Watuhumiwa wa mande ya Ubakaji na ulawiti waliotumwa na afande wakamatwa

Watuhumiwa wa mande ya Ubakaji na ulawiti waliotumwa na afande wakamatwa

Daah! Tutayasikia mengi sana Mtani.

Saa ingine ukute ni Wahuni tu na hicho walichofanya ndio kazi zao, hapo sababu wamemtaja Afande basi wamegeuzwa gumzo na kupewa vyeo visivyo hata vyao kama yule muuza madafu.
Hadi muda huu siaminii km wale ni wajeda, inawezekana ni yule m1 ambaye wasifu wake unatambulishwa wazi.

Nachokihisi mie, yule jamaa anayewekwa wazi ndo mjeda alotumwa na boss wake, yeye akaenda kutafuta vibaka wa mtaani na kuingia nao mzigoni.

Makomando ndo wawe vilee huu utani wa wazi wazi, wallah. Khaaah

Aaaaaah wee!!!
 
Tunahitaji taarifa zaidi, ni wakina nani?, wamekamatwa lini?,wakiwa wapi?, walitumwa na nani? Na huyo afande ni nani? Na yeye amekamatwa? Wako kituo gani? Wako wangapi? Hilo kosa wamefanyia wapi na ni lini? Acheni kumangamanga toeni taarifa
 

Attachments

  • 20240806_150936.jpg
    20240806_150936.jpg
    82.9 KB · Views: 2
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amesema tayari vyombo vya dola vimeshawatia nguvuni watuhumiwa wa ubakaji na ulawiti wa msichana anayedaiwa kuwa ni mkazi wa Yombo Dovya jijini Dar es Salaam.

Agosti 4, 2024 zilisambaa video katika mitandao ya kijamii zikiwaonyesha vijana watano wakimbaka na kumlawiti binti huyo, huku wakimtuhumu kwa kile kilichosikika katika video hiyo kuwa ametembea na mume wa mtu.

Kadhalika, katika video hiyo inayodaiwa kuchukuliwa na vijana hao, binti huyo alisikika akieleza anakotokea na kumwomba msamaha mtu aliyetambulishwa kwa jina la afande.

Masauni amethibitisha kutiwa nguvuni kwa vijana hao leo, Jumanne Agosti 6, 2024 alipotafutwa na Mwananchi Digital kwa njia ya WhatsApp.

Katika ujumbe mfupi aliotumiwa kuulizwa iwapo watuhumiwa hao wameshakamatwa, Masauni alijibu kwa kuandika “tayari” kupitia ujumbe huohuo wa njia ya WhatsApp.

Hata hivyo, Waziri Masauni hajafafanua zaidi kwani amesema bado yupo kwenye mkutano kwa sasa.

Pia soma
Taarifa ya Tanpol inasema wanaendelea na uchunguzi haijasema imewakamata. ova.
 
Sheria za kijeshi wale watavuliwa uaskari halafu watakabidhiwa kwa polisi,sasa hivi watakua chini ya military police nimeona waziri gwajima kule x kasema kuna taratibu zinafuatwa baada ya hapo kila kitu kitakua wazi
Em kuweni serious, wale vijana ni askari? Tena wa JWTZ?
mbona nazidi kupata taharukiii, wallah. Lol
 
1. Ni akina nani....majina yao
2. Wapelekwe mahakamani

In summary, We need to know them and bottom line wapelekwe mahakamani.

short of that tunaomba Madeleka autwae mzigo huu tutachanga fedha ya kumweesha kuendesha kesi
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amesema tayari vyombo vya dola vimeshawatia nguvuni watuhumiwa wa ubakaji na ulawiti wa msichana anayedaiwa kuwa ni mkazi wa Yombo Dovya jijini Dar es Salaam.

Agosti 4, 2024 zilisambaa video katika mitandao ya kijamii zikiwaonyesha vijana watano wakimbaka na kumlawiti binti huyo, huku wakimtuhumu kwa kile kilichosikika katika video hiyo kuwa ametembea na mume wa mtu.

