Watu watatu wafikishwa Mahakamani kwa kosa la mauaji yaliyotokea miaka 20 iliyopita

Watu watatu wafikishwa Mahakamani kwa kosa la mauaji yaliyotokea miaka 20 iliyopita

Aliwataja watuhumiwa hao na umri wao ulivyokuwa wakati wa tukio ni; Rajabu Songo (34), kazi wa mtaa wa Machinjioni, Kata ya Mkuti Wilayani Masasi, Stanley Mtweve (32), Mkazi wa Mtaa wa Makaburini Kata ya Mkuti Wilayani Masasi na Yusuph Pahala (30), mkazi wa Mtaa wa Maendeleo Kata ya Mkomaindo wilayani Masasi.


Jitahidi kusoma between the line kiongozi wangu. Nadhani hakuna utata wa aina yoyote katika hili. Maana yake ni kwamba, chukua umri wa kila mtugumiwa kwa wakati huu, kisha jumlisha miaka 20 ili upate umri halisi wa sasa wa kila mtuhumiwa.
Kama mwalimu nakupa "Excellent" bro.
 
Aliwataja watuhumiwa hao na umri wao ulivyokuwa wakati wa tukio ni; Rajabu Songo (34), kazi wa mtaa wa Machinjioni, Kata ya Mkuti Wilayani Masasi, Stanley Mtweve (32), Mkazi wa Mtaa wa Makaburini Kata ya Mkuti Wilayani Masasi na Yusuph Pahala (30), mkazi wa Mtaa wa Maendeleo Kata ya Mkomaindo wilayani Masasi.


Jitahidi kusoma between the line kiongozi wangu. Nadhani hakuna utata wa aina yoyote katika hili. Maana yake ni kwamba, chukua umri wa kila mtugumiwa kwa wakati huu, kisha jumlisha miaka 20 ili upate umri halisi wa sasa wa kila mtuhumiwa.
hiyo habari imekuwa edited mkuu, pitia post baada ya post utaelewa
 
  • Thanks
Reactions: y-n
Kosa miaka 20 iliyopita, watumiwa miaka 30, 32 na 34; maana yake walikuwa miaka 10,12 na 14. Okay
Ungesoma vizuri kabla ya ku coment.
Aliwataja watuhumiwa hao na umri wao ulivyokuwa wakati wa tukio ni; Rajabu Songo (34), kazi wa mtaa wa Machinjioni, Kata ya Mkuti Wilayani Masasi, Stanley Mtweve (32), Mkazi wa Mtaa wa Makaburini Kata ya Mkuti Wilayani Masasi na Yusuph Pahala (30), mkazi wa Mtaa wa Maendeleo Kata ya Mkomaindo wilayani Masasi.
 
Aliwataja watuhumiwa hao na umri wao ulivyokuwa wakati wa tukio ni; Rajabu Songo (34), kazi wa mtaa wa Machinjioni, Kata ya Mkuti Wilayani Masasi, Stanley Mtweve (32), Mkazi wa Mtaa wa Makaburini Kata ya Mkuti Wilayani Masasi na Yusuph Pahala (30), mkazi wa Mtaa wa Maendeleo Kata ya Mkomaindo wilayani Masasi.


Jitahidi kusoma between the line kiongozi wangu. Nadhani hakuna utata wa aina yoyote katika hili. Maana yake ni kwamba, chukua umri wa kila mtugumiwa kwa wakati huu, kisha jumlisha miaka 20 ili upate umri halisi wa sasa wa kila mtuhumiwa.
Hii habari imekuwa mtoa mada atuombe radhi 🤣🤣🤣
1650362220322.png
 
Kosa miaka 20 iliyopita, watumiwa miaka 30, 32 na 34; maana yake walikuwa miaka 10,12 na 14. Okay
Inaonekana hujasoma hiyo habari vzuri

Mwandishi amesema "umri wao ulivyokuwa wakati wa mauaji yaani 2002"

Kwa hiyo jumlisha huo umri na miaka 22

Soma tena habari hiyo.
 
