Watanzania wana bidii ya maombi sana, bila dhana ya Mungu watakosa maana ya maisha kabisa

Watanzania wana bidii ya maombi sana, bila dhana ya Mungu watakosa maana ya maisha kabisa

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Katika mkasa wa jengo la Kariakoo kuanguka nimewasikia watu wengi wanaotegemea watu kutolewa au ambao waliangukiwa na jengo wakiomba na kushukuru Mungu, Allah au Yesu katika mkasa huo mkasa. Kila posti niliyosoma mtandaoni, kila clip au maongezi ya kila mtu aliyefukuliwa huwezi kuyakosa haya maneno(Maombi, Mungu, Allah, Ya Rabbi, Alhamdulillah na Yesu)

Hakika Watanzania dini imewakaa, ni viumbe wa kidini, bila dini na mungu sidhani kama wana tumaini lolote au muelekeo wowote wa maisha.
 
Maisha Bila Mungu hayafai kitu Yoda

Ukiwa Mpumbavu Huwezi elewa haya Mambo.
Na Moja ya Sifa ya Mpumbavu ni upumbavu usiojificha na kujifanya, kuwaza, kusema Hakuna Mungu au kutomtegemea Mungu.
Nasikia kuna watu bado wamefukiwa kwenye kifusi, jitahidini kuongeza maombi waweze kufukuliwa, lakini zaidi sana mfanye maombi watawala waboreshe huduma za uokozi na usimamizi wa ujenzi na mipango miji.
Fanyeni maombi kwa haya pia ndio ya muhimu zaidi.
 
Hakika Sisi sote ni wa Allah na Hakika Sisi kwake (Allah) tutarejea.

Mitihani inaweza kuwa sababu ya kusamehewa madhambi kwetu Waislam, mitihani inaweza kuwa sababu ya kupandishwa daraja, mitihani inaweza kuja ill kuwakumbusha walioghafilika warudi kwa Mola wao kwa kutubia.


Sisi Waislam tumefundishwa kumdhania kheri Mola wetu. Na kuwa na subra na kushukuru.
 
Kwa hyo hao walio kufa watakuwa walikuwa c wafuasi wa hayo majinaa au cyo mkuu😔

Kuna wengine vifo hivyo ni mwanzo wa kheri isiyokatika kwao. Wengine kwao ni mwanzo wa adhabu (Allah atuepushe na adhabu). Kuna watu wamepata mwisho mwema kwa kifo cha namna hiyo. Kwetu Waislam kufa kwa kuangukiwa na jengo ni kifo cha shahidi. Allah awakubalie Waislam waliokufa kwa kwa kuangukiwa na jengo kuwa mashahidi, Aameen.

Allah awafanyie wepesi watu wote walioumia katika ajali hii na waliopoteza mali zao, Aameen.

Nsmuomba Allah anipe mwisho mwema na anifishe katika Tawheed na Sunnah. Aameen.
 
Katika mkasa wa jengo la Kariakoo kuanguka nimewasikia watu wengi wanaotegemea watu kutolewa au ambao waliangukiwa na jengo wakiomba na kushukuru Mungu, Allah au Yesu katika mkasa huo mkasa. Kila posti niliyosoma mtandaoni, kila clip au maongezi ya kila mtu aliyefukuliwa huwezi kuyakosa haya maneno(Maombi, Mungu, Allah, Ya Rabbi, Alhamdulillah na Yesu)

Hakika Watanzania dini imewakaa, ni viumbe wa kidini, bila dini na mungu sidhani kama wana tumaini lolote au muelekeo wowote wa maisha.
Upo sahihi watanzania ni watu wa imani sana
 
Hakika Sisi sote ni wa Allah na Hakika Sisi kwake (Allah) tutarejea.

Mitihani inaweza kuwa sababu ya kusamehewa madhambi kwetu Waislam, mitihani inaweza kuwa sababu ya kupandishwa daraja, mitihani inaweza kuja ill kuwakumbusha walioghafilika warudi kwa Mola wao kwa kutubia.


