#COVID19 Watendaji na walimu wakuu wanavyoenda kuteseka na fedha za COVID‐19 za IMF

Ml 20 darasa 1 mbona nyingi sana

Upumbavu mtupu na kutupotezea muda bila sababu

Milioni 20 najenga madarasa matano na hela inabaki
mkuu,
madarasa hayo ma5 yatakua navigezo vilivyo tajwa hapo kweli???
 
Wizi wizi wizi mtupu
Bwana wewe hakuna darasa linalojengwa kwa mil 10 usidanganye watu,usifikili darasa ni kibanda Cha kuuzia miwa,emu achana na story za vijiweni tafakari fanya upembuzi yakinifu tena,Watu Kama nyie ndo wale makandarasi mkipewa miradi mnaishia njiani kwakua mlikosea kukadilia GHARAMA mwisho wa siku miradi inakwama na hela za walipakodi mshapewa zote mifukoni imekauka
 
Aluminum gani izo za 150,000/=, mkuu
 
Nlipata tenda ya kujenga madarasa 20 kwa 2mln kila darasa nikabidhi likiwa limeisha nimeitema tenda mchana kweupe
 
Tofali 500 zinaishia kwenye msingi
 
Mkuu kachukue tenda ya kujenga madarasa Tena Jenga kwa hela yako mwenyewe,Ukimaliza serikali wakayapitisha madarasa hayo uchukue mpunga wote mkuu kwa faida kubwa.
Tatizo mkuu ni rushwa ndani yake, tukienda kiuhalisia 12M inamaliza darasa la kisasa na chenchi inabaki
 
Mkuu kuna balance ya 3,720,000 kwenye 12? tumia hiyo kwa vitu vilivyobaki
 
Ninachojua ni kwamba kuna Walimu hata huo Ualimu wenyewe hawaupendi.Hao ni wale wenye One na Two zao ambao baada ya kukosa connection zingine ikabidi waingie huko ili kupoza njaa.Na ni wengi sana huko kwa sasa!
Hapa sijaelewa kaka,baada ya kukosa Connection kwenye ajira au kwenye kozi aipendayo ndiyo akaona asomee ualimu ?
 
Kuna balance ya 3,720,000 ita-cover hayo yote

kwa viwango vinavyo itajika na serikali, io pesa ni ndogo,
ila kwa kujenga jenga tuu, ili kuzuia wanafunzi wasilowe mvua,
io pesa inaweza tosha jenga ilo darasa moja..
 
 
Ahsante, hofu yangu ni kama hayo maagizo yatafuatwa au la!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…