Wazazi acheni uhuni na visingizio, toeni urithi kwa watoto. Elimu sio urithi!

Wazazi acheni uhuni na visingizio, toeni urithi kwa watoto. Elimu sio urithi!

Umesema ukweli kabisa
Waache visingizio urithi sio elimu
Shenzy urithi mkipewa mnakuwa walevi mbwa.Mi.mwanangu nimepanga asome mwisho form four nauza nyumba anaenda kusomea MAGIC aje kufanya maonesho tupige hela Africa bado kuja wehu wengi
 
Shenzy urithi mkipewa mnakuwa walevi mbwa.Mi.mwanangu nimepanga asome mwisho form four nauza nyumba anaenda kusomea MAGIC aje kufanya maonesho tupige hela Africa bado kuja wehu wengi



🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Hivi anadhani kila mtu ana nyumba zaidi ya moja? Au benki ana billion?

Kwanza elewa kuwa mtu mwenye nyumba zaidi ya moja mjini ni mtu aliyezaliwa kijijini katika umaskini na nyumbani kwao alipokulia waliishi nyumba ya nyasi au matope! Huwezi kukuta mfano mtoto wa Nyerere ana nyumba zaidi ya moja. Mtoto wa mzee ruksa anatawala vizuri Zenji sababu hakuzaliwa katika family za kifukara kama zetu - tamaa na uroho!
Fikiria mtu unaoa ukiwa na 30! Unastaafu mtoto akiwa naye anaoa wewe upo 60! Kiinua mgongo unapata 300M na tunatumai bado una miaka 30 mbele ya kuishi. Hiyo pesa unanunua bondi ili kila mwezi upate million 3, ili maisha yasonge. Huyu mvuta bangi anaona uzigawe kwa watoto ili ule mafi (kichagga)? Ukijaliwa unakufa wakati mjukuu anaoa! Je, urithi wa mtoto una maana kweli?
Kumbe mchaga, nilijua tu nyie wazee ndio mana mnapigwa ndele na watoto/wake zenu kisa roho mbaya za ubinafsi zilowajaa.
Wazee wengi wa kichaga wana roho mbaya sana tena za uchoyo hasa wale waliozaliwa ama kukulia huko uchagani ndio mana hawanaga maelewano mazuri na watoto wao pamoja na wake zao mifano ninayo mingi sana, waze wa kule ni kavu sana.
 
Shenzy urithi mkipewa mnakuwa walevi mbwa.Mi.mwanangu nimepanga asome mwisho form four nauza nyumba anaenda kusomea MAGIC aje kufanya maonesho tupige hela Africa bado kuja wehu wengi
🤸🏼‍♀️😂
 
Ndio uwape watoto Urithi usilete uhuni wako hapa.

Wewe sio Kwa vile ulikuwa na uwezo wa ku-fight ukadhani hata watoto wako au wajukuu watakuwa hivyo. Kama unafikiri hivyo jua akili zako zinamashaka,

Ninapoandika hapa simaanishi Mimi nategemea Urithi Hasha! Isipokuwa najaribu kuangalia Wale wenzangu na miye wasio na uwezo wa kupambana na maisha.
Tatizo hata mtoto akipewa urithi, inapofikia hali ya mzazi anahitaji msaada mtoto hudai yeye ana majukumu ya kuangalia familia yake (yaani wajukuu wa mzazi) hivyo siyo kipaumbele.

Kuna wazazi wameshuhudia wenzao wakipitia hali ngumu huku watoto waliopewa mali wakitanua mjini, hivyo wameamua heri kila mtu ashinde vita vyake.
 
