Watoto wa siku hizi hawajui kabisa enzi zetu uliweza kuchapwa kwa sababu zifuatazo...

πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ™ŒπŸΏ izo point;
-Ukipigwa ukalia unapigwa unyamaze😁
-ukipigwa usilie unapigwa tena ili ulieπŸ˜‚
 
Ukila tonge kubwa wakati wa kula unapigwa!
 
Mkulungwa vipi tena na picha nayo ndio kielelezo cha haya uliyobainish hap ama
 
Hiyo No.30. Mimi na dadaangu nnaemfuata tulipita kwenye shamba la mzee mmoja tukaiba karanga. Yule mzee kumbe katuona bana akaja kuturipoti kwa bi. Mkubwa.

Bi mkubwa akasikiliza maelezo ya mzee weee, halafu bila kutuhoji, akachukua bakola. Tulichezea mikwaju hiyo siku aisee... hadi nikawa nawaza hivi ni karanga tuu au kunakingine!!

Ikafikia pahala hadi yule mzee akaanza kutuonea imani nadhan. Akaanza kumsihi mama atuache.
 
Nimetoka kuzungumza na Mtu hapa.
Week kama tatu zilizopita nilikuwa pahala.

Kuna mtoto wa kizungu umri 4-5 Years alikiwa akicheza na Dada yake mdogo kwenye vile vigali vya watoto.

Kwa bahati mbaya yule mtoto alinigonga na lile kile kigari.

Mama yake akamwita kwa sauti, Please say Sorry to........ (Akimaanisha mwanaye Mdogo wa kiume aniombe msamaha kwa kosa lile)

Kijana akaja akasogea na akaomba msamaha.
Nilipomuitikia na mazungumzo kidogo akafurahi sana,baadae wazazi wakapita pale pia ku appology.

Narudia kusema kuna tabia tunaziona kwa TV na mitandao sio maisha ya hawa watu hasa kwenye malezi ya watoto.

Mnaofuatila,sheria za mabinti kujihusisha na mahusiano kwa baadhi ya Nchi za Ulaya na Japan miaka imeongezwa kulinda Wanawake.

Kuna makundi ya kihuni yapo kwa ajili ya sisi ku copy na kupaste tabia ambazo tunaaminishwa sana.

Wanaweza kuwa hawako sahihi kwa sehemu.Ila hawa wenzetu wapo makini sana na watoto.

Nina visa vingi vya vijana wa kizungu ambao hata wazazi wao huuliza tabia zao na mienendo hasa wakiwa huku kwetu kuja kujitolea kazi.

Kama unafamilia lea watoto wako kwa umakini na jitahidi waijue jamii na mambo mengi.

Tulipewa mapigo na wazazi kuna pahala palisaidia sana.

Kuna umri tulifika tuliobahatika tulipewa maonyo kwa maneno makali na yenye vitisho vikasaidia sana.

Wazazi walihangaika sana nasi.
Lakini kwa sasa sisi wazazi wa kileo na tabia tulizotoa kusikoeleweka au ulimbukeni tunaharibu watoto kwa 100%
 
Hapa sina cha kuongeza umepiga pale pale nafarijika nikijua bado kuna watu wanaona thamani ya malezi na kuipeleka kwa jamii inayomzunguka. Barikiwa sana.
 
Point kaka.
 
Akijamba mkubwa na wewe uko around imekula kwako labda pawe na mbwa
 
MAKOSA 34 AMBAYO WATOTO WA ZAMANI WALIKUWA WAKILA BAKORA!!
WATOTO WA ZAMANI WALIISHI MAJUMBANI KAMA WAKO MAFUNZO YA KIJESHI!! WAKIKUA NI FULL ADABU KUHESHIMU WATU, UTU, BUSARA NA KUJITETEGEMEA WAKIWA NA UMRI MDOGO TU


1: Usiposalimia wakubwa asubuhi unapigwa
2: Usiposalimia wageni unapigwa
3: Ukinawa kabla ya wageni unapigwa
4: Ukilia bila sababu unapigwa
5: Ukinyanyuka wakati wa kula kabla ya wakubwa kuinuka unapigwa
6: Wakubwa wakiwa wamekaa wewe ukaenda kusimana pembeni unapigwa
7: Ukikaa wakubwa wamesimama unapigwa
8: Ukitumwa dukani ukachelewa kurudi unapigwa
9: Ukichelewa kurudi toka shuleni unapigwa
10. Ukiwahi kurudi shuleni unapigwa
11: Ukililia wageni wakati wanaondoka , wakitoka unapigwa
12: Kujipitisha pitisha wageni wakiwa wanakula unapigwa
13: Kujibu ovyo wakubwa unapigwa
14: Kutukana watu wazima, watoto au rika lako unapigwa
15: Ukiwa mbishi bila sababu unapigwa
16:Ukipigwa ukalia unapigwa ili unyamaze
17: Ukipigwa umenyamaza unapigwa ili ulie
18: Ukipigwa shuleni ukaenda kusema nyumbani, unapigwa
19: Ukianza kula nyama kabla ya wakubwa unapigwa
20: Ukila kwa jirani ukabainika unapigwa
21: Ukianza kunawisha wenyeji badala ya wageni mkimaliza kula unaitwa chumbani unapigwa
22: Ukianza kunawisha watoto badala ya wakubwa unapigwa
23. Ukimkuta mtu nzima hujampokea unapigwa
24. Ukienda kusema kama umepigwa unapigwa.
25. Mtu mzima akipita kama mnacheza hamjamshughulikia unapigwa.
26. Ukienda nyumba za watu, ukaona kitu au ukasikia story ukaileta nyumbani unapigwa
27. Ukipewa hela na mtu asiefahamika au hata anaejulikana inategemea mazingira gani unapigwa
28. Ukianza kuchaguwa chakula hiki nakula hiki sili unapigwa
29. Ukianza kuwa na marafiki wasioleweka makwao unapigwa
30. Mtu mkubwa akija kukuchongea nyumbani hata kama sio cha ukweli unapigwa
31.Ukikaa na wakubwa halafu ukaanza kucheka bila sababu unapigwa.
32.Ukimwuliza Baba/ Mama umetoka wapi unapigwa.
Endapo umepigwa na Ukasusa chakula unapigwa .
33.Ukilala bila kulna unapigwa.
34.Ukiitwa ukaja kimyakimya bila ya kuanza kuitika unapigwa.
Wahenga njoooni tukumbushane [emoji2][emoji2]πŸ₯±

MENGINE MTAONGEZEA
 
1: Usiposalimia wakubwa asubuhi unapigwa

2: Usiposalimia wageni unapigwa
3: Ukinawa kabla ya wageni unapigwa
4: Ukilia bila sababu unapigwa
5: Ukinyanyuka wakati wa kula kabla ya wakubwa kuinuka unapigwa
6: Wakubwa wakiwa wamekaa wewe ukaenda kusimana pembeni unapigwa
7: Ukikaa wakubwa wamesimama unapigwa
8: Ukitumwa dukani ukachelewa kurudi unapigwa
9: Ukichelewa kurudi toka shuleni unapigwa
10. Ukiwahi kurudi shuleni unapigwa
11: Ukililia wageni wakati wanaondoka , wakitoka unapigwa
12: Kujipitisha pitisha wageni wakiwa wanakula unapigwa
13: Kujibu ovyo wakubwa unapigwa
14: Kutukana watu wazima, watoto au rika lako unapigwa
15: Ukiwa mbishi bila sababu unapigwa
16:Ukipigwa ukalia unapigwa ili unyamaze
17: Ukipigwa umenyamaza unapigwa ili ulie
18: Ukipigwa shuleni ukaenda kusema nyumbani, unapigwa
19: Ukianza kula nyama kabla ya wakubwa unapigwa
20: Ukila kwa jirani ukabainika unapigwa
21: Ukianza kunawisha wenyeji badala ya wageni mkimaliza kula unaitwa chumbani unapigwa
22: Ukianza kunawisha watoto badala ya wakubwa unapigwa
23. Ukimkuta mtu nzima hujampokea unapigwa
24. Ukienda kusema kama umepigwa unapigwa.
25. Mtu mzima akipita kama mnacheza hamjamshughulikia unapigwa.
26. Ukienda nyumba za watu, ukaona kitu au ukasikia story ukaileta nyumbani unapigwa
27. Ukipewa hela na mtu asiefahamika au hata anaejulikana inategemea mazingira gani unapigwa
28. Ukianza kuchaguwa chakula hiki nakula hiki sili unapigwa
29. Ukianza kuwa na marafiki wasioleweka makwao unapigwa
30. Mtu mkubwa akija kukuchongea nyumbani hata kama sio cha ukweli unapigwa
31.Ukikaa na wakubwa halafu ukaanza kucheka bila sababu unapigwa.
32.Ukimwuliza Baba/ Mama umetoka wapi unapigwa. Endapo umepigwa na Ukasusa chakula unapigwa . 33.Ukilala bila kula unapigwa.
34.Ukiitwa ukaja kimyakimya bila ya kuanza kuitika unapigwa.
35. Kuna muda unapigwa tu sababu umekaa siku nyingi haujapigwa
36. Kesi yoyote ikifika kwenu unapigwa ndio uhojiwe, ukikubari unapigwa tena na ukikataa wanasema yule ni mtu mzima hawezi kudanganya unapigwa tena

Wahenga njoooni tukumbushane
 
Hii namba 35 nimecheka sana[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Hii namba 35 nimecheka sana[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
24. Ukienda kusema kama umepigwa unapigwa
Mshua wangu umwambie eti Mangesho kanipiga, nachukua fimbo unakula za kutosha, anakwambia kwanini na wewe hukupigana?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…