Watanganyika msihofu bandari zenu zitarudishwa mikononi mwenu na mahakama mkataba uloridhiwa na Bunge ni Void ab initio

Watanganyika msihofu bandari zenu zitarudishwa mikononi mwenu na mahakama mkataba uloridhiwa na Bunge ni Void ab initio

Binafsi nimekuwa nikijiuliza, kama mkataba wenyewe una mapungufu ya kisheria, unaweza vipi kusimama katika mahakama za kimataifa?

 
Dubai sio state na haina capacity ya kuingia mkataba wa aina yoyote.

Mahakama itatenda haki
Mafisadi wa CCM chini ya mwenyekiti wao wataaibika

Huyu Wasira na pumba zake za kumtusi Lissu ataona aibu
Mimi siukubali mkataba, mkataba una matatizo mengi.

Lakini, hii hoja ya "Dubai sio state" ni hoja mufilisi.

Dubai ni Emirate ya UAE. UAE ina mamlaka ya kuipa uwezo Dubai kuingia mkataba kama huu na nchi nyingine.

Ingekuwa UAE inalalamika kwamba Dubai imeingia mkataba huu kinyemela, hapo ungekuwa na point.

Lakini, UAE ina uwezo wa kuipa idhini Dubai iingie mkataba huu, na haijalalamika, zaidi, UAE inafanya kazi pamoja na Dubai kufanikisha biashara za DPW.

Hivi, unafikiri wanasheria wa DPW ni wajinga waingie mkataba huu bila kupata idhini ya UAE?

Na kama mkataba una idhini ya UAE, serikali za UAE na Tanzania zimeikubalia Dubai kuingia mkataba, uharamu wake unatoka wapi?
 
Binafsi nimekuwa nikijiuliza, kama mkataba wenyewe una mapungufu ya kisheria, unaweza vipi kusimama katika mahakama za kimataifa?

Mapungufu ya kisheria kama yapi mkuu?
 
Upande mmoja umesainiwa na state na upnde wa pili umesainiwa na Kampuni. Na IGA ni two state agreement
IGA si two state agreement, ni two governments agreement. Kuna tofauti.

Unaweza kusaini IGA hata kati ya serikali ya wilaya na serikali ya mkoa. Hizo si states.

Suala la muhimu si nani anasaini, suala la muhimu ni anasaini kwa niaba ya nani na kama ana idhini ya kusaini.

Upande uliosainiwa na kampuni ni upi? aliyesaini ni nani? je, ana full instruments of power ku saini?
 
Suala la muhimu si nani anasaini, suala la muhimu ni anasaini kwa niaba ya nani na kama ana idhini ya kusaini.

Upande uliosainiwa na kampuni ni upi? aliyesaini ni nani? je, ana full instruments of power ku saini?
Upande uliosainiwa na kampuni ni upande wa Dubai na aliyesaini ni mkurugenzi wa bandari na hana hiyo full instruments of power kusaini mkataba wa IGA
 
Mimi siukubali mkataba, mkataba una matatizo mengi.

Lakini, hii hoja ya "Dubai sio state" ni hoja mufilisi.

Dubai ni Emirate ya UAE. UAE ina mamlaka ya kuipa uwezo Dubai kuingia mkataba kama huu na nchi nyingine.

Ingekuwa UAE inalalamika kwamba Dubai imeingia mkataba huu kinyemela, hapo ungekuwa na point.

Lakini, UAE ina uwezo wa kuipa idhini Dubai iingie mkataba huu, na haijalalamika, zaidi, UAE inafanya kazi pamoja na Dubai kufanikisha biashara za DPW.

Hivi, unafikiri wanasheria wa DPW ni wajinga waingie mkataba huu bila kupata idhini ya UAE?

Na kama mkataba una idhini ya UAE, serikali za UAE na Tanzania zimeikubalia Dubai kuingia mkataba, uharamu wake unatoka wapi?
Emirate ni nini?
 
Upande uliosainiwa na kampuni ni upande wa Dubai na aliyesaini ni mkurugenzi wa bandari
Unaelewa kwamba mkurugenzi wa bandari wa Dubai ni mfanyakazi wa serikali na alikuwa na full instruments of power kutoka serikali ya Dubai kusaini mkataba?

Umesoma instruments of full powers za Dubai ukurasa wa mwisho?

Nauweka mkataba tena hapa kwa wale ambao hawana wausome na kuuchambua.
 

Attachments

Mimi siukubali mkataba, mkataba una matatizo mengi.

Lakini, hii hoja ya "Dubai sio state" ni hoja mufilisi.

Dubai ni Emirate ya UAE. UAE ina mamlaka ya kuipa uwezo Dubai kuingia mkataba kama huu na nchi nyingine.

Ingekuwa UAE inalalamika kwamba Dubai imeingia mkataba huu kinyemela, hapo ungekuwa na point.

Lakini, UAE ina uwezo wa kuipa idhini Dubai iingie mkataba huu, na haijalalamika, zaidi, UAE inafanya kazi pamoja na Dubai kufanikisha biashara za DPW.

Hivi, unafikiri wanasheria wa DPW ni wajinga waingie mkataba huu bila kupata idhini ya UAE?

Na kama mkataba una idhini ya UAE, serikali za UAE na Tanzania zimeikubalia Dubai kuingia mkataba, uharamu wake unatoka wapi?
Kama mkataba uwe halali Dubai inahitaji idhini ya UAE, si kuna umuhimu wa hiyo idhini iwe sehemu ya mkataba na isiwe tu assumption kuwa idhini ilitolewa?
 
Kama mkataba uwe halali unahitaji idhini ya UAE, si kuna umuhimu wa hiyo idhini iwe sehemu ya mkataba na isiwe tu assumption kuwa idhini ilitolewa?
Mkataba wenyewe tumeupata kwa kuvuja, hatujaupata kwa njia rasmi.

Unajuaje kwamba tumeupata wote?

Unajuaje hiyo idhini haijatolewa sema tu haijawa sehemu ya mkataba iliyovuja?

Ukiangalia mkataba niliouweka hapa utaona kuwa hata instruments of full powers za Dubai tu zimewekwa kama atachment ambayo haipo katika numbered pages za mkataba. Angalia attachment (IGA) nimeiweka post #17.

Pages zote za mkataba zina margin ya kijani, instruments of full powers ya Dubai haina margin ya kijani, ina maana imeletwa separately. Unajuaje kwamba idhini ya UAE haipo separate pia?

Sasa utajua vipi idhini ya UAE haipo, ila haijawa leaked tu, labda aliyeleak mkataba hakuwa nayo, au hakuwa na uda wa kuiscan alikuwa anaibia.

Kitu muhimu ni kwamba, lalamiko la kwamba Dubai hana nguvu ya kusaini mkataba ni lalamiko linalotakiwa kutolewa na UAE. UAE isipotoa lalamiko hili, Watanzania hamtakiwi kulilalalimikia.

Serikali yenu ishakubali kusaini mkataba na Dubai. Dubai ina serikali. Mkataba ni wa serikali ya Tanzania na serikali ya UAE.

Ni kama vile serikali ya Zanzibar isaini mkataba na serikali ya Oman, kama serikali ya Jamhuri ya Muungano haikatazi, au imeipa idhini serikali ya Zanzibar kuingia mkataba huu, watu wa Oman watakosea kuanza kuhoji kama serikali ya Zanzibar ina mamlaka ya kusaini mkataba na Oman, hilo ni jambo kati ya Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

Pia, si makubaliano yote yako wazi, IGA yenyewe ian kipengele cha kuweka makubaliano siri.
 
Back
Top Bottom