Wataalam wa mambo ya uzazi naombeni msaada wenu, nimechanganyikiwa

Wataalam wa mambo ya uzazi naombeni msaada wenu, nimechanganyikiwa

majibu ya ultra sound huwa ni 100% correct/accurate e?
Sio 100% me wakati naanza clinic nilikuwa namimba ya miezi 3 ultra sound ikaonesha miezi 6 yani tare za kujifungua waka kadiria badala nijifungue miezi 9 wakarudisha miezi 6😀 nilibishana na manes hadi nikawauliza me ndo nimebeba mimba najua mwezi nilio beba bado mnabishia.. wakaniambie niende hospital nyingine nikafanye ultra sound tena nikaenda.. wao kidogo japo haikuwa sawa walisema mwezi wa 2 najifungua nikajifungua wa kwanza katikati.. kwaiyo hivo vitu hapana labda umuangalie mwanao km yupo hai tuu.
 
Mimba haipimwi kama hesabu za kichwan kwako zinavofanya yaana wewe unawaza december
Mara ya mwisho kuona period zake ndio siku mimba inaanza kusoma
 
Nipe huyo mwanamke mkuu niko tayari kulea mimba..

nitakulipa fidia za usumbufu..
IMG_20250124_175054_775.jpg
 
Toka 28 desemba bado mkuu
Inamaa wewe ulimkojolea tarehe 28 tu, Tena siku yangu ya kuzaliwa
Ziko sawa wewe unatatizo zimefika wiki 8 na siku kadhaa ambapo ni wiki 9

Desemba ilikuwa na siku 3 za ziada vile vile January ilikuwa na siku 3 za ziada fanya wiki 5 tarehe 15-02-2025 zilifika wiki 8 Leo Kuna siku 4 we jamaa hauko sawa
 
Kwenye kujua umri wa mimba cha muhimu sana ni tarehe ya mwisho ya mama kuona siku zake. Njia hii ndiyo hutoa majibu ambayo ni sahihi hasa kwa umri wa mimba kama mama anaikumbuka vizuri.

Kama mama hakumbuki tarehe ya mwisho kuona siku zake basi njia mbadala ya kupima umri wa mimba ni hiyo ya kutumia ultrasound.

Kipimo cha ultrasound kwenye kupima umri wa mimba hakitoi majibu sahihi kwa 100%, mara nyingi hupishana na umri wa mimba kwa tarehe za mwisho kwa wiki 2 au zaidi kulingana na hatua ya mimba (trimester).

Kupishana huko ni kawaida wala sio tatizo kwa sababu kunakuwa na makosa madogomadogo (errors) ya mashine inayotumika na ya mpimaji (uzoefu nk).

Hongereni sana, muendelee na utaratibu wa mama kuanza clinic.

Kila la kheri.
Alianza tarehe 17 desemba hadi tarehe 21 desemba ndiyo siku zake
 
Bado nadhani akisema siku ya mwisho kumaliza hedhi utata utaisha,yy mwenyewe nahisi amejisikia vibaya akutarajia haya majibu
Ameniambia alianza tarehe 17 desemba hada tarehe 21 desemba ndiyo zilikuwa siku zake
 
Mimba inapinwa depending na siku ya kwanza ya hedhi ya mwisho ndo maana hospitali nyingi utakuta anatumia LMP kumaanisha last menstrual period… mimba ni miezi 9 lakini tunahesabiwa mpaka wiki 40 ili kueradicate zile wiki 2-4 za ovulation after periods (depending na mzunguko wa mtu)
Siku ya kwanza ya hedhi ilikuwa 17 desemba na alimaliza kati ya trh 20 hadi 21 desemba
 
Leo nimetoka kufanya kipimo cha ultrasound na mpenzi wangu, kipimo kikasema kuwa mpenzi wangu ana ujauzito wa wiki tisa na siku tatu, kinachotuchanganya ni mara ya mwisho kufanya nae mapenzi ilikuwa tarehe 28 desemba ambazo hadi leo wiki 9 hazifiki, je changamoto ni nini?
Duh!
 
Ameniambia alianza tarehe 17 desemba hada tarehe 21 desemba ndiyo zilikuwa siku zake
Ulimkojolea siku ya hatari sana siku salama ni kuanzia siku ambayo mwanamke anaenda Jupiter hadi siku ya 8, ya 9-10 mmm haina uhakika sana ila ya 11,12,13,14,15 hizo za moto, (fireworks) 🔥,

Ilitakiwa uchimbe mgodi kuanzia tarehe 22-26, ulifurahia live wire ili upate raha za dunia, (ze utamu), ila matokeo ya live wire huwa kinakatikia, unapata gono ama VVU

Ina maana wewe umechomeka mdudu siku ya 12 ambayo ni hatari lazima mwanamke apate mimba, hapo nimetumia elimu ya biology ya mwaka 1978 nikiwa form two, kikikiki
 
24.12 mlikutana, 28.12 mkawekana bila ndomu, na huenda hata hamkupimana. Ukimwi uko sehemu mbaya sana wakuu. Ndio maana wengine tumeamua sasa basi.

BTW, uliza huyo mdada LM ilikuwa lini, yaani lini aliingia hedhi yake ya mwisho. Ultrasound inasoma kuanzia tar ya kwanza ya hedhi yake ya mwisho.
 
24.12 mlikutana, 28.12 mkawekana bila ndomu, na huenda hata hamkupimana. Ukimwi uko sehemu mbaya sana wakuu. Ndio maana wengine tumeamua sasa basi.

BTW, uliza huyo mdada LM ilikuwa lini, yaani lini aliingia hedhi yake ya mwisho. Ultrasound inasoma kuanzia tar ya kwanza ya hedhi yake ya mwisho.
Tarehe 17 desemba
 
Leo nimetoka kufanya kipimo cha ultrasound na mpenzi wangu, kipimo kikasema kuwa mpenzi wangu ana ujauzito wa wiki tisa na siku tatu, kinachotuchanganya ni mara ya mwisho kufanya nae mapenzi ilikuwa tarehe 28 desemba ambazo hadi leo wiki 9 hazifiki, je changamoto ni nini?
Ultrasound inaestimate tu, mimba ni yako Mkuu
 
Back
Top Bottom