Watanzania tuelezwe ni wapi alipo Rais wetu Mpendwa John Magufuli, ni haki yetu kujua

Watanzania tuelezwe ni wapi alipo Rais wetu Mpendwa John Magufuli, ni haki yetu kujua

Status
Not open for further replies.
QUOTE="Papaa_Mobimba, post: 33197991, member: 541097"]
USHAURI WA BURE KWA MHE. RAIS MAGUFULI.

Wakati Unaendelea kupata Ahueni kutokana na Yasemwayo Mitandaoni naomba Nikutie moyo kuwa bado ww ni Mkuu wa Nchi .

Tafadhali Muite Mhe.Lissu Mpe Uhakika wa Usalama wake muombe Msamaha kwa Yaliyotokea September 07 2017 natumaini atasamehe na Kusahau kama wewe ulivyowasamehe akina Nape na January, waite pia Wapinzani wako wa Kisiasa kaa Nao Meza Moja Maliza nao Tofauti hata ikibidi nyuma ya Camera.

Ukifanya Hivyo Nchi yetu itakuwa imeanza Upya Kidemokrasia Zaidi Huku Amani Upendo vikitataradi.

NAKEYIIIIII
[/QUOTE]
Ni kwamba Kuna watu kawakosea ndo maana Kuna habari nyingi humu jf? Fafanua papa mobimba tupate abc
 
Yeye mwenyewe alofurahia Madhira yaliyompata Lissu
mara nyingi nakuaga pande wa upinzani. Lakini hata kama humpedi Magufuli kiasi gani huwezi ukachekelea kuumwa kwake hadharani. Hata kama moyoni kwako unataka iwe hivyo, sio kitu smart kuonyesha hisia hizo kwa umma, ni kosa moja kubwa sana kisiasa.
Ndio maana hata Tundu Lissu alipopigwa risasi Magufuli alitweet kumpa pole, japo naamini serikali yake inahusika, lakini alifanya kinachotakiwa kufanywa na mwanasiasa. Hutakiwi kushangilia ugonjwa wala kifo cha mpinzani wako hadharani.

Walichonishangaza zaidi hawa Wapinzani walikuwa wakichekelea wakati hata mtu mwenyewe haijulikani kama ana afya kweli ama mgonjwa, sasa ukishangilia halafu mtu akajitokeza mzima kabisa utajificha wapi?

Najua ni viongozi wachache wa Upinzani wamefanya hivi, lakini wapinzani wanapaswa kufundishana namna ya ku behave mbele ya public, samaki mmoja akioza watatangaza mmeoza wote, wanaangaliwa na watu wengi, na kila wanachoandika watu wanaki judge.

Hapa wanawafanya CCM kama akina Musiba hivi kuaminika zaidi kuwa Wapinzani wapo kwa ajili ya kumduru magufuli na wanashirikiana na mabeberu kufanya hivyo, yaani wanajipiga risasi ya mguuni kama sio kichwani kabisa.

Wamenisikitisha sana
 
Nilipata Ghadhabu sana, nikiwa kama mdau wa Demokrasia na haki za binadamu kuona kuna kiongoz anathubutu kuwaita Watanzania wenzake "wadudu " tena mbele ya kadamnasi na mbele ya media

Niliona hii ni dalili nyingine ya vijana walio aminiwa na Mh Rais JPM, lakin wanajimwambafy na kujivika mamlaka wasio kuwa nayo

Ila leo nimeamini jamaa hakukosea sana, nafuta kauli zangu za kejeli nilizotoa kwake siku ile,

Na inawezekana neno wadudu lilikuwa ni understatement

Nimeelewa kuwa

1)Ni Wadudu tu, wanaoweza kushinda mitandaoni wakifurahia jambo na wakifurahia au kusubiri kwa hamu ujio wa taarifa mbaya za mwanadamu mwenzao, tena kiongoz wao. Na tena wadudu hao sio jamii ya Nyuki, Siafu au jamii nyingine ya wadudu wenye akili, siafu, Nyuki na baadhi ya wadudu wana upendo, Ushirika, uzalendo kwa makundi na vichuguu vyao kuliko wapinzani wa Tz, wanaheshimu viongozi wao balaa, nawaza labda wadudu jamii ya nzi,mende na wengineo ambao hawana ustaarabu wa kuishi kijamii ndo watakuwa na sifa za wapinzani tulio nao Tz.

2) Ni wadudu tu ndo ambao kila kitu hupiga kelele ,liwe jema au baya, Mchukulie nzi, kutwa kucha yeye ni nzeee, nzeee, nzeee, anapiga kelele, anacholilia hukion, hujui kuwa anafurahia au anahuzunika, na mbaya zaid ni kuwa anapiga kelele bila kufanya hatua yoyote, Nzi hang'ati,
Ni aheri kama nyuki, akitulia anatengeneza asali, ukimzingua anapiga yowe kidogo, huelewi anang'ata. Sasa kuwalinganisha wapinzani wa Tz na wadudu aina ya Nyuki sio sawa, hawa hawang'ati ,na wala hawatengenezi asali ,kazi kupiga domo tu, yee yee yee ,hawa ni wadudu jamii ya nzi na mende

3)Ni wadudu tu ambao watakuwa na usahaulifu kama walio nao wapinzani wa Tz

Juzi juzi tu mtu wanae muona leo ni hero kwa kuwaletea habar za uzushi, alikuwa ameweka kambi la mashambulizi kwa mwenyekiti wao,

Mwenyekiti wao hajajibu hata hoja moja, na wala halijawa tatizo, leo hii mtu huyo kazusha ya kuzusha, Msigwa ameendelea na majukumu yake ya kutangaza teuzi, wanabak wanalalama, mbona tuhuma hazijawekwa sawa? Wadudu mbona mnakuwa wasahaulifu? Tuhuma za mwenyekiti mliweka lini sawa? Na imagine tuhuma za mwenyekiti zilikuw zinahusu majukumu yake ya kazi, tuhuma hiz za leo ni binafsi (afya ni mambo binafsi) .

