Wazanzibar kuongoza Wizara/Taasisi zisizo za Muungano imekaaje kisheria?

Wazanzibar kuongoza Wizara/Taasisi zisizo za Muungano imekaaje kisheria?

Mkuu Gagi, hili liko straight forward wala halihitaji tafsiri yoyote ya kisheria. Muungano wetu ni muungano very unique. Kwa upande mmoja, kitaifa na kimataifa, muungano wetu ni union, hivyo Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye rais mmoja, rais wa JMT, uraia mmoja tuu, uraia wa JMT, na raia wote wa JMT wana haki sawa. Lakini ndani ya muungano, muungano wetu ni federation, wenye nchi mbili, marais wawili na uraia wa aina mbili. Raia wa JMT na Ukaazi wa Zanzibar. Wazanzibari wote ni Watanzania na haki zote za uraia, ikiwemo kuajiriwa kuteuliwa kuongoza taasisi yoyote. Ila kwa upande wa Zanzibar, wenye haki ya kuajiriwa ni Wazanzibari wakaazi pekee.
P
Sheria ya uzanzibari ukaazi imetungwa lini?
Naamini kipindi cha mwalimu haikuwepo
 
Aisee,
Mkuu hivi ndo ilivyokaa ama umeamua wewe?
Mambo ambayo siyo ya Muungano ni mambo yanayohusu Tanganyika japo yatakuwa chini ya Rais wa muungano na hayahusu Zanzibar. Inakuwaje Mzanzibar ni Mtanzania lakini Manganyika si Mtanzania wakat Zanzibar ni sehemu ya Tanzania.
Binadamu tumeumbwa unique tofauti na wanyama wengine. Tutumie hata common sense Basi. Mzanzibar anaweza kuwa raisi wa Tanzania ambaye anaongoza , wizara zote, mikoa na wilaya. Inakuaje ashindwe kuteuliwa nafasi ya dc au rc? Wakati cheo Hiko Ni kidogo zaidi juu ya nafasi ya uraisi.
 
Katiba mpya, narudia tena katiba mpya.

Zanzibar kuna wizara ya fedha. Masauni anakuwaje tena huku kama waziri wa fedha?

Iko fyongo kwa wizara iliyoko Zanzibar kuwa na waziri au waajiriwa katika wizara ya kufanana huku.

Jipu hili laelekea kubaya.
Mwalimu Nyerere na Karume walikuwa na lengo zuri tu walipounda huu muungano. Shida ilikuja kwa waliopokea kijiti. Viongozi wa Zanzibar wakaanza ubinafsi wa kuilinda Zanzibar yao na viongozi wa Tanganyika wakaanza kuvuna Mali za nchi ili wawe matajiri.
Wote wakasahau lengo la Muungano sasa kilichobaki sijui ni nini?
 
Binadamu tumeumbwa unique tofauti na wanyama wengine. Tutumie hata common sense Basi. Mzanzibar anaweza kuwa raisi wa Tanzania ambaye anaongoza , wizara zote, mikoa na wilaya. Inakuaje ashindwe kuteuliwa nafasi ya dc au rc? Wakati cheo Hiko Ni kidogo zaidi juu ya nafasi ya uraisi.
Zanzibar nayo ni Tanzania kumbuka. Kwanini "uzanzibari ukaazi" na sio "utanganyika ukaazi"
 
Mwalimu Nyerere na Karume walikuwa na lengo zuri tu walipounda huu muungano. Shida ilikuja kwa waliopokea kijiti. Viongozi wa Zanzibar wakaanza ubinafsi wa kuilinda Zanzibar yao na viongozi wa Tanganyika wakaanza kuvuna Mali za nchi ili wawe matajiri.
Wote wakasahau lengo la Muungano sasa kilichobaki sijui ni nini?

Hapa kimebaki katiba mpya ya kuyaweka mambo sawa.

Mezani hakuwahi kuharibika jambo.
 