Sisi Waislam tumefundishwa kumdhania kheri Mola wetu. Na kuwa na subra na kushukuru.
Hakuna mtihani wala nini, hakuna cha kupanda daraja na hapo kwenye hiyo ajali kuna watoto wadogo ambao hawajui hata maana ya dhambi na kutubu.
 
Maisha Bila Mungu hayafai kitu Yoda

Ukiwa Mpumbavu Huwezi elewa haya Mambo.
Na Moja ya Sifa ya Mpumbavu ni upumbavu usiojificha na kujifanya, kuwaza, kusema Hakuna Mungu au kutomtegemea Mungu.
Mzee we ndyo mpumbavu wa wapumbavu jamaa kajenga hoja kaleta na wewe jenga hoja yako mjibu kwa hoja na si kutukana mak* wewe
 
Katika mkasa wa jengo la Kariakoo kuanguka nimewasikia watu wengi wanaotegemea watu kutolewa au ambao waliangukiwa na jengo wakiomba na kushukuru Mungu, Allah au Yesu katika mkasa huo mkasa. Kila posti niliyosoma mtandaoni, kila clip au maongezi ya kila mtu aliyefukuliwa huwezi kuyakosa haya maneno(Maombi, Mungu, Allah, Ya Rabbi, Alhamdulillah na Yesu)

Hakika Watanzania dini imewakaa, ni viumbe wa kidini, bila dini na mungu sidhani kama wana tumaini lolote au muelekeo wowote wa maisha.
Ndio maana kuna ujio wa manabii wengi wenye ukwasi mkubwa wa kutisha kupitia hawa watanzania imani na kuamini kumepelekea utajiri na ajira kwa matapeli!
 
Mtoa hoja ana point yenye code ukisoma kama gazeti la serikali unajaza server 😂!.

Ila ukweli hii issue ya dini imetulevya wengi sana, hata eneo ambalo tunatakiwa kutumia akili hii tuliyopewa na Maulana bado tunaweka dini.

Jambo baya sana hili, mwenyeezi Mungu alitupa mamlaka ya kutawala kila kitu duniani, lakini leo binadamu ndiye anatawaliwa na hivyo vitu, kalaghabao!.

Hapo kwenye jengo badala ya kufanya jitihada kuokoa watu wanamuomba subhuanah/ Mola afanye wepesi wengine waokoke humo!, HAIWEZEKANI KAMWE, lazima wewe ndiye ukatoe msaada wa kumuokoa siyo Mungu aje kuokoa.

Yeye ashakupa mamlaka ya kufanya lolote mtu apone, unapomuacha afe basi unabeba jukumu la hukumu kwa kuua - note that!.
 
Hakuna mtihani wala nini, hakuna cha kupanda daraja na hapo kwenye hiyo ajali kuna watoto wadogo ambao hawajui hata maana ya dhambi na kutubu.
Mimi Muislam ndio naamini hivyo. Maisha hayaishii hapa. Kwako kama unaamini kuwa maisha yanaishia hapahapa, unaamini hakuna maisha ya barzakh, unaamini hakuna kufufuliwa na kulipwa, hilo ni tatizo kwako, Allah akuongoze.

Hao watoto Allah atawalipa

Sisi Waislam tunamdhania dhana njema Mola wetu. Na tuna jihimiza subra.


155. Hapana shaka tutakujaribuni kwa chembe ya khofu, na njaa, na upungufu wa mali na watu na matunda. Na wabashirie wanao subiri

156. Wale ambao ukiwasibu msiba husema: Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake Yeye hakika tutarejea
(Qur'an 2: 155- 156)


Sisi hatumdhanii Mola wetu dhana mbaya. Tunamdhania dhana nzuri. Na wala hatusemi ila analoliridhia Allah; Hakika sisi ni wa Allah na hakika sisi kwake Yeye tutarejea.

