kuliko hao wanadamu ambao mara nyingine wanakosa kabisa hekima ya kuwa wameumbwa na Mungu. Hebu mlinganishe mtu anaemnajisi mtoto wa miaka mitatu, je, katika uumbaji wa Mungu, si utaona nzi ni kiumbe wa maana kuliko mtu kama huyo?

Na unaweza kuona kama kiumbe kama mbu anaeeneza malaria, ni namna ya udhaifu katika uumbaji wa Mungu, au kwa mfano funza (maggots) ambao utaona ni disgusting. Waliumbwa kwa sababu nzuri tu zinazomfaa binadamu, hawakufanywa wawepo ili kueneza magonjwa au kufanya uharibifu, kama vile tu simba hakuumbwa ili awinde wanyama na kuwala. Haya ni matokeo ya uasi wa shetani ibilisi. Kwa hiyo andiko hilo lipo katika context hiyo. Hivyo hata katika hali hizi, usiviangalie vitu katika context ya kuona ni kitu cha kipumbavu au udhaifu cha Mungu.

Lakini pia kuna suala ambalo linahusu amri za Mungu, ambazo wewe unawza kuona ni za kijinga au ni udhaifu kuzifuata. Akishasema usifanye hivi, hata kama unaona ni udhaifu, ni ujinga, watu hawatakuelewa, ujue kwamba yeye kama Mungu anaona mbali sana kuliko wewe kama mwanadamu. Fuata. Usichukue position ya kutaka kumshauri Mungu, au kuona kama alikosea, au hakufikiria mbali alipotoa agizo fulani. Kuna mtu anaona ni udhaifu kuomba msamaha pale ambapo unajua hujafanya kosa, lakini Mungu anasema wewe fanya hivyo hata kama unajua sio kosa lako, ili ulete amani na mtu mliekorofishana.

Vitu kama hivi muwe mnawatafuta mashahidi wa Yehova wawafafanulie. Nimejifunza mengi sana toka kwao, pamoja na hili. Huu sio ujuzi wangu, bali ni ufafanuzi wao.
 
Mungu aliye mkamilifu, asiye fananishwa na kitu, Alfa na Omega; hapa anatamkwa namna hii?

Ama kuna namna ilimaanishwa na Mwandishi wa Wakorinto?
View attachment 2853435
Mungu anasema natuumbe mtu kwa sura na mfano wetu lakini Mungu sii mtu.
Anasema mimi ni moto ulao lakini Mungu sii moto .
Mungu akanena kutoka katika upepo wa kisulisuli lakini Mungu sii upepo wa kisulisuli.
Sauti ikatoka katika lile giza kuu kunena na Musa lakini Mungu sii giza kuu.
Mungu akanena kwa kinywa cha Eliya nabii lakini Mungu sii eliya.
Mungu akanena na Musa kutoka katika kijiti cha moto kisichoteketea lakini Mungu Mungu sii kichaka cha moto nk.
Mungu anaweza kujifananishia chochote lakini huwezi sema katika vile alivyojifananishia ndiyo Mungu.
Mungu ni roho nao wamwabuduo yawapasa kumwabudu katika roho na kweli ambayo ni neno lake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mstari wa 1 Wakorintho 1:25 unamaanisha kwamba hata kitu ambacho watu wanaweza kukiona kuwa dhaifu au kipumbavu katika mtazamo wao, kwa upande wa Mungu ni cha hekima zaidi na nguvu zaidi. Hii ni kusema kuwa hekima na nguvu za Mungu ziko juu sana kuliko hekima na nguvu za binadamu. Hapo huo mstari haumaanishi MUNGU ni mjinga, bali unaonesha kuwa Sisi wanadamu kuna vitu MUNGU katuamuru, lakini kuna wengine wataona ni vya kijinga au kina udhaifu, lakini ichi kitu unachokiona cha kijinga toka kwa MUNGU, basi amini kwamba kina Hekima mara dufu kuliko hekima ya mwanadamu.

Mfano kumsamehe muuaji au mwizi au kutokulipiza Kisasi kama MUNGU anayotaka, Kwa mtu mwingine anaweza kutafsiri huo kama Ujinga, yani kumsamehe Mwizi, au jambazi au kutokulipiza kisasi mtu mwingine anaona ni upumbavu tu, kumbe hapo MUNGU alikuwa na hekima zaidi kutuamuru kusamehe.
 
Napitia comment hapa taaratibu niyaone maelezo kuhusu ujinga na udhaifu wa mungu. Doohh job true true.
 
si kila mstari kwenye bible unaweza kuuelewa wenyewe kama wenyewe anzia juu kidogo at least mstari wa 15 au 16 utapata kuelewa paulo alimaanisha nini

unless uwe na lingine ulilolikusudia
Tueleze tu ulivoelewa mkuu, sio mbaya kufundisha mambo ya Mungu wetu mkuu.
 
