Watu watano washikiliwa na polisi kwa tuhuma za mauaji ya watu wa familia moja Mwanza

Watu watano washikiliwa na polisi kwa tuhuma za mauaji ya watu wa familia moja Mwanza

Shetwani lazima atajwe!

Kwa nini asitajwe sasa!

Ile "desire" ama "lust" to kill utaipataje bila ushawishi wa kaka ibilisi?

Tena akiweka ushawishi wake "maridhawa" hadi utasahau na kuziba mianya ya kufikiwa kirahisi kukamatwa kwako!

Inakuwa kama umevuliwa nguo na mwanamke uliyemhonga hadi kukufirisi, leo kwanza ndiyo umempata!

Unamkabili huku ukitetemeka na udenda ukikuchuruzika, akili zimezibwa na pazia kwa muda, hauoni mbali wala hausikii, tena bila kujali kuna maradhi na kifo, wewe unajisunda kavu kavu tu.

Akili zitakurudia baadaye ukishatenda, tena wakati huo umeshakwenda na maji kudadadeki!

Hapo shetwani anakuwa keshawajibika na kukuachia upambane na hali yako.
shetani anahusikaje mkuu ushawahi kumuona unamjua au kumbuka umeumbwa umekamilika maamuzi yetu tusitafute wa kumtupia lawama
 
Ingekuwa hili limefanyika kaskazini, kilimanjaro au arusha ungekuta uzi upo page ya 20,

Na uhakika watu wataelewa sasa kwamba watu wabaya wapo kila mahali duniani!!
Huyo ndiko mauaji ya kutisha yanatokea kila uchwao,kanda ya ziwa kwa wiki mauaji yanaweza kufikia watu 6,huko watu wanaroho za kichawi tu
 
Shetani amevamia inchi yetu. Kila kukicha ni habari za mauaji ya kikatili. Hii ni dalili ya kuwa na serikalini haramu isiyotokana na ridhaa ya wananchi.
Watu wauane huko kwa mambo yao, lawama kwa serikali. Acheni chuki zisizo na maana.
 
Huyo ndiko mauaji ya kutisha yanatokea kila uchwao,kanda ya ziwa kwa wiki mauaji yanaweza kufikia watu 6,huko watu wanaroho za kichawi tu
Wachawi wanahaja gani ya kutumia mapanga wakati uchawi unatosha
 
Yaani alipokua akiishi huyu Mama na familia yake si mbali sana ninapofanyiaga mazoezi make ni njia yangu napopita kuelekea zoezi, majuzi asubuhi nafika Mecco niingie zoezi nilishangaa kukuta watu wamejaa kwake kuulizia ndo nikaambiwa wame uawawa wote waliokua wanakaa hapo na miili yao kutupwa mtoni, afu alkua na binti mzuri huyo alikua kazalishwa na jamaa wa hapo hapo Mecco, hata house girl wao alikua si haba mzuri kweli.

Mwenyezi Mungu awarehemu wote na tuwaombee awape pumziko la milele kwa amani , AMIN!
 
Hivi mecco ile rami yake imeshaisha. Nakumbuka kampuni ya ujenzi ndio ilizalisha jina la eneo
 
Back
Top Bottom