Wazazi acheni uhuni na visingizio, toeni urithi kwa watoto. Elimu sio urithi!

Wazazi acheni uhuni na visingizio, toeni urithi kwa watoto. Elimu sio urithi!

Huu uzi tuwatoe wazazi wetu ambao hapo awali walisoma huku wakijua baada ya kuhitimu naenda kuajiriwa. Kwa sasa anayemaliza darasa la saba akaingia mtaani mwingine akaenda shule baada ya miaka 6 (sec) +3 Chuo = 10, aliyeachwa mtaani tayari ana familia na fani ya kumwezesha kuendesha maisha. Aliyetoka chuo hafai kwa wazazi wala kwa ulimwengu. Inabidi arudi kwa washkaji wa kitaa wamfundishe fani alizoziacha akaenda shule.

Mambo yamebadilika. Tusiache kusomesha lakini tusiache kuandaa rasilimali za urithi. Ni kweli Elimu si urithi


Hii inamgusa yeyote hata niliyeandika.

Shida Wanadamu hawapendi ukweli
 
Anapiga bange huko kwenye metaverse
Hivi anadhani kila mtu ana nyumba zaidi ya moja? Au benki ana billion?

Kwanza elewa kuwa mtu mwenye nyumba zaidi ya moja mjini ni mtu aliyezaliwa kijijini katika umaskini na nyumbani kwao alipokulia waliishi nyumba ya nyasi au matope! Huwezi kukuta mfano mtoto wa Nyerere ana nyumba zaidi ya moja. Mtoto wa mzee ruksa anatawala vizuri Zenji sababu hakuzaliwa katika family za kifukara kama zetu - tamaa na uroho!
Fikiria mtu unaoa ukiwa na 30! Unastaafu mtoto akiwa naye anaoa wewe upo 60! Kiinua mgongo unapata 300M na tunatumai bado una miaka 30 mbele ya kuishi. Hiyo pesa unanunua bondi ili kila mwezi upate million 3, ili maisha yasonge. Huyu mvuta bangi anaona uzigawe kwa watoto ili ule mafi (kichagga)? Ukijaliwa unakufa wakati mjukuu anaoa! Je, urithi wa mtoto una maana kweli?
 
Huu uzi tuwatoe wazazi wetu ambao hapo awali walisoma huku wakijua baada ya kuhitimu naenda kuajiriwa. Kwa sasa anayemaliza darasa la saba akaingia mtaani mwingine akaenda shule baada ya miaka 6 (sec) +3 Chuo = 10, aliyeachwa mtaani tayari ana familia na fani ya kumwezesha kuendesha maisha. Aliyetoka chuo hafai kwa wazazi wala kwa ulimwengu. Inabidi arudi kwa washkaji wa kitaa wamfundishe fani alizoziacha akaenda shule.

Mambo yamebadilika. Tusiache kusomesha lakini tusiache kuandaa rasilimali za urithi. Ni kweli Elimu si urithi
Hivi mzazi wako ana kipi cha ziada ili akurithishe? Au unataka a distributed poverty tu
 
Huo ndio Uelewa wako.

Mtu anaweza kupewa Urithi hata mzazi akiwa hai. Ni wazazi wapumbavu AMBAO husubiri kifo ndio warithishe watoto.

Mali inayosubiri kifo cha mzazi ni Yale makazi yake ambayo humrithisha mtoto wa Kwanza au wamwisho kulingana na Mila na tamaduni husika.

Hujaona watu wakipewa mashamba, nyumba au viwanja siku ya Harusi?
Unadhani zile zawadi ni nini wewe usiye mjinga?

Kwahiyo zawadi ni urithi! Hovyo kabisa.
 
Kuna kina sie ambao tuna hakika hatuna cha kurithi hata itokee mshua kaitwa leo hii na Bwana!mali zote zinarithiwa na watoto wa mama mwingine,
Kwenye uzi inabidi tupite kimyakimya!
 
