Watoto wangu wote hufariki baada ya kuzaliwa au mimba kuharibika

Watoto wangu wote hufariki baada ya kuzaliwa au mimba kuharibika

Jitibie bro

Hiyo ya miguu sio poa,nilipatwa na gonjwa aisee lililoambatana na miguu yaani nilirudi utotoni
Ndio nipo najishughulikia mkuu, mwanzo nilikua napuuzia maana sikuwa nikiamini ila sasa nimesurrender baada ya kuona natibu tatizo hili linaibuka jingine, yaani ni bandika bandua[emoji1430]
 
1:mimi kinyama changu hakiumi mkuu kipo kawaida kama kinefifia

2:Mahusiano yangu hayayumbi wala hatugombani kama kuachana tunaachana kwa amani kabisa

3:Biashara zangu zinaenda fresh hazina misukosuko
Basi tuna vyanzo tofauti za tatizo. Lako naona ni la hospitali zaidi, fuata ushauri wa hao walozungumzia Rh factor unaweza pata mwanga.
 
Ndio nipo najishughulikia mkuu, mwanzo nilikua napuuzia maana sikuwa nikiamini ila sasa nimesurrender baada ya kuona natibu tatizo hili linaibuka jingine, yaani ni bandika bandua[emoji1430]
Fanya hivyo aisee,,,Afya ndio mtaji,
 
Acha ujinga wewe, nani ambaye hajawahi kupitia misuko suko?
mbona unatok povu mkuu,,jamaa alihisi labda kuna maagano yalifanyika ndio nikamjibu hilo linawezekana maana huko nyuma nilipitia misukosuko mingi sana hasa upande wa baba kidogo walimwengu waniondoe duniani lakini ndio vile Mungu alinipigania sana pamoja na wazazi kuhangaika zaidi ya miaka m3 ndio nikakaa sawa..Ni stori ndefu ipo siku nitaiweka hapa
 
Basi tuna vyanzo tofauti za tatizo. Lako naona ni la hospitali zaidi, fuata ushauri wa hao walozungumzia Rh factor unaweza pata mwanga.
lakini wote si tuna vinyama!
 
Kabisa, Siku moja nitaleta mrejesho wa kupona tatizo na nikiwa nalea mtoto[emoji4]
Hata mimi mkuu ipo siku nitaleta mrejesho wa huu uzi,,tena ikimpendeza Mungu mwakani[emoji120]
 
Wakuu poleni na majukumu ya kujenga nchi..

Nimekuja kwenu kama mwana Jamii Forums nikiwa na uzoefu wa takriban miaka 10 na huu mtandao wetu pendwa unatusaidia kwenye mambo mbalimbali kwenye maisha. Nipo mkoani Dodoma kwa sasa ambapo nafanya biashara zangu na kupata riziki.

Nikiwa kama kijana na approach 30's nimekumbwa na matukio mfululizo ya kufiwa ama kuondokewa na watoto wangu punde tu wanapozaliwa wengine kabla ya kuzaliwa au hata muda mrefu baada ya kuzaliwa

Miaka ya hivi karibuni nilipita kwenye mahusiano na wasichana kadhaa, kati ya hao watano niliwapa ujauzito na mchanganuo wake ulikuwa kama ifuatavyo..

Wa kwanza alitoa mimba ikiwa na miezi minne ilimsumbua sana nusu na yeye aondoke na hakunipa taarifa juu ya hilo hadi nilipobaini na nikamuacha papo hapo.

Wapili aliharibikiwa mimba ikiwa na mwezi mmoja(huyu alikuwa na matatizo ya tumbo kabla ya kukutana na mimi alikuwa hashiki ujauzito hivyo alikuwa anajaribu kama amepona bila mimi kujua badala yake mimba ikaharibika).

Watatu alijifungua mapacha wanne kwa vipindi viwili tofauti na wote walifariki ndani ya wiki moja baada ya kujifungua.Yeye ni mwenyeji wa Tanga na ana uzao mzuri wa watoto mapacha.

Wanne alijifungua mtoto wa kiume mwaka mmoja uliopita na amekaa naye huku akimsumbua sana kwa homa za hapa na pale na wiki moja iliyopita nilipewa taarifa kuwa amefariki baada ya kuugua mfululizo.

Watano alishika ujauzito wa mapacha uliodumu kwa miezi sita na mimba ikaharibika pasi na kutegemea. Alichanganyikiwa sana maana alikuwa na matarajio mengi juu ya hao watoto pindi watakapozaliwa..

Kiujumla nimepoteza watoto 9 ndani ya miaka mitatu kwa sababu mbalimbali, hii kitu imekuwa ikinitesa sana na nashindwa kuelewa tatizo hasa ni nini na nini suluhisho lake maana napoteza viumbe wasio na hatia inaniumiza sana[emoji22]..

Naombeni ushauri wenu juu ya hili tatizo linalonikumba nifanyeje niweze kuepukana nalo na kama ni mpango wa Mungu kwanini kila siku mimi ukizingatia umri nao unakwenda wazazi wanataka wajukuu.

Naombeni msaada wenu wa mawazo na ushauri juu ya suala hili
Nimesoma maelezo yako lakini naona kama mimba zote zilikuwa na sababu ambazo hazihusiani na wewe kuharibika. Nadhani umepata tu bahati mbaya ya kukutana na wanawake ambao sababu za mimba zao kuharibika ziko wazi.
Wa kwanza umesema alitoa mwenyewe kwa sababu ya mimba kumsumbua. Sioni wewe ulihusika vipi na mimba yake kusumbua.
Wa pili aliharibikiwa mimba kwa sababu umeshasema alikuwa na tatizo hata kabla hamjakutana.
Wa tatu alijifungua mapacha wanne na wote wakafa. Hili nalo halina ajabu yoyote kwani mapacha wanne uwezekano wa kufariki ni mkubwa.
Wa nne naye alijifungua vizuri lakini akamsumbua sana kwa homa na akafariki. Hapa inawezekana alikutana na matatizo mengine tu na sababu siyo wewe.
Wa tano aliharibikiwa mimba ya mapacha. Hapa napo sioni kitu special sana kwani mimba ya mapacha kuharibika siyo ajabu sana.
 
mkuu kukatwa sehemu ya mwili tena kwenye haja sio jambo dogo[emoji3]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]usiogope,wenzio wanaenda kuoga makaburini usiku was manane kutafuta Tiba[emoji23]
 
Back
Top Bottom