Watoto wa siku hizi hawajui kabisa enzi zetu uliweza kuchapwa kwa sababu zifuatazo...

Hahahaha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiweka kiwembe kwenye kaptula ya Shule mama wakati anafua akakikuta aisee kichapo chake balaa...[emoji23][emoji23]

Ukila kwa jirani kichapo...

Usiposalimia asubuhi kichapoo...

Ukipigwa ukasusa chakula eti usilee ukaenda kulala aisee mboko zitakufata huko kitandani hutaamini[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukivaa nguo za kike nawewe ni wakiume lazima Nichape

Ukichelewa kuoga,Usiku unaogeshwa maji ya baridi (kwa tuliokulia sehemu za baridi)
 
Kwa wale wenzangu wa chandimu, umetoka shule badala ya kwenda nyumbani, mkaweka mawe barabarani mkaanza kucheza mpira. Hiyo hata atokee jirani tu anayekufahamu, utakula kipigo halafu anakushika shati hadi nyumbani huko ndo utaenda kukutana na holy brutal
 
Halafu ukifanya kosa mtaani mfano mkikutwa mnapigana,anaweza atokee mzee yeyote ambaye hata hawafahamu akawachapa na ukienda kusema nyumbani utachapwa tena

Sent from my TECNO F1 using Tapatalk
 
Furaha ilikua pale mzazi anataka akuchape mara paap anatokea mgeni, halafu anasena mwache mtoto

Sent from my TECNO F1 using Tapatalk
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Jr[emoji769]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…