Si ndo alikuwa anasema oooh naendaga south kupumzika sababu wananaume wa bongo wanamsumbua sababu ya makalio yake
Huwa sin imani na kamanda Nzowa! Nakumbuka aliwahi kutuhumiwa kutaka kumbambika mtoto wa Mengi drugs lakini hiyo issue ilipotezewa kiaina hebu tukumbushane iliishaje??
Wacha fix wewe kamongo, unadhani airport ni sawa na bandarini? hata ukisafiri vile vindege vidogo ni lazima ukaguliwe, wewe kama ujakaguliwa basi ulisafiri kwa ungo na siyo ndege.Ilikuaje ukakaguliwa mizigo kwenye local airport,, kusema kweli sijawai kukaguliwa mizigo mwanza hata mara moja,,
Sehemu wanayokagua mizigo ni JKIA tena ukiwa unaenda nje ya nchi.. But kwa safari za ndani sijawai kusachiwa
Wacha fix wewe kamongo, unadhani airport ni sawa na bandarini? hata ukisafiri vile vindege vidogo ni lazima ukaguliwe, wewe kama ujakaguliwa basi ulisafiri kwa ungo na siyo ndege.
hawa Madada ni Ndugu nawajuwa toka wanaingia Bongo mwishoni mwa Mwaka 2008 wakafika Hostels za KAM Mwananyamala wakawa wanazuga wanasoma CBE mara wakisema wapo Tumaini University siku Mmoja wakatibuwana Na Rafiki yao waliokuwa wanaishi nae Somebody Magige akaniambia hawa waongo Mmoja anatoka na Jamaa wa hotel flan maarufu mitaa ya kwa Hayati Baba wa Kaya Mikocheni Ndie Good father wake Wewe anakuzuga tu Duh! Night yake nikampa kipondo huyo Mata.ko makubwa ikabidi aseme ukweli kumbe mdogo mtu Nae alikuwa akienda Rosse Garden kila jioni kupiga Deal Hostel KAM wakafukuzwa akiwemo Pia Elizabeth Michael Lulu Baada ya kubainika hawalali pale ikifika Usiku mlinzi anavuta chake watu wanabeba mizigo Melissa hatimaye akazichanga akapangisha Sinza jirani na Mori tokea kipindi hicho Agnes kashawabadilisha wabongo fleva wote kuanzia Mwanafatuma, Ndomo, Kiba, Tonya, Mnyalu, Blue na wengine wengi Ma Dj wa Clubs na Radio kibao.
Mungu atusitiri Mbaya zaidi Hapendi Kinga na Mchezo wake Ni Ule Ule Simu ya Mchina Line Mbili Ndio anaupenda Saana Mini Kabaaang Zamani alipenda kujiita Riziki Ila siri ikatoka siku moja Rafiki yake anafahamika kwa jina la Ms C Shirima alimwita mbele yangu Agnes hapo Ndugu ndipo nilipoanza kujuwa nipo na Msanii
Sembe ndio nini mkuu, ni huu unga wa ugali naoujua mimi? Kwani south katiba yao hairuhusu ugali wa sembe wanataka dona tu?
Mkuu uliyoeleza ni kweli tupu nakumbuka pale Hostel siku za mwisho Agness alikuwa anakula sana vichwa vya serikalini....madereva wa serikali...walikuwa wanaambizana kwamba 0713 yako ni tight...Kwa ujumla mtoto alifanya sana ufedhuli huyu hapo mwananyamala..Ila ni kutokana na taste ya mtu mimi nilikuwa namuona havutii halafu kafupi sana.
Waliokamatwa na 'unga' wa mabilioni ni mabinti
- Wote ni Watanzania, walianzia safari Dar, washikiliwa Afrika Kusini
NA THOBIAS MWANAKATWE | 9th July 2013
Wanawake wawili raia wa Tanzania wametambuliwa kuwa ndiyo wanaodaiwa kuingiza shehena ya dawa za kulevya zenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 6.8 nchini Afrika Kusini wakitokea Tanzania.
Akizungumza na NIPASHE jana, Kamanda wa Polisi Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Geofrey Nzoa, alisema haijafahamika wanawake hao wanatoka mikoa gani.
Kamanda Nzoa aliwataja wanawake hao kuwa ni Agnes Jerald ambaye alisema hajapiga hesabu ya umri wao, ila alizaliwa mwaka 1988 kwa maana hiyo ana umri wa miaka 25 na Melisa Edward ambaye alisema amezaliwa mwaka 1989 kwa maana hiyo atakuwa na umri wa miaka 24. Wawili hao bado wanaendelea kuhojiwa na polisi wa Afrika Kusini.
Alisema Jeshi la Polisi Nchini kwa upande wake linaendelea kufanya uchunguzi kubaini kama dawa hizo walitoka nazo wapi na pia linawasaka watu ambao watakuwa ndiyo wamiliki wa dawa hizo.
Jumapili iliyopita NIPASHE ilipata taarifa za kukamatwa kwa dawa za kulevya aina ya Crystal Methamphetamine zenye thamani hiyo nchini Afrika Kusini wakati zikisafirishwa kutoka Tanzania.
Taarifa hizo zilionyesha kuwa wanawake wawili walikamatwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Oriver Tambo uliopo eneo la Kempton Park siku ya Ijumaa wiki iliyopita wakitokea Tanzania.
Wanawake hao walikamatwa na maofisa wa Mamlaka ya Mapato ya Afrika Kusini wakiwa na masanduku sita ambayo yalipokaguliwa yalikutwa na takribani kilo 150 za dawa hizo ambazo pia zinajulikana kama Tik zikiwa na thamani ya bei ya mtaani ya Randi milioni 42 sawa na Sh. bilioni 6.8.
Baada ya kukamatwa na dawa hizo wanawake hao walikabidhiwa polisi.
Tukio hilo linatoka takribani wiki moja baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Juni 28, mwaka huu kutangaza kuwa tatizo la dawa za kulenya hivi sasa ni janga la kitaifa nchini.
Alisema kumekuwa na wimbi kubwa la Watanzania wanaojiingiza katika biashara haramu ya dawa za kulevya ndani na nje ya nchi na kwamba, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, watuhumiwa 10,799 walikamatwa kwa kujihusisha na dawa hizo.
Pia alisema katika kipindi hicho, Watanzania 240 walikamatwa katika nchi za Brazil, Pakistan na Afrika Kusini, na hivyo kuharibu taswira ya nchi na kusababisha Watanzania wasio na hatia kupata usumbufu na masharti magumu wanapotaka kusafiri kwenda nchi mbalimbali duniani.
Pinda alisema mwaka huu pekee kumekuwa na ukamataji mkubwa wa dawa za kulevya katika eneo la kimataifa la Bahari ya Hindi karibu na Tanzania.
Alisema hivi sasa mikate, maandazi na askrimu zinazouzwa kwenye shule za msingi, zinawekwa dawa za kulevya.
Alisema vitendo hivyo vinafanya vijana wengi wa shule za msingi na hata sekondari kuwa na tabia za ajabu, ikiwamo kuingia darasani wakiwa na kiatu kimoja mguuni, mkufu wenye nyembe na kidani chenye nyembe kifuani.
CHANZO: NIPASHE Home
###########
Kwa wasomaji
Agnes Gerald, maarufu kama Agnes Masogange Alizaliwa Aprili 23, 1988 kwenye hospitali ya Mkoa wa Mbeya na akasoma Shule ya Msingi na Sekondari ya Sangu.