Wakuu hapa hamkusoma kwa makini: Aliwataja watuhumiwa hao na umri wao ulivyokuwa wakati wa tukio ni; Rajabu Songo (34), kazi wa mtaa wa Machinjioni, Kata ya Mkuti Wilayani Masasi, Stanley Mtweve (32), Mkazi wa Mtaa wa Makaburini Kata ya Mkuti Wilayani Masasi na Yusuph Pahala (30), mkazi wa Mtaa wa Maendeleo Kata ya Mkomaindo wilayani Masasi.

Yaani, kwasasa washtakiwa wana miaka 54, 52 na 50.
 
"Aliwataja watuhumiwa hao na umri wao ulivyokua wakati wa tukio" Ina maana watuhumiwa wote sasa hvi ni 50+ years. Kwa miaka 20 Polisi bado walikua wanafanya uchunguzi?
Nafikiri uchunguzi ulifanyika ila watuhumiwa waliingia mitini
 
😂😂😂😂
Mtoa mada ulichowafanyia wenzio siyo kitu kizuri, wameanza kuchanganyana wenyewe kwa wenyewe maskiini wakati kosa siyo lao na ukajikausha zako..!
 
Nimekusoma mkuu. Kumbe mada alikuwa edited.
Sawa. Kama imekuwa edited tatizo ni nini? Aliyeandika Si ni yy mwenyewe amesahihisha ili wasomaji waweze kuelewa vizuri? Kung'ang'ania na kushupalia ile yenye kosa la kiuandishi sio sawa. Tukubali kuwa flexible. Hata yule "Jamaa" alimwambia Jaji kwenye ile kesi maarufu kuwa kosa lile ni Curable.
 
Hii habari imekuwa mtoa mada atuombe radhi 🤣🤣🤣 View attachment 2192856
Kabisa yani 😂😂😂 na wanao comment saiv nao hawajielewi. Inawezekana vipi watu zaidi ya watatu wasome
Wakuu hapa hamkusoma kwa makini: Aliwataja watuhumiwa hao na umri wao ulivyokuwa wakati wa tukio ni; Rajabu Songo (34), kazi wa mtaa wa Machinjioni, Kata ya Mkuti Wilayani Masasi, Stanley Mtweve (32), Mkazi wa Mtaa wa Makaburini Kata ya Mkuti Wilayani Masasi na Yusuph Pahala (30), mkazi wa Mtaa wa Maendeleo Kata ya Mkomaindo wilayani Masasi.

Yaani, kwasasa washtakiwa wana miaka 54, 52 na 50.
Amerekebisha huyo mwanzo haukua hivyo. Inawezekanaje watu wa mwanzo wote comments ziwe za kushangaa umri.
 
Sawa. Kama imekuwa edited tatizo ni nini? Aliyeandika Si ni yy mwenyewe amesahihisha ili wasomaji waweze kuelewa vizuri? Kung'ang'ania na kushupalia ile yenye kosa la kiuandishi sio sawa. Tukubali kuwa flexible. Hata yule "Jamaa" alimwambia Jaji kwenye ile kesi maarufu kuwa kosa lile ni Curable.
Ni vizuri kusema.... Maana watu wame-comment kulingana na habari ilivyokuja.
 
Wakuu hapa hamkusoma kwa makini: Aliwataja watuhumiwa hao na umri wao ulivyokuwa wakati wa tukio ni; Rajabu Songo (34), kazi wa mtaa wa Machinjioni, Kata ya Mkuti Wilayani Masasi, Stanley Mtweve (32), Mkazi wa Mtaa wa Makaburini Kata ya Mkuti Wilayani Masasi na Yusuph Pahala (30), mkazi wa Mtaa wa Maendeleo Kata ya Mkomaindo wilayani Masasi.

