sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,407
- 19,264
Wasanii wengi wametoka kwenye maisha magumu ya kuishi chumba kimoja familia nzima tena hapo wamepanga. Wengine wametoka mikoani wamekuja Dar hawana pa kulala wanalala stendi, mitaroni, Kariakoo shimoni au wakibahatika ndio ile wanaishi maisha ya ghetto chumba kimoja mtu sita, yaani kifupi wametaabika sana hadi kufika hapo walipo.
Licha ya hivyo kuna wasanii wachache ambao angalau wazazi / walezi wao walikuwa na nafasi ya kuwahudumia vizuri mfano kuwasomesha shule binafsi zenye ada kubwa, milo mitatu kwa siku ya uhakika a.k.a mboga saba, n.k. Yaani kifupi kwenye ukuaji wao hawajakumbana sana na suluba za maisha.
Vanessa Mdee
Baba yake alikuwa kwenye ubalozi Marekani, karudi Tanzania akiwa na miaka 12 anatema yai sio mchezo (aliwahi kuwa mtangazaji MTV), pia Kifaransa anaichapa vizuri tu.
Kukulia kwenye mazingira ya kidini kulimfanya kuwa msanii alejitahidi angalau kwenye nidhamu.
Makamua
Alisomeshwa Feza Boysys na St Mary's, ada ya Feza ni kama milioni 6.
Jux
Shule aliyosoma ni private ya gharama kimtindo, chuo kasomea nje ya nchi. Pesa ya studio + video ya wimbo wake wa kumtambulisha kweye game alilipiwa na mzazi wake, mama yake alikuwa anafanyia kazi bandarini.
Licha ya hivyo kuna wasanii wachache ambao angalau wazazi / walezi wao walikuwa na nafasi ya kuwahudumia vizuri mfano kuwasomesha shule binafsi zenye ada kubwa, milo mitatu kwa siku ya uhakika a.k.a mboga saba, n.k. Yaani kifupi kwenye ukuaji wao hawajakumbana sana na suluba za maisha.
Vanessa Mdee
Baba yake alikuwa kwenye ubalozi Marekani, karudi Tanzania akiwa na miaka 12 anatema yai sio mchezo (aliwahi kuwa mtangazaji MTV), pia Kifaransa anaichapa vizuri tu.
Kukulia kwenye mazingira ya kidini kulimfanya kuwa msanii alejitahidi angalau kwenye nidhamu.
Makamua
Alisomeshwa Feza Boysys na St Mary's, ada ya Feza ni kama milioni 6.
Jux
Shule aliyosoma ni private ya gharama kimtindo, chuo kasomea nje ya nchi. Pesa ya studio + video ya wimbo wake wa kumtambulisha kweye game alilipiwa na mzazi wake, mama yake alikuwa anafanyia kazi bandarini.