Kadhalika, katika video hiyo inayodaiwa kuchukuliwa na vijana hao, binti huyo alisikika akieleza anakotokea na kumwomba msamaha mtu aliyetambulishwa kwa jina la afande.

Masauni amethibitisha kutiwa nguvuni kwa vijana hao leo, Jumanne Agosti 6, 2024 alipotafutwa na Mwananchi Digital kwa njia ya WhatsApp.

Katika ujumbe mfupi aliotumiwa kuulizwa iwapo watuhumiwa hao wameshakamatwa, Masauni alijibu kwa kuandika “tayari” kupitia ujumbe huohuo wa njia ya WhatsApp.

Hata hivyo, Waziri Masauni hajafafanua zaidi kwani amesema bado yupo kwenye mkutano kwa sasa.

Pia soma
App ya mange kimambi naweza kuipataje kwenye simu yanu?
 
Mtanii unaambiwa ni captain wa jeshi katuma wajeda wambake na kumlawiti binti huyo, kisa alitembea na mume wake. Lol

Sheria ifuate mkondo wake, Wallah.
Siwezi kuamini kabisa kama kweli captain wa jeshi anaweza fanya ujinga huo!? Labda kama ni captain wa kuteuliwa, captain alipitia kwenye mafunzo halisi ya u captain hawezi thubutu fanya ujinga huo!!
 
sijui ni UMASIKINI!, sijui ni WENDA WAZIMU,mimi hata sielewi!.

kama Mungu hata ingilia kati waliopo kuzimu watajiona wanahadhari kuliko Nkazi wa Afrika.
yaani,ukimsiliza kila mtu anaeongelea ili jambo anasikitika zaidi hawa vijana kupoteza KAZI zao na sio kupoteza MORALITY.
yule kijana wa kizungu alijichoma Moto si kutete kazi yake bali HUMANITY plus MORALITY.
ila uku Africa kila Mtu anaweza kazi tu!.
 
Siwezi kuamini kabisa kama kweli captain wa jeshi anaweza fanya ujinga huo!? Labda kama ni captain wa kuteuliwa, captain alipitia kwenye mafunzo halisi ya u captain hawezi thubutu fanya ujinga huo!!
Kwenye captain kutuma vijana wafanye revenge kwa huyo mtoto naamini, ila hawa vijana kuwa ni wajeda na ni makomandoo, hapa hapanaa hadi muda huu nakataaa.

Hawa ni vibaka wa mtaani tyuuh.
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amesema tayari vyombo vya dola vimeshawatia nguvuni watuhumiwa wa ubakaji na ulawiti wa msichana anayedaiwa kuwa ni mkazi wa Yombo Dovya jijini Dar es Salaam.

Agosti 4, 2024 zilisambaa video katika mitandao ya kijamii zikiwaonyesha vijana watano wakimbaka na kumlawiti binti huyo, huku wakimtuhumu kwa kile kilichosikika katika video hiyo kuwa ametembea na mume wa mtu.

Kadhalika, katika video hiyo inayodaiwa kuchukuliwa na vijana hao, binti huyo alisikika akieleza anakotokea na kumwomba msamaha mtu aliyetambulishwa kwa jina la afande.

Masauni amethibitisha kutiwa nguvuni kwa vijana hao leo, Jumanne Agosti 6, 2024 alipotafutwa na Mwananchi Digital kwa njia ya WhatsApp.

Katika ujumbe mfupi aliotumiwa kuulizwa iwapo watuhumiwa hao wameshakamatwa, Masauni alijibu kwa kuandika “tayari” kupitia ujumbe huohuo wa njia ya WhatsApp.

Hata hivyo, Waziri Masauni hajafafanua zaidi kwani amesema bado yupo kwenye mkutano kwa sasa.

Pia soma
Ningekuwa Polisi, ningehakikisha kuwa ni mmojawapo wa wapelelezii kwenye kesi hii. Hili tukio ni la kutengeneza makusudi na kwa sababu ambazo siyo zile ambazo zinazojadiliwa na watu kwenye mitandao

Tukio hili limetengenezwa kwa sababu zingine tofauti kabisa
 
Back
Top Bottom