Yaani, kwasasa washtakiwa wana miaka 54, 52 na 50.
Acha tu, nyie mmekuja kwa kuchelewa. Haikuandikwa hivyo mwanzoni

1650362220322.png
 
Kuna mmoja aliua mkoani huko.
Miaka na miaka akaenda kujificha bagamoyo zinga.
Damu ya mtu nzito askari mpelelezi wa kesi Yake akahamishiwa bagamoyo .
Siku moja amekwenda kwa fundi viatu.
Anashangaa kuona ile sura mbona Kama anaijua anajiuliza alishawahi kumuona wapi.
Ahaa kesho yake akakumbuka.
mbona alikamatwa akapelekwa alipofanya tukio
 
Watu watatu wamefikishwa Mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya kuua mwanamke Mkoani Mtwara miaka 20 iliyopita.

Watuhumiwa hao ni wakazi wa Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Masasi kwa tuhuma za mauaji ya mwanamke aliyetambulika kwa majina ya Nora Hamisi.

Nora aliyekuwa Mkazi wa Kata ya Mkuti Wilayani Masasi, aliuawa na mwili wake kutupwa katika Mtaa wa Machinjioni katika Kata ya Mkuti.

Watuhumniwa hao walifikishwa kortini mwishoni mwa wiki mbele ya Hakimu wa Wilaya ya Masasi, Batista Kashusha na kusomewa mashtaka ya mauaji wanayodaiwa kuyafanya miaka 20 iliyopita.

Mwendesha Mashtaka wa Polisi Insepta Jovina alidai kuwa watuhumiwa hao wanakabiliwa na kesi hiyo namba 2 ya mwaka 2002 mbele ya Mahakama hiyo.

Aliwataja watuhumiwa hao na umri wao wa sasa kuwa ni; Rajabu Songo (34), kazi wa mtaa wa Machinjioni, Kata ya Mkuti Wilayani Masasi, Stanley Mtweve (32), Mkazi wa Mtaa wa Makaburini Kata ya Mkuti Wilayani Masasi na Yusuph Pahala (30), mkazi wa Mtaa wa Maendeleo Kata ya Mkomaindo wilayani Masasi.

Inspekta Jovina alidai kuwa watuhumiwa hao walimuua Nora kisha kuuchukua mwili wake na kuutupa katika Mtaa wa Machinjioni kisha kutoweka.

Alidai waliutupa mwili eneo hilo kwa lengo la kupoteza ushahidi, lakini baada ya uchunguzi wa Jeshi la Polisi walikamatwa. Watuhumiwa hawakutakiwa kuzungumza lolote kwa kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji.

Kwa mujibu wa sheria, Mahakama yenye mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji ni Mahakama Kuu.

Wote walirejeshwa mahabusu na kesi hiyo itatajwa tena Aprili 24, 2022.


============

Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara ni kuwa watuhumiwa hao wanatuhumiwa kutenda kosa hilo walipokuwa na umri mdogo na siyo kwamba ripoti ya umri wao imekosewa. Hivyo, umri uliotajwa mwenye habari yao ni umri walionao kwa sasa mwaka 2022.



Source: Nipashe
Walikuwa wadogo Sana,waliwezaje kumuua??
 
Inawezekana coz hata mie nikiwa skul kuna dogo nadhani alikua na miaka 14 aliuwa na yy akajaribu kujiua ikashindikana, alienda kondem sijui siku hizi yupo gereza lipi.
 
Kuna mmoja aliua mkoani huko.
Miaka na miaka akaenda kujificha bagamoyo zinga.
Damu ya mtu nzito askari mpelelezi wa kesi Yake akahamishiwa bagamoyo .
Siku moja amekwenda kwa fundi viatu.
Anashangaa kuona ile sura mbona Kama anaijua anajiuliza alishawahi kumuona wapi.
Ahaa kesho yake akakumbuka.
mbona alikamatwa akapelekwa alipofanya tukio
Safi sana
 
Back
Top Bottom