Watanzania 34.3% ni wachawi, hawaamini Mungu, Mtume wala Jah

Watanzania 34.3% ni wachawi, hawaamini Mungu, Mtume wala Jah

Unakielewa unachokiandika au umeandika na wewe uonekane umeandika?

Nakielewa vizuri sana, ndio maana mimi sio mfuasi wa dini! Hapa kipi hujakielewa ndugu? Au hujui waliomsulubisha Kristo ni watu wakubwa kwenye dini zao?
 
Dini ni mifumo ya kiutawala yenye kulenga kurahisisha matakwa ya mamlaka husika. Kitu cha msingi tunachopaswa kujua na kukiamini ni kwamba yupo Mungu atakayekuja kutuhukumu kwa matendo na si maneno yetu la muhimu kuzingatia ni Upendo kwa kila mtu.
Nawasilisha.
 
Nakielewa vizuri sana, ndio maana mimi sio mfuasi wa dini! Hapa kipi hujakielewa ndugu? Au hujui waliomsulubisha Kristo ni watu wakubwa kwenye dini zao?

Kulikuwa na maaskofu pale?
Kulikuwa na mashekhe pale?

Ni kwanini unadhani kumsulubisha Yesu kulikuwa ni kosa?
 
Dini za jadi (34.3%), Ukristo (33.5%), Uislamu (31.4%), wengineo (0.8%)

Takwimu hizi zinaweza kuwa hazina maana lakini zinatoa taswira ya imani za Watanzania.

Ulitumia sampuli ya Watanzania wangapi? Wa bara walikuwa wangapi na wa Tanzania visiwani (wanaoamini katika utanzania)? Ulichukua watu wa kada zipi? Na huu utafiti ulidhaminiwa na nani na nini maslahi yake!
 
Nashukuru na namshukuru Yesu Kristo kwa kusikia ni mzima mtumishi .....

Kule tunaendelea tu mkuu ........!!
Amina Mtumishi. Nipo salama kabisa na Yesu anaendelea kushinda kila siku.
 
Kulikuwa na maaskofu pale?
Kulikuwa na mashekhe pale?

Ni kwanini unadhani kumsulubisha Yesu kulikuwa ni kosa?

Asante. Twende taribu mkuu.

Tatizo letu hapa ni dogo sana, nalo ni titles nilizotumia- Mashehe na Maaskofu! Labda tujiulize, Shehe ni nani, na Askofu ni nani? Katika muktadha wa kawaida, hawa ni viongozi wa kidini bila kujali ni dini gani. Tukisogea mbele kidogo ndipo tunapata kujua kuwa Askofu ni Kiongozi wa dini ya Kikristo, na Shehe ni kiongozi wa dini ya Kiislamu.

Tukisogea mbele kidogo, utaona kuwa hata baadhi ya madhehebu ya Kikristo hawatumii hii title ya Askofu na badala yake wanatumia cheo-Mwenyekiti.

Kwa nini nimetumia vyeo hivyo kuwa wao walimsulubisha? Ni kwa kuwa ni wakuu wa Makuhani ambao ni Wakuu wa dini ya Kiyahudi wa madhehebu yote- Mafarisayo na Masadukayo ndio waliomwandalia Yesu mashitaka na kupendekeza adhabu ya kifo kwa kusulubiwa kwa Pilato....

Sio ajabu kuwa hata leo Wakuu wa dini na Maaskofu wakuu wanafanya yaleyale! Wanaketi kwenye mabaraza yao na kwa uwazi, bila aibu, wanajadili namna ya kuhalalisha dhambi kama vile kuhalalisha ndoa za jinsia moja kutambuliwa na kubarikiwa Madhabahuni. Waonaje, kufanya hivyo si kumsulubisha Yesu mara ya pili?

Kuhusu kumsulubisha Yesu kuwa ni kosa au la? Naamini kuwa ilikuwa vyote-Kosa na sio kosa! Ilikuwa ni kosa kwa viongozi wa dini kumsulubisha Yesu-rejea ole ya Yesu kwa Yuda , lakini ilikuwa sio kosa Yesu kusulubiwa maana kwa njia hiyo tulipata ukombozi.

Tujifunze kuwa wafuasi na wanafunzi wa Yesu badala ya kuwa wanafunzi na wafuasi wa dini zetu


Vv
 
Amina Mtumishi. Nipo salama kabisa na Yesu anaendelea kushinda kila siku.

Tah ha ha h aha ha!
Gongo za asubuhi mbaya sana!

Huyo yesu anashindana kwenye Olympic au?
Mbona kwenye Orodha ya Washindanaji hayumo! Au mashindano ya Kwaya! Na Kunanihii!
Hebu funguka kidogo mtumishi mjakazi!
 
Kulikuwa na maaskofu pale?
Kulikuwa na mashekhe pale?

Ni kwanini unadhani kumsulubisha Yesu kulikuwa ni kosa?

Kama KUUA MTU kwa KUMPIGILIA MSALABANI SIO KOSA.
basi hata ubakaji wa watoto makanisani SIO KOSA.
Kwa mtazamao km huu Ndio maana hata hawa wahalifu hawafikishwi kwenye vyombo vya Sheria.
 
Salama Mtumishi, vipi kule kwenye jukwaa takatifu, kunaendeleaje?

Nashukuru na namshukuru Yesu Kristo kwa kusikia ni mzima mtumishi .....

Kule tunaendelea tu mkuu ........!!

Jukwaa takatifu ndio lipi?

Halafu acheni kuleta maigizo hapa.
Kwani huyo dada Ishmael anashindwa kwenda mwenyewe huko mpaka Akuulize wewe Eiyer?

Bangi sio nzuri ukiwa huna kazi!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom