Watanzania kushangilia kuangushwa kwa Makonda katika kura za maoni Jimbo la Kigamboni kunaashiria nini?

Watanzania kushangilia kuangushwa kwa Makonda katika kura za maoni Jimbo la Kigamboni kunaashiria nini?

Kura za maoni zisikupumbaze mimi naamini Makonda ndio mkuu wa mkoa bora kabisa kuwahi kutokea, ni kiongozi mwenye uthubutu na mwenye maono na anayependa kujaribu. Naamini kama Makonda akifanikiwa kuingia kwenye baraza la mawaziri na akapewa wizara ya kilimo ambayo imeajiri watu wengi basi kutakuwa na mapinduzi makubwa sana ya kilimo wakulima watanufaika sana

Nilichokigundua mimi ni kwamba kuna nguvu kubwa sana ya media hasa mitandao ya kijamii inatumika kuaminisha uma kuwa Makonda ni kiongozi mbaya, na hii ni kutokana na ujasiri wale uliochangia kuokoa vijana wengi wa Tanzania waliokuwa wakiteketea, sasa wanufaika wote wakahakikisha wanaelekeza nguvu zao kuhakikisha wanamchafua. Kiongozi mzuri hawezi pimwa kwa wingi wa kura pekee yawezekena wake wajumbe waliopiga kura za maoni wakawa sio wafuasi wake, lakini ikumbukwe wananchi hawapigi kura kwa kuangalia ufuasi, wao huangalia ni kipi kiongozi alichowafanyia au atachowafanyia, na kama hivi ndivyo ilivyo naamini Makonda anaweza shinda jimbo lolote lile ndani ya Tanzania kutokana na kazi kubwa aliyoifanya ya kuokoa kizazi chetu hasa vijana . Ni binadamu wachache sana wenye uthubutu hapa duniani na hawa huwa ni tunu.
Ndiyo mlikuwa mnashirikiana nae kuteka watanzania ?
 
Media influence, unaweza mfananisha Makonda na mkuu wa mkoa yupi Tanzania, binadamu amejazwa chuki bila kuchambua mwenyewe kichwani mwake.

Nina imani na Makonda, hata kama hapo amekosa, ila kuna sehemu atapata bureee kabisa bila kupingwa.

Sometimes watanzania tumezoea kuongozwa na wapiga dili na wasanii sanii tu, watanzania wamefika sehemu hawataki kiongoz anayeleta maaendeleo, hawataki mabadiliko.

Magufuli ameingia, watu wanamtukana, wanabeza, hv tangu mtu umezaliwa kuna rais amewah kuwa namna hii kama ya Magufuli? Sasa watanzania mnataka nini? The same to Makonda, mtaona mengi sana na mtateseka sana mioyo yenu isiyotaka positive changes.. change ur mind
 
Wewe mtoa mada nafikiri kichwani hauko vizuri. Kwani makonda amekatwa? Mkutano mkuu wa jimbo au wilaya unapitisha majina matatu ambayo yanajadiliwa na kamati ya siasa ya wilaya, mkoa na Nec wanapitisha jina moja. Unafurahi kwani mchakato umeisha? Kufikiri kwa kutumia makamasi ni tatizo kubwa sana. Kwa nini usisubiri mchakato uishe? Sababu kuw namba moja sio kupita.
Sawa, apakatwe tu kama alivyozoea kupakatwa labda toka utotoni lakini kura za raia huru wenye akili huyo shetani hapati ng'o! Mtu mzima unapakatwa kama kitoto kichanga, hiyo ni aibu kubwa. Halafu alivyo mhuni, anaweza akawanyea waliompakata halafu kazi ya kuzoa uharo wanaachiwa akina chagu wa malunde🤣
 
Wewe mtoa mada nafikiri kichwani hauko vizuri. Kwani makonda amekatwa? Mkutano mkuu wa jimbo au wilaya unapitisha majina matatu ambayo yanajadiliwa na kamati ya siasa ya wilaya, mkoa na Nec wanapitisha jina moja. Unafurahi kwani mchakato umeisha? Kufikiri kwa kutumia makamasi ni tatizo kubwa sana. Kwa nini usisubiri mchakato uishe? Sababu kuw namba moja sio kupita.
Umemjibu mtoa mada kijinga na kishabiki tuu. Point yake haikuelemea kushindwa kwake bali mapokeo ya matokeo sio kwa Kigamboni tuu bali kwa nchi nzima.
Nadhani Rais Magufuli hana fikra kama zako zilizo lala hivyo anaona reaction ya Watanzania kuhusu mapokeo yao kwa kupigwa chini maoni ya awali kwa "RC bora nchini" kama alivyokuwa anamnadi.
Pengine anajiuliza jee Makonda alikuwa amenishika kwa nguvu za Giza hadi sioni asivyokubalika?
Maana sasa sio siri kama unatumia akili kujua kuwa mama Samia hamkubali, Majaliwa na Bashiru hawamuungi mkono na hata mawaziri na viongozi wenza mkoani walikuwa hawaendi sambamba naye.
Kuna somo ambalo hata yeye Rais atakuwa amejifunza, watanzania waweza kuwa wamekuchoka lakini wanakushangilia jukwaani ila ukibwagwa na kama ulikuwa na kiburi watakuzodoa hadi waweza kukonda kwa siku mbili tuu.
 
Makonda utendaji na tabia ake ni nakala halisi ya Magufuli.

Kama watu walitunza moyoni hasira dhidi ya Makonda, ina maana hata Magufuli wana fundo nae, ni suala la wakati tu
 
Sawa, apakatwe tu kama alivyozoea kupakatwa labda toka utotoni lakini kura za raia huru wenye akili huyo shetani hapati ng'o! Mtu mzima unapakatwa kama kitoto kichanga, hiyo ni aibu kubwa. Halafu alivyo mhuni, anaweza akawanyea waliompakata halafu kazi ya kuzoa uharo wanaachiwa akina chagu wa malunde🤣
Mchakato wa uchaguzi ndani ya Ccm mbona mmeutolea macho sana? Waacheni Ccm wapitishe watu wao alafu msubiri kichapo Oktoba.
 
Sawa, apakatwe tu kama alivyozoea kupakatwa labda toka utotoni lakini kura za raia huru wenye akili huyo shetani hapati ng'o! Mtu mzima unapakatwa kama kitoto kichanga, hiyo ni aibu kubwa. Halafu alivyo mhuni, anaweza akawanyea waliompakata halafu kazi ya kuzoa uharo wanaachiwa akina chagu wa malunde🤣
Hahaaaaaa.......... 😁 😀
 
Wewe ndio umechemka unajadili na kuongea kama mass

Wakati unajua kabisa hata mshindi wa tatu anaweza kusimamishwa


Wanasiasa wanapenda watu kama wewe,


Ndugulile ashaondoka kuwa chagua la mkuu, kumbuka hilo

"Ndugulile ashaondoka kuwa chaguo LA mkuu" kwa hiyo unatuaminisha kuwa maoni ya wanaccm hayana maana kama wewe sio "chaguo la mkuu"? Sasa hicho ni chama cha siasa au Mali ya Bwana na Bibi Magufuli! (Family party)?
 
Kuth
Kura za maoni zisikupumbaze mimi naamini Makonda ndio mkuu wa mkoa bora kabisa kuwahi kutokea, ni kiongozi mwenye uthubutu na mwenye maono na anayependa kujaribu. Naamini kama Makonda akifanikiwa kuingia kwenye baraza la mawaziri na akapewa wizara ya kilimo ambayo imeajiri watu wengi basi kutakuwa na mapinduzi makubwa sana ya kilimo wakulima watanufaika sana

Nilichokigundua mimi ni kwamba kuna nguvu kubwa sana ya media hasa mitandao ya kijamii inatumika kuaminisha uma kuwa Makonda ni kiongozi mbaya, na hii ni kutokana na ujasiri wale uliochangia kuokoa vijana wengi wa Tanzania waliokuwa wakiteketea, sasa wanufaika wote wakahakikisha wanaelekeza nguvu zao kuhakikisha wanamchafua. Kiongozi mzuri hawezi pimwa kwa wingi wa kura pekee yawezekena wake wajumbe waliopiga kura za maoni wakawa sio wafuasi wake, lakini ikumbukwe wananchi hawapigi kura kwa kuangalia ufuasi, wao huangalia ni kipi kiongozi alichowafanyia au atachowafanyia, na kama hivi ndivyo ilivyo naamini Makonda anaweza shinda jimbo lolote lile ndani ya Tanzania kutokana na kazi kubwa aliyoifanya ya kuokoa kizazi chetu hasa vijana . Ni binadamu wachache sana wenye uthubutu hapa duniani na hawa huwa ni tunu.
Unadhani Kuthubutu nayo ni sifa inayojibeba?

Muongelee Pompeo kwa sentesi tatu zinazomuhusu makonda!

Alithubutu pia kuiba simu!

Alithubutu pia kumchapa makofi MZEE Warioba.

Alithubutu pia kutoa 10m kwa kuchezewa vizuri na kolikipa mmoja.
 
Yaaan furaha haielezeki niliyonayo, tangu nmezaliwa sijawahi hata kunywa soda maan nna allergy na vinywaji vya viwandani,
Lakini leo nimedufua heinken nzima. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23],
jamani sijui wajumbe wa CCM kigamboni niwape zawadi gani wallah
Alikukosea nini Msukuma wa watu yule??.
 
WEWE itakuwa ndio Bashite mwenyewe...ulichopatia kuhusu makonda ni kuwa anapenda kujaribu na kila muda huwa anajaribu
Kura za maoni zisikupumbaze mimi naamini Makonda ndio mkuu wa mkoa bora kabisa kuwahi kutokea, ni kiongozi mwenye uthubutu na mwenye maono na anayependa kujaribu. Naamini kama Makonda akifanikiwa kuingia kwenye baraza la mawaziri na akapewa wizara ya kilimo ambayo imeajiri watu wengi basi kutakuwa na mapinduzi makubwa sana ya kilimo wakulima watanufaika sana

Nilichokigundua mimi ni kwamba kuna nguvu kubwa sana ya media hasa mitandao ya kijamii inatumika kuaminisha uma kuwa Makonda ni kiongozi mbaya, na hii ni kutokana na ujasiri wale uliochangia kuokoa vijana wengi wa Tanzania waliokuwa wakiteketea, sasa wanufaika wote wakahakikisha wanaelekeza nguvu zao kuhakikisha wanamchafua. Kiongozi mzuri hawezi pimwa kwa wingi wa kura pekee yawezekena wake wajumbe waliopiga kura za maoni wakawa sio wafuasi wake, lakini ikumbukwe wananchi hawapigi kura kwa kuangalia ufuasi, wao huangalia ni kipi kiongozi alichowafanyia au atachowafanyia, na kama hivi ndivyo ilivyo naamini Makonda anaweza shinda jimbo lolote lile ndani ya Tanzania kutokana na kazi kubwa aliyoifanya ya kuokoa kizazi chetu hasa vijana . Ni binadamu wachache sana wenye uthubutu hapa duniani na hawa huwa ni tunu.
 
Hana utendaji wowote na hizi ziwe ni salaam kwa mteuzi wake kuwa wana dsm tuliishi maisha magumu kwa kulazimishwa kuongozwa na mtu tusiyo mtaka.
Kuangushwa katika kura za maoni za CCM, katika jimbo la Kigamboni, kwa Paul Makonda na Faustine Ndugulile, kumepokelewa kwa shangwe kubwa sana na watanzania wa nchi nzima

Hivi hali hiyo inaweza ikawa inaashiria nini?

Hivi inawezekanaje kwa mkuu wa mkoa, ambaye mara kwa Mara amekuwa akisifiwa hadharani na Rais Magufuli aliyemteua na kumtaja kuwa ndiye mkuu wa mkoa bora kabisa hapa nchini na wakuu wa mikoa wengine, wanapaswa waige mfano wa uchapaji kazi wa huyo Paul Makonda, wanaccm wa Kigamboni waamue kumnyima kura?

Licha ya malalamiko mengi sana ya wananchi kuwa Mkuu huyo wa mkoa hafai na kumwomba Rais Magufuli atengue uteuzi wake................

Hata hivyo Rais Magufuli amekuwa akiweka pamba masikioni na kutotaka kabisa kusikiliza maoni hayo ya wananchi, hadi wakati fulani aliwahi sikika Rais Magufuli akimwambia Mkuu huyo wa mkoa aendelee kuchapa kazi na asisikilize hizo shutuma zinazotolewa na wananchi walio wengi na akaendelea kumsifia kuwa yeye Makonda ndiye RC bora kabisa hapa nchini, ambapo maRC wengine wanapaswa wamuige yeye Makonda kwa.uchapaji kazi wake!

Je ni kiburi hicho alichopewa na Mheshimiwa Rais, ndicho kilichompa kichwa hadi kuwadharau watanzania wote hadi wakuu wake wa kazi?

Bila shaka wananchi bado hawajasahau lile sakata la namna mkuu huyo wa mkoa, Paul Makonda, alivyoweza kutunushiana "msuli" na waziri wa Fedha, Mheshimiwa Philipo Mpango, kuhusu yale makontena yake ya "fanicha" aliyotaka kuyaingiiza nchini bila ya kuyalipia ushuru, hadi pale Mheshimiwa Rais alipoingilia kati na "kumwamuru" mkuu hiyo wa mkoa ayalipie ushuru stahiki makontena hayo

Kutokana na kiburi chake kilichopitiliza wananchi walifikia hatua ya kumbatiza cheo kisichokuwepo cha "Naibu Rais" wa Tanzania!

Hata hivyo wananchi wote wa nchi nzima, hatuna budi kuwapa pongezi wajumbe wa mkutano wa kutoa mapendekezo kwa Jimbo la Kigamboni kwa kufanya kazi iliyotukuka ya "kulikata" jina la Paul Makonda!

Ni matumaini ya wananchi wote kuwa kwenye vikao vilivyosalia vya juu zaidi vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, vitatia "tiki" uamuzi wa wanakigamboni na kutolirejesha jina la Paul Makonda kuwa ndiye mpeperusha bendera za ubunge kwa tiketi ya CCM na kuunga mkono mapendekezo yaliyotolewa na wanaccm wa Kigamboni kuwa Faustine Ndugulile ndiye apeperushe bendera ya CCM kugombea ubunge huo baadaye mwaka huu kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika hapa nchini

Mungu ibariki Tanzania
 
Lakini makonda aliendaje kugombe bila kushauriana na boss wake
Ona
IMG_20200719_084852.jpeg
 
Wape salaaaaam
Ni ujumbe kuwa Makonda na Magufuli aliyemkumbatia muda mwingi tumewachoka.
Ndio maana Magufuli alihakikisha anasimama mwenyewe kwenye kura za maoni.
Angeacha kampenyo tu asingetoboa
 
Kuangushwa katika kura za maoni za CCM, katika jimbo la Kigamboni, kwa Paul Makonda na Faustine Ndugulile, kumepokelewa kwa shangwe kubwa sana na watanzania wa nchi nzima

Hivi hali hiyo inaweza ikawa inaashiria nini?

Hivi inawezekanaje kwa mkuu wa mkoa, ambaye mara kwa Mara amekuwa akisifiwa hadharani na Rais Magufuli aliyemteua na kumtaja kuwa ndiye mkuu wa mkoa bora kabisa hapa nchini na wakuu wa mikoa wengine, wanapaswa waige mfano wa uchapaji kazi wa huyo Paul Makonda, wanaccm wa Kigamboni waamue kumnyima kura?

Licha ya malalamiko mengi sana ya wananchi kuwa Mkuu huyo wa mkoa hafai na kumwomba Rais Magufuli atengue uteuzi wake................

