Watanzania wanaishi Nchi ya Uchumi wa Kati?

Watanzania wanaishi Nchi ya Uchumi wa Kati?

Zitto ahsante kwa maelezo maana tumejitahidi kuwaelimisha siku hizi mbili tunaonekana ni wapingaji

Nyumbani kwangu pia kuna mwanafunzi wa uchumi naye anafagili nikampa shule akakaa sawa inabidi nimuongezee na hizi notes ili aelewe uchumi wa dunia kabla hajajitosa kwenye fani chuokikuu nwakan

Uchumi wa kati

Binafsi kipato changu kilikuwa 264000 jumlisha faida ni 547000 lkn leo nina 223000 pekee

Biashara tatu zimeanguka kwa vyuma kukaza halafu unasema pato letu la mtanzania linakua!!? İtabidi uwe kichaa ili uelewe


Kama kikwete angeongoza awamu ya tano basi nchi ingekuwa inakaribia dola 2500 maana mzee wa msoga ile anaingia akakutana na ukame+ njaa ikaleta mgawo wa umeme uliosababisha mafuta kupanda kisha infalation ikalipuka na imports zikaongezeka na kuangusha value ya sh dhidi ya dola hivi vitu vyote magu hakukuvkkuta bali amekuta kila sehemu kuna mipango na hela standby ila kauli zake zikasababosha inflation kupanda kidogo pamoja na sh kuporomoka kwa wawekezaji kuondoa mitaji yao Tz na wengine kugoma kuja kuwekeza na wengine kuuchuna kuangalia huku fedha zikipumua( magu angekuwa na akili kama watu wa pwani ambao wao wanajua kutafuta hela na matumizi ya hela ambayo ni kuonekana unatumia mpaka watu wajue hela ipo
 
"wakati tumetumia Shilingi 1.8 Trilioni kwenye matumizi ya kununua Ndege 11 zinazotumiwa na 5% ya Watanzania, katika miaka 5 tumetumia Shilingi Trilioni Moja tu kwenye matumizi ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi zinazotegemewa na 67% ya Watanzania. Bajeti hii ya Kilimo ni 0.6% ya Bajeti yote ya Tanzania kwa miaka 5."

800 billion nawaza ingewafanyia mengi sana wakulima, wafugaji na wavuvi.
 
Kama ni uchumi wa kati through GDP Tanzania imefikia na kupita muda mrefu tu, tatizo ni kutumia vipimo vya mabeberu badala ya vyetu.

Mkulima wa chini analima si chini ya hector 2 on average na wengi wanazidisha hiyo. Kama ni mkulima mzuri yield yake ni 5 ton/h na anavuna on average two to three times annually, hizo bidhaa zake kwa bei ya soko zinaweza kabisa vuka dolla 1000.

Wakulima wengi wanatumia chakula chao wenyewe, wana mifugo yao wenyewe, wengine wanauza maziwa hizi ni expenditure and income ambazo hazipo reflected kwenye GDP kama vile ilivyo bidhaa za kwenye black market, wakati uchumi wa mkulima ni halali.

Serikali ya Tanzania inagawa thousands of hectors for free kila mwaka kwa wakulima wafugaji na wawekezaji ata kama kuna malipo ni way below market value (watu hao hao wakitumia ardhi waliopewa kuombea mikopo kama shamans) hizi initiative ni either sehemu ya government expenditure au investments in the GDP equation maana worth billions zinazalisha, and yet this economic activities is not reflected in the GDP.

Mapato ya wakulima wanayopata nje ushirika hakuna anaejua, savings za wakulima hakuna anaejua, huko mipakani si ajabu warundi, wanyarwanda, wazambia, wamalawi, wakenya wanaleta hela nyingi sana ndani ya nchi katika masoko ambayo income yake hatujui wala multiplier effect yake is not quantified in the economy.

Tukiweza rasimisha hii mifumo GDP ya Tanzania inaweza fika $2000 easily. Asilimia kubwa ya wafanyakazi wa serikali wa kima chini before tax annually they earn more than $2000 na awana chochote. Je mkulima mwenye asset ya ardhi na mifugo avuki kiwango icho hii nchi ni tajiri kushinda nyingi za africa.
 
Natak niulize tu,iv ikitokea hyo rate ikashuka na kufikia may b $1000 tutatolewa tena kweny hyo wanayoita uchumi wa kati?
 
Hata US yenye GDP ya $62,000 more than 2/3 of the population don’t earn that much ndio maana kwenye GDP kuna debate kubwa sana kwenye maswala ya income distribution maskini wa Qatar uwezi mfananisha na wa US in terms of quality of life and opportunities to life chances.

Vilevile uwezi mfananisha mkenya wa chini taifa ambalo kwa madai ya GDP ni tajiri kushinda Tanzania. Wakati mtanzania wa chini ambae maisha mjini yakimshinda anaweza rudi kijijini na kupata ardhi ya kulima wananchi wengi wa mataifa ya Africa waliotuzidi GDP hawana hizo option ukiwa maskini you are stuck there kilichobaki ukimbie nchi (ndio maana mtanzania utamuona alikuwa kwenye mtumbwi uliozama kwenye bahari ya Italy au kafungiwa kwenye camp ya ukimbizi Spain shida hizo hatuna za kufika Europe ikabidi upoteze maisha yako).

Nchi nyingi za africa ukiwa maskini huna namna tofauti na mtanzania sisi tunapokea wanyarwanda, warundi, wakongo na wamalawi kila siku wanaokuja Tanzania kama safe heaven lakini sisi atuendi huko hii nchi ni tajiri serikali inaweza tumia value ya usable land reserve as income na GDP ikapaa sio lazima tuige formula zao we got to value things in our contexts.
 
Hata US yenye GDP ya $62,000 more than 2/3 of the population don’t earn that much ndio maana kwenye GDP kitu kinachoangaliwa ni income distribution.