1972 Mwl Nyerere alimchagua Ally Hassan Mwinyi kuwa Waziri wa Afya japo Wizara hiyo haikuwa sehenu ya Mambo ya Muungano

Mwaka 2000 Mzee Benjamin Mkapa alimteua Hussein Ally Hassan Mwinyi kuwa Naibu Waziri wa Afya

Hata Mwana dada Engineer sikumbuki jina lake ambae kwa sasa ndio Katibu Mkuu Kiongozi Znz aliteuliwa na Hayati Dr Magufuli kuwa RAS wa Tanga japo Tamisemi sio sehemu ya Mambo ya Muungano

Kila Mzanzibar ni Mtanzania lakin sio Kila Mtanzania ni Mzanzibar

Hata Hussein Mwinyi alishakuwa Mbunge wa Mkuranga
 
Habari wanajamvi,

Wiki hzi tatu au mwezi huu tumekuwa na mijadala mingi hasa inayohusu uteuzi na teuzi mbalimbali.

Kinacholeta mjadala kingine ni katika masuala ya Muungano, Nacho nauliza kama ifuatavyo:

1. Je, inaruhusiwa kwa Mzanzibari kuongoza Wizara/taasisi ambayo haipo katika masuala ya Muungano, mfano Afya?

2. Kama ni sahihi, je mbona Watanganyika hatupewi nafasi za kuongoza wizara/taasisi zisizo za muungano kule Zanzibar?

3.Kama si sahihi, je ni kwa nini kinafanywa na nini kifanyike?
Ndio unastuka leo? Hii nchi inakaribia kuwa ya Wazanzibari pekee na kusilimishwa.

Wabikkah Tawfiq,
 
Ni either tuwe na serikali moja au tuwe na serikali tatu. Hiki kilichopo sasa hivi ni uhuni.
Serikali tatu ni mzigo ,kutaongezea gharama bure kwa ajili ya faida ya wachache, hao wote watajipangia kujengewa mihekalu ya kufa mtu, watajipangia mibenzi, kifupi muungano usiwepo kila mtu achukue 50 zake. Ukisema serikali moja jamaa zetu wabishi watasema watamezwa , wao wanaona kama bara ndio tunawahitaji zaidi kuliko wao wanavyotuhitaji. Pia mimi naona zile sababu za kuwepo muungano kwa wakti huu hazina mshiko, mambo ya vita baridi kati ya nchi za Magharibi na Mashariki hayapo, hatuihitaji Zanzibar kwa ajili ya usalama wa bara!
 
Habari wanajamvi,

Wiki hzi tatu au mwezi huu tumekuwa na mijadala mingi hasa inayohusu uteuzi na teuzi mbalimbali.

Kinacholeta mjadala kingine ni katika masuala ya Muungano, Nacho nauliza kama ifuatavyo:

1. Je, inaruhusiwa kwa Mzanzibari kuongoza Wizara/taasisi ambayo haipo katika masuala ya Muungano, mfano Afya?

2. Kama ni sahihi, je mbona Watanganyika hatupewi nafasi za kuongoza wizara/taasisi zisizo za muungano kule Zanzibar?

3.Kama si sahihi, je ni kwa nini kinafanywa na nini kifanyike?
Maajabu ukienda Mtanganyika ukitafuta kazi za serikalini hawakubali ila Wazanzibar kibao wako kwenye taasisi mbali mbali za serikali. Nashindwa kuelewa hapo hizi ni nchi mbili tofauti au ni Jamhuri ya Wadanganyika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binadamu tumeumbwa unique tofauti na wanyama wengine. Tutumie hata common sense Basi. Mzanzibar anaweza kuwa raisi wa Tanzania ambaye anaongoza , wizara zote, mikoa na wilaya. Inakuaje ashindwe kuteuliwa nafasi ya dc au rc? Wakati cheo Hiko Ni kidogo zaidi juu ya nafasi ya uraisi.
Ndiyo tunajua anaweza. Tatizo wewe unaonaje , imekaa sawa hiyo?
 
Back
Top Bottom