Excel, hapa tatizo lipo katika udhaifu wa kutafsiri, na pia kuelewa maana ya andiko. Mungu hana upumbavu wala ujinga, na ni hatari sana kumfikiria Mungu katika muktadha huo kwa sababu unaweza ukafanya kufuru au dhambi isiyosameheka kwa sababu ya utakatifu wake.

Maneno yaha ya Paulo katika andiko hili katika lugha sanifu ya Kiswahili yanapaswa kusomeka hivi, "Kwa sababu kitu kipumbavu cha Mungu ni chenye hekima kuliko wanadamu, na kitu dhaifu cha Mungu ni chenye nguvu kuliko wanadamu."

Sasa nini maana ya andiko hili? Ni wazi Mungu aliumba vitu vyenye complexity tofauti tofauti, na kama ni katika suala la design, basi utasema kuna uumbaji wa Mungu ni wa design iliyotumia akili ya juu sana. Kwa mfano, fikiria alivyoumba ubongo wa mwanadamu, ambao ni wa kipekee kuliko compyuta zenye nguvu sana. Lakini pia fikiria kiumbe rahisi sana alichoumba Mungu, kama earthworm. Katika macho ya kibinadamu, unaweza kuona kiumbe kama earthworm ni cha kipumbavu, au mwingine akaona Mungu kuumba vitu kama nzi halikuwa jambo la hekima.

Lakini sasa, ndio Paulo anawakumbusha watu, kwamba katika mtazamo wa kibinadamu, kile tunachoona kuwa cha " kipumbavu au kitu dhaifu" ni chenye hekima kuliko hao wanadamu ambao mara nyingine wanakosa kabisa hekima ya kuwa wameumbwa na Mungu. Hebu mlinganishe mtu anaemnajisi mtoto wa miaka mitatu, je, katika uumbaji wa Mungu, si utaona nzi ni kiumbe wa maana kuliko mtu kama huyo?

Na unaweza kuona kama kiumbe kama mbu anaeeneza malaria, ni namna ya udhaifu katika uumbaji wa Mungu, au kwa mfano funza (maggots) ambao utaona ni disgusting. Waliumbwa kwa sababu nzuri tu zinazomfaa binadamu, hawakufanywa wawepo ili kueneza magonjwa au kufanya uharibifu, kama vile tu simba hakuumbwa ili awinde wanyama na kuwala. Haya ni matokeo ya uasi wa shetani ibilisi. Kwa hiyo andiko hilo lipo katika context hiyo. Hivyo hata katika hali hizi, usiviangalie vitu katika context ya kuona ni kitu cha kipumbavu au udhaifu cha Mungu.

Lakini pia kuna suala ambalo linahusu amri za Mungu, ambazo wewe unawza kuona ni za kijinga au ni udhaifu kuzifuata. Akishasema usifanye hivi, hata kama unaona ni udhaifu, ni ujinga, watu hawatakuelewa, ujue kwamba yeye kama Mungu anaona mbali sana kuliko wewe kama mwanadamu. Fuata. Usichukue position ya kutaka kumshauri Mungu, au kuona kama alikosea, au hakufikiria mbali alipotoa agizo fulani. Kuna mtu anaona ni udhaifu kuomba msamaha pale ambapo unajua hujafanya kosa, lakini Mungu anasema wewe fanya hivyo hata kama unajua sio kosa lako, ili ulete amani na mtu mliekorofishana.

Vitu kama hivi muwe mnawatafuta mashahidi wa Yehova wawafafanulie. Nimejifunza mengi sana toka kwao, pamoja na hili. Huu sio ujuzi wangu, bali ni ufafanuzi wao.
Proud to be mkristo. Maelezo yaliyonyooka na yenye hekima itokayo juu barikiwa sana mtu wa mungu
 
Anhaa inshu yake ni maelezo mengi sana ee
ili apate mantik vizuri ila kwa kifupi

mtume paulo alikua anajaribu kuwaelezea wakorintho kuhusiana na wayahudi na wayunani jinsi walivyokuwa wanadharau habari za Yesu wao walikua wanaziona kama ni upuuzi ila akisoma hiyo sura yote ataelewa

mtume paulo anakwambia Mungu alichagua mambo mapumbavu ili awaiibishe wenye hekima
 
Excel, hapa tatizo lipo katika udhaifu wa kutafsiri, na pia kuelewa maana ya andiko. Mungu hana upumbavu wala ujinga, na ni hatari sana kumfikiria Mungu katika muktadha huo kwa sababu unaweza ukafanya kufuru au dhambi isiyosameheka kwa sababu ya utakatifu wake.