Mkuu, mzee baba, umepiga pale pale penye tatizo, la umaskini wetu wa fikra. Ni kweli elimu siyo urithi. Mungu akujaze nguvu ya kuzidisha mashambulizi katika ngome ya adui yetu namba moja aitwaye ujinga yaani ukosefu wa maarifa.
 
Mzee akiwa bado hai huo sio urithi ni uvivu wa kufikiri na uzembe wa kutafuta vyako, mzazi kukazaa, kakutunza,amekusomesha kuanzia chekechea mpaka umehitimu chuo kikuu au hiyo form four yako,nenda katafuta mali zako ili uishi maisha yako na umsaidie huyo aliyesababisha ukaweza kuleta huu uzi.
 
Kama kweli aisee yani kanakuja flani hivi ila sema n? kila mtu na familia yake tusizoeane sana
 
WAZAZI ACHENI UHUNI NA VISINGIZIO VYA KIPUUZI. TOENI URITHI KWA WATOTO. ELIMU SIO URITHI

Anaandika Robert Heriel.
Yule shahidi kutoka Nyota ya Tibeli.

Andiko hili laweza waumiza wengi. Ikiwa unajihisi unamoyo dhaifu nakusihi usisome. Na ikiwa utasoma basi nisihusike na maumivu na madhara yatakayojitokeza nafsini mwako.

Niite Taikon wa Fasihi, Kuhani katika Hekalu jeusi.

Baba anamajukumu makuu matatu ndani ya familia, nayo ni;
1. Kuhakikisha ulinzi na usalama ndani ya familia(mke na watoto wake)
2. Kuihudumia familia( mke na watoto wake)
3. Kuzalisha Mali na kuandaa Urithi Kwa kizazi chake.

Hivyo Sisi Vijana tunapaswa tutambue mambo hayo matatu, mambo hayo hayana excuse nilazima yafanyike ili heshima ya Baba ilindwe.
Kabla hujaoa na kuzaa watoto lazima ujiulize, je unauwezo wa kumlinda na kumfanya Mkeo na watoto wawe salama?
Pili, unauwezo wankuwahudumia mke na watoto? Mwisho je mipango yako na uwezo wako ukoje katika kuzalisha na kuandaa Mali za Urithi Kwa watoto wako kulingana na nyakati na Zama watoto wako watakazoishi?

Siku za hivi karibuni kumezuka uhuni Fulani hivi Kwa wazazi hasa wababa kuleta visingizio vya kitoto kuhusiana na masuala ya kumuandaa mtoto na ulimwengu.

Wazazi acheni UHUNI, najua hampendi kuambiwa ukweli lakini hakuna jinsi acheni UHUNI. Najua wengine watakuja na maneno Yao ya kipumbavu na kutisha kuhusu laana lakini ukweli ni kuwa acheni uhuni. Hapa hakuna cha laana wala ndugu yake Radhi, huu ni ukweli, mnazingua.

Nawaambiaga Vijana kuwa kama Mzazi wako alishindwa kukupa Urithi usiondoke hapo nyumbani, kaa hapo hapo mpaka akupe kilichochako. Na Kama wazazi wako hawana makazi, muandame kokote mpaka kieleweke.
Vitisho vyao visikuogopeshe havina msingi wowote.

KIJANA ATAONDOKA NYUMBANI KWA BABA NA MAMA YAKE IKIWA HAYA YATAFANYIKA
1. Atapewa Urithi wake,
Na Kama ni mzaliwa wa Kwanza au wamwisho ndiye anayepaswa kurithi Mali kulingana na utamaduni wa kabila Lenu basi huyo atabaki.

2. Endapo atajiweza hata bila kupewa Urithi.
Wapo Vijana ambao wamejaliwa uwezo wankupambana mara wanapokua wakubwa, kijana Kama unajiona unauwezo wa kuendesha maisha yako pasipo Urithi pia inaruhusiwa.

