Waumini wa Kanisa Katoliki ni wavumilivu sana

Waumini wa Kanisa Katoliki ni wavumilivu sana

Roma ni Italia. Waingereza, wajerumani, wagiriki, wahispaniola, na hata wahindi na wachina nao hawahusiki na Catholic.

Na wao wakatafute Mungu wao.
Catholic ni kwa ajil ya watu wote sio kwa waroma peke yao.Ukiangalia official badge zao au ukikuta post zinazonyesha sehemu makanisa yao yalipo utakuta wameandika " kanisa katoliki parokia ya ......." Hutakuta neno Roma
 
Kanisa la Roma lina miaka 2000 toka limeanzishwa.
Hivi mtu mwenye umrinwa miaka 2000 atabishana nini na mtu aliyeanzisha karne ya 20?

Kanisa la Roma limewekeza kwenye
elimu ndo maana wana shule na vyuo vikuu vya kutosha nchi nzima.
Afya
Kanisa la Roma lina hospital na dispensary nchi nzima.

Fedha
Kanisa la Roma lina Mkombozi bank.
Kanisa la Roma ni taasisi imara na kongwe kabisa.

Waumini wake ni sehemu ya taasisi kwa hiyo hawana muda wa kuanza kujibizana na walokole ni kupoteza energy.
Hata shetani naye ni mkongwe na anamiradi lukuki ambayo hata Yesu aliambiwa akimsujudia atapewa..pia shetani ana taasisi na wengi wanadamu yawezekana hata wewe mtoa mada ni mwanachama mwaminifu..hivyo kaa kutulia huna hoja katika hili.

Kimsingi rc wameharibu ukristo kwa kuchanganya tamaduni za kipangani.

#MaendeleoHayanaChama
 
Halafu Roman Catholic ni kwaajili ya Italy tu.Mmakonde,Mmachinga,Mmsai,Mchagga au Mnyakyusa na Catholic wapi na wapi !.Umewahi kuona au kusikia Pope Mwafrika au Mungu wa wa Catholic ni Mungu kwaajili ya wazungu pekee yake.
Nenda kaangalie kalenda ya mapapa utawaona waafrika
 
Imani sahihi ni kumuabudu Mungu katika roho na kweli huku ukijiepusha na ibada za sanamu.

Kuwa na masanamu yaliyojaa makanisani mwenu ni ibada ya kishetani.

Kumuamini Mariam ni ibada ya kishetani. Mariam anaitwa Malkia wa Mvinguni katika Ukatoliki. Hii title ya Malkia wa Ulimwengu imekatazwa kutumika katika Biblia.

Yeremia 7:18
[18]Watoto huokota kuni, na baba zao huwasha moto, na wanawake hukanda unga, ili kumfanyizia mikate malkia wa mbinguni, na kuwamiminia miungu mingine sadaka za kinywaji, wapate kunikasirisha mimi.

Vile vile ukisoma Yeremia 44 :17-19

17 Lakini bila shaka tutalitimiza kila neno lililotoka katika vinywa vyetu, kumfukizia uvumba malkia wa mbinguni, na kummiminia sadaka za kinywaji, kama tulivyotenda sisi, na baba zetu, na wafalme wetu, na wakuu wetu, katika miji ya Yuda, na katika njia kuu za Yerusalemu; maana wakati huo tulikuwa na chakula tele, na kufanikiwa, wala hatukuona mabaya. 18Lakini tulipoacha kumfukizia uvumba malkia wa mbinguni, na kummiminia sadaka za kinywaji, tumepungukiwa na vitu vyote; na kuangamizwa kwa upanga, na kwa njaa. 19 Nasi tulipomfukizia uvumba malkia wa mbinguni, na kummiminia sadaka za kinywaji, je! Tulimwandalia mikate, ili kumwabudu, na kummiminia mimiminiko, waume zetu wasipokuwapo?

Hizo ndizo ibada za sanamu zinazokatazwa.

Sisi waumini wa kanisa katoliki tunafundishwa tusipoteze muda kubishana.

Kwetu kanisa ninsehemu ya maisha.
Nikihitaji shule bora kwa mwanangu nitampeleka shule ya kanisa.

Naumwa nitakwenda Bugando hospital na nitapata huduma bora za matibabu.

Nikihitaji hudumaa za kibank kwa ajili ya akiba yangu nifungua account mkombozi bank.

Nahitaji ujirani mwema.kupitia jumuiya nitajumuika na waumini wenzangu kupata social service.


Hivi ndivyo ambavyo kanisa Catholic linavyo deal na waumini wake ndo maana hatuna muda wa kuanza kujibizana na muumini wa dhehebu lingine.

Kama uko sahihi ni sawa.
Kama unajua sana biblia ni sawa.
Kama wewe ni mtakatifu ni sawa.
Kama utaenda mbinguni ni sawa pia.
Hatuna muda wa kuanza kuonyeshana nani yupo sahihi na nani hayupo sahihi.

Na kutokubishana na waumini wa madhehebu mengine ndo sababu ya kwanini kanisa hili bado lina nguvu na linawaumini miaka yote.
 
Ushawahi kuona mkatoliki mwenye akili ndogo?
Umeongea kitu kikubwa mno, japo kipo katika mfumo wa swali, Mimi kwa kweli sijawahi kuona hata mkatoliki akiipambania Imani yake na kuponda ponda hovyo za wengine, wakatoliki wamestick kwenye mafundisho yao tuu! Hawanaga muda wa kujieleza

Utawaponda wee lakini Catholics are very loyal to their faith japo hakuna sehemu isiyokosa mapungufu Ila wanajitahidi kwa kweli
 
Hata shetani naye ni mkongwe na anamiradi lukuki ambayo hata Yesu aliambiwa akimsujudia atapewa..pia shetani ana taasisi na wengi wanadamu yawezekana hata wewe mtoa mada ni mwanachama mwaminifu..hivyo kaa kutulia huna hoja katika hili.

Kimsingi rc wameharibu ukristo kwa kuchanganya tamaduni za kipangani.

#MaendeleoHayanaChama
Sawa haya unayosema tunaambiwa kila siku
 
Habari za wakati huu wapendwa

Bila kupoteza wakati naomba niende moja kwa moja kwenye uzi husika

Katika dini zote au madhehebu yote au makanisa yote hakuna kanisa au waumini ambao wanaongoza kupigwa vita na kusemwa vibaya kama wakatoliki.

Ukienda kwenye mikusanyiko ya waislamu wanaopondwa ni wakatoriki ukienda kwenye mikutano ya injili ya walokole wanaopondwa na
Binafsi huwa nashangaa sana nikihudhuria misiba, padre au askofu akiwa pale mbele akianza kuhubiri, hakuna hata tone la nguvu za Mungu, hata harufu tu ya uwepo wa Mungu haipo, mahubiri makavuuuu yasiyookoa. kusali dini inahitaji uvumilivu sana na ni kifungo kikubwa mno.
 
Kanisa la Roma lina miaka 2000 toka limeanzishwa.
Hivi mtu mwenye umrinwa miaka 2000 atabishana nini na mtu aliyeanzisha karne ya 20?

Kanisa la Roma limewekeza kwenye
elimu ndo maana wana shule na vyuo vikuu vya kutosha nchi nzima.
Afya
Kanisa la Roma lina hospital na dispensary nchi nzima.

Fedha
Kanisa la Roma lina Mkombozi bank.
Kanisa la Roma ni taasisi imara na kongwe kabisa.

Waumini wake ni sehemu ya taasisi kwa hiyo hawana muda wa kuanza kujibizana na walokole ni kupoteza energy.
Hizo taasisi hazina msaada kwa waumini wao, Ukihitaji chochote utapigwa hela kama yeyote asiye mkatoliki.
 
Circle ya dini zoote mwisho ni kuabudu, mwezi, jua, nyota na Miungu na Wazungu, we jali mambo yako Mkuu hayo mambo ya dini wanachelewesha maendeleo yako na familia yako, labda uwe ule upande wa pili.
 
Halafu Roman Catholic ni kwaajili ya Italy tu.Mmakonde,Mmachinga,Mmsai,Mchagga au Mnyakyusa na Catholic wapi na wapi !.Umewahi kuona au kusikia Pope Mwafrika au Mungu wa wa Catholic ni Mungu kwaajili ya wazungu pekee yake.
We dini yako ni kwajili ya watu gani?
 
Waislamu siwezi kuwasemea lakini Wakristo wengine wanawashutumu Wakatoliki kwa sababu wanafundisha mambo ambayo ni unbiblical na mambo ambayo yalirithiwa kutoka katika desturi za Dini za Kipagani za Kirumi na Kiyunani
Unajuwa maana ya bidaa kwa waislamu?
 
binafsi huwa nashangaa sana nikihudhuria misiba, padre au askofu akiwa pale mbele akianza kuhubiri, hakuna hata tone la nguvu za Mungu, hata harufu tu ya uwepo wa Mungu haipo, mahubiri makavuuuu yasiyookoa. kusali dini inahitaji uvumilivu sana na ni kifungo kikubwa mno.
Hata uende wapi kama umeenda Kwa ajiri ya kuangalia Nini kitatokea basi hutakuja kukiona hata kidogo miaka yote ambayo Mungu atakujalia
Lakini ukieenda Sehemu yoyote Ile Kwa miadi ya kubadilika basi haitachukua hata sekunde kushudia vitu ambayo hujawahi kuviota.
#Mpaka sasa hajapatikana mwenye Imani angalau ndogo kama chembe ya haradali coz hakuna alieweza kuhanisha hata mawe tu
 
Kuna msemo kwamba usibishane na mjinga (Don't argue with a fool). Kwa msemo huo sijui fool ni mkatoliki au hao wengine uliowataja ila ukiwa unajielewa huwezi jishughulisha na dini/dhehebu la mwingine wala kuliponda kama wafanyavyo hao unaowesema.
 
Back
Top Bottom