Watanzania watia moto vifaranga wengine 5,000 kutoka Kenya



Vifaranaga 5000 vilivyokamatwa kutoka nchini Kenya vikiingizwa nchini kinyemela vimeteketezwa kwa moto ili kuepusha tishio la kuwepo kwa ugonjwa wa mafua ya ndege.

Vifaranga hivyo vimekamatwa katika eneo la mpakani mwa Kenya na Tanzania, Namanga ambapo baada ya kukamatwa vifaranga wa kuku wa mayai 5000 wenye thamani ya Tsh 11,500,000 na Trei 416 zenye mayai, yenye thamani ya 3,120,000/ kwa pamoja vimeteketezwa kwa moto kwa kuzingatia haki za wanyama (Animal welfare) ambapo kabla ya kuteketezwa mifugo hiyo ililazwa kwa kutumia dawa aina ya Farmaldehyde na kuhakikisha wamekufa kabla ya kuchomwa.

Hata hivyo, Mayai hayo pamoja na vifaranga vimekamatwa vikiingizwa nchini kinyume na sheria, ambapo kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la chakula (FAO) ya mwezi Desemba ilitoa tahadhari kuwa nchi ya Tanzania pamoja na nchi jirani Kenya na Uganda na nchi nyingine za Afrika ziko hatarini kuambukizwa mafua ya ndege.
 
Inaonyesha ni kwa jinsi gani ujinga umekujaa kichwani mwako..
 
Kwahiyo wewe unasemaje, serikali inafanya vile inavyopenda, wewe kama hupendi ni bora uhame nchi, acha kutujazia choo bure hapa nchini.
Povu la nini mzee? Serikali inayoongozwa na wajinga wajinga wa design yako haitaleta maendeleo yeyote..
 
Undugu wetu jamani tunaelekea wapi?
 
Tumechoma tena ili tuone kama mna la kufanya p*mbavu zenu.

Uchome mali ya Mtanzania mwenzako halafu utambie Wakenya, kweli nyie Nyerere aliwaharibu na itachukua muda mrefu sana kuja kufunguka kiakili, bado mpo kwenye giza sana.
 
Povu la nini mzee? Serikali inayoongozwa na wajinga wajinga wa design yako haitaleta maendeleo yeyote..
Nenda huko kwa wenye akili kama wewe ukaishi, wewe ni mass with weight na unajaza nafasi tu hapa nchini, sana sana unajaza vyoo tu.
 
Hawa wakenya huwa ninawashangaa sana, vifaranga vilipochomwa mara ya kwanza, wao ndiyo waliopiga kelele kulaumu kwamba Tanzania ina nia mbaya na Kenya, leo hii wanasema hawahusiki kwa sababu vifaranga ni vya mtanzania, sasa mbona mlilalamika ile mara ya kwanza kwani vile havikuwa vya mtanzania?, au mlitaka kutingisha kibiriti?. HATUJARIBIWI.
 
Wewe endelea tu kusema " hatujaribiwi" na nyinyi ni ldc
 
Yaani serikali yako inakuulia hata mende? Wonderful!

Hawa jamaa wana matatizo makubwa kwa kweli, yaani hapo wamemrudisha nyuma mjasiria Mtanzania na kumpeleka hasara kubwa, halafu wanatutambia sisi Wakenya wakati Mkenya keshatia hela yake mfukoni. Ukishanunua kutoka kwangu na kuvuka mpaka, mtajuana wenyewe huko huko, mimi kuanzia hapo nawaza mengine.

Tatizo kubwa Tanzania ni ujamaa, uliwalemaza kiakili kwamba akiona mwenzake anatoka kimaisha anajaribu kila mbinu za kumkwamisha. Ujamaa ulikua hivyo, ilikua ukionekana umenunua gari kijijini yaani hata serikali inakuvuruga, sasa hilo tatizo limewaingia mpaka vizazi vya leo. Huwa wanafiki sana na kuchekeana na kuitana mkuu lakini kimya kimya wanatafunana sana hawa.
Utakuta aliyechoma hivyo vifaranga alipata raha sana kwamba amemkwamisha Mtanzania mwenzake na kumrudisha nyuma, hamna cha hizi rhetoric wanazozirusha humu eti safety bird flue sijui sheria, hizo ndio MACCM ambayo hukesha huku Kenyan forums bila hata kunawa uso yamekaririshwa kama PR.
Nenda Dar uone vile wao hukwamishana hata kwenye maofisi.

Hzo roho mbaya ndio zimesababisha ndugu zao wanaikimbia nchi na kuja kuwa omba omba Kenya.

 
Imekula kwao! Ongeza na hasara wanaopata wakulima wa kuku Tz, maanake vifaranga hivo vya Kenya nakuhakikishia ni top quality, kuna siku nimewafuga kule Kajiado. Kuku kama mia nane hivi na faida niliyopata nilikula bata sana.
Wabaki na top quality yao tunataka vifaranga watotolewe hapa nyumbani watu wapate kazi(ajira)lkn sera yetu(viwanda)inatekelezwa.
 
Sio msimamo ni sheria ndivyo inavyosema.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…