Ngoma ikiwambwa sana hupasuka. Putin yuko vizuri sana lakini nahisi sifa zinampanda kichwani sasa. Akiivamia Ukraine itakuwa keshwapa chance kubwa mahasimu wake hasa USA kummaliza kabisa...
Mkuu kitu pekee ambacho tunapaswa kujua Ni kuwa mgogolo huu una sura 2, sura ya kwanz Ni hii inayo onekana kwamba Ni wa kimasirahi, kwamba kunakuivamia Ukraine(ambayo leo tayari puttin amelianzisha)
Ila sura ya pili Ni ya kimgogolo wa ulinzi, yaan ngoja nikupe mfan rahis, Ni sawa na Tanzania, yenye nchi 2, leo hii zijitenge kila mmoja awe kivyake, atakae faidika Sana na upande wake Ni zanziba, maana kuna nchi watataka kuitumia zanziba kwa masilahi yao, ili kuidhoofisha tanganyika, na kwa kulijua hlo tanganyika itafanya kila liwezalo kujirida hata ikiwezekana kwa Vita, nmesema tu mfano,
Kinachoendele urusi ndo hicho, Kwanza ukeine ilikuwa inatawaliwa kwa remote na urusi, then watu wakampindua wakawake wa kwako, urusi ikasema isiwe tabu ikachukua majimbo mawili ndani ya Ukraine, ikatangaza nchi huru, baada ya happy Ukraine akakimbia mbio kusema kaonewa wakamwambia ajiunge na Nato, na hapo ndpo alikuwa anapataka mrusi, wakamwambia achague kutokujiunga au ajiunge, nahisi alichagua kujiunga au kuunga mkono Kama sikosei,
Ahaaa puttin kaseme Sasa tunakuchukua na ww, hapo ndpo walipofika,
Kwa hyo Vita hvyo vimeihamisha dunia nzima kwa Sasa hakuna anaezungumzia c19, Wala nn ila wote wanaangalia masilahi ya matumbo yao, na wasipo kubaliana kitaumana, athari itakuwa mbaya zaidi kwenye matokeo ya Vita, nnaona maisha ya watu yanakwenda kuathirika,
Nko tayari kukosolewa Kama kunasehem cjaeleza vzr
Mr, Bonny.