Uwezi mfananisha mkenya wa chini taifa ambalo kwa madai ya GDP ni tajiri kushinda Tanzania. Wakati mtanzania wa chini ambae maisha mjini yakimshinda anaweza rudi kijijini na kupata ardhi ya kulima wananchi wengi wa mataifa ya Africa waliotuzidi GDP hawana hizo option ukiwa maskini you are stuck huna namna tofauti na mtanzania hii nchi ni tajiri serikali inaweza tumia value ya usable land reserve as income na GDP ikapaa sio lazima tuige formula zao we got to value things in our contexts.
Tanzania ina rasilimali nyingi kuliko mataifa mengi Duniani na kama siyo CCM kuzitumia vibaya mda huu Tanzania ingekuwa ni Nchi tajiri kuliko South Africa German hata America na ungekuwa kwenye uchumi wa juu zaidi hata kuliko India china korea japan England, chini ya CCM pesa zote za maendeleo zinatumika kukandamiza demokrasia kuwahujumu kuwadhoofisha wapinzani.
 
Natak niulize tu,iv ikitokea hyo rate ikashuka na kufikia may b $1000 tutatolewa tena kweny hyo wanayoita uchumi wa kati?
Ndiko tunaenda tena mda si mrefu kwani Tanzania ilizoea misaada na ukiwa na uchumi wa kati misaada hupungua sana
 
Tanzania ina rasilimali nyingi kuliko mataifa mengi Duniani na kama siyo CCM kuzitumia vibaya mda huu Tanzania ingekuwa ni Nchi tajiri kuliko South Africa German hata America na ungekuwa kwenye uchumi wa juu zaidi hata kuliko India china korea japan England, chini ya CCM pesa zote za maendeleo zinatumika kukandamiza demokrasia kuwahujumu kuwadhoofisha wapinzani.
We are rich than the GDP wanayotuonyesha maisha ya maskini wa Tanzania ni far better kushinda maskini wa Nigeria na South Africa nchi zinazo ongoza kwa GDP africa huko ukiwa maskini utaji JJ hakuna ardhi.

Nyie tusifanye mchezo hizo nchi ukisikia kuna maskini mjomba ni kasheshe kuna documentary unaangalia kuna watu huko asia wanavizia ngozi za kuku zinazotupwa kwenye migahawa ndio wakale na familia zao mpaka mtu unasema duh. Wakati machinga akiamua kwenda kulima kesho ardhi anapata tatizo letu sisi ni lege lege tu.

wacha Magu awatie adabu kidogo watu wafanye kazi.
 
Watanzania wanaishi Nchi ya Uchumi wa Kati? - Zitto Kabwe



Tangu jana nimeona shamrashamra kubwa kuhusu kinachoitwa mafanikio ya Tanzania kuwa nchi ya Uchumi wa Kati. Kuingia Uchumi wa Kati ni hatua nzuri lakini inayohitaji ufafanuzi wa kiuongozi. Hatua hii ikifanyiwa propaganda itaonekana kuwa Serikali ya Awamu ya Tano wana uhaba wa mafanikio au hawajui wanachoshangilia. Ni muhimu sana kutambua kuwa kufikia hatua hii ni mchango wa awamu zote zilizotangulia na wananchi wa Tanzania na si matokeo ya awamu moja au miaka 5 tu.



Benki ya Dunia inaitambua nchi kuwa ya Uchumi wa Kati pale ambapo Pato la Wastani la Wananchi wake lipo kati ya Dola za Marekani 1,090 hadi 12,235 kwa mwaka. Katika kundi hili kuna Uchumi wa kati wa chini kabisa, Uchumi wa kati wa chini, Uchumi wa kati kati na Uchumi wa kati wa Juu. Kwa kimombo zinaitwa Lower Middle Income, Low Middle Income, Middle Income, Upper Middle Income.

Hiki kinachoshangiliwa hapa kwetu ni ile hatua ya kwanza, yaani tupo Getini kabisa. Pato la Wastani la kila Mtanzania limevuka Dola za Marekani 1,090 ( taarifa pia zinaonyesha kuwa Benki ya Dunia imeshusha vigezo na hivyo kupanua Goli ).



Hichi kipimo kinachotumika ni nini ?



Pato la Wastani (income per capita) ni jumla ya Pato la Taifa (GDP) ukiligawa kwa kila Mtanzania mpaka mtoto mdogo aliyezaliwa leo.

Yaani unachukua mapato ya Watanzania matajiri kama kina Bakhresa, Rostam Aziz, Mohamed Dewji na kadhalika, pamoja na Mapato ya vijana waendesha bodaboda, wakulima wa nyanya Ilula-Iringa na watu wasio na kipato kabisa kisha ugawe kwa kila Mtanzania kwa sawa. Kinachopatikana ndio wastani wa Pato la kila Mtu.

Ni hesabu za nadharia tu. Ni muhimu sana kuelewa nadharia hii kwamba wastani wa Pato la mtu ni Hesabu tu ya kujumlisha na kugawanya lakini sio uhalisia wa Pato la Mtu.



Pato la Taifa la Tanzania kwa bei za mwaka 2019 lilikuwa shilingi Trilioni 139. Mwaka 2019, Tanzania Bara ilikadiriwa kuwa na Watu Milioni 54 ambapo Pato la wastani la kila mtu lilifikia shilingi 2,577,967. Kiasi hicho cha pato la wastani kwa kila mtu kwa mwaka 2019 ni sawa na dola za Marekani 1,096 hivyo kuwa tumevuka kiwango cha Benki ya Dunia cha kuwa na Uchumi wa Kati.



Mwaka 2015, Pato la wastani la Mtanzania lilikuwa limefikia wastani Dola za Marekani 1,060. Kwa hiyo tulikuwa tumepungukiwa Dola za Marekani 30 tu ili kufikia ‘Lower Middle Income’ ambayo ndio tumeifikia sasa. Imetuchukua miaka 5 kuongeza $30 kwa kila Mtanzania kama wastani wa Pato lao.

