Watu wenye vimradi vya kufuga kuku na kelele za kujiajiri

Ajira nyingi za Tanzania znakuhakikishia kula, kodi, na mavazi, ila kwa mambo makubwa utakuwa ukimezea mate wenzio tu

Watu waliojiajiri nawaheshimu sana ,nawaheshimu sana

Nmejaribu kuangalia nyumba nyingi tunazopanga huku mtaani ni za kina Nani?, nmejijibu mwenyewe kuwa nyumba nyingi ni za watu waliojiajiri .kwahiyo wewe endelea na dharau zako

Huenda umepanga na unaish kwenye nyumba ya mjasiriamali afu unaleta nyodo hapa.

Kaa kimya kama umepata ajira na inakulipa vizuri, sio kuongea umbea kama hu.
 
Nakataa dada, kuku hawawezi kosa soko hata siku moja...
 
Hapo mdau ndiyo unakosea, familia hawaachiwi urithi wa hela. Ila urithi wa wazo la ubunifu lililozaa hela ndicho unatakiwa kuwaachia familia. Pia usipende kuingilia majukumu yasiyokihusu, Mungu kawaandalia wanao namna ya kutoka kimaisha.
Nimependa hii pt, kujilundikia mali kisa watoto watarithi tunakosea, nguvu tupeleke kwenye malezi bora na elimu, umenikosha kwa hili..
 
Ahsante mkuu kwa mchango wako,bado umepanga kwenye nyumba ya mjasiriamali au umeshajenga kwako?😛😛😛😛😛😛
 
Moja ya akili za hovyo kuwahi kutokea katika uso wa dunia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…