Wazanzibar hatuutaki Muungano na Tanganyika

Wazanzibar hatuutaki Muungano na Tanganyika

Huu uzi haufai kujadiliwa JF kwani unachochea ukatili na umwagaji damu.Tafadhari Mods uondoeni haraka iwezekanavyo kwa maslahi ya taifa.
 
Anzeni kwanza kuondoka huku bara , mnapiga kelele wakati bado mpo tanganyika!
 
pamoja na yote yanayojiri, ikiwa ni pamoja na kutetea kwa hoja umuhim wa muungano, uwepo wa serikali mbili au 3, hadi kufikia malumbano makubwa katika bunge la katiba na hata mitaani

tuongee ukweli kabisa bila kubabaisha maneno kwa kujiuliza mbona bara tunaonekana kuutaka sana mungano ukilinganisha na wazanzibari?imefikia kiasi cha kuugaramia kwa mapesa mengi, inasemekana wazanzibar wamekuwa wakitegea kulipia garama za muungano lakini bara tunalipia tu tena bila kinyongo

hilo dogo, kubwa ni hili hapa, miaka ya 1980s kuzungumzia habari za muungano ilikuwa sawa na kuweka reheni kibarua chako kama ilivowatokea akina abou jumbe, si hivo tu kuweka rehani kibarua bali pia hata hatari ya kupoteza uhai kisa tu, umehoji swala la muungano, speech alio itoa tundu lissu,bungeni kuhusu muungano asingesubutu miaka ya sabini na themanini, sasa jiulize jambo gani jema liendeshwe on that way

siku ya muungano, naona katika picha palichanganywa mchanga wa bara na visiwani, na inasemekana (sijui kweli) eti ule mchanga ulienda mwagwa baharini, sijui kama kweli na kama ni kweli kulikuwa na sababu gani?

kama kweli zile ni hati sahihi za muungano, ukitaka kuona kihoja tuombe na nakala iliyopelekwa UNO nauhakika zitakuwa tofauti kabisa, maana kama hii iliyoletwa inakasoro hasa katika sahihi ya karume, swali la kujiuliza kama muungano ni very crucial na una muhimu na faida pande zote iweje bara tuonekane ndio tunaojua zaid kuliko hao zanziba?sikatai kuwa kuna wazanzibar wanotaka muungano,ki ukweli wapo lakini tunaangalia wimbi kubwa.

tusidanganyane muungano unajambo, jambo lenyewe hatulijua, wapo wnao lijua akina government officials, ni mtazamo tu jamani
 
ndo unaamka sasa!? Haya siku njema.
 
Unataka muungano gani zaidi ya huo wako na demu wako.
 
usiogope watanganyika kibao hatuutaki muungano,tumekuwa masikini 7babu pesa za walipa kodi zinapelekwa zenji kuendesha serikal,huku wapemba wakipata viwanja tanganyika bila matatizo,amkeni WATANGANYIKA
 
Nyerer aliipigania uhuru nchi kwa hio yafaa aheshimiwe, maamuzi aliyofanya yalikuwa ya kimkakati zaidi kuja kutufaiasha.

Najua watu wanalalamika na kusikia maumivu wanapoona wazanzibar inabidi wapewe asilimia 21 za ajira Tanzania, kupewa uongozi sekta / taasisi nyeti, kuwa na vitambulisho vyao, kumiliki ardhi, n.k. hivi ni vitu vidogo sana na ilibidi wapewe ili wakubali muungano.

Faida moja wapo kwa Tanganyika kwenye huu muungano ni ulinzi, Zanzibar ipo eneo ambalo limekaa kimkakati, inaweza kutumika kimkakati kuivamia Tanzania bara na kupora ardhi.

Nashangaa sana watu wanaompinga Nyerere
 
Najaribu kufikiri nje ya boksi. Hivi tusingekuwa na maisha fulani hivi hata kama tusingekuwa na muungano. Si tungekuwa wananchi wa nchi fulani hivi hata kama sio hii Tanzania tunayoiona leo. Nawaza zaidi, hivi asingekuwepo JN ndio tusingepata uhuru kabisa?
 
Wanaopinga muungano n wale vizaz vya mababu waoga na wauza nchi ambao kpnd kile cha ukolon, wenye akil walkuwa bze kupambania uhuru, wakat haya mababu mengne yako bze kukmbzana uch maporin.
 
Tangu tumepata uhuru migogoro ya mipaka imetokea Uganda na Malawi. Idi Amin ndiye aliyevamia Tanzania
 
Asikosolewe kwani yeye ni nani? BTW mambo mengi aliyafanya kwa wakati ule ilimlazimu kufanya yale aliyofanya ila kwa dunia ya sasa hayana relevance Tena.

Pia mengi aliyofanya alilazimika kwa sababu dunia aliyokuwa anashindana nayo ilikuwa mbele sana kwa kila kitu especially teknolojia tofauti na Sasa mambo mengi yapo wazi.

Wakati huo alichagua wrong side ambayo ilikuwa USSR na wakomunisti ambao hakujua kwamba walikuwa kwenye stage mbaya ya kusambaratika despite ya upelelezi tuliokuwa tunajisifia.
 
Kwanin Nyerere asipingwe? Kama hoja zake zimepitwa na wakati au kuna hoja nzuri zaidi kwanin asipingwe?
 
Najaribu kufikiri nje ya boksi. Hivi tusingekuwa na maisha fulani hivi hata kama tusingekuwa na muungano. Si tungekuwa wananchi wa nchi fulani hivi hata kama sio hii Tanzania tunayoiona leo. Nawaza zaidi, hivi asingekuwepo JN ndio tusingepata uhuru kabisa?
Nadhani baba wa taifa angekuwa Kambona, hadi sasa nchi ingekuwa imefika ilipofikia kwa mawazo ya Kambona
 
Hakika.....

Wengi wanaoupinga na kuukosoa vibaya muungano ni WATU WANAOANGALIA MAMBO KIFUPI/WAROHO WA MADARAKA/WABAGUZI NA WASIOPENDA UMOJA WETU WA KITANZANIA NA KIAFRIKA!!!

Siempre JMT
 
Think again; you’re wrong, my friend! Kwanza, Karume (sio Nyerere) ndiye aliyeomba uwepo huu muungano. Pili, majirani zetu wote potentially wanaweza kutumiwa na maadui zetu. Kumbuka, kuna visiwa vya Mombasa pia.
 
Back
Top Bottom