Kwa wastani kila Mwaka Serikali imeweza kuongeza wastani wa Dola 6 tu kwa Mwaka kwa kila Mtanzania, yaani shilingi 14,000 tu kwa fedha za kitanzania.



Hatujafikia Lengo



Maendeleo ya Tanzania yanaongozwa na Mpango wa Maendeleo ya Taifa. Lengo letu kwenye Mpango huo ni “Tanzania kuwa nchi ya Uchumi wa kati wa wastani wa Pato la mtu kufika Dola za Marekani 3,000 ifikapo 2025. Kuvuka mpaka na kufikia hatua tuliyofikia ni hatua muhimu na ya kufurahisha lakini bado hatujafika safari yetu.



Kama imetuchukua miaka 5 kuongeza Dola 30, itatuchukua miaka mingapi kuongeza Dola 2,100? Hii maana yake ili kufikia Wastani wa Pato la Mtanzania la Dola za Marekani 3,000 kwa Mwaka, katika miaka 5 ijayo, tunapaswa kuongeza pato letu maradufu. Bado tuna mwendo mrefu kufikia lengo letu la kuwa na Uchumi wa Kati.



Nimeshangaa sana kuona Kuwa Baadhi yetu wakiwemo viongozi wanatamka kuwa Tanzania imefikia lengo la uchumi wa Kati miaka 5 kabla ya muda uliopangwa. Sio kweli kwani lengo tulilojiwekea ni Dola za Marekani angalau 3,000 kama Pato la Wastani la kila Mtu kwa Mwaka. Kusema kuwa tumefikia lengo ni dalili kuwa tuna uhaba wa mafanikio, tena uhaba mkubwa. Lakini pia kuna hatari kubwa ya kutoka kwenye mstari wa utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo kwa kujidanganya kuwa tayari tumefikia lengo.



Hata kama tungekuwa tumefikia lengo tulilojiwekea bado tunapaswa kupokea habari ya nyongeza ya wastani wa pato kwa kila mtu kwa tahadhari kubwa sana. Kuna faida na hasara ya kupanda daraja hili. Ukiwa ‘under developed low income country’, faida yake ni kupata misaada na mikopo yenye unafuu mkubwa. Ni sawa na mtoto mdogo anayepewa vyakula vya kupondwa pondwa. Hii inatoa ahueni kubwa kwa nchi kujijenga kiuchumi. Ukifaulu na kuingia kwenye kundi la uchumi wa kati hii mbeleko inaondoka. Sasa utapaswa kukopa mikopo ya kibiashara zaidi ambayo riba yake ni kubwa. Kwa lugha nyingine, mikopo inakuwa ghali na misaada inapungua sana. Yaani matarajio ni kuwa sasa umekuwa mkubwa ujitafunie. Mikopo ya Biashara ambayo tayari tumeanza kuchukua kiasi cha kuwa 34% ya Deni la Taifa. Benki ya Dunia imetoa mwanya wa Deni letu la Taifa kuwa kubwa na lenye gharama kubwa kulihudumia.



Faida ya kuwa uchumi wa kati ni kwamba ukomo wa Nchi wa kukopa katika masoko ya Fedha na mitaji inapanuka kuliko sasa. Hivyo unaweza kufanya mambo makubwa zaidi. Hasara yake ni gharama ya mikopo hiyo inaumiza uchumi ambapo mara nyingi sana unakuwa si imara sana kwa kuwa mara nyingi, uchumi huo hubebwa na takwimu tu ambazo zinaweza zisiakisi maisha halisi ya watu.



Mathalan, nchi zenye madini na mafuta, pato la Taifa linaweza kuonekana kubwa lakini vigezo vya hali ya maisha ya watu (Human Development Index) ikawa chini sana. Nchi nyingi za Low Middle Income zinalalamika sana kuomba zifikiriwe upya na mashirika ya kifedha. Baadhi ya Nchi zinaomba kwa Benki ya Dunia zishushwe daraja ili kukwepa hasara hizi. Sisi tunashangilia sana. Nadhani hatujui tunachoshangilia ni nini.



Kwa Nchi kama yetu ni muhimu sana Viongozi kuwa na uwezo mkubwa wa kutofautisha kati ya Uchumi wa Takwimu na Uchumi Halisi wa Wananchi. Uhalisia ni kuwa uchumi wa wananchi ni goi goi sana. Hali ya maisha ya wananchi imeanguka kutokana na kupungua kwa shughuli za uchumi za uzalishaji mali. Katika miaka 5 Serikali ya Awamu ya Tano imetumia Bajeti ya Shilingi Trilioni 162 sawa na wastani wa Dola za Marekani 1,173 ukizigawa kwa kila Mtanzania. Hata hivyo katika miaka hiyo 5 Pato la Mtanzania limeongezeka kwa Dola za Marekani 30 tu. Hii maana yake ni kuwa Matumizi yetu ya Bajeti hayaongezi shughuli za Uchumi za Wananchi wengi.



Kwa mfano, wakati tumetumia Shilingi 1.8 Trilioni kwenye matumizi ya kununua Ndege 11 zinazotumiwa na 5% ya Watanzania, katika miaka 5 tumetumia Shilingi Trilioni Moja tu kwenye matumizi ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi zinazotegemewa na 67% ya Watanzania. Bajeti hii ya Kilimo ni 0.6% ya Bajeti yote ya Tanzania kwa miaka 5.



Kutokana na Hali hiyo ya matumizi yasiyozingatia shughuli za uchumi za wananchi, taarifa ya Benki ya Dunia (Tanzania Economic Upadte number 11 ) inaonyesha kuwa jumla ya Watanzania 2.7 milioni wameingia kwenye dimbwi la umasikini Kati ya Mwaka 2017-2019. Unakuwaje Nchi ya Uchumi wa Kati wakati mamilioni ya Wananchi wanakuwa masikini kila mwaka ?