Kutoka kwa Suhaib -Radhi za Allah ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na amani ziwe juu yake:
"Ajabu iliyoje ya jambo la muumini, hakika jambo lake lote ni kheri, na hakuna hilo kwa yeyote ila kwa muumini, akipatwa na jambo lenye kufurahisha anashukuru ikawa hilo ni kheri kwake, na akipatwa na madhara anasubiri likawa hilo ni kheri kwake."
[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim] - [صحيح مسلم - 2999]


Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Mtihani utaendelea kumpata Muumini mwanamume na Muumini mwanamke katika nafsi yake na watoto wake, na mali yake mpaka akutane na Allaah akiwa hana dhambi)) [At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Hasan Swahiyh].

Kutoka kwa Anas kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Allaah Anapompendelea mja Wake kheri, Humharakishia adhabu duniani. Na Allaah Anapomtakia mja Wake shari Humzuilia dhambi zake hata Amlipe Siku ya Qiyaamah)). Na amesema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ((Hakika malipo makubwa kabisa yapo pamoja na mtithani mkubwa, na hakika Allaah Anapopenda watu Huwapa mtihani. Basi atakayeridhika atapata radhi (za Allaah) na atakayechukia atapata ghadhabu)) [At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Hasan]

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Mfano wa Muumini ni kama mti ulio na rutuba, upepo unaupiga huku na kule, na ataendelea Muumini kufikwa na mitihani. Na mfano wa mnafiki ni kama mti wa seda [aina ya mti wa mbao ya mkangazi], hautikisiki hadi ung’olewe wote mara moja)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

Kutoka kwa Sa’iyd bin Abi Waqqaasw (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilisema: “Ee Rasuli wa Allaah! Watu gani wanaopata mitihani migumu zaidi? Akasema: ((Manabii, kisha mfano wake, na mfano wake. Hupewa mtihani mtu kulingana na Dini [imani] yake. Ikiwa Dini yake ni imara, mtihani wake huwa mkubwa. Na ikiwa Dini yake ni dhaifu hupewa mtihani kulingana na Dini yake. Husibiwa sana na mtihani mmojawapo hadi atatembea ardhini bila ya kuwa na dhambi)) [At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Hasan Swahiyh, Ibn Maajah, na Al-Albaaniy kadhalika kasema ni Swahiyh].


Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy na Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Muislamu hatopatwa na tabu, wala maradhi, wala hamu wala huzuni wala udhia wala ghamu [sononeko] hata mwiba unaodunga isipokuwa Allaah Humfutia madhambi yake kwa sababu ya hayo)) [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hivyo sisi Waislam tunamdhania kheri Mola wetu, na tunasubiri na kutaraji malipo kutoka kwake
 
Hapo kwenye jengo badala ya kufanya jitahihada kuokoa watu wanamuomba subhuanah/ Mola afanye wepesi wengine waokoke humo!,

Juhudi zinafanyika kwa yaliyo ndani ya uwezo wetu na kumuomba Allah hatuachi.

Au uliona watu wamekaa tu?

Mleta mada ni kama anaumia Mola kutajwa na kusifiwa.

Allah atatukuzwa tu katika hali zote. Sifa zote njema zinamstahiki Allah. Aliye Mmoja tu hana mshirika.
 
Katika mkasa wa jengo la Kariakoo kuanguka nimewasikia watu wengi wanaotegemea watu kutolewa au ambao waliangukiwa na jengo wakiomba na kushukuru Mungu, Allah au Yesu katika mkasa huo mkasa. Kila posti niliyosoma mtandaoni, kila clip au maongezi ya kila mtu aliyefukuliwa huwezi kuyakosa haya maneno(Maombi, Mungu, Allah, Ya Rabbi, Alhamdulillah na Yesu)

Hakika Watanzania dini imewakaa, ni viumbe wa kidini, bila dini na mungu sidhani kama wana tumaini lolote au muelekeo wowote wa maisha.
Na hapo ndio mzungu na mwarabu alipotupiga bao.
 
Back
Top Bottom