Pre GE2025 ‘Watanzania wanyonge’ wataka Paul Makonda agombee na kupewa Urais 2030

Pre GE2025 ‘Watanzania wanyonge’ wataka Paul Makonda agombee na kupewa Urais 2030

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Nani kakudanganya?

You niggas are so delusional aisee

Hebu come back to reality,stop dreaming

Mngekua mmeshausambaratisha usingeleta huu uzi to begin with

Upinzani upo ndio maana upo hapa kusukuma uzi za namna hii,otherwise ungekua umekaa na popcorn zako unacheck movie maana hakuna tena upinzani
Hakuna upinzani nchi hii zaidi ya kuwa na magenge ya wasaka tonge wanaohangaikia matumbo yao tu.
 
Hakuna upinzani nchi hii zaidi ya kuwa na magenge ya wasaka tonge wanaohangaikia matumbo yao tu.
Usingekuwepo hata hiyo sentensi uliyotoa usingeitoa,ungekua umekaa baharini unapunga upepo bila stress

Upo hapa full stressed coz unajua upinzani upo well and alive!
 
Ndugu zangu Watanzania,

Na ili kazi nzuri anazofanya Mheshimiwa Rais ziwe na muendelezo mzuri na kuendelea kwa kasi hii hii, basi ni vema mwaka 2030 kumpa ushirikiano na kumuunga mkono Paul Makonda kushika nchi.

Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Naunga mkono hoja, tena mimi nimempangia 2025 Baada ya Magufuli, 2025 Makonda atatufaa sana, kwasababu ana uthubutu kuliko hata JPM!. Apunguze... hili litawezekana tuu, endapo sauti HII
ni ya kweli ya kwake YEYE!.
P
 
Ndugu zangu Watanzania,

Uchapakazi wa Mheshimiwa Makonda, ujasiri wake, uzalendo wake, kujitoa kwake kutetea wanyonge, ushupavu na umadhubuti wake umewakosha na kukonga mioyo ya watanzania mitaani .ambao kwa sasa wana kiu ya kutaka kuona Paul Makonda anagombea urais na kuchaguliwa kwa kishindo kumpokea kijiti cha urais Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hasssan mwaka 2030.

Sauti zinaendelea kupazwa na wananchi kupitia mitandao ya kijamii,vyombo vya habari, sauti za wananchi vilingeni na magengeni kuona kuwa siku moja Taifa hili linawekwa mikononi mwa Paul Makonda kama mkuu wa nchi, kiongozi wa serikali na Amiri jeshi mkuu wetu. Kutokana na kuona namna anavyo chapa kazi bila kuchoka wala kupumzika wala kupata hata muda wa kula chakula cha mchana.muda wote yupo kazini kuwasikiliza wananchi kwa unyenyekevu na upole wa hali ya juu sana na kuchukua hatua papo kwa papo kwa kuwaita watu wa serikali kutoa majibu.

Nami naunga mkono kuwa ili kazi nzuri anazofanya Mheshimiwa Rais ziwe na muendelezo mzuri na kuendelea kwa kasi hii hii, basi ni vema mwaka 2030 kumpa ushirikiano na kumuunga mkono Paul Makonda kushika nchi. Kwa hakika ndugu zangu nawaambieni ya kuwa kwa huyu Mwamba na jasiri kuwahi kutokea kusini mwa jangwa la sahara hakika nchi itakwenda mchaka mchaka katika maendeleo. Maendeleo yatakimbia kwa kasi na kukimbizwa kama mashindano ya mbio ndefu, watumishi wa umma watachapa kazi kama nyuki,cheo kitakuwa dhamana na wananchi watabaki mabosi huku kila mtu akifurahia kuzaliwa Tanzania kama ilivyo sasa chini ya uongozi wa Rais Wetu mpendwa kipenzi cha watanzania mama Samia Suluhu Hasssan.

Jiulize kama leo ni Mwenezi wa chama anaitetemesha na kuiteka nchi kiasi hiki kwa uchapa kazi wake .vipi Tukimpa Urais ili aendeleze pale alipoishia mama yetu mpendwa na mchapa kazi aliyetukuka? Kwa sababu ni lazima Anapotoka mchapa kazi kama mama Samia tukakikishe Nchi inakwenda katika mikono ya mchapa kazi na jasiri aina ya Makonda ili kazi zisisimake na kusua sua..

Tanzania inamhitaji sana Mheshimiwa Paul Makonda 2030 kuliko wakati mwingine wowote ule. Ndio maana jana nilisema alindwe kwa nguvu zote na gharama zozote zile ili aje kutupatia matokeo makubwa na Chanya Watanzania. Tuendelee kumuombea afya njema tu.

Ni lazima Makonda aandaliwe na kuwekwa tayari kwa nafasi za juu maana amejaliwa kipawa na Kalama ya uongozi kutoka kwa Mwenyezi Mungu.nyote mnajionea namna kifua chake kilivyojaa ujasiri wa hali ya juu. Angalieni namna mchaka mchaka unavyopigwa huko kwenye ziara zake,angalieni namna watu nyuso zao zilivyo na tabasamu zimuonapo Paul Makonda ,angalieni namna watu wanalivyo na imani na matumaini na Mheshimiwa Makonda. Hapo hata mwaka mmoja tu hajamaliza ofisini.

vipi akipewa miaka kumi kama Rais wa nchi? Mnafikiri Tanzania hiii ya Rais wetu mpendwa Mama Samia itakuwa wapi? Ikumbukwe kwanza atakuta kazi kubwa imefanywa na Mheshimiwa Rais mama Samia,Ambapo atakuta umeme ni wa uhakika baada ya kuwa tayari bwawa la mwalimu Nyerere limeshakamilika.mnafikiri nani ataipita kiuchumi Tanzania Hii yenye rutuba nzuri ya kutosha na yenye kukubali kila aina ya mazao,yenye mlima mrefu barani Afrika,yenye mbuga za wanyama wa kila aina,yenye madini ya Tanzanite yanayopatikana Tanzania pekee, yenye madini ya kutosha karibu kila ukanda, yenye rasilimali watu ya kutosha,yenye mito,maziwa na bahari kwaajili ya kilimo cha umwagiliaji na hata usafiri wa majini.

Yenye bandari kila kanda,yenye faida ya kuzungukwa na nchi zaidi ya saba ambazo zinategemea kupitishia mizigo yao katika bandari yetu,yenye misitu mingi kwaajili ya kutengenezea vitu vya aina mbalimbali badala ya kuagiza nje na hivyo kupunguza hazina ya pesa za kigeni.mnafikiri Tanzania ya kijana jasiri na imara mwamba Paul Makonda itakuwaje?

Mnafikiri Tanzania ya Makonda yenye utajiri wa makaa ya mawe ya kutosha ,vivutio vya utalii ,Kimondo cha pili kwa ukubwa Duniani baada ya kile cha Marekani, hamuoni Tanzania hiyo itatiririsha maziwa na asali katika mabomba yake kwa kila kaya? Kumbuka kwa sasa anacho fanya Rais Samia anaweka mazinginra mazuri ya kiuchumi ambapo ni wakati huo wa Urais wa Makonda miradi ya kimkakati itakuwa imeanza kutoa na kuleta faida.

Tujiandae kumpa nchi Mheshimiwa Paul Makonda mwaka huo wa 2030 ili Dunia ikae chini na kuishangaa Tanzania ikipaa kama ndege vita kiuchumi, na kupokea wageni watakao kuwa wanapanga foleni na kupishana pale airport wakija kuitembelea Tanzania na kujifunza.

Paul Makonda chapa kazi sana kaka yangu.mama amekuamini na anaimani na matarajio makubwa sana kutoka kwako.chama tunakuamini sana na tuna matarajio makubwa sana kutoka kwako.chapa kazi na kila upitapo waambie wananchi na watanzania mambo makubwa aliyoyafanya mama yetu na Rais wetu Mama Samia.waeleze mabillioni aliyoyapeleka Katika maeneo yao.waambie kila mwezi mama yao na Rais wao anatoa zaidi ya Billion 33 ili watoto wao wasome bure.