Au ndo muendelezo wa yale yale ya double standards, chama mnataka kitawaliwe kidikteta, miaka nenda rud,mwenyekiti ni huyo huyo, et hakuna mwingine mwenye vigezo, ila mkiambiwa na sisi kama nchi hatuoni mwenye vigezo vya kumpokea JPM tunataka aendelee, mnaanza kung'aka kuwa haiwezekani ktk watanzani m50 akosekane mwenye vigezo, wadudu mbona mnashindwa kutumia logic ndogo tu?

Hivyo kwa heshima na taadhima, naomba nimtake radhi yule mheshimiwa alie waita wapinzani wa Tz kuwa ni wadudu, sababu siku ile nilimlaani vikali kwa kutumia maneno yasiyo na staha kwa watanzania wenzake

Ila kwa yanayoendelea leo, yamenifanya nitafakari, na kugundua kuwa jamaa alikuwa anajua kitu cha ziada ambacho mimi sikuwa na najua kwa wakati ule

Hivyo namtaka na kumtia moyo, ajitokeze aongezee na kutolea ufafanuzi kwa msisitizo kuwa wapinzani wa Tanzania ni wadudu wa jamii ya nzi Na mende, sio wadudu wa jamii zinazojielewa kama Siafu wanaopiga kazi balaa(hapa kazi tu), nyuki wanaotengeneza asali (wanaunga mkono serikali ya viwanda) Vipepeo wanaoruka na kusaidia ktk pollination (kama Bombadier zetu tu)Na wadudu wengine wa aina hii.

Viva JPM, Viva Tanzania.
*Anaandika Sam Ruhuza*

Hali Hii inatisha!

Unapoona watoto wanatamani kusikia Baba yao amevuta, basi ujue aliyewafikisha hapo ni Baba yao mwenyewe!
Malezi bora unayompa mtoto ya Upendo na kumthamini ndio yanamjenga mtoto kukupenda na kukuheshimu kama Baba na atakulinda na kukutea kwa kila hali, Ukiona kila saa unamkumbusha mtoto kuwa mimi ndio Baba yako, ujue kuna shida kubwa Sana kwenye Malezi.
Baba anatakiwa alee familia yake kwa Mapenzi yote ili watoto watamani kuishi na Baba yao. Inatisha sana pale unaposikia watoto wakifurahia kumuhesibia time Baba yao bila hata kujua ni kweli au sio lakini wanaonekana kutamani kuwa kweli!

Ninaomba sana Baba mwenye malezi ya chuki, hasira, kutukana hovyo, kuchapachapa, kumfunga ndani, kumzuia kuongea,... matendo yote ya hovyo unyanyasaji kwa wanao, basi tegemea hata ukiumwa mafua, watatamani uzime jumla!
Watoto wanahitaji upendo, kumjali na kumheshimu, usimnyanyase hata kidogo!

Kama unaumwa, sawazisha na wanao na ikiwezekana waambie na wengine wakuombee upone!
Ninawatakia malezi mema kwa watoto wenu.
 
Kadri tetesi zinavyozidi kuenezwa na radio mbao ni wazi kuwa huko tuendako ulinzi wa anayeitwa Rais wa nchi utaimairishwa ajabu.

Ndiyo, juhudi kubwa zitaongezwa kuimarisha ulinzi wa huyo Rais - karibu yake, around him, katikati ya kadamnasi. Juu na angani, Wanaoonekana na wasioonekana, Wanaojulikana na Wasiojulikana.
Like we never experienced before...

Na hatua hiyo itathibitisha kuwa tetesi zile za radio mbao zilikuwa zaidi ya tetesi..!

#FuturePost
 
QUOTE="Papaa_Mobimba, post: 33197991, member: 541097"]
USHAURI WA BURE KWA MHE. RAIS MAGUFULI.

Wakati Unaendelea kupata Ahueni kutokana na Yasemwayo Mitandaoni naomba Nikutie moyo kuwa bado ww ni Mkuu wa Nchi .

Tafadhali Muite Mhe.Lissu Mpe Uhakika wa Usalama wake muombe Msamaha kwa Yaliyotokea September 07 2017 natumaini atasamehe na Kusahau kama wewe ulivyowasamehe akina Nape na January, waite pia Wapinzani wako wa Kisiasa kaa Nao Meza Moja Maliza nao Tofauti hata ikibidi nyuma ya Camera.

Ukifanya Hivyo Nchi yetu itakuwa imeanza Upya Kidemokrasia Zaidi Huku Amani Upendo vikitataradi.

NAKEYIIIIII
Ni kwamba Kuna watu kawakosea ndo maana Kuna habari nyingi humu jf? Fafanua papa mobimba tupate abc[/QUOTE]Ndg. Kinusikwetu watu wengi wanamuombea Mabaya Mhe.Rais sio kwa Kupenda Bali ni Kutokana na Vitendo kadhaa vya Uhalifu dhidi ya Binaadamu vilivyowahi Kutokea huko Nyuma yeye akiwa Rais,kwa Mfano Tukio la Mhe.Lissu Kupigwa Risasi trh 07 sept 2017. Na Madhila Mbali mbali yanayowakuta Wapinzani nchi hii.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom