Wauza mchele, weka changamoto zenu hapa tusaidiane kuzitatua

Wauza mchele, weka changamoto zenu hapa tusaidiane kuzitatua

IMG_2294.jpg
IMG_2301.jpg

Morogoro mbingu hiyo super yenyewe haina chenga,chuya,wala biriani kwa elfu 2000 tu bei ya shamba/ya mkulima ushuru kwa gunia ni 3000 ghalama ya usafiri 10k mpaka dar.
 
Kwa sasa kuna mgomo wa wanunuzi juu ya ushuru kuwa hii serikali sijui tunaelekea wapi kutoka kwenye 2000 kwa gunia mpaka 4500 inaelekea 5000 saivi
 
Kwa sasa kuna mgomo wa wanunuzi juu ya ushuru kuwa hii serikali sijui tunaelekea wapi kutoka kwenye 2000 kwa gunia mpaka 4500 inaelekea 5000 saivi
Aisee, wanasema haswa tatizo nini mpaka kupanda kiasi hiko...?
 
Kwa sasa kuna mgomo wa wanunuzi juu ya ushuru kuwa hii serikali sijui tunaelekea wapi kutoka kwenye 2000 kwa gunia mpaka 4500 inaelekea 5000 saivi
Ushuru wa gunia la mpunga au mchele?
 
Habari wakuu, nafikilia kuanzisha biashara ya kununua na kuuza nafaka.... Kama vile michere nk...

Muongozo plz kwa wazoefu wanipe zile taratibu za awali Bidhaa ipi naweza Anza nayo ambaya itanipush mtaji wangu especially kwa sisi tunaoanza from scratch...

Mtaji 2ML.

-fanya survey ya sehemu inayohitaji kuweka goli lako na bidhaa zikatoka vizuri
Pia nenda kafanye survey maeneo kati ya haya michele ndio ipo kwa wingi…

-Ubaruku
-morogoro mbingu,mngeta,mlimba
-kyela
-kamsamba mbozi

Saivi mchele bora na super yenyewe inapatikana kamsamba hamna sehemu inafikia huo mchele kwa utamu na uzuri

-ukishapata sehemu yenye uhakika wa mchele kwa wingi na kufunga mzigo tafuta darali atatafutia gari kwa ajili ya kupakia lets say…

Umefunga mchele bei ya 2000 kwa super lbda gunia 60 hiyo ni 6ton na ushuru ni 2000 kwa gunia yani 100kg unapiga sasa hesabu mfano 2000x60= ukipata jobu unapigia na garama ya usafiri + garama ya ushuru unazidisha umetumia kiasi gani mpaka mzigo utafika dar sababu ukishapakia mzigo kwenye gari wewe ni kuupokea tu ukishapiga hesabu sasa na wewe unapgia hesabu ni bei gani utauza dsm ikulipe lets say mchele mpaka unafika ofisini kwako unafika kwa 2250/2300 sasa unapiga hesabu bei kuuza hapo ofisini kwao nafaida unaipata hapo hapo labda na wengine wakija wataelezea experience zao pia na garama ya usafiri kwa lori haizidi 10k.
 
Wewe ni mwenyeji wa Ifakara au upo Dar?
Kwa mzigo huo gari uhakika. Gharama kwa gunia la kilo mia ni 12000.
Usafiri 9000
Ushuru 2500
Kupakia 500
 
Wewe ni mwenyeji wa Ifakara au upo Dar?
Kwa mzigo huo gari uhakika. Gharama kwa gunia la kilo mia ni 12000.
Usafiri 9000
Ushuru 2500
Kupakia 500
Kiongozi umesema ushuru ni 2500 lakini pia kuna mdau hapo juu Itscharlie amesafirisha magunia kadhaa ya mchele na amesema wafanyabiashara wamelalamika kuwa ushuru umepanda mpaka 4500 yupi yuko sahihi kati yako na yeye kiongozi...?
 
Kiongozi umesema ushuru ni 2500 lakini pia kuna mdau hapo juu Itscharlie amesafirisha magunia kadhaa ya mchele na amesema wafanyabiashara wamelalamika kuwa ushuru umepanda mpaka 4500 yupi yuko sahihi kati yako na yeye kiongozi...?
Geti gani kalipia 4500. Maana ushuru inategemea na geti la halmashauri husika. Mimi nimeweka geti la halmashauri ya Ifakara mji
Huyo yupo Mbingu, ni halmashauri ya wilaya ya Mlimba. Ushuru ni mapato ya ndani ya halmashauri hivyo kiwango kinaamuliwa na halmashauri husika
 
Wakuu naomba kufahamu,
Gharama ya kusafirisha mchele kutoka Ifakara mjini hadi Dar kwa gunia la kilo 100 ni shilingi ngapi?
Na vipi upatikanaji wa usafiri ni rahisi au hadi connections na madalali?

Nina gunia 200 za mpunga nataka nizikoboe nije kuuzia Dar.

Usafiri ifakara sio wakuwaza kabisa hapo elf 10 ushuru nadhani ni elf 3 au elf 2
 
Kiongozi umesema ushuru ni 2500 lakini pia kuna mdau hapo juu Itscharlie amesafirisha magunia kadhaa ya mchele na amesema wafanyabiashara wamelalamika kuwa ushuru umepanda mpaka 4500 yupi yuko sahihi kati yako na yeye kiongozi...?

Bei ya ifakara na huku mbingu mkuu ni tofauti huku wanatuonea tu ifakara ushuru na nauli ya mzigo vipo chini
 
Geti gani kalipia 4500. Maana ushuru inategemea na geti la halmashauri husika. Mimi nimeweka geti la halmashauri ya Ifakara mji
Huyo yupo Mbingu, ni halmashauri ya wilaya ya Mlimba. Ushuru ni mapato ya ndani ya halmashauri hivyo kiwango kinaamuliwa na halmashauri husika

Ndio hivyo saivi ni 4500 unajua kama mahenge wanalipa 5000
 
Back
Top Bottom