Usikimbilie kurithi mali tu,
Madeni nayo pia hurithiwa,
Ila elimu unaipata hata kabla ya kufariki wazee so hiyo sio urithi ni haki yako na ni lazima kuipata na ikitokea ukaikosa utataabika ingawa unaweza ukawa tajiri wa mali lakini masikini wa elimu
 
Anapiga bange huko kwenye metaverse
Ni kweli, hizi kama sio bangi basi ni kuchanganyikiwa. Badala ya kijna kuwaza amepata mtaji wa elimu atafute mali yake mwenyewe, yeye anang'ang'ania urithi kutika kwa wazazi? Kwani mzazi yeye amepata wapi mali? Na mawazo kama haya ni sumu kwa vijana, matokeo yake ni vijana kuwaua wazazi wao ili waweze kurithi mali
 
WAZAZI ACHENI UHUNI NA VISINGIZIO VYA KIPUUZI. TOENI URITHI KWA WATOTO. ELIMU SIO URITHI

Anaandika Robert Heriel.
Yule shahidi kutoka Nyota ya Tibeli.

Andiko hili laweza waumiza wengi. Ikiwa unajihisi unamoyo dhaifu nakusihi usisome. Na ikiwa utasoma basi nisihusike na maumivu na madhara yatakayojitokeza nafsini mwako.

Niite Taikon wa Fasihi, Kuhani katika Hekalu jeusi.

Baba anamajukumu makuu matatu ndani ya familia, nayo ni;
1. Kuhakikisha ulinzi na usalama ndani ya familia(mke na watoto wake)
2. Kuihudumia familia( mke na watoto wake)
3. Kuzalisha Mali na kuandaa Urithi Kwa kizazi chake.

Hivyo Sisi Vijana tunapaswa tutambue mambo hayo matatu, mambo hayo hayana excuse nilazima yafanyike ili heshima ya Baba ilindwe.
Kabla hujaoa na kuzaa watoto lazima ujiulize, je unauwezo wa kumlinda na kumfanya Mkeo na watoto wawe salama?
Pili, unauwezo wankuwahudumia mke na watoto? Mwisho je mipango yako na uwezo wako ukoje katika kuzalisha na kuandaa Mali za Urithi Kwa watoto wako kulingana na nyakati na Zama watoto wako watakazoishi?

Siku za hivi karibuni kumezuka uhuni Fulani hivi Kwa wazazi hasa wababa kuleta visingizio vya kitoto kuhusiana na masuala ya kumuandaa mtoto na ulimwengu.

Wazazi acheni UHUNI, najua hampendi kuambiwa ukweli lakini hakuna jinsi acheni UHUNI. Najua wengine watakuja na maneno Yao ya kipumbavu na kutisha kuhusu laana lakini ukweli ni kuwa acheni uhuni. Hapa hakuna cha laana wala ndugu yake Radhi, huu ni ukweli, mnazingua.

Nawaambiaga Vijana kuwa kama Mzazi wako alishindwa kukupa Urithi usiondoke hapo nyumbani, kaa hapo hapo mpaka akupe kilichochako. Na Kama wazazi wako hawana makazi, muandame kokote mpaka kieleweke.
Vitisho vyao visikuogopeshe havina msingi wowote.

KIJANA ATAONDOKA NYUMBANI KWA BABA NA MAMA YAKE IKIWA HAYA YATAFANYIKA
1. Atapewa Urithi wake,
Na Kama ni mzaliwa wa Kwanza au wamwisho ndiye anayepaswa kurithi Mali kulingana na utamaduni wa kabila Lenu basi huyo atabaki.

2. Endapo atajiweza hata bila kupewa Urithi.
Wapo Vijana ambao wamejaliwa uwezo wankupambana mara wanapokua wakubwa, kijana Kama unajiona unauwezo wa kuendesha maisha yako pasipo Urithi pia inaruhusiwa.

3. Atataka kuoa.
Kijana akitaka kuoa itampasa aondoke nyumbani kwao, wazazi wampe kilichochake, sehemu ya Urithi wake aondoke nao. Na huo Urithi uwe reasonable sio umpe Redio au Feni useme ndio Urithi, Urithi utakaomsaidia mtoto aendeshe maisha yake.
Mara nyingi Urithi wa wazazi Bora hujikita katika nyenzo za uzalishaji Kama vile mashamba, viwanja, visima vya maji au Nyumba, mifugo Kama NG'OMBE au Mbuzi, Miradi ya biashara Kama maduka, viwanda, n.k.
Sio umpe mtoto vitu havieleweki ndio uote Nimempa Urithi, huo ninauita UHUNI.

Siku hizi wazazi wamekuja na visingizio vya hovyo kabisa. Unakuta mzazi anasema, Mimi mwanangu Nimempa Elimu ndio Urithi wake. Pumbavu!
Elimu sio Urithi elimu ni basic need Kwa mwanadamu ambayo mzazi lazima umpe mwanao.

Ni ujinga na upumbavu kusema mtoto wangu namrithisha Elimu, Mimi nilipokuwa naambiwa hivyo nilikuwa nakataa katakata kuwa elimu niendayo kusoma sio Urithi isipokuwa ni sehemu ya basic need kwa binadamu.

Urithi lazima kiwe kitu unachokimiliki, sasa unakuta mzazi hata hajasoma anakuambia nimekupa elimu kuwa Urithi wako, ajabu hii! Elimu ambayo hauna?
Au unakuta mzazi anaelimu kubwa tuu labda ni Daktari, alafu anamuambia mtoto wake ambaye anaelimu ya sheria au Mwalimu, anamwambia, nimekurithisha elimu, sio kweli.

Unaposema Urithi unazungumzia Jambo ambalo unalomilikilulilonalo na unalompa mtu Kwa hiyari au pasipo hiyari. Mfano Mtoto anawezarithi Sura au maumbile ya wazazi wake, sauti, akili, miondoko, magonjwa miongoni mwa mambo mengine. Hiyo tunasema huo ni Urithi.

Elimu sio sehemu ya Urithi labda AKILI inaweza kurithiwa.

Elimu lazima mzazi Ampe mtoto mbali na Urithi ili kumfanya mtoto aweze kuyakabili Mazingira na Mali alizozirithi kutoka Kwa wazazi wake.

Mfano;
Mzazi WA kimasai au kisukuma kabla hajamrithisha mtoto Mali/mifugo ni lazima amfundishe/Ampe elimu ya mifugo na namna ya kuchunga NG'OMBE, Mbuzi na Kondoo. Mtoto akishakua mtu mzima Baba ndio humrithisha mtoto wake Sehemu ya mifugo Kama Urithi na Kwa vile mtoto anaelimu ya mifugo basi haitamsumbua.

Kumbuka mzazi hawezi sema nimekupa Urithi WA elimu ya kufaga NG'OMBE Bali atasema nimekupa Mali/mifugo Kama Urithi, Kwa vile unaelimu ya mifugo basi waweza kutenda Kwa Amani na Mungu akufanikishe.

Mfano wa pili,
Kwa familia za Wakulima,
Mtoto hufundishwa kulima, kutambua magonjwa ya mimea na namna ya kuhifadhi chakula. Kisha akishakua na kutaka kujitegemea Mtoto atapewa Urithi WA mashamba ambayo atayatumia kuendesha familia yake.

Sio umpe mtoto elimu ya kilimo alafu akatafute mwenyewe Shamba huo ni uhuni.
Ni Bora umpe Shamba alafu akatafute mwenyewe Elimu ya kilimo, hivyo ndivyo ilivyo.

Sasa wazazi wa kileo Kwa ujanja ujanja hujiingiza gharama zisizo na maana kumpa mtoto elimu ambayo kimsingi Kama hataajiriwa basi itakuwa haina kazi yoyote.

Unamsomesha mtoto Ada Kwa mwaka milioni mbili Kwa miaka minne mpaka sita alafu akimaliza shule anakosa chakufanya alafu unamuambia asikulaumu, wewe si kichaa tuu.

Mtoto anamaliza shule, humpi hata Urithi WA Shamba au hata kiwanja ambacho kimsingi ungeweza kumnunulia Kwa Ada Ileile aliyosomea.
Yaani umsomeshe mtoto Kwa Ada ya milioni mbili alafu ushindwe kumfurahisha mtoto hata Shamba la laki tano[emoji1787][emoji1787][emoji1787] wewe Kama sio mwendawazimu ni Nani.

