Watu tunasherekea utajiri wa Elon Musk kushuka

Watu tunasherekea utajiri wa Elon Musk kushuka

Nimekuangalia kwenye nyuzi na comments zako nyingi inaonekana ni mtu wa wivu na Roho mbaya, mfano unavyoserekea musk kushuka inafaida gani kwenye maisha yako
Dah brethren mgalatia mwenzangu
 
Yaani huyu Elon simpendi. Ana nyodo yaani na ile idea yake ya kupandikiza kipichi kwenye ubongo. Stupid kabisa aanze yeye kwanza kupandikizwa. Anajiona yeye ndo yeye na sometimes anaongea ujinga tu. Silipendi hili li baba. Tena ninaomba lishuke na lishuke tena.
Alisema ataaza yeye kupacikliwa mkuu...vipi sasa utampenda?
 
Kuna msemo wa kiingerza unasema ukitaka kufanikiwa

Dont hate the champions,learn from them.
Dont hate,be inspired
Dont throw salt at them, throw roses and confettis
 
BECOMING number ONE is EASIER than REMAINING NUMBER ONE
 
Una akili sana ndugu. Unaona vitu wengi hawawezi kuviona kwa macho ya kawaida.

Hata project ya space x nayo ni project ya kipumbavu tu, openai OpenAI Musk anafikiri anaweza kutengeneza mashine iwe kama binadamu, anajiona mungu mtu.

Anapita njia zile zile za akina Gate.

Hawatafanikiwa.
Haya nimateso yaumasikini kuhisi mwenyemali anajitapa anajiona lakini ukweli utabaki palepale anaejituma kwaufanisi namaalifa zaidi hufanikiwa minamuombea huyu mwamba ikiwezekana apambane zaidi lipatikane suluhisho lakifo
 
Ngebe, nyodo, madharau, majigambo, kiburi, kujiona na kujiinua vimefika ukingoni.

Ni chereko na vifijo.

Elon Musk (Mwafrika Uchwara) mmiliki wa Tesla, Space X na Twitter utajiri wake umeshuka kutoka dollar billion 230 hadi dollars billion 168 na kujikuta kupoteza nafas ya kwanza utajiri duniani. Sasa hivi namba moja ni mfaransa billionaire mstaarab Bernard Arnault akiwa na utajiri wa dollars 172.

Wadau wengi tumepokea hii habari kwa furaha na shangwe. Watu tumefurahi hadi tumepata faraja kwenye umaskini wetu.

Musk alijionaga mungu mtu akidhani dunia ipo mabegani mwake. Na tunaomba utajiri wake uzidi kushuka asiwe hata kumi bora.

Kazaliwa Africa na kukulia Africa lakini hana msaada kwenye bara ilipomfikisha alipo. Watu tunakula mara moja baada ya siku tatu lakini hatukumbuki na hana fadhila.

Bora wote tu tuwe sawa kuwe na uihano.

Furaha ya maskini ni masahibu ya tajiri hasa kufulia.

Maskini Jeuri!
Dish liko imara kweli kweli
 
... ila likitokea Afrika lenye maslahi kwao hujinasibisha na uafrika! Hawa ni popo; sio ndege, sio mnyama!
Hata hivyo Leo tutawashangilia kwa kuwa hatuna chaguo zaidi la Timu ya Afrika.
 
Mafukara mnafarijiana kwa wingi wenu, taabu iko pale pale dadadeeki.
 
Ukute uko itigi kwenye mashamba ya mpunga umejibanza chini ya mwembe na simu yako ya Tecno unamkoa tajiri
 
Yaani huyu Elon simpendi. Ana nyodo yaani na ile idea yake ya kupandikiza kipichi kwenye ubongo. Stupid kabisa aanze yeye kwanza kupandikizwa. Anajiona yeye ndo yeye na sometimes anaongea ujinga tu. Silipendi hili li baba. Tena ninaomba lishuke na lishuke tena.
Unasema humpendi kumbe kinyume chake, by the way Sina uhakika kama hata yy anakujua achilia mbali kukupenda.

Tafuta hela v Ben ten vile [emoji1]
 
Aisee Kuna watu mnamatatizo kweli[emoji23]

Kwanza kabisa dua la kuku halimpati mwewe

Pili wale jamaa wenye hela nyingi akili,fikra na mawazo yao yapo beyond your thinking

Wenyewe hawawazi sijui awe wa kwanza au wa mwisho, yani no competition they just minding their own business ikitokea Kawa wa kwanza sawa, Kawa wa kumi sawa as long as mipango yake ipo sawa

Hapo juzi kanunua Twitter ambayo ni sabab moja wapo ya utajiri wake kushuka na alikuwa analijua hili lakini haikumzuia yeye kununua kwasabab tu anaamnin katika freedom of speech, anataka dunia nzima iwe huru kuongea, hakuwaza kabisa hata kama angeshuka mpaka tajiri wa 10 kwake sawa tu lakini Twitter ameshaichukua

Ni kweli as a human being ana mapungufu yake mengi sana na idea zake nyingi ni hatari Kwa future ya binadam lakini chuki za mpita njia kama wewe haziwezi kubalisha chochote

N.:B Mwamba ni miongoni mwa watu wachache sana kama sio yeye peke ake wenye umaarufu mkubwa na hela chafu alafu anapiga vita ushoga waziwazi[emoji23]



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom