Watanzania tujifunze kukubali kuna vitu hatuwezi, tunaposhindwa tukubali kusaidiwa au tukomae? Baada ya Bandari ni ATCL na SGR au Tusubirie?

Watanzania tujifunze kukubali kuna vitu hatuwezi, tunaposhindwa tukubali kusaidiwa au tukomae? Baada ya Bandari ni ATCL na SGR au Tusubirie?

Wanabodi,

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za kwa maslahi ya taifa.

Hii ndio makala ya leo swali la wito kwa Watanzania wenzangu, jee jjifunze kujikubali kuwa hatuwezi kila kitu!, hakuna nchi yoyote duniani wanaweza kila kitu wao wenyewe!. Kuna vitu sisi Watanzania wenyewe hatuwezi!, na inapptokea kuna vitu hatuwezi, tunapojaribu tukashindwa, lazima tujikubali hili tumeshindwa, hatuwezi!. Swali ni unaposhindwa kuna ubaya wowote kubali kusaidiwa au tuendelee tuu kujitutumua tukomae tuu mpaka tuweze?
Kawaida yetu sisi tukiwa kwenye mitandao huwa tunaweza kila kitu lakini tukipewa tunaharibu.

Ni kweli kabisa huwa hatupangi mipango ya muda mrefu hasa kwa investments kubwa kama hizo ulizozisemea.

Hata hiyo JNHPP hatuna mpango wo wote wa muda mrefu, huwa tunajisemea tu tutatumia umeme kwa hivi na vile.....

Tunamuomba Mungu atusaidie kuzidi kutupa hekima.
 
Pascal una mawazo kama yangu, hongera kwa uzi mzuri sana.
Jamani ndugu zangu Watanzania tukubali tu sisi hatuwezi kuleta ufanisi. Tunachoweza ni kuiba tu kufirisi haya mashirika.
Jana nimetoa mfano wa Customs ya Tunduma border Zambia, Lori moja kupita kwenye scanner linatumia mpaka dakika 30, kwa saa 1 ina maana yatapita 4 au 5 tu out of hundreds yaliyopo kwenye foleni. Je tupo serious kweli?
Scanner ya upande wa Zambia ni dakika 5 tu chap Lori limetoka.

CAG Professor Assad aliwahi kusema Watumishi wengi kwenyeTaasisi za Serikali ni incompetent. Mavyeti tu wanayo, ubunifu na uwajibikaji zero. Wanawaza madili tu.
Wawekezaji waje tu sisi hatuwezi.
 
Mi nafikir tuanze na Rais.ABINAFSISHWE.
Hana afanyalo tukajivunia ukiachilia mbali kudandia cheap popularity ya Yanga ili tujue yupo. Zaid ya hapo hana ajuacho zaid ya kukopa kopa tu na kuzidi kulitia taifa hili kwenye matatizo mazito ya madeni mbele ya safar.
Matatizo wanayopitia Kenya sasa hiv hayakuanza ghafla tuu, ni kwa style hii hii ya kopa hapa..kopa palee na mwisho wa siku pesa zinaliwa na wajinga wachache aliowachomeka kwenye idara za wizara mbali mbali ..na pia anawapa maelekezo kabisaa kwamba WALE KWA UREFU WA KAMBA ZAO kiasi kwamba leo hii mkurugenzi wa halmashauri ya Mkuranga mkoani pwani anawaamuru wafanyakazi woote chini ya halmashauri hiyo walipe 70,000 kwa ajili ya kugharamia send-off party yake
Naungana na hili rais na mawazili tuwape wawekezaji wawe katika ivyo vyeo kwanza
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za kwa maslahi ya taifa.

Hii ndio makala ya leo swali la wito kwa Watanzania wenzangu, jee jjifunze kujikubali kuwa hatuwezi kila kitu!, hakuna nchi yoyote duniani wanaweza kila kitu wao wenyewe!. Kuna vitu sisi Watanzania wenyewe hatuwezi!, na inapptokea kuna vitu hatuwezi, tunapojaribu tukashindwa, lazima tujikubali hili tumeshindwa, hatuwezi!. Swali ni unaposhindwa kuna ubaya wowote kubali kusaidiwa au tuendelee tuu kujitutumua tukomae tuu mpaka tuweze?

Kiukweli kabisa uamuzi wa kulipa kampuni ya Dubai kutuendeshea Bandari yetu ya Dar es Salaam, Dar Port, kwanza msiuamini upotoshaji wa miaka 100!, ni uzushi tuu!, lakini uamuzi huu ni uamuzi sahihi, na kwa maoni yangu, baada ya Bandari, hata ATCL peke yetu hatuwezi, lazima tongue ubia!. Tukija kwenye SGR ndio kabisa!

Kuna vitu Watanzania hatuwezi na tunashindwa sio kwasababu ni vilaza, au hatuna uwezo, tunashindwa kwasababu tuu hatujui kutazama mbali!

Mfano saa hizi tuko busy kujenga SGR, lakini hatuna mkakati wowote wa kujiandaa kwa mzigo wa kuendesha SGR kwa faida. Waona mbali hili tukaliona, tukashauri Reli ya SGR: Je, Tujifunze kwa wenzetu Kenya kuepusha SGR yetu kuwa ‘A White Elephant’? Wenzetu yameshawakuta..., sasa tusubirie SGR yetu ikamilike, tujaribu kuioparate tushindwe ndipo tutafute usaidizi?, au wakati ujenzi unaendelea, tutazame mbali kwa kujenga uwezo wa uendeshaji na maandalizi ya kutafuta mzigo wa kushiba wa kubebwa na SGR?.

Hivi tuu tuna reli ya TAZARA tumeshindwa kuiendesha!, Tunduma ndio the busiest border kwa mizigo ya Zambia inabebwa na malori, huku mabehewa ya Tazara yamelala bure!.

Reli ya kati tumeshindwa kuiendesha to it's full capacity!, nenda Bandari kavu ya Isaka!, ukiwa mzalendo mwenye machozi ya karibu, unaweza kutoa machozi!. Reli ya Tanga, Moshi, Arusha, almost zimetelekezwa!. Mtu aliyeshindwa kuendesha kidogo hiki uje umpe kukuendeshea li SGR!, nategemea nini?. Kuna ubaya kuwaita watu wenye uwezo wakuendeshee kwa kipindi fulani huku unajenga uwezo wa ndani kuendesha, ukiwa tayari ndipo uendeshe?.

ATCL, tushukuru Magufuli kwa kuwa bold kukimbilia kununua midege kwa cash kwa mtindo wa kupiga tanchi, bila kuwa na business plan!.

Tumenunua midege ya masafa marefu, long hauls, tunaizungusha Dar-Mwanza-Kia!, tunaichosha bure, wear and tear ni kubwa!, matokeo yake by now, tume ground midege 4 kwa uchovu wa engine, tutatengeneza kwa millions of dollars halafu tuje kuharibu tena!. Ukiangalia abiria wa Tanzania wanaokwenda Ulaya na America kwa ndege za mashirika mengine ni abiria wa kujaza a 7 day flights, lakini sisi wenyewe hatuwezi!, lazima tusaidiwe!.

Pale unaposhindwa kitu fulani, hakuna ubaya wowote kuomba msaada kwa wenye uwezo usaidiwe!.

Tuliwahi kujaribu kwa ATC, TTCL, Tanesco, Dawasco, tukaja kuvunja mikataba kwasababu tulikuwa kuzaliwa!. Ukitaka kula ni lazima uliwe!, hivyo hata huu mkataba wa Bandari, kwavile tunataka kula, ni lazima tuliwe!. You can't eat your cake and have it!.

Kuna vitu vingi tuu tunashindwa lakini hatusemi!. Juzi kati Tundu Lissu kashambuliwa kwa kupigwa risasi mchana kweupe, Ben Saanane wetu humu, kakosoa kitu, kayeyuka!. Azory Gwanda kaandika kitu, kafuatwa na Toyota Land cruiser ya mkonga, kapotezwa!.

Serikali yetu imeshindwa kufanya uchunguzi kwasababu hatuna uwezo huo wa.... Watu tumejitokeza humu tukasema tuna uwezo kusaidia, tunachotaka ni serikali ijitokeze tuu na kukiri imeshindwa, na kuomba msaada kwa wenye uwezo!. Kuna watu wanadhani Scotland Yard, wanazaliwa na uwezo huo!, no!, Scotland Yard wanafanya scouting kuwapata watu wenye uwezo huo!, hapa Tanzania watu hao tunao lakini hatuwatumii!.

Niliwahi kuuliza WanaJF, je tuisaidie Serikali yetu inaposhindwa au tusubiri ishindwe, tuibeze na kuizomea kuwa haiwezi?

Paskali
Watu wa kulaumiwa kwanza ni mkapa,kikwete,Samia,maghu Hawa ndio waliofanya madudu,serikali imejaa wezi watupu,huko Ttcl,wakurugenzi Wana vikampunicvyao vya kutoa internet,deal hazitaenda serikalini,watajipigia pande TU,Ttcl "iliingiliwa "kimwili ikazaa Airtel,mkapa,kikwete walikuwepo walikuwa wanapiga makofi TU!!
Na kwa watumishi wa umma,wengi ni wezi,hawajuhi kazi,wamepata kazi kimaghumashi,Sasa wanatumia nafssi zao kuiba,boss wao Rais nae nidhaifu,analetewa wezi anashindwa kuchukua hatua,
Kubaki na bandsri mikononi mwa wazawa,wakati wizi ukiendelea na pesa kuingia mifuko binafsi,Bora tuibinafsishe,tupate pesa nyingi zijenge zahanati.
Tulishindwa kuendesha TBL,alikuwepo manager yeye kazi yake ilikuwa kujaza ndugu vilaza watupu!,,ikabidi iuzwe Sasa hv,IPO mbali sana,
Halotel, wa likuja juzi TU lakini wameishaipita TTCL ambayo IPO tangu mkoroni!!
Kwa ufupi,hii miradi mikubwa,atcl,tanesco,dawasa,ni Bora tuwakabidhi watu binafsi waendeshe sio Hawa wabongo wasio na nidhamu ya kazi,
Na ajira ziwe za mkataba
 
Pascal una mawazo kama yangu, hongera kwa uzi mzuri sana.
Jamani ndugu zangu Watanzania tukubali tu sisi hatuwezi kuleta ufanisi. Tunachoweza ni kuiba tu kufirisi haya mashirika.
Jana nimetoa mfano wa Customs ya Tunduma border Zambia, Lori moja kupita kwenye scanner linatumia mpaka dakika 30, kwa saa 1 ina maana yatapita 4 au 5 tu out of hundreds yaliyopo kwenye foleni. Je tupo serious kweli?
CAG Professor Assad aliwahi kusema Watumishi wengi kwenyeTaasisi za Serikali ni incompetent. Mavyeti tu wanayo, ubunifu zero .
Wawekezaji waje tu sisi hatuwezi.
Ila "we should not throw a baby and bathtab"
Tusitupe mti na jongoo wake,
Ubovu wa watumishi kwanza wanapatikana kimaghumashi,wapo watz wenye uwezo mkubwa,ila ndio hawana connections,yanapata mavilaza matupu
 
Ni tamaa tu. Kila Rais akiingia anaangalia cha kupiga mnada. Nini kimetushinda kwenye bandari zetu hadi za Maziwani huko? Tunashindwa kufanya maamuzi na kujiendeleza, tunamchukua mwekezaji ambaye naye anataka profit. Mwekezaji ndio mwenye kutupenda? mwenye kuipenda Tanzania? Mwenye uchungu na TZ? Mwenye kuijivunia Tanzania? This will be one of the riskiest decision kufanywa na Taifa hili kupitia kwa viongozi wake vilaza. Kwani waliounda DP World sio binadamu? Kwanini tunaamnini katika kufanyiwa vitu? Kwanini tunaamini katika kuendelezwa na siyo kujiendeleza?
Watanzania ni kama ma ng'ombe yanayo swagwa wala hayajui yanapo pelekwa ni kupelekwa msobe msobe tu.

Uafrika hasa utanzania ni LAANA.

Wale Raia 66 walio ukana utanzania na wengineo wengi waliokimbia hii nchi na hili Bara wamefanya jambo sahihi kabisa la kuvua Laana na kujitakasa kutoka kwenye Laana.
 
Hakuna anayeipenda Tanzania hata ukiweka watanzania ni mwendo wa kuiba mwanzo mwisho hakuna cha maana watakachofanya
Uafrika hasa utanzania ni LAANA.

Wale Raia 66 walio ukana utanzania na wengineo wengi waliokimbia hii nchi na hili bara wako sahihi kabisa kuvua Laana na kujitakasa kutoka kwenye Laana.
 
nothing impossible under the sun the word it self say am possible,ni aibu kubwa kwa taifa kushindwa,hata huyo mwarabu hajawahi kuwa mwema kwa lipi? ni biashara kama zingine tu anategemea faida.

*Ni bora tudeme na wezi wetu(sawa na mwanao akiiba ndani) tutafika tu.
 
Sisi kama nchi tunaweza tena kwa ufanisi mkubwa tuu.
Tatizo ni kwemba akiibuka aliyebarikiwa uwezo wa hali ya juu atachukiwa na kizimwa na kupotezwa kwa namna yoyote iwe kwa risasi,kutekwa na kupigwa hata kulogwa inapobidi. Na hii itaanzia ngazi ya familia,ukoo,jamii na kiserikali.
Akipewa mtu nafasi ataanza kuvimba na kuiba,kunaynyasa wengine na kujifanya Mungu mtu.
Utakosa ushirikiano mpaka utamani kuhama nchi.
So,tatizo lipo kwa wanaadamu wenyewe
 
Sisi kama nchi tunaweza tena kwa ufanisi mkubwa tuu.
Tatizo ni kwemba akiibuka aliyebarikiwa uwezo wa hali ya juu atachukiwa na kizimwa na kupotezwa kwa namna yoyote iwe kwa risasi,kutekwa na kupigwa hata kulogwa inapobidi. Na hii itaanzia ngazi ya familia,ukoo,jamii na kiserikali.
Akipewa mtu nafasi ataanza kuvimba na kuiba,kunaynyasa wengine na kujifanya Mungu mtu.
Utakosa ushirikiano mpaka utamani kuhama nchi.
So,tatizo lipo kwa wanaadamu wenyewe
hebu waambie hawa mazuzu wanaozusha uongo
 
Tunashindwa kwasababu tumechagua kushindwa! Mifumo yetu ya utawala tayali ni collapse huwezi kupata ufanisi kwenye mfumo uliyokufa!

Mkurugenzi wa shirika kubwa kama bandari anachaguliwa na Rais! Na Rais amepatikana kwa kuiba kura!! Mwizi ndio anachagua mtu wa kuongoza bandari!!

Hakuna uwazi uyo mtu amepatikanaje na kwa vigezo gani? Ili mradi tu Rais kamchagua!! Utasikia tiss wamemfanyia vetting! Tiss awa ambao wanaiba kura!? Tena wanaiba kwa mbinu za kiganga za kienyeji!!wala sio za kisayansi!

Tiss ambao hawana exposure yeyote zaidi ya kuchoma nyama mnadani na kununua wanawake malaya, pale chako ni chako bar!! Watu wa dizaini hio watamfanyia vetting ya maana nani? zaidi sana uwa wanaangalia kama mlengwa ana kadi ya kijani tu.

Harafu tunakaa kabisa tunategemea ufanisi kwenye bandari ambako upatikanaji wa mkurugenzi wake umegubikwa na rushwa,ukabila,udini na wizi!! Ni sawa na kusubili meli jangwani.
 
Kwani nchi hii haina what we saw call them wataalam
Tupo karne ya 21 yenye teknlogy ya hali ya juuu
Ni muda wa kuamka kutoka kwenye usingizi wa pono
Kwani kizazi kijacho kitatushangaaa
Ni bora kina mkwawa na wengineo kuliko uongozi wa sasa
 
Serikali haikuwa kunufaika na ubinafsishaji. Mashirika mengi yalikufa kabisa, mengi tukaja kushtuka yapo hoi trc, tanesco, atcl, ttcl
Serikali kwa maana ya watendaji waliokabidhiwa mamlaka kuendesha mashirika, viongozi wa juu Serikalini, wafanyabiashara wakubwa ndio walionufaika kwenye ubinafsishaji uliopita. Ushahidi upo TTCL, kwa miaka mingi tu wafanyakazi wa kampuni ile ya Serikali ndio wanufaika wa ubinafsishaji ule. Takukuru wako kimya tu, hata zile sheria za uhujumu uchumi nadhani hazitumiki kabisa. Nchi inaenda kienyeji kama vilabu vyetu vya mpira na vyama vya ushirika aka ushirikina!.
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za kwa maslahi ya taifa.

Hii ndio makala ya leo swali la wito kwa Watanzania wenzangu, jee jjifunze kujikubali kuwa hatuwezi kila kitu!, hakuna nchi yoyote duniani wanaweza kila kitu wao wenyewe!. Kuna vitu sisi Watanzania wenyewe hatuwezi!, na inapptokea kuna vitu hatuwezi, tunapojaribu tukashindwa, lazima tujikubali hili tumeshindwa, hatuwezi!. Swali ni unaposhindwa kuna ubaya wowote kubali kusaidiwa au tuendelee tuu kujitutumua tukomae tuu mpaka tuweze?

Kiukweli kabisa uamuzi wa kulipa kampuni ya Dubai kutuendeshea Bandari yetu ya Dar es Salaam, Dar Port, kwanza msiuamini upotoshaji wa miaka 100!, ni uzushi tuu!, lakini uamuzi huu ni uamuzi sahihi, na kwa maoni yangu, baada ya Bandari, hata ATCL peke yetu hatuwezi, lazima tongue ubia!. Tukija kwenye SGR ndio kabisa!

Kuna vitu Watanzania hatuwezi na tunashindwa sio kwasababu ni vilaza, au hatuna uwezo, tunashindwa kwasababu tuu hatujui kutazama mbali!

Mfano saa hizi tuko busy kujenga SGR, lakini hatuna mkakati wowote wa kujiandaa kwa mzigo wa kuendesha SGR kwa faida. Waona mbali hili tukaliona, tukashauri Reli ya SGR: Je, Tujifunze kwa wenzetu Kenya kuepusha SGR yetu kuwa ‘A White Elephant’? Wenzetu yameshawakuta..., sasa tusubirie SGR yetu ikamilike, tujaribu kuioparate tushindwe ndipo tutafute usaidizi?, au wakati ujenzi unaendelea, tutazame mbali kwa kujenga uwezo wa uendeshaji na maandalizi ya kutafuta mzigo wa kushiba wa kubebwa na SGR?.

Hivi tuu tuna reli ya TAZARA tumeshindwa kuiendesha!, Tunduma ndio the busiest border kwa mizigo ya Zambia inabebwa na malori, huku mabehewa ya Tazara yamelala bure!.

Reli ya kati tumeshindwa kuiendesha to it's full capacity!, nenda Bandari kavu ya Isaka!, ukiwa mzalendo mwenye machozi ya karibu, unaweza kutoa machozi!. Reli ya Tanga, Moshi, Arusha, almost zimetelekezwa!. Mtu aliyeshindwa kuendesha kidogo hiki uje umpe kukuendeshea li SGR!, nategemea nini?. Kuna ubaya kuwaita watu wenye uwezo wakuendeshee kwa kipindi fulani huku unajenga uwezo wa ndani kuendesha, ukiwa tayari ndipo uendeshe?.

ATCL, tushukuru Magufuli kwa kuwa bold kukimbilia kununua midege kwa cash kwa mtindo wa kupiga tanchi, bila kuwa na business plan!.

Tumenunua midege ya masafa marefu, long hauls, tunaizungusha Dar-Mwanza-Kia!, tunaichosha bure, wear and tear ni kubwa!, matokeo yake by now, tume ground midege 4 kwa uchovu wa engine, tutatengeneza kwa millions of dollars halafu tuje kuharibu tena!. Ukiangalia abiria wa Tanzania wanaokwenda Ulaya na America kwa ndege za mashirika mengine ni abiria wa kujaza a 7 day flights, lakini sisi wenyewe hatuwezi!, lazima tusaidiwe!.

Pale unaposhindwa kitu fulani, hakuna ubaya wowote kuomba msaada kwa wenye uwezo usaidiwe!.

Tuliwahi kujaribu kwa ATC, TTCL, Tanesco, Dawasco, tukaja kuvunja mikataba kwasababu tulikuwa kuzaliwa!. Ukitaka kula ni lazima uliwe!, hivyo hata huu mkataba wa Bandari, kwavile tunataka kula, ni lazima tuliwe!. You can't eat your cake and have it!.

Kuna vitu vingi tuu tunashindwa lakini hatusemi!. Juzi kati Tundu Lissu kashambuliwa kwa kupigwa risasi mchana kweupe, Ben Saanane wetu humu, kakosoa kitu, kayeyuka!. Azory Gwanda kaandika kitu, kafuatwa na Toyota Land cruiser ya mkonga, kapotezwa!.

Serikali yetu imeshindwa kufanya uchunguzi kwasababu hatuna uwezo huo wa.... Watu tumejitokeza humu tukasema tuna uwezo kusaidia, tunachotaka ni serikali ijitokeze tuu na kukiri imeshindwa, na kuomba msaada kwa wenye uwezo!. Tumewasaidia kupata pa kuanzia Taifa linahangaika na wasiojulikana waliomshambulia Tundu Lissu! Je, ni hawa?! Mhe. Mwigulu, IGP, anzieni hapa! bado wakashindwa!. Tumejitokeza tena live Mubashara kupitia kwenye TV, tukasema tunaweza kusaidia Serious Media inaweza kuwabaini "wasiojulikana" Deo Masakilija lakini wapi!.

