Watanzania tujiulize: Ikiwa sisi ndiyo wenye mali, nini kinatukimbiza nje kutafuta wa kuja kuzila (eti kuwekeza)?

Kwanza Tanzania hatuna rasilimali za thamani kama tunavyoaminishana utasikia eti tuna mito, mabwawa, ardhi, madini, wanyama pori, maziwa ni rasilimali sawa ila hazina thamani kama tunavyoaminishana.

Kabisa mkuu, raslimali zipo ila thamani yake ni ndogo sana.
 
Umenielewa.
 
na maana ya "maneno" na "blaa blaa" unajua??!!
Nilifikiri una hoja, wake up man!
HaIwezekani kama Kiongozi utuoni wote tuna akili kama za ndugu zako uliowateua kisa ulaji,never on earth! Tanzania tuna watu competent kuwekeza au kuzalisha Ajira kuliko unavyofikiri !??
Inakuwaje leo u amuuzia mtu Kitalu cha kuzalisha mifugo, keshokutwa anaanza kuuza mifugo nje,ilhali wewe kwa miaka 40 ulishindwa? Hiyo nayo inahitaji Mzungu?.
Tujipime.
 
Hao wabunge watoe kabisa hapo kwenye list,tusiwategemee hao kabisa kabisa.
 
Tulimtumia nani hapa nchini kupata hizo options? CCM?,Bunge? Vyama?, Vyuo vikuu na wasomi wao? Je, na wao wanatumia kina Nani kuziona hizo option tena nchi sio yap? We are wrong somewhere.
Sema hata hapa hapa.... huwezi jua nani anaona.
 
Inasikitisha sana ati leo hii tunatafuta hadi wawekezaji wa sekta ya KILIMO...kweli kweli watanzania..?
yaani miaka 60 ya uhuru wetu hata kilimo nacho tunatafuta watu wa kuja kutufundisha...we're not serious aisee !!

Haya ngoja waje wachukue mapori yote ya akiba tubakie mjini kuuziana soksi.
 
Unapoteza muda kwa kupiga siasa, dada na kaka zako wanatafuta kazi kupitia hayo makampuni ya wawekezaji.Achana na hizi fikra za kurithishwa na wanasiasa, ubongo wako na usimame wenyewe.
 
Pengine kabla hujazaliwa wewe wazee wetu kina Nyerere walihubiri kujitegemea kinadharia lakini kivitendo walishindwa.

Ni dunia ya kutegemea, punguza maumivu ya kichwa yasiyo na sababu.
 
Mkuu usimfananishe Samia na JPM, kila rais anayo haki ya kupita njia anazoona zinaifaa Tanzania. Kipaji alichokuwa nacho JPM Samia hana.

Kipaji alichonacho Samia JPM hana, hivyo msitake kulazimisha hisia zenu za kumpenda JPM ndizo hizo hizo zimeongoze Samia, mnatwanga maji kwenye kinu, mnapoteza muda.
 
Kutokuwajibika kwa waliojipa uongozi pasina malengo mapana na wasio wabunifu.Badala ya kutafuta njia shirikishi ili kuzitumia raslimali zetu.Tangia awamu ya 5 iingie madarakani kimagumashi ndipo teuzi nyingi zilipoegemea kwa maDR na maProfesor,lakini kwa kukosa kwa ubunifu tukashuhudia deni la Taifa likipaa kwa kiwango karibia au sawa na deni la awamu zote zilizotangulia.
CCM hata ingeongozwa na malaika anaweza kufanya mabaya kuliko shetani mwenyewe.Tunavutia wawekezaji kutokea enzi za Mzee wa Lupaso lakini nchi ndiyo inazidi kudidimia.
Tatizo la Tanzania ni aina ya viongozi wabovu wanaopatikana kwa njia ovu na wenye tamaa za kujineemesha wao na ndugu/jamaa zao kwa miaka yote nasi wananchi kukosa njia mbadala ya kuwaondoa.Sheria na Katiba mbovu ni kikwazo kikubwa.
Tusipobadilika na kupigania mabadiliko sisi wenyewe,tusitarajie mapya.
 
Brains... (lack of)

Brainwashed (kuthamani vingine / vya nje)

Not being serious (kutengeneza / kufanya vitu vyenye mediocre quality)

Investing on wrong things (wakati wengine walitumia nguvu sana ku-invest kwenye research, development na kuwezesha watu wao) sisi tunawekeza kwenye kujaza ujinga...

Marginalization na Developed Countries kuzibana nchi kama zetu ili tuendelee kuwa wazalishaji wa malighafi na watumiaji wa their junks products...
 
Hapo ndio kosa la sisi kuwa hapa tulipo...., No one is clever / bright than all of us...., Kumpa mamlaka mtu mmoja ndio achague nini cha kufanya au njia gani za kupita ni matumizi mabaya ya Human Resources..., Wadau na Wataalamu inabidi wachague njia Rais ni kusimamia tu....
 
Watu wanakufa kwa njaa hata chai ya asubuhi shida. Sasa immediate rescue imekuja utafikilia hayo yote!!!
 
Mtoa mada yupo sahihi kuuliza hilo alilohoji.Nchi hii ina mipango ya zimamoto na umaskini wa fikra.Tuna madini,bahari,maziwa,mito yenye kutiririsha maji,ardhi yenye rutuba,watu wenye nguvu nk ambapo kasoro kubwa zipo katika uongozi bora.Kubali kataa ila huo ndiyo ukweli.
 

"uomba pesa na uwekezaji" Unapotosha pesa za uwekezaji haziombwi kwasababu sio za serikali. Serikali inahimiza uwekezaji na hii inatokea kila mahali. Huku nje mfano hapa USA hata miji na majimbo yanafanya hivyo hapa Texas Governor wetu anaenda California kujaribu kuwashawishi wawekezaji waje hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…