Watendaji Wizara ya Fedha wasimamishwa kazi kwa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha

waziri wa fedha mwigulu lameck nchemba tunaomba ulisaidie taifa kuthibiti ubadhilifu huo kwa kuwa rais amekuamini kukaa hapo na katibu wako msisubiri waziri mkuu kufika na kuongelea hayo.
Kitendo cha PM kwenda pale na kuyabaini hayo madudu ni sababu tosha kabisa kwa Waziri husika kuachia ngazi, ni kashfa kubwa
 
Bado unaendelea kulala au kuamka
 
Magufuli alisema mtanikumbuka kwa mazuri na si kwa mabaya huu ni mwanzo tu...makubwa yanakuja.............
 
Katika mambo ambayo nilimshangaa mama,ni kumteua Mwigulu kuwa waziri wa fedha.Hapo nilikata tamaa kabisa na kuona mama hayuko serious.

Wizara ya fedha unataka mtu ambaye yuko committed, asiyekuwa mwamasiasa,mtendaji muadilifu asiyechoka.Si mpenda sifa na utukufu bali mnyenyekevu anayemcha Mungu.Mwigulu hana sifa hizo japo kidogo.

Nakuombea rais wangu Mungu awe nawe kwani najua kazi uliyonayo ni ngumu,ijapo sie tunaiona rahisi.

Kumbuka huyo ni mgombea urais.Atafanya chochote apate pesa ya kuandika maandishi ya kampeni kwenye mawe yote nchi nzima
 
Kiini machoz hakuna lolote hawa wamepangwa wasimame kwa niaba ya pm na bashiru et al ndio walilamba mshiko wakati wa sekeseke la mswiba wa jpm
 
"Sisi tulikuwa Mwanza tunasherehekea siku ya wafanyakazi duniani nyinyi hapa ndani mnalipana posho,” amesema Majaliwa.
Naomba ku-paraphrase... "Sisi tulikuwa Mwanza tunalipana Posho na nyinyi hapa ndani mnalipana Posho"

Au Mwanza kulikuwa hakuna Posho ?
 
Magufuli alisema mtanikumbuka kwa mazuri na si kwa mabaya huu ni mwanzo tu...makubwa yanakuja.............
Kwahio unadhani enzi zake kulikuwa hakuna upigaji ? Tofauti ni kwamba enzi zake upigaji mwingine usingesikia ingawa hata sasa angalau tunasikia robo tatu ingawa sio wote..., enzi za mwendazake ungesikia tu ule aliotaka yeye usikie...
 
Hii Wizara kama wameweza kufanya hayo basi wafanyakazi wote wa hii wizara wanatakiwa kuondolewa kabisa serikalini. Dawa ni kuisafisha hiyo wizara. Bila hivyo hakuna kitakachorekebika bila hatua stahiki.
Ni watu wawili tu hapo waziri na katibu mkuu, hao wengine ni kuwaonea
 
Tutamkumbuka JPM..

Waziri wa fedha ivi ni nani?
Una shida wewe
Hizi pesa zimetumika wakati jpm akiwa hai au mara baada ya kufariki..
Mbona wakati wa jpm kila siku alikuwa anatumbua na kusimamisha watumishi
Akili umeipeleka likizo.
Jpm alikuwa mfujaji wa fedha za umma kuliko rais yoyote
 
True umesema kweli ndugu,
 
Kweli kabisa. Mishahara midogo isiyokidhi mahitaji hata yale ya muhimu ndiyo tatizo linalosababisha yote hayo. Mtu umekaa miaka ishirini kazini lakini mshahara wenyewe mmmmmh, tena hapo unazo degree zako mbili tayari.
 
Si kuna wakaguzi wa ndani ambao kazi yao kubwa ni kufanya pre-audit kabla ya payment yoyote na kuhakikisha utaratibu unafuatwa
Kawaida hawana nguvu au nao wako kwenye orodha, nakama walikuwa kwenye payroll hapo vocha inatembea kama msg ya whatsap
 
Hii inatisha sana!!!
wakati baadhi ya watumishi wanadai haki zao za malimbikizo ya mishahara tangu mwaka 2018 kumbe kuna watumishi hazina wanajilipa mamilioni kwa wiki mbili!!!
haki za watu wamezikalia, kwa hili Mungu hawezi kuwasamehe.
 
Ni kweli Wizara ya Fedha inatakiwa apewe Mchumi mahili ambaye hana ambitions za kisiasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…