Watanzania wanaishi Nchi ya Uchumi wa Kati?

Ni muhimu sana kutambua kuwa kufikia hatua hii ni mchango wa awamu zote zilizotangulia na wananchi wa Tanzania na si matokeo ya awamu moja au miaka 5 tu.
Hili ndilo mnalotakiwa kuwafafanulia wananchi walielewe pasipo shaka.

Propaganda za awamu ya tano ziko wazi hazijifichi na Mweyewe hafichi kwamba mafanikio haya yote ni juhudi zake, na asipochaguliwa tena haya yote yatapotea. Si anayasema haya, kwani anaficha?

Na unashangaa watu na akili zao wanaamini.
 
Zitto wewe ni mbabaishaji tuu, yaani hua sikuelewi upo katika kingdom ipi, animalia, plantaé au N'dudu tuu wewe...
 
Kwanza kabisa, ni vyema kufahamu kwamba kulingana na tarakimu zilizo tolewa na benki ya dunia, nchi ya uchumi wa kati inatakiwa kuwa na Gross national index per capita (GNI per capita) ya dola za Ki Marekani 1,036-12,535. Ambapo 1,036-4,045 ni lower middle income na 4,046-12,535 ni upper middle income. Kwa mujibu wa ripoti ya benki ya dunia, tarehe moja mwezi wa saba mwaka 2020, Tanzania ina GNI per Capita ya dola za Ki Marekani 1,080.

GNI ni tofauti kidogo na GDP (Gross Domestic product), vile vile per capita income ni tofauti kidogo na GNI per capita ila benki ya dunia inatumia GNI per capita ku orodhesha nchi katika vigezo hivyo kama nchi ya kipato cha chini, Kipato cha kati, na kipato cha juu. GDP ni kipato cha nchi kwa mwaka, GNI ni kipato cha nchi kwa mwaka uki jumlisha na vipato kutoka nchi zingine (yaani GDP kwa mwaka + Vipato kutoka nchi zingine kwa mwaka). Per capita income ni GDP kwa mwaka iki gawanywa kwa idadi ya watu kwenye nchi. Hii inasaidia kufahamu kwamba kama unge amua kugawanya kipato cha nchi kwa kila mtanzania, kila mtu ange pata shilingi ngapi. Vile vile GNI per capita ni GDP kwa mwaka + Kipato kutoka nchi zingine kwa mwaka uki gawia idadi ya watu kwenye nchi. GDP sio kiashiria kizuri cha ukuaji wa uchumi wa nchi lakini per capita na GNI per capita ni tarakimu zinazo weza kuku eleza zaidi kuhusu hali ya nchi. Kwa mfano tuki angalia GDP ya nchi kama Nigeria, utagundua kuwa inaweza kuwa kubwa kuliko nchi karibia zote za Afrika lakini kulingana na population yao, per capita income sio kubwa sana. Viwango vya GNI per capita vya kila kundi la nchi (low income, middle income na high income) vina badilika kila mwaka kwasababu ya inflation, exchange rate na vitu vingine. Benki ya dunia huwa ina ripoti mabadiliko hayo kila mwaka.

New World Bank country classifications by income level: 2020-2021
New country classifications by income level: 2019-2020


Uki angalia link nilizo weka hapo juu kitu cha kwanza utakacho gundua ni kwamba ili kuingia kwenye nchi ya uchumi wa kati GNI per capita ime badilika kila mwaka. 2018-$996, 2019-$1,026, 2020-$1,036, kwa hiyo imepanda kila mwaka kwa sababu nilizo orodhesha hapo juu kwa hiyo hawaja tanua wigo. GNI per capita ya Tanzania mwaka 2020 ni 1,080. Haijawahi kufika 1,096 kama ulivyo andika na Tanzania haijawahi kutangazwa kuwa nchi ya uchumi wa kati. Vile vile GNI per capita ya Tanzania mwaka 2015 ilikuwa Dola za ki Marekani 948. Ina maanisha ongezeko ndani ya miaka mitano ni kutoka 948 mpaka 1,080. Nina kubaliana na wewe unaposema kwamba ni too ambitious kufikia GNI per capita ya $3000 mwaka 2025 na inahitaji nguvu za ziada kuvuka daraja na ku orodheshwa kama upper middle income country. Ni vyema ku fahamu pia kwamba tarakimu hizo zinaweza zisikupe picha halishi kwasababu ni wastani ya watu wote waliopo Tanzania. GNI per capita ya $1,080 ina maanisha kwamba kila mtanzania anatakiwa kuwa na kipato hicho kwa mwaka. Hio sio uhalisia. Jambo lingine la kutambua ni kazi kubwa ambayo lazima ifanyike ilikufikia malengo ya kuongeza GNI per capita. Kwa mfano, GNI per capita ya Tanzania mwaka 2015 ilikuwa $948 na 2020 ni $1,080. Hii ina maanisha kwamba katika miaka mitano kumekuwa na ongezeko la $132 kwa kila mtu ambayo ni sawa sawa na $132* watu 54,000,000. Ongezeko la kipato cha serikali kwa 7,128,000,000 ndani ya miaka mitano sio mchezo, hata kama fedha hizo zinaweza zisiwe mikononi mwa wananchi.