Waambie Rais wao ametiririsha zaidi ya Trilioni sita katika Secta ya Afya pekee,waambie Rais wao ameongeza bajeti ya kilimo kufikia Billion mia tisa tisini ili wakulima wapate pembejeo kwa bei nzuri,waambie mama yao ameagiza zaidi ya tani laki moja za sukari kuja kuingiza sokoni, waambie mama yao anawapa mikopo wanafunzi wote wa elimu ya juu wenye sifa bila ubaguzi. Waambie mama yao ametoa maelfu ya ajira kwa vijana na muda siyo mrefu anakwenda kumwaga mitaani zaidi ya elfu ishirini na tatu katika Secta ya Elimu na afya.

Waambie watumishi wa umma wachape kazi maana mama yao yupo pamoja nao na ataendelea kuwaongeza misharaha na kuwalipa madai yao, lakini nao wahakikishe kuwa wanachapa kazi kwa bidii na uadilifu wa hali ya juu na wasifanye kazi kwa mazoea. Waambie mama amefanya mengi ambayo huwezi kumaliza kuyataja.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Yaani tuko kwenye dunia ya ubepari, halafu wewe na ndugu yako Bashite bado mnaongelea habari za unyonge/wanyonge!! Nyinyi kweli hamna akili.
 
MLETA UZI ANA JUHUDI.....
ANAJITAHIDI SANA KUKIDHI MATAKWA...
 
Nilitaka nishangae,,,,bashite apige tu mamikutano yote yale bila kuwa agenda zake flani flani za siri za kuwalipa watu wampigie chapuo chini chini ili achukue form mwakani, ningeshangaa sana
 
Nilitaka nishangae,,,,bashite apige tu mamikutano yote yale bila kuwa agenda zake flani flani za siri za kuwalipa watu wampigie chapuo chini chini ili achukue form mwakani, ningeshangaa sana
Mheshimiwa Makonda halipo watu wala kutoa pesa kwa ajili ya kufanya chochote kile kwa ajili yake .bali ni kutokana na kazi njema na uchapa kazi wake uliotukuka ndio umegusa mioyo ya mamilioni ya watanzania mpaka sasa kuwa na kiu ya kutaka kuongozwa na yeye kama Rais wetu mwaka 2030. Mheshimiwa Makonda amekonga na kugusa mioyo ya watanzania wanyonge ambao wanamuona Mheshimiwa kama mtetezi na sauti yao
 
Yaani tuko kwenye dunia ya ubepari, halafu wewe na ndugu yako Bashite bado mnaongelea habari za unyonge/wanyonge!! Nyinyi kweli hamna akili.
Kasome katiba yetu ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania kurasa za mwanzo kabisa ufahamu inafuata mfumo upi .
 
Huo utafiti wa hao watu mamilioni uliufanyia wapi na kwa muda gani? Acha kuandika kishabiki boss. Kama ni hisia zako binafsi na una hoja za msingi za kwa nin unataka makonda agombee uraisi basi ziweke hapa na sisi tuzisome na tuzipime....kama zina mashiko basi tuta kuunga mkono,

Ila sio kuja tu mbio mbio eti mamilioni "wanataka", .....kaka humu ndani kuna watu wanajielewa na wana uelewa wa mambo. Nenda kwa step basi.
 
Kasome katiba yetu ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania kurasa za mwanzo kabisa ufahamu inafuata mfumo upi .
Hivi kumbe kuna Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!! Mimi siku zote ninachofahamu kama nchi, tuna Katiba ya CCM ya mwaka 1977!

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ilitakiwa iwe ni ile tuliyoipendekeza sisi wananchi mwanzoni mwaka 2010! Na kufanikiwa kupata Rasimu yake, ambayo kwa makusudi kabisa mkaamua kuifanyia uhuni. Na siyo hiyo takataka iliyoandaliwa na makada wachache wa chama chenu, halafu mnaiita eti ni Katiba!
 
Back
Top Bottom