Sisemi kuwakamia hapa, najaribu Kueleza na kuamsha akili zetu.

Elimu sio Urithi, Hilo mkae mkilijua.

Mimi pia ni mzazi, siwezi waambia watoto wangu ati nimewarithisha Elimu [emoji3][emoji3]
Kwa kweli waliniona Baba Yao ni mhuni sitawalaumu.

Mzazi Bora ni Yule anayeacha Urithi Kwa watoto wake.
Elimu sio Urithi.

Elimu inatabia ya kubadilika kulingana na wakati. Unamsomesha mtoto hiki Kwa vile wakati huu kinalipa akimaliza kitu hicho kimepitwa na wakati, nazungumzia thamani yake imeshuka, thamani ya elimu inashuka kutokana na kuwa siku hizi kila mtu anaouwezo wa kuipata.

Elimu ya sasa sio elimu ya baadaye.

Lakini ardhi ya sasa, au Shamba la sasa ni hilohilo hata miaka Mia ijayo, tena thamani yake ndio inaongezeka.

Rithisha mtoto viwanja, nyumba, mashamba, viwanda Kama unavyo, visima vya maji, migodi Kama unayo, hotel au lodge, Mifugo sio Sana kwani tabia ya nchi na Hali ya hewa haitabiriki.

Sio mzazi unakazi ya kusumbua watoto wakutumie pesa kisa uliwazaa na kuwasomesha, uliwasomesha vitu visivyoeleweka. Mrithishe mtoto Mradi Kama mashamba au Nyumba au viwanja, ndio umuombe akuhudumie.

Sasa mtoto hata Mradi wankumuingizia kipato Hana, kuishi kwenyewe anaishi Kama Ndege, Kodi inamsumbua, chakula kinamsumbua, bado na wewe umsumbue, Doooh!! Huo unaitwa uhuni hata Kama watoto wanashindwa kutuambia.

Nani asiyejua maisha magumu pasipo kuwa na chakuanzia, Urithi ndio starting point ya mtoto.
Vijana wa sasa wanahangaika kutokana na makosa ya Sisi wazazi. Alafu tunatishia na laana. Pumbavu hakuna laana za hivyo.

Mtoto awaze Kodi.
Mtoto awaze chakula
Mtoto awaze mavazi yake,
Mtoto awaze atapata wapi mahari, alafu unakuta mzazi anakuuliza mbona hauoi utafikiri alikupa mahari, pumbavu.
Mtoto awaze namna ya kwenda ukweni,
Mtoto awaze Harusi,
Mtoto awaze kumhudumia mzazi wake
Mtoto awaze serikali.
Hayo kisa kisingizio cha kumsomesha?

Urithi haupitwi na wakati kwani ni Jambo la miungu, Mungu ndio kaliweka.
Elimu Kwa vile ni man-made lazima ipitwe na wakati.
Ndio maana Kwa miaka ya 90 mtu mwenye elimu alikuwa keshatoboa lakini sio Kwa Zama za sasa.

Wazazi tuache UHUNI, turithishe watoto Mali za uhakika zitakazowasaidia kuzalisha Mali au kuendesha maisha yao.

Ulikuwa nami, Baba mhuni.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Mabwepande, DAR ES SALAAM
Katika wazazi wabinafsi nadhani wa Tanzania wanaongoza kwa kuwa na msimamo wa eti mtoto atafute chake mfano mzuri mtoto wa Magu akuwaipewa gari kuendesha cha ajabu mzee kaondoka mali ndio zimebaki kwake sasa anafanya atavyo lakini mzee angeweza kumjenga jinsi yakuzutumia akiwa hai no wonder mali za urithi zinatumiwa vibaya sababu ya visasi na chuki.