Tanzania, Benin, Mauritius move up World Bank income rankings | Africanews
Tanzania GDP Per Capita 1988-2020

Kuwa nchi ya uchumi wa kati kunaweza ku maanisha ongezeko la riba kwenye mikopo lakini hivyo ndio vitu ambavyo tuna paswa kufikiri kuachana navyo.

Human development index(HDI) inahusisha vitu vitatu - life expectancy, elimu na GNI per capita. Nchi inayo pata score nzuri ya HDI inatakiwa kuwa na viashiria vizuri vya life expectancy, literacy rate na GNI per capita. HDI yenyewe inaweza isikupe picha halisi ya maendeleo na hali ya nchi.

Naku baliana na wewe unaposema kwamba kidogo kumekuwa na misplaced priorities kwenye serikali ya awamu ya tano lakini ni vyema kutambua kwamba hata kufikia hatua tuliyo fika lazima kazi nzito imefanyika. Tuji vunie kuwa nchi ya uchumi wa kati, tu sherehekee, mambo mazuri zaidi yana kuja.
 
Watanzania tunashukuru Rais Magufuli kwa kutupeleka Tanzania katika uchumi wa kati ndani ya miaka mitano tu

Tukimpa muda zaidi tunaweza kuipiku USA
naona ushatimiza wajibu wako wa kuwa wa kwaanza kbs kumsifu yesu wa Kangi Lugola...hongera!.
 
aise nimegain kitu! thx much bro!
umeona eeh...na watawala wetu ni ama nao hawaelewi kitu juu ya dhana nzima ya uchumi wa kati au wanapiga propaganda kuwaaminisha wananchi wasiodadisi kupata ukweli kujua kipi ni kipi.
 
Inategemea ni maendeleo gani kwa hiyo hela? Kwa tafsiri finyu ya maendeleo ndiyo hiyo uliyoitaja

Ukishakuwa na fedha ni lazima utakuwa na maendeleo, utamzidi nani na nani, that is another case.
 
Tatizo nilionalo hapa ni "Wivu wa Kimapenzi" na "upigaji" hivyo ulinzi wa Raisi uongezwe
 
Ni juzi tu Walikuwa wanatuambua watanzania ni maskini tunabangaiza hivyo lockdown itatuua,mwezi mmoja ghafla tumekuwa matajiri Kama laizer
 
Ukishakuwa na fedha ni lazima utakuwa na maendeleo, utamzidi nani na nani, that is another case.
Kwa tafsiri hiyo unapingana na wanaodai kuna maendeleo ya vitu na watu, au?
 
Asante kwa ufafanuzi
====
Mkuu naweza kupata utaratibu wa kitafiti uliotumiwa kupata takwimu hii ya 2.7 mil kuingia kwenye dimbwi la umaskini? Je. NBS yetu ilihusishwa kwenye utafiti huu?

NBS imehusishwa kutangaza uchumi wa Kati? Kama mnapenda Benki ya Dunia kuwatangaza kuwa Uchumi wa Kati, mpende pia wanaposema kuwa Watu masikini wameongezeka
 
Rushwa ipo ya kutisha, waulize madereva wa malori watakupa issue zote
 

Nikishaona mtu anazungumzia maendeleo/uchumi kisha matarajio yake yakawa ni mtu nachafukwa kabisa. Haya maendeleo ya kutegemea mtu mmoja ndio yalitukwamisha wakati wa Nyerere. Tulikwenda vizuri sana mwanzo, lakini mwisho wake tukaishia kuvaa viraka na kugeuka masikini wa kutupwa.

Unasema kuwa huko vijijini kuwa ukienda unapewa zawadi kadhaa kama mahindi nk. Hilo ni kweli kabisa, lakini kwenye utoaji wao, wanatoa kwakuwa wametosheka au wako nje ya poverty circle? Ninachoona huwa wanatoa kwa sababu ya upendo, na mazoea yetu waafrika ya kumkirimu mgeni. Hayo masoko anayowapigania ni kama kilichotokea kwenye korosho?

Wakati wa Nyerere tulikwama, maana watu kama akina Zito wenye mitazamo mbadala walionekana maadui, na mawazo ya mtu mmoja tu yakawa ndio sahihi! Na ww hapa naona unaelekea kulekule kuwa Magufuli yuko sahihi, na michango ya kina Zito ndio inamkwamisha Magufuli ambaye unajua atakutoa ulipo kwa mawazo yake sahihi! Hapa naona unaoongozwa na mahaba niue zaidi. Nimecheka sana hapo paragraph ya mwisho, kuwa kwa sasa kila mtu anapaswa kuelewa Magufuli anatupeleka wapi!
 
Kwa tafsiri hiyo unapingana na wanaodai kuna maendeleo ya vitu na watu, au?

Kaka niwe mkweli tu, hapa ninaona sentensi ya kiswahili inayoishia na alama ya kuuliza, lakini unataka kuniuliza nini, nimekwama. Huenda una swali au hoja nzuri, ila unapungukiwa na maneno sahihi ya kuyaweka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…