Hata hivyo Rais Magufuli amekuwa akiweka pamba masikioni na kutotaka kabisa kusikiliza maoni hayo ya wananchi, hadi wakati fulani aliwahi sikika Rais Magufuli akimwambia Mkuu huyo wa mkoa aendelee kuchapa kazi na asisikilize hizo shutuma zinazotolewa na wananchi walio wengi na akaendelea kumsifia kuwa yeye Makonda ndiye RC bora kabisa hapa nchini, ambapo maRC wengine wanapaswa wamuige yeye Makonda kwa.uchapaji kazi wake!

Je ni kiburi hicho alichopewa na Mheshimiwa Rais, ndicho kilichompa kichwa hadi kuwadharau watanzania wote hadi wakuu wake wa kazi?

Bila shaka wananchi bado hawajasahau lile sakata la namna mkuu huyo wa mkoa, Paul Makonda, alivyoweza kutunushiana "msuli" na waziri wa Fedha, Mheshimiwa Philipo Mpango, kuhusu yale makontena yake ya "fanicha" aliyotaka kuyaingiiza nchini bila ya kuyalipia ushuru, hadi pale Mheshimiwa Rais alipoingilia kati na "kumwamuru" mkuu hiyo wa mkoa ayalipie ushuru stahiki makontena hayo

Kutokana na kiburi chake kilichopitiliza wananchi walifikia hatua ya kumbatiza cheo kisichokuwepo cha "Naibu Rais" wa Tanzania!

Hata hivyo wananchi wote wa nchi nzima, hatuna budi kuwapa pongezi wajumbe wa mkutano wa kutoa mapendekezo kwa Jimbo la Kigamboni kwa kufanya kazi iliyotukuka ya "kulikata" jina la Paul Makonda!

Ni matumaini ya wananchi wote kuwa kwenye vikao vilivyosalia vya juu zaidi vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, vitatia "tiki" uamuzi wa wanakigamboni na kutolirejesha jina la Paul Makonda kuwa ndiye mpeperusha bendera za ubunge kwa tiketi ya CCM na kuunga mkono mapendekezo yaliyotolewa na wanaccm wa Kigamboni kuwa Faustine Ndugulile ndiye apeperushe bendera ya CCM kugombea ubunge huo baadaye mwaka huu kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika hapa nchini

Mungu ibariki Tanzania
Hii yote ni rushwa! Unataka kuinfluence vikao vya juu! Makonda mpaka sasa ni number 2 na wanahitajika watatu! Kwenye duru linalofuata hao watatu wanaanza moja wote na Makonda anaweza akatoboa au akashindwa kabisa. Ndungulile anaweza akatoboa au akashindwa - hiyo ndiyo demokrasi. Msifurahi mwanzoni!
 
Wala sio kampeni meneja wala sipendelei mtu. Ila nazungumzia utaratibu wa kupata jina moja bado unaendelea. Na haijulikaani nani atapitishwa huko mbele mbona nyie mnaanza kufurahia upuuzi na Makonda ameingia kwenye mchujo wa majina matatu.
Tumia akili wewe ebo! Mbona unachosha watu kukuelimisha?
Mleta mada haongelei kushindwa kuchaguliwa maana bado, lakini maoni ya wana Kigamboni (jimbo ndani ya mkoa aliokuwa kiongozi wake) kumkataa na jinsi jamii ilivyopokea habari hiyo!
Mbona wenye mamlaka wanaweza kumpa cheo chochote wakipenda?
Mfano Magufuli akibahatika kutangazwa kashinda nani anaweza kumzuia kumteua kuwa mbunge na kuanzisha cheo nje ya katiba NAIBU WAZIRI MKUU na akampa? Hakuna.
Lakini hiyo inaondoa funzo alilolipata Magufuli na Makonda kuhusu imani ya wananchi kwa wenye viburi?
Haiondoi na inabaki palepale. Ndio kiini cha mada yake.
 
Sema tu kuwa makonda hakubaliki mkoa mzima wa dsm
Siyo "ku-influence" bali nimetoa rai kwa vikao vya juu viheshimu maamuzi yaliyofanywa na kikao cha mapendekezo cha wanaccm wa jimbo la Kigamboni
 
Back
Top Bottom