Kuna watu wanadhani Scotland Yard, wanazaliwa na uwezo huo!, no!, Scotland Yard wanafanya scouting kuwapata watu wenye uwezo huo!, hapa Tanzania watu hao tunao lakini hatuwatumii!.

Niliwahi kuuliza WanaJF, je tuisaidie Serikali yetu inaposhindwa au tusubiri ishindwe, tuibeze na kuizomea kuwa haiwezi?.

My Take:
Rais Nyerere japo alitupatia uhuru, lakini kulikuwa na watu wengine wenye uwezo kuliko Rais Nyerere, wangeweza kutututawala vizuri zaidi na kutufikisha mbali zaidi, ila ni Nyerere ndiye aliyechaguliwa na Mungu kuwa rais wetu!. Vivyo hivyo kwa Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli na sasa Samia, haina maana kuwa ndio they are the best, but the chosen ones!, lakini the best wapo wanajijua wanaangalia tuu huku wamejinyamazia kwasababu hawajaombwa au kushirikishwa!.

Wito kwa serikali yetu Tukufu, mkishindwa jambo lolote, kabla hamjakimbilia huko nje kuomba msaada, exhaust the local remedies!. Serikali ijitokeze kwa uwazi kabisa very transparently iseme wazi kabisa kuwa hili limetushinda, kama kuna Mtanzania au kampuni ya Kitanzania inaweza kusaidia, na ina uwezo huo, ijitokeze isaidie.

Ikitokea hakuna hakuna Mtanzania au kampuni ya Kitanzania ina uwezo huo, ndipo tutafute wabia kwa kutangaza kwa uwazi kabisa, mabingwa wa uendeshaji wa Bandari ni Bandari kama ya Rotterdam wangejitokeza!.

Kuna kushindwa na kushindwa, kushindwa kungine ni aibu!. Sherehe zote za ndoa za kiasili na kidini, zilikuwa zinasherehekewa ndoa inapokuwa ndoa na sio ndoa inapofungwa!, ma bi harusi lazima awe sealed!. Sasa ikitokea ndoa imefungwa, ikakutikana ndugu ameshindwa kufungua seal ili sherehe iendelee!, ili kuepuka aibu, huyo ndugu anasaidiwa in a very closed guarded secret, kwa kaka mtu, and some tribes hata baba mtu!.

Hivyo Watanzania tunaposhindwa jambo fulani, tuanze kuomba msaada kwa Watanzania kwanza, tukikosa ndio twende kwa wageni kutafuta msaada!.

Paskali
Shida na ujinga wote huu ni matokeo ya mifumo ya kipuuzi ya ujamaa,Huwa haijengi hoja ila inategemea propaganda,hisia na Imani..

Hao hao wajinga na wapuuzi wenye hizo mentality over years wameshindwa kuleta Ufanisi na ndio maana Mwingi na Mkapa waliachna na hayo mawazo ya ujima..

Imagine pamoja na kujaza sijui wanajeshi na Tisa huko bandarini chini ya awamu ya 5 hakuna Ufanisi wowote sana sana wafanyabiashara walimkimbia Bandari Kwa sababu hao hao Watumishi wa Umma na wao wanataka pesa ,na hawawezi kuwa na Ufanisi kama private sector..

Private sector hainaga urasimu Wala Mlmilolongo ya urasimu wa kindezi,ukizingua unakuwa fired ndio maana Kuna Ufanisi..eg Dart pamoja na kuwa na njia zake binafsi ni hasara daily Kwa sababu ni Mali ya Umma shamba la bibi
 
Acha zako wewe.

Tumeshindwa wapi wakati nafasi za juu kwenye taasisi zote mnaweka watoto wenu wasio na SIFA

Fungueni milango na wekeni uwazi wa mishahara watu waombe hizo nafasi halafu uangalie ufanisi.
Mishahara iliyowaz ni walimu tu laki laki hao vitengo wanakula kwa urefu wa kamba
 
ATCL, TRC, TTCL, na mashirika mengine lukuki huko nyuma yalishawahi kubinafishwa kwa wageni! Na matokeo yake kila mtu aliyaona. Kwa hiyo watu wanapotikia shaka huo uwekezaji, wana sababu za msingi.

Viongozi wengi wenye dhamana kwenye hii nchi siyo wazalendo! Mara nyingi wamekuwa wakiingia mikataba tata yenye manufaa binafsi zaidi kuliko Taifa.
Nimekumbuka ubinafsishwaji wa TANESCO enzi za Mkapa, kumbe ulikuwa ni mpango wa kupiga hela
 
Back
Top Bottom