Maneno yaha ya Paulo katika andiko hili katika lugha sanifu ya Kiswahili yanapaswa kusomeka hivi, "Kwa sababu kitu kipumbavu cha Mungu ni chenye hekima kuliko wanadamu, na kitu dhaifu cha Mungu ni chenye nguvu kuliko wanadamu."

Sasa nini maana ya andiko hili? Ni wazi Mungu aliumba vitu vyenye complexity tofauti tofauti, na kama ni katika suala la design, basi utasema kuna uumbaji wa Mungu ni wa design iliyotumia akili ya juu sana. Kwa mfano, fikiria alivyoumba ubongo wa mwanadamu, ambao ni wa kipekee kuliko compyuta zenye nguvu sana. Lakini pia fikiria kiumbe rahisi sana alichoumba Mungu, kama earthworm. Katika macho ya kibinadamu, unaweza kuona kiumbe kama earthworm ni cha kipumbavu, au mwingine akaona Mungu kuumba vitu kama nzi halikuwa jambo la hekima.

Lakini sasa, ndio Paulo anawakumbusha watu, kwamba katika mtazamo wa kibinadamu, kile tunachoona kuwa cha " kipumbavu au kitu dhaifu" ni chenye hekima kuliko hao wanadamu ambao mara nyingine wanakosa kabisa hekima ya kuwa wameumbwa na Mungu. Hebu mlinganishe mtu anaemnajisi mtoto wa miaka mitatu, je, katika uumbaji wa Mungu, si utaona nzi ni kiumbe wa maana kuliko mtu kama huyo?

Na unaweza kuona kama kiumbe kama mbu anaeeneza malaria, ni namna ya udhaifu katika uumbaji wa Mungu, au kwa mfano funza (maggots) ambao utaona ni disgusting. Waliumbwa kwa sababu nzuri tu zinazomfaa binadamu, hawakufanywa wawepo ili kueneza magonjwa au kufanya uharibifu, kama vile tu simba hakuumbwa ili awinde wanyama na kuwala. Haya ni matokeo ya uasi wa shetani ibilisi. Kwa hiyo andiko hilo lipo katika context hiyo. Hivyo hata katika hali hizi, usiviangalie vitu katika context ya kuona ni kitu cha kipumbavu au udhaifu cha Mungu.

Lakini pia kuna suala ambalo linahusu amri za Mungu, ambazo wewe unawza kuona ni za kijinga au ni udhaifu kuzifuata. Akishasema usifanye hivi, hata kama unaona ni udhaifu, ni ujinga, watu hawatakuelewa, ujue kwamba yeye kama Mungu anaona mbali sana kuliko wewe kama mwanadamu. Fuata. Usichukue position ya kutaka kumshauri Mungu, au kuona kama alikosea, au hakufikiria mbali alipotoa agizo fulani. Kuna mtu anaona ni udhaifu kuomba msamaha pale ambapo unajua hujafanya kosa, lakini Mungu anasema wewe fanya hivyo hata kama unajua sio kosa lako, ili ulete amani na mtu mliekorofishana.

Vitu kama hivi muwe mnawatafuta mashahidi wa Yehova wawafafanulie. Nimejifunza mengi sana toka kwao, pamoja na hili. Huu sio ujuzi wangu, bali ni ufafanuzi wao.
Umeeleza vizuri ila hapo kwenye kumsingizia shetani umebugi...so Simba aliumbwa ale majani alikuwa ana matumbo manne ila baada ya mtu kula tunda akawa na meno makali na tumbo la kusaga nyama .. hamna sehemu yoyote duniani inayosema Simba alikuwa Hali nyama...acha uwongo na upotoshaji..na hao wadudu kuleta magonjwa ndo chakula Chao hicho so unabidi utuambie Mungu aliwaumba wale Nini kabla ya magonjwa unayomsingizia shetani
 
Mungu aliye mkamilifu, asiye fananishwa na kitu, Alfa na Omega; hapa anatamkwa namna hii?

Ama kuna namna ilimaanishwa na Mwandishi wa Wakorinto?
View attachment 2853435
Nakupa mfano wa tendo la Mungu unaloweza kuliona halifai lakini matokeo yake makubwa
"mate ya Mungu yanauponyaji"

Marko 7: 32-35

33 Akamtenga na mkutano faraghani, akatia vidole vyake masikioni mwake, akatema mate, akamgusa ulimi,
 
Back
Top Bottom