Nimalizie kwa kusema kuwa, kwa kasi tuliyokuwa nayo kwa miaka 5 iliyopita inatia mashaka ikiwa tutafika lengo letu la Uchumi wa Kati miaka 5 ijayo iwapo tukiendelea na maono haya, fikra hizi na matendo haya. Kuvuka mpaka ni hatua muhimu na ya kufurahisha lakini bado hatujafika safari yetu. Mpango wa Taifa unatutaka tufikia Pato la Kila Mtu la walau Dola za Marekani 3,000 kwa Mwaka ifikapo 2025.



Kufikia lengo hili inakuja na wajibu mkubwa kwa kila mmoja wetu kama Taifa na tunahitaji Uongozi na maono mapya. Tunahitaji Wananchi wawe na Raha na Furaha, wakifanya Kazi kwa bidii na kufurahia matunda ya jasho lao ( #KaziNaBata ).



Lindi, Tanzania

3/7/2020

Huu ndio ufafanuzi wa kiuchumi tunaouhitaji. Asante Bw. Zito.
 
We are rich than the GDP wanayotuonyesha maisha ya maskini wa Tanzania ni far better kushinda maskini wa Nigeria na South Africa nchi zinazo ongoza kwa GDP africa huko ukiwa maskini utaji JJ hakuna ardhi.

Nyie tusifanye mchezo hizo nchi ukisikia kuna maskini mjomba ni kasheshe kuna documentary unaangalia kuna watu huko asia wanavizia ngozi za kuku zinazotupwa kwenye migahawa ndio wakale na familia zao mpaka mtu unasema duh. Wakati machinga akiamua kwenda kulima kesho ardhi anapata tatizo letu sisi ni lege lege tu.

wacha Magu awatie adabu kidogo watu wafanye kazi.
Nchi zingine ulipo ndipo umefika ndipo utafia milele ukikwama huna pa kwenda, ni tofauti na Tanzania ambapo kuna Ardhi nyingi haina mtumiaji ukirudi kijijini maisha yanaendelea kama kawaida
 
Watanzania wanaishi Nchi ya Uchumi wa Kati? - Zitto Kabwe



Tangu jana nimeona shamrashamra kubwa kuhusu kinachoitwa mafanikio ya Tanzania kuwa nchi ya Uchumi wa Kati. Kuingia Uchumi wa Kati ni hatua nzuri lakini inayohitaji ufafanuzi wa kiuongozi. Hatua hii ikifanyiwa propaganda itaonekana kuwa Serikali ya Awamu ya Tano wana uhaba wa mafanikio au hawajui wanachoshangilia. Ni muhimu sana kutambua kuwa kufikia hatua hii ni mchango wa awamu zote zilizotangulia na wananchi wa Tanzania na si matokeo ya awamu moja au miaka 5 tu.



Benki ya Dunia inaitambua nchi kuwa ya Uchumi wa Kati pale ambapo Pato la Wastani la Wananchi wake lipo kati ya Dola za Marekani 1,090 hadi 12,235 kwa mwaka. Katika kundi hili kuna Uchumi wa kati wa chini kabisa, Uchumi wa kati wa chini, Uchumi wa kati kati na Uchumi wa kati wa Juu. Kwa kimombo zinaitwa Lower Middle Income, Low Middle Income, Middle Income, Upper Middle Income.

Hiki kinachoshangiliwa hapa kwetu ni ile hatua ya kwanza, yaani tupo Getini kabisa. Pato la Wastani la kila Mtanzania limevuka Dola za Marekani 1,090 ( taarifa pia zinaonyesha kuwa Benki ya Dunia imeshusha vigezo na hivyo kupanua Goli ).



Hichi kipimo kinachotumika ni nini ?



Pato la Wastani (income per capita) ni jumla ya Pato la Taifa (GDP) ukiligawa kwa kila Mtanzania mpaka mtoto mdogo aliyezaliwa leo.

Yaani unachukua mapato ya Watanzania matajiri kama kina Bakhresa, Rostam Aziz, Mohamed Dewji na kadhalika, pamoja na Mapato ya vijana waendesha bodaboda, wakulima wa nyanya Ilula-Iringa na watu wasio na kipato kabisa kisha ugawe kwa kila Mtanzania kwa sawa. Kinachopatikana ndio wastani wa Pato la kila Mtu.

Ni hesabu za nadharia tu. Ni muhimu sana kuelewa nadharia hii kwamba wastani wa Pato la mtu ni Hesabu tu ya kujumlisha na kugawanya lakini sio uhalisia wa Pato la Mtu.



Pato la Taifa la Tanzania kwa bei za mwaka 2019 lilikuwa shilingi Trilioni 139. Mwaka 2019, Tanzania Bara ilikadiriwa kuwa na Watu Milioni 54 ambapo Pato la wastani la kila mtu lilifikia shilingi 2,577,967. Kiasi hicho cha pato la wastani kwa kila mtu kwa mwaka 2019 ni sawa na dola za Marekani 1,096 hivyo kuwa tumevuka kiwango cha Benki ya Dunia cha kuwa na Uchumi wa Kati.



Mwaka 2015, Pato la wastani la Mtanzania lilikuwa limefikia wastani Dola za Marekani 1,060. Kwa hiyo tulikuwa tumepungukiwa Dola za Marekani 30 tu ili kufikia ‘Lower Middle Income’ ambayo ndio tumeifikia sasa. Imetuchukua miaka 5 kuongeza $30 kwa kila Mtanzania kama wastani wa Pato lao.

Kwa wastani kila Mwaka Serikali imeweza kuongeza wastani wa Dola 6 tu kwa Mwaka kwa kila Mtanzania, yaani shilingi 14,000 tu kwa fedha za kitanzania.