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Tatizo hata mtoto akipewa urithi, inapofikia hali ya mzazi anahitaji msaada mtoto hudai yeye ana majukumu ya kuangalia familia yake (yaani wajukuu wa mzazi) hivyo siyo kipaumbele.

Kuna wazazi wameshuhudia wenzao wakipitia hali ngumu huku watoto waliopewa mali wakitanua mjini, hivyo wameamua heri kila mtu ashinde vita vyake.


Kosa bado linabaki Kwa mzazi
 
Katika wazazi wabinafsi nadhani wa Tanzania wanaongoza kwa kuwa na msimamo wa eti mtoto atafute chake mfano mzuri mtoto wa Magu akuwaipewa gari kuendesha cha ajabu mzee kaondoka mali ndio zimebaki kwake sasa anafanya atavyo lakini mzee angeweza kumjenga jinsi yakuzutumia akiwa hai no wonder mali za urithi zinatumiwa vibaya sababu ya visasi na chuki.

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app


Ogopa kitu inaitwa uvivu na Kupenda Dezo
 
Usikimbilie kurithi mali tu,
Madeni nayo pia hurithiwa,
Ila elimu unaipata hata kabla ya kufariki wazee so hiyo sio urithi ni haki yako na ni lazima kuipata na ikitokea ukaikosa utataabika ingawa unaweza ukawa tajiri wa mali lakini masikini wa elimu


Unafikiri mzazi akifa madeni yake yanalipwa na Nani?
 
Ogopa kitu inaitwa uvivu na Kupenda Dezo
Uvivu ni character inayojengwa once motivation ikiwepo uvivu hauwezi kuwepo so ni jinsi unavyo mlea na misingi unayoweka kwa vijana wako..Leo hii Jack Chan kadeclare mali zake zote akifa zienda kwa yatima kitu ambacho watu awajui hamna mtu mwenye mentality ya kibabylon kama huyo Jack japo anasababu ya msingi baada ya mtoto wake kuwa na skendo za madawa akasema kama nikiwa hai ameshindwa tumia mali zangu ata nikifa hataweza zitumia vizuri bora niwape yatima zote...

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Huo ndio Uelewa wako.

Mtu anaweza kupewa Urithi hata mzazi akiwa hai. Ni wazazi wapumbavu AMBAO husubiri kifo ndio warithishe watoto.

Mali inayosubiri kifo cha mzazi ni Yale makazi yake ambayo humrithisha mtoto wa Kwanza au wamwisho kulingana na Mila na tamaduni husika.

Hujaona watu wakipewa mashamba, nyumba au viwanja siku ya Harusi?
Unadhani zile zawadi ni nini wewe usiye mjinga?
 
Uko sahihi Elimu inaweza isiwe Urithi.

Kwangu mimi mambo ya urithi naona ni ujinga unaofanya familia zizidi kuwa masikini hivyo hakuna kitu nakichukia kama urithi kwenye mambo ya familia.

Urithi unafanya watoto wabweteke wasichangamshe akili kutafuta vyao na kutengeneza mategemezi, hii inapelekea familia kuwa masikini zaidi sababu watoto watakaa kusubiria ufe wachukue chao (kama mzazi ulivyowaaminisha).

Na urithi wa mali ni mpaka mmiliki afe au kama wakikurithisha wakati yeye yupo hai then atabaki na nini?
Pia urithi wa mali unagawanya familia sababu kila mtu atakuwa anachomoa chake na kuondoka na kama hakuna umoja na ushirikiano then hakuna familia wala hakuna nguvu tena.

Na wewe umeshawahi kujiuliza kwanini baba yako haishi kwa wazazi wake?
Unajua jinsi gani baba yako alipata alivyonavyo sasa hivi? Je alitegemea urithi?
Kama hakutegemea urithi kwanini wewe ulilie urithi?

Maana ya Familia ni kukusanyika pamoja ili kuleta ushirikiano na umoja ili kuzalisha nguvu.
Kama ule msemo maarufu wa "umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu"..

Sasa badala ya wazazi kugawa urithi.
Cha kufanya ni kumwambia kila kima mmoja atafute chake na baada ya hapo basi aende kuongezea kwenye mali za familia.
Hii italeta umoja na ushirikiano kwenye familia na kwenye umoja na ushirikiano kuna Nguvu.
Nguvu hii itatumika na itafanya Familia izidi kuimarika kila uchwao badala ya kugawanyika na kudhoofika baada ya kugawana urithi.

Mtu unayempa ugali kila siku lazima atakuja kwako kila siku kufuata ugali, badala ya kumpa ugali mpe njia ulizotumia kuupata huo ugali ili atafute wake.

Mtu ukimpatia urithi haijarishi ni kiasi gani cha mali basi hazitofika popote lazima zitapotea tu na kuisha kabisa.
Sababu hajui jinsi gani umezipata au mangapi umepitia na kuhangaika kiasi gani, hana uchungu nazo wala hajui moto wa jiwe.
Na hiyo ndio sababu familia tajiri huwa masikini ghalfa baada ya mmiliki kufa na kurithisha mali kwa watoto.

Lakini ukimwambia na kumfundisha njia ulizopita mpaka kupata vya kwako na yeye apite hizo'hizo mpaka kupata vya kwake.
Basi lazima atakuwa na uchungu wa mali zake kutokana na msoto aliopitia na atakuwa na nidhamu nazo na kamwe hatojaribu kuzichezea na kuzipoteza kizembe. hivyo hata zile za kwako atakuwa na uwezo wa kuziendeleza.

Kulilia Urithi ni dalili ya Uvivu wa kimwili, kufikiri na kiakili na ni vibaya zaidi ukimfundisha hivi mtoto wa kiume sababu ataamini ni haki yake kupewa now that's really bad.
Sababu mtoto wa kiume anatakiwa afundishwe kupambana na kutafuta vyake mwenyewe no matter what.

Wanangu nitawaambia jinsi ya kupamba na maisha na kuwa adaptable na mazingira yoyote huku wakiendeleza nilichokianzisha kwa kuongeza vya kwao juu yake haijalishi ni wakike au wakiume wote nitawakazia kibabe ila wakiume itakuwa more severe..
Ni kufight till you drop dead hakuna cha bure hata kama nilikuzaa.
 
Uko sahihi Elimu inaweza isiwe Urithi.

Kwangu mimi mambo ya urithi naona ni ujinga unaofanya familia zizidi kuwa masikini hivyo hakuna kitu nakichukia kama urithi kwenye mambo ya familia...
Urithi ungekuwa ujinga hii nchi ingekuwa Yenu?

Itashangaza mtu ni msomi asielwe concept ndogo niliyoieleza, pia itashangaza Kama mtu anaumri wa zaidi ya miaka 25 asielewe mantiki ha kile kilichozungumzwa hapa.
 
Urithi ungekuwa ujinga hii nchi ingekuwa Yenu??

Itashangaza mtu ni msomi asielwe concept ndogo niliyoieleza, pia itashangaza Kama mtu anaumri wa zaidi ya miaka 25 asielewe mantiki ha kile kilichozungumzwa hapa.
Sidhani hata kama umemaliza kusoma nilichokiandika.
Post nilipost dk 4 zilizopita na wewe umejibu dk 3 zilizopita.

Means umesoma andiko lote ndani ya dk 1 that's impossible.
 
Sidhani hata kama umemaliza kusoma nilichokiandika.
Post nilipost dk 4 zilizopita na wewe umejibu dk 3 zilizopita.

Means umesoma andiko lote ndani ya dk 1 that's impossible.
Nimesoma Mkuu.

Nimekuelewa,

Ninachojaribu Kueleza hapa ni kuwa wazazi tuhakikishe tunaacha Urithi Kwa watoto, nchi kubwa hivi ushindwe kuacha Urithi Kwa kweli itakuwa uzembe.

Labda sababu za Maradhi makuu, na kifo yaingilie kati
 
Back
Top Bottom