Wawili niliowabakisha kama marafiki nao nimewafuta!

Wawili niliowabakisha kama marafiki nao nimewafuta!

[emoji848]hyo yesu uungu nani kampa....na toka lini yesu akawa mungu....
WEWE UNAMUABUDU MUNGU WA KIARABU ALLAH.
UTACHANGANYIKIWA KUTAKA KUMJUA YESU MUNGU NA BABA YAKE MUNGU WA WAYAHUDI NA WAKRSTO YEHOVA.
NB: MTOFAUTISHE MUNGU WA WAISLAMU NA MUNGU WA WAYAHUDI NA WAKRSTO.
 
Mi marafiki ninao wachache sana ila nikifa nitazikwa na wengi maana kila mtu ni rafiki yangu na huwa ni apo kwa apo
 
Ukiachana na wale wa mbali kidogo kama washikaji ambao huibuka mara kadhaa pale tu wanapokuwa na shida, nilibakisha watu wawili ambao niliamini ni wa kweli ila sasa nimefikia hatua ya kuwafuta pia.

1. Huyu wa kwanza yeye huwa karibu sana pale anapokuwa na matatizo ya kifedha, atakuwa na mawasiliano ya mara kwa mara hata kuja nyumbani na vitu kama hivyo, uchumi ukikaa sawa anapotea na inafika wakati hata ukipiga simu mchana atakuja kutafuta usiku kabisa au atume tu text ya "Vipi kaka?" hapo imeisha.

2. Huyu wa pili yeye ana matatizo kwenye ndoa yake, huwa anavurugikiwa sana anapokuwa na changamoto za kimahusiano, basi huwa anakupigia simu hata mara 10 kwa siku mjadili na umsaidie mawazo jinsi ya kutatua matatizo yake. Mimi humpa full support lakini yeye nikijaribu kumueleza yangu kwanza anayadogolesha na hana muda wa kuyasikiliza, anakejeli pia.

Sasa nimeona msela wangu atakuwa mke wangu tu. Jambo ambalo sitaweza kuongea nalo nitabaki nalo mimi mwenyewe. Kwasasa mimi sina rafiki zaidi ya mke wangu.
Rafiki wa kweli ni MUNGU tu.
 
Karibu kwenye utu uzima. Ukifanikiwa kupata mke/mume/partner bora huyo ndiye atakuwa rafiki yako.

If you are lucky enough, your childhood friends can be your forever friends.

Otherwise mtoto wako anaweza kuwa rafiki yako japo kuna vitu hawezi kukuelewa na pia akikua atachagua marafiki zake wengine na hatokuwa rafiki yako.

Mwisho jifunze kuwa mwenyewe kihisia (pale unapotafuta kuziba gape la urafiki). Zaidi sana kuwa na washkaji ambao hawahusiki kukukamilisha kihisia bali kijamii.
ulilolisema kwenye aya ya mwisho lina ukweli wote.
 
Pole! Jitahidi kuishi nao kwa akili sana namaanisha sana.

Kwani kuona marafiki ni tatizo ni kosa lako la kutojua maana ya urafiki. Wengi hutaka wanachowafanyia marafiki nao wawafanyie, jambo hilo hupelekea magomvi makubwa na ni kitu ambacho hakiwezekani.

Kumbuka urafiki huunganishwa na jambo moja, mfano, urafiki wenu unaweza kuunganishwa na kufanya kazi au tabia inayofanana kama biashara, kilimo, wezi, kuvuta bangi n.k.

Igawa mambo mengine havitafanana kabisa, Mfano
1. Wewe unapenda kupiga simu lakini rafiki yako yeye anapenda kutuma sms.
2. Wewe usipopigiwa simu unaumia lakini mwingine umpigie usimpigie wala siyo tatizo.
................................
Kwa kifupi usiwekeze muda wako mwingi kwa marafiki.
kabisa inabidi tubadilike
 
Huwa nakereka sana na tabia ya unamtumia mtu meseji asubuhi, anakujibu usiku. Eti ubize?!. Kawaida ya binadamu wakijua wewe ni mtu wa kuanza kuwapandia hewani, wanakuona unajipendekeza, hivyo wanareact wanavyotaka, mara wakujibu neno moja "P", mara wakate simu.
Lakini bro kwanini tunafanya maisha yawe magumu kiasi hiko?kwanini usimpigie tu hewani mkasikilizana maisha yakaenda.

Kuondoa lawama mpigie kwanza huyo unayetaka kum-text inawezekana ana muda wa kukusikiliza kama hana yeye ndiye akufahamishe kwamba tuma msg siyo unatuma tu wengine text za kawaida hawagangaiki nazo kwa sababu wanadhani ni za makampuni ya simu.
 
“Siku mbili sijalala sijakula
Ninastress
Nyumba imegeuka chumba cha dharura
Emergency
Sioni marafiki ama mashosti
Au mnasubiri nife ndio mniposti
Bora nitafute pesa
Ndugu wa kweli mafanikio
Watu feki watu feki
Sitaki marafiki siwataki ng'o
Sitaki wanafiki sitaki watu feki
Wambie walio nicheat
Wakaniumiza roho
Sitaki wanafiki sitaki watu feki
Sijui ninyamaze ama niseme wanicheke
Ama nijikaze nilie ninyamaze nijiliwaze
“[emoji350][emoji444][emoji444]
 
ukishaanza kuwa mtu mzima na kufikia hatua ya kuoa ,huwezi ukapata muda wa kulalamikia marafiki
 
Mara nyingi nakaa chini, nawaza hawa ninaoita washkaji/marafiki, wanafaida gani na mimi? Nini wananiongezea ktk Maisha? Nikipata changamoto flani je kuna hata mmoja wa kunisaidia kwa haraka?

Mara nyingi mimi ndio backup yao, mtu anakupigia simu anakwambia shida zake na anakazia kabisa kwamba ameona mimi ndio wa kumuokoa haoni sehemu nyingine. Sasa nawaza kwanini kwenye shida ndio mtu unapewa kipaumbele?..

Kwa kweli Maisha ya Urafiki ni kwa vijana waliovyuoni etc.. ila ukishaanza Maisha ya kujitafuta, Maisha ya kujijenga kiuchumi Marafiki sio wa kuwaweka karibu..

Inatakiwa kutofautisha neno MTU wa KARIBU na RAFIKI.

Pia watu unaofahamiana nao na RAFIKI.

Soo kuna levels..
 
Inasikitisha sana....lkn chakushangaza mm hua nasaidiwa nawatu nisiowatarajia kabisa in hard times..hadi najisemea hivi marafiki zangu mbona wanafeli hivi..asimlia 99%ya misaaada niliyowahi kuiomba kutoka kwa marafiki hawakunisaidia bali nimesaidiwa nawatu ambao wamejitokeza tu on the way .hata sikuwahi kuwafikiria kabisa..hii ni personal life experiences.
 
Paragraph ya mwisho mzee umebugi big time.... Kama kweli ndio ilivyo kama ulivyoandika hapo I promise you utakuja kulia hapa tena, just a matter of time.
 
Back
Top Bottom