Hatujafikia Lengo



Maendeleo ya Tanzania yanaongozwa na Mpango wa Maendeleo ya Taifa. Lengo letu kwenye Mpango huo ni “Tanzania kuwa nchi ya Uchumi wa kati wa wastani wa Pato la mtu kufika Dola za Marekani 3,000 ifikapo 2025. Kuvuka mpaka na kufikia hatua tuliyofikia ni hatua muhimu na ya kufurahisha lakini bado hatujafika safari yetu.



Kama imetuchukua miaka 5 kuongeza Dola 30, itatuchukua miaka mingapi kuongeza Dola 2,100? Hii maana yake ili kufikia Wastani wa Pato la Mtanzania la Dola za Marekani 3,000 kwa Mwaka, katika miaka 5 ijayo, tunapaswa kuongeza pato letu maradufu. Bado tuna mwendo mrefu kufikia lengo letu la kuwa na Uchumi wa Kati.



Nimeshangaa sana kuona Kuwa Baadhi yetu wakiwemo viongozi wanatamka kuwa Tanzania imefikia lengo la uchumi wa Kati miaka 5 kabla ya muda uliopangwa. Sio kweli kwani lengo tulilojiwekea ni Dola za Marekani angalau 3,000 kama Pato la Wastani la kila Mtu kwa Mwaka. Kusema kuwa tumefikia lengo ni dalili kuwa tuna uhaba wa mafanikio, tena uhaba mkubwa. Lakini pia kuna hatari kubwa ya kutoka kwenye mstari wa utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo kwa kujidanganya kuwa tayari tumefikia lengo.



Hata kama tungekuwa tumefikia lengo tulilojiwekea bado tunapaswa kupokea habari ya nyongeza ya wastani wa pato kwa kila mtu kwa tahadhari kubwa sana. Kuna faida na hasara ya kupanda daraja hili. Ukiwa ‘under developed low income country’, faida yake ni kupata misaada na mikopo yenye unafuu mkubwa. Ni sawa na mtoto mdogo anayepewa vyakula vya kupondwa pondwa. Hii inatoa ahueni kubwa kwa nchi kujijenga kiuchumi. Ukifaulu na kuingia kwenye kundi la uchumi wa kati hii mbeleko inaondoka. Sasa utapaswa kukopa mikopo ya kibiashara zaidi ambayo riba yake ni kubwa. Kwa lugha nyingine, mikopo inakuwa ghali na misaada inapungua sana. Yaani matarajio ni kuwa sasa umekuwa mkubwa ujitafunie. Mikopo ya Biashara ambayo tayari tumeanza kuchukua kiasi cha kuwa 34% ya Deni la Taifa. Benki ya Dunia imetoa mwanya wa Deni letu la Taifa kuwa kubwa na lenye gharama kubwa kulihudumia.



Faida ya kuwa uchumi wa kati ni kwamba ukomo wa Nchi wa kukopa katika masoko ya Fedha na mitaji inapanuka kuliko sasa. Hivyo unaweza kufanya mambo makubwa zaidi. Hasara yake ni gharama ya mikopo hiyo inaumiza uchumi ambapo mara nyingi sana unakuwa si imara sana kwa kuwa mara nyingi, uchumi huo hubebwa na takwimu tu ambazo zinaweza zisiakisi maisha halisi ya watu.



Mathalan, nchi zenye madini na mafuta, pato la Taifa linaweza kuonekana kubwa lakini vigezo vya hali ya maisha ya watu (Human Development Index) ikawa chini sana. Nchi nyingi za Low Middle Income zinalalamika sana kuomba zifikiriwe upya na mashirika ya kifedha. Baadhi ya Nchi zinaomba kwa Benki ya Dunia zishushwe daraja ili kukwepa hasara hizi. Sisi tunashangilia sana. Nadhani hatujui tunachoshangilia ni nini.



Kwa Nchi kama yetu ni muhimu sana Viongozi kuwa na uwezo mkubwa wa kutofautisha kati ya Uchumi wa Takwimu na Uchumi Halisi wa Wananchi. Uhalisia ni kuwa uchumi wa wananchi ni goi goi sana. Hali ya maisha ya wananchi imeanguka kutokana na kupungua kwa shughuli za uchumi za uzalishaji mali. Katika miaka 5 Serikali ya Awamu ya Tano imetumia Bajeti ya Shilingi Trilioni 162 sawa na wastani wa Dola za Marekani 1,173 ukizigawa kwa kila Mtanzania. Hata hivyo katika miaka hiyo 5 Pato la Mtanzania limeongezeka kwa Dola za Marekani 30 tu. Hii maana yake ni kuwa Matumizi yetu ya Bajeti hayaongezi shughuli za Uchumi za Wananchi wengi.



Kwa mfano, wakati tumetumia Shilingi 1.8 Trilioni kwenye matumizi ya kununua Ndege 11 zinazotumiwa na 5% ya Watanzania, katika miaka 5 tumetumia Shilingi Trilioni Moja tu kwenye matumizi ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi zinazotegemewa na 67% ya Watanzania. Bajeti hii ya Kilimo ni 0.6% ya Bajeti yote ya Tanzania kwa miaka 5.



Kutokana na Hali hiyo ya matumizi yasiyozingatia shughuli za uchumi za wananchi, taarifa ya Benki ya Dunia (Tanzania Economic Upadte number 11 ) inaonyesha kuwa jumla ya Watanzania 2.7 milioni wameingia kwenye dimbwi la umasikini Kati ya Mwaka 2017-2019. Unakuwaje Nchi ya Uchumi wa Kati wakati mamilioni ya Wananchi wanakuwa masikini kila mwaka ?



Nimalizie kwa kusema kuwa, kwa kasi tuliyokuwa nayo kwa miaka 5 iliyopita inatia mashaka ikiwa tutafika lengo letu la Uchumi wa Kati miaka 5 ijayo iwapo tukiendelea na maono haya, fikra hizi na matendo haya. Kuvuka mpaka ni hatua muhimu na ya kufurahisha lakini bado hatujafika safari yetu. Mpango wa Taifa unatutaka tufikia Pato la Kila Mtu la walau Dola za Marekani 3,000 kwa Mwaka ifikapo 2025.



Kufikia lengo hili inakuja na wajibu mkubwa kwa kila mmoja wetu kama Taifa na tunahitaji Uongozi na maono mapya. Tunahitaji Wananchi wawe na Raha na Furaha, wakifanya Kazi kwa bidii na kufurahia matunda ya jasho lao ( #KaziNaBata ).



Lindi, Tanzania

3/7/2020
expand...
Kwa tafasiri nyingine ni kwamba ni vyema watanzania mkaendelea kuonyesha unyonge wenu, msifanye kazi kwa kujituma, msijenge miundombinu kwa ajili yenu ili world bank iwaonee huruma na kuwapa mikopo ya mashariti nafuu, ili wakubwa wa walete misaada kwa ajili ya maendeleo yenu. Eti huyu naye anastahili hata 1% ya kura zenu!!
 
Nchi zingine ulipo ndipo umefika ndipo utafia milele ukikwama huna pa kwenda, ni tofauti na Tanzania ambapo kuna Ardhi nyingi haina mtumiaji ukirudi kijijini maisha yanaendelea kama kawaida
Umeona kiongozi huo ndio ukweli wenyewe sisi atuwezi kuwa chini ya wakenya sijui wa S.A kama tungekuwa na upimaji wetu wa GDP.

Watanzania wana privilege kubwa sana. Halafu mijitu aitaki kuchangamkia fursa ndio maana mzee baba anasema hapa kazi tu na asiefanya kazi asile no charity under Magu he is a conservative at heart.

Magu anachofanya ni kuwajengea fursa wakulima ambazo watu awaelewi kwanza kwa kujaribu kuhakikisha wanapata access ya masoko (you know what they say; built it and they will come).

Miaka kumi tu nyuma mpunga wa Songea, mahindi Rukwa, mananasi Geita to name a few of farm produce hizo bidhaa zilikuwa zina haribika kisa wafanya biashara kufuata bidhaa hizo sehemu kutokana na miundombinu walikuwa wanaoshida.

Hizi fujo za Magufuli za miundombinu ni kutaka kuwapa hao watu access ya masoko na kuwapa wafanyabiashara food for thought unaweza fika sehemu yoyote Tanzania. Hizo faida inaweza zisionekane leo but hila ni kazi ambayo lazima ifanyike na hakuna aliyekuwa yupo tayari au mtu sahihi zaidi ya Magu.

Najua wewe sio shabiki wa Magufuli vile and to be honest ana mapungufu yake but he is a genius I am telling you sio kwa faida yangu na wewe hila kwa Tanzania ya baadae anachofanya akimaliza kujenga mazingira sahihi uchumi wa Tanzania utapaa watu watashangaa baada ya miaka 10-15 if not soon.

Issue ni Tanzania ya kesho sio Magu (personal issues watu waweke pembeni) miaka 5 mingine ya Magu will be something else he has tricks under his sleeves.
 
Mkuu ni kweli pesa imeongezeka thamani Kwasababu Rais Magufuli amefuta rushwa, amefuta ufisadi, amekomesha madawa ya kulevy,amekomesha majangili na majizi

Kama ulikuwepo kwenye hiyo cheni lazima pesa ikupige chenga uone maisha magumu

Makundi mengine yanafurahia maisha Kwasababu hawajaathiriwa na kitu chochote, ukizingatia Rais Magufuli anawatetea sana watu wa kipato cha chini
Mkuu watu wanakuona katuni hapa JF

Huwezi kujenga hoja ,wewe umekaa kushabikia vyama tu ccm au chadema

Wetu wengi humu JF ni wasomi na wataalamu


Punguza umbea na ushabiki,kama hujasoma uchumi kaa kimya
 
Sasa unakuja kulialia huku jf si upande tu ndege Tena mpaka Kwenye ofisi za hao WB walioitangaza kuwa Imefika Uchumi wa Kati.

Sasa unatuumiza vichwa Sisi ambao hatukuhusika na kutangaza huo Uchumi..

Kama umeishiwa pesa ya karamu na karatasi ya kuandikia barua world bank + nauli ya ndege we anzisha tu Uzi wa kukuchangia uende Tena.

Msaliti mkubwa wewe utaendelea kuweweseka na maombi yako ya mabaya juu ya taifa hili kamwe hayatafua dafu.

Proud to be Tanzanian[emoji1241][emoji1241][emoji1241]
Povu la nini
Mkuu elimu yako ni ndogo kwenye uchumi
.
Ahaaa umesoma na zitto udsm lakini yeye ana Firsr clasa wewe una Pass
Mmmh
 
Watetezi wa CCM mitandaoni wengi hawajui kusoma vizuri wao kazi yao ni kukariri zidumu fikra za mwenyekiti wa CCM tu
Huwa nawaona kule youtube, kwakweli youtube wameiteka lakini huku jf wanajificha wapi? Wengi wao hawana hoja zaidi ya matusi, chuki na kejeli.
 
Tatizo la Upinzani wa nchi hii huwa hakubali lolote kwao kila Kitu ni kukosoa tu!!

Zitto Kabwe ndio ulibaki mpinzani Pekee niliekukubali Sana Ila nilikuona mtu ambae huna jema siku ya kuvunjwa Bunge la TZ kwà mwaka 2015-2020, Ile siku unahojiwa ukadai et Rais wa awamu ya 3 na 4 walihutubia Bunge Mara 3 Hadi 4 ndani ya mhula mmoja Sasa amekuja Rais awamu ya 5 kahutubia Mara mbili tu na ukasisitiza et hiyo ni ishara kuwa mihimili hiyo miwili haina mahusiano mazuri kwà awamu hii, wakati hapo kabla niwewe ndio ulikuwa unatuaibisha kuwa Bunge halina maamuzi linatekeleza Yale yote yanayoamuliwa na Rais Mara Mhimili wa bunge upo chini ya Rais Sasa Mimi nikawa nahoji hivi Kama hiyo mihimili miwili haina mahusiano mazuri yaan haisikilizani iweje leo Sasa Rais aingilie majukumu ya Bunge na Bunge hilohilo unalolalamikia halina mahusiano mazuri na Rais litii maagizo Toka kwà Rais!!

Kimsingi hata hapo tulipofikia sio HABA tushukuru kwà hiki kidogo tulichonacho!!!
Acha taarabu,Jibu mambo ya uchumi haya
.unadhani mambo ya Forced labour haya
 
Mkuu ni kweli pesa imeongezeka thamani Kwasababu Rais Magufuli amefuta rushwa, amefuta ufisadi, amekomesha madawa ya kulevy,amekomesha majangili na majizi

Kama ulikuwepo kwenye hiyo cheni lazima pesa ikupige chenga uone maisha magumu

Makundi mengine yanafurahia maisha Kwasababu hawajaathiriwa na kitu chochote, ukizingatia Rais Magufuli anawatetea sana watu wa kipato cha chini
Kwani huwezi fikiria lolote?
 
Hivyo ukiwa kama kiongozi na mwana uchumi unashauri serikali ichukue hatua zipi ili kufikia lengo hiyo 2025..??
Wahusika huwa hawapo tayari kupokea mawazo yenye tija kama hayo, wanataka kile mtu awapigie makofi na kuwaimbia pambio za sifa.
 
Watanzania wanaishi Nchi ya Uchumi wa Kati? - Zitto Kabwe



Tangu jana nimeona shamrashamra kubwa kuhusu kinachoitwa mafanikio ya Tanzania kuwa nchi ya Uchumi wa Kati. Kuingia Uchumi wa Kati ni hatua nzuri lakini inayohitaji ufafanuzi wa kiuongozi. Hatua hii ikifanyiwa propaganda itaonekana kuwa Serikali ya Awamu ya Tano wana uhaba wa mafanikio au hawajui wanachoshangilia. Ni muhimu sana kutambua kuwa kufikia hatua hii ni mchango wa awamu zote zilizotangulia na wananchi wa Tanzania na si matokeo ya awamu moja au miaka 5 tu.



Benki ya Dunia inaitambua nchi kuwa ya Uchumi wa Kati pale ambapo Pato la Wastani la Wananchi wake lipo kati ya Dola za Marekani 1,090 hadi 12,235 kwa mwaka. Katika kundi hili kuna Uchumi wa kati wa chini kabisa, Uchumi wa kati wa chini, Uchumi wa kati kati na Uchumi wa kati wa Juu. Kwa kimombo zinaitwa Lower Middle Income, Low Middle Income, Middle Income, Upper Middle Income.

Hiki kinachoshangiliwa hapa kwetu ni ile hatua ya kwanza, yaani tupo Getini kabisa. Pato la Wastani la kila Mtanzania limevuka Dola za Marekani 1,090 ( taarifa pia zinaonyesha kuwa Benki ya Dunia imeshusha vigezo na hivyo kupanua Goli ).



Hichi kipimo kinachotumika ni nini ?



Pato la Wastani (income per capita) ni jumla ya Pato la Taifa (GDP) ukiligawa kwa kila Mtanzania mpaka mtoto mdogo aliyezaliwa leo.

Yaani unachukua mapato ya Watanzania matajiri kama kina Bakhresa, Rostam Aziz, Mohamed Dewji na kadhalika, pamoja na Mapato ya vijana waendesha bodaboda, wakulima wa nyanya Ilula-Iringa na watu wasio na kipato kabisa kisha ugawe kwa kila Mtanzania kwa sawa. Kinachopatikana ndio wastani wa Pato la kila Mtu.

Ni hesabu za nadharia tu. Ni muhimu sana kuelewa nadharia hii kwamba wastani wa Pato la mtu ni Hesabu tu ya kujumlisha na kugawanya lakini sio uhalisia wa Pato la Mtu.



Pato la Taifa la Tanzania kwa bei za mwaka 2019 lilikuwa shilingi Trilioni 139. Mwaka 2019, Tanzania Bara ilikadiriwa kuwa na Watu Milioni 54 ambapo Pato la wastani la kila mtu lilifikia shilingi 2,577,967. Kiasi hicho cha pato la wastani kwa kila mtu kwa mwaka 2019 ni sawa na dola za Marekani 1,096 hivyo kuwa tumevuka kiwango cha Benki ya Dunia cha kuwa na Uchumi wa Kati.



Mwaka 2015, Pato la wastani la Mtanzania lilikuwa limefikia wastani Dola za Marekani 1,060. Kwa hiyo tulikuwa tumepungukiwa Dola za Marekani 30 tu ili kufikia ‘Lower Middle Income’ ambayo ndio tumeifikia sasa. Imetuchukua miaka 5 kuongeza $30 kwa kila Mtanzania kama wastani wa Pato lao.

Kwa wastani kila Mwaka Serikali imeweza kuongeza wastani wa Dola 6 tu kwa Mwaka kwa kila Mtanzania, yaani shilingi 14,000 tu kwa fedha za kitanzania.



Hatujafikia Lengo



Maendeleo ya Tanzania yanaongozwa na Mpango wa Maendeleo ya Taifa. Lengo letu kwenye Mpango huo ni “Tanzania kuwa nchi ya Uchumi wa kati wa wastani wa Pato la mtu kufika Dola za Marekani 3,000 ifikapo 2025. Kuvuka mpaka na kufikia hatua tuliyofikia ni hatua muhimu na ya kufurahisha lakini bado hatujafika safari yetu.



Kama imetuchukua miaka 5 kuongeza Dola 30, itatuchukua miaka mingapi kuongeza Dola 2,100? Hii maana yake ili kufikia Wastani wa Pato la Mtanzania la Dola za Marekani 3,000 kwa Mwaka, katika miaka 5 ijayo, tunapaswa kuongeza pato letu maradufu. Bado tuna mwendo mrefu kufikia lengo letu la kuwa na Uchumi wa Kati.



Nimeshangaa sana kuona Kuwa Baadhi yetu wakiwemo viongozi wanatamka kuwa Tanzania imefikia lengo la uchumi wa Kati miaka 5 kabla ya muda uliopangwa. Sio kweli kwani lengo tulilojiwekea ni Dola za Marekani angalau 3,000 kama Pato la Wastani la kila Mtu kwa Mwaka. Kusema kuwa tumefikia lengo ni dalili kuwa tuna uhaba wa mafanikio, tena uhaba mkubwa. Lakini pia kuna hatari kubwa ya kutoka kwenye mstari wa utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo kwa kujidanganya kuwa tayari tumefikia lengo.



Hata kama tungekuwa tumefikia lengo tulilojiwekea bado tunapaswa kupokea habari ya nyongeza ya wastani wa pato kwa kila mtu kwa tahadhari kubwa sana. Kuna faida na hasara ya kupanda daraja hili. Ukiwa ‘under developed low income country’, faida yake ni kupata misaada na mikopo yenye unafuu mkubwa. Ni sawa na mtoto mdogo anayepewa vyakula vya kupondwa pondwa. Hii inatoa ahueni kubwa kwa nchi kujijenga kiuchumi. Ukifaulu na kuingia kwenye kundi la uchumi wa kati hii mbeleko inaondoka. Sasa utapaswa kukopa mikopo ya kibiashara zaidi ambayo riba yake ni kubwa. Kwa lugha nyingine, mikopo inakuwa ghali na misaada inapungua sana. Yaani matarajio ni kuwa sasa umekuwa mkubwa ujitafunie. Mikopo ya Biashara ambayo tayari tumeanza kuchukua kiasi cha kuwa 34% ya Deni la Taifa. Benki ya Dunia imetoa mwanya wa Deni letu la Taifa kuwa kubwa na lenye gharama kubwa kulihudumia.



Faida ya kuwa uchumi wa kati ni kwamba ukomo wa Nchi wa kukopa katika masoko ya Fedha na mitaji inapanuka kuliko sasa. Hivyo unaweza kufanya mambo makubwa zaidi. Hasara yake ni gharama ya mikopo hiyo inaumiza uchumi ambapo mara nyingi sana unakuwa si imara sana kwa kuwa mara nyingi, uchumi huo hubebwa na takwimu tu ambazo zinaweza zisiakisi maisha halisi ya watu.



Mathalan, nchi zenye madini na mafuta, pato la Taifa linaweza kuonekana kubwa lakini vigezo vya hali ya maisha ya watu (Human Development Index) ikawa chini sana. Nchi nyingi za Low Middle Income zinalalamika sana kuomba zifikiriwe upya na mashirika ya kifedha. Baadhi ya Nchi zinaomba kwa Benki ya Dunia zishushwe daraja ili kukwepa hasara hizi. Sisi tunashangilia sana. Nadhani hatujui tunachoshangilia ni nini.



Kwa Nchi kama yetu ni muhimu sana Viongozi kuwa na uwezo mkubwa wa kutofautisha kati ya Uchumi wa Takwimu na Uchumi Halisi wa Wananchi. Uhalisia ni kuwa uchumi wa wananchi ni goi goi sana. Hali ya maisha ya wananchi imeanguka kutokana na kupungua kwa shughuli za uchumi za uzalishaji mali. Katika miaka 5 Serikali ya Awamu ya Tano imetumia Bajeti ya Shilingi Trilioni 162 sawa na wastani wa Dola za Marekani 1,173 ukizigawa kwa kila Mtanzania. Hata hivyo katika miaka hiyo 5 Pato la Mtanzania limeongezeka kwa Dola za Marekani 30 tu. Hii maana yake ni kuwa Matumizi yetu ya Bajeti hayaongezi shughuli za Uchumi za Wananchi wengi.



Kwa mfano, wakati tumetumia Shilingi 1.8 Trilioni kwenye matumizi ya kununua Ndege 11 zinazotumiwa na 5% ya Watanzania, katika miaka 5 tumetumia Shilingi Trilioni Moja tu kwenye matumizi ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi zinazotegemewa na 67% ya Watanzania. Bajeti hii ya Kilimo ni 0.6% ya Bajeti yote ya Tanzania kwa miaka 5.



Kutokana na Hali hiyo ya matumizi yasiyozingatia shughuli za uchumi za wananchi, taarifa ya Benki ya Dunia (Tanzania Economic Upadte number 11 ) inaonyesha kuwa jumla ya Watanzania 2.7 milioni wameingia kwenye dimbwi la umasikini Kati ya Mwaka 2017-2019. Unakuwaje Nchi ya Uchumi wa Kati wakati mamilioni ya Wananchi wanakuwa masikini kila mwaka ?



Nimalizie kwa kusema kuwa, kwa kasi tuliyokuwa nayo kwa miaka 5 iliyopita inatia mashaka ikiwa tutafika lengo letu la Uchumi wa Kati miaka 5 ijayo iwapo tukiendelea na maono haya, fikra hizi na matendo haya. Kuvuka mpaka ni hatua muhimu na ya kufurahisha lakini bado hatujafika safari yetu. Mpango wa Taifa unatutaka tufikia Pato la Kila Mtu la walau Dola za Marekani 3,000 kwa Mwaka ifikapo 2025.



Kufikia lengo hili inakuja na wajibu mkubwa kwa kila mmoja wetu kama Taifa na tunahitaji Uongozi na maono mapya. Tunahitaji Wananchi wawe na Raha na Furaha, wakifanya Kazi kwa bidii na kufurahia matunda ya jasho lao ( #KaziNaBata ).



Lindi, Tanzania

3/7/2020
political rubbish
 
Back
Top Bottom