3. Atataka kuoa.
Kijana akitaka kuoa itampasa aondoke nyumbani kwao, wazazi wampe kilichochake, sehemu ya Urithi wake aondoke nao. Na huo Urithi uwe reasonable sio umpe Redio au Feni useme ndio Urithi, Urithi utakaomsaidia mtoto aendeshe maisha yake.
Mara nyingi Urithi wa wazazi Bora hujikita katika nyenzo za uzalishaji Kama vile mashamba, viwanja, visima vya maji au Nyumba, mifugo Kama NG'OMBE au Mbuzi, Miradi ya biashara Kama maduka, viwanda, n.k.
Sio umpe mtoto vitu havieleweki ndio uote Nimempa Urithi, huo ninauita UHUNI.

Siku hizi wazazi wamekuja na visingizio vya hovyo kabisa. Unakuta mzazi anasema, Mimi mwanangu Nimempa Elimu ndio Urithi wake. Pumbavu!
Elimu sio Urithi elimu ni basic need Kwa mwanadamu ambayo mzazi lazima umpe mwanao.

Ni ujinga na upumbavu kusema mtoto wangu namrithisha Elimu, Mimi nilipokuwa naambiwa hivyo nilikuwa nakataa katakata kuwa elimu niendayo kusoma sio Urithi isipokuwa ni sehemu ya basic need kwa binadamu.

Urithi lazima kiwe kitu unachokimiliki, sasa unakuta mzazi hata hajasoma anakuambia nimekupa elimu kuwa Urithi wako, ajabu hii! Elimu ambayo hauna?
Au unakuta mzazi anaelimu kubwa tuu labda ni Daktari, alafu anamuambia mtoto wake ambaye anaelimu ya sheria au Mwalimu, anamwambia, nimekurithisha elimu, sio kweli.

Unaposema Urithi unazungumzia Jambo ambalo unalomilikilulilonalo na unalompa mtu Kwa hiyari au pasipo hiyari. Mfano Mtoto anawezarithi Sura au maumbile ya wazazi wake, sauti, akili, miondoko, magonjwa miongoni mwa mambo mengine. Hiyo tunasema huo ni Urithi.

Elimu sio sehemu ya Urithi labda AKILI inaweza kurithiwa.

Elimu lazima mzazi Ampe mtoto mbali na Urithi ili kumfanya mtoto aweze kuyakabili Mazingira na Mali alizozirithi kutoka Kwa wazazi wake.

Mfano;
Mzazi WA kimasai au kisukuma kabla hajamrithisha mtoto Mali/mifugo ni lazima amfundishe/Ampe elimu ya mifugo na namna ya kuchunga NG'OMBE, Mbuzi na Kondoo. Mtoto akishakua mtu mzima Baba ndio humrithisha mtoto wake Sehemu ya mifugo Kama Urithi na Kwa vile mtoto anaelimu ya mifugo basi haitamsumbua.

Kumbuka mzazi hawezi sema nimekupa Urithi WA elimu ya kufaga NG'OMBE Bali atasema nimekupa Mali/mifugo Kama Urithi, Kwa vile unaelimu ya mifugo basi waweza kutenda Kwa Amani na Mungu akufanikishe.

Mfano wa pili,
Kwa familia za Wakulima,
Mtoto hufundishwa kulima, kutambua magonjwa ya mimea na namna ya kuhifadhi chakula. Kisha akishakua na kutaka kujitegemea Mtoto atapewa Urithi WA mashamba ambayo atayatumia kuendesha familia yake.

Sio umpe mtoto elimu ya kilimo alafu akatafute mwenyewe Shamba huo ni uhuni.
Ni Bora umpe Shamba alafu akatafute mwenyewe Elimu ya kilimo, hivyo ndivyo ilivyo.

Sasa wazazi wa kileo Kwa ujanja ujanja hujiingiza gharama zisizo na maana kumpa mtoto elimu ambayo kimsingi Kama hataajiriwa basi itakuwa haina kazi yoyote.

Unamsomesha mtoto Ada Kwa mwaka milioni mbili Kwa miaka minne mpaka sita alafu akimaliza shule anakosa chakufanya alafu unamuambia asikulaumu, wewe si kichaa tuu.

Mtoto anamaliza shule, humpi hata Urithi WA Shamba au hata kiwanja ambacho kimsingi ungeweza kumnunulia Kwa Ada Ileile aliyosomea.
Yaani umsomeshe mtoto Kwa Ada ya milioni mbili alafu ushindwe kumfurahisha mtoto hata Shamba la laki tano[emoji1787][emoji1787][emoji1787] wewe Kama sio mwendawazimu ni Nani.

Sisemi kuwakamia hapa, najaribu Kueleza na kuamsha akili zetu.

Elimu sio Urithi, Hilo mkae mkilijua.

Mimi pia ni mzazi, siwezi waambia watoto wangu ati nimewarithisha Elimu [emoji3][emoji3]
Kwa kweli waliniona Baba Yao ni mhuni sitawalaumu.

Mzazi Bora ni Yule anayeacha Urithi Kwa watoto wake.
Elimu sio Urithi.

Elimu inatabia ya kubadilika kulingana na wakati. Unamsomesha mtoto hiki Kwa vile wakati huu kinalipa akimaliza kitu hicho kimepitwa na wakati, nazungumzia thamani yake imeshuka, thamani ya elimu inashuka kutokana na kuwa siku hizi kila mtu anaouwezo wa kuipata.

Elimu ya sasa sio elimu ya baadaye.

Lakini ardhi ya sasa, au Shamba la sasa ni hilohilo hata miaka Mia ijayo, tena thamani yake ndio inaongezeka.

Rithisha mtoto viwanja, nyumba, mashamba, viwanda Kama unavyo, visima vya maji, migodi Kama unayo, hotel au lodge, Mifugo sio Sana kwani tabia ya nchi na Hali ya hewa haitabiriki.

Sio mzazi unakazi ya kusumbua watoto wakutumie pesa kisa uliwazaa na kuwasomesha, uliwasomesha vitu visivyoeleweka. Mrithishe mtoto Mradi Kama mashamba au Nyumba au viwanja, ndio umuombe akuhudumie.

Sasa mtoto hata Mradi wankumuingizia kipato Hana, kuishi kwenyewe anaishi Kama Ndege, Kodi inamsumbua, chakula kinamsumbua, bado na wewe umsumbue, Doooh!! Huo unaitwa uhuni hata Kama watoto wanashindwa kutuambia.

Nani asiyejua maisha magumu pasipo kuwa na chakuanzia, Urithi ndio starting point ya mtoto.
Vijana wa sasa wanahangaika kutokana na makosa ya Sisi wazazi. Alafu tunatishia na laana. Pumbavu hakuna laana za hivyo.

Mtoto awaze Kodi.
Mtoto awaze chakula
Mtoto awaze mavazi yake,
Mtoto awaze atapata wapi mahari, alafu unakuta mzazi anakuuliza mbona hauoi utafikiri alikupa mahari, pumbavu.
Mtoto awaze namna ya kwenda ukweni,
Mtoto awaze Harusi,
Mtoto awaze kumhudumia mzazi wake
Mtoto awaze serikali.
Hayo kisa kisingizio cha kumsomesha?

Urithi haupitwi na wakati kwani ni Jambo la miungu, Mungu ndio kaliweka.
Elimu Kwa vile ni man-made lazima ipitwe na wakati.
Ndio maana Kwa miaka ya 90 mtu mwenye elimu alikuwa keshatoboa lakini sio Kwa Zama za sasa.

Wazazi tuache UHUNI, turithishe watoto Mali za uhakika zitakazowasaidia kuzalisha Mali au kuendesha maisha yao.

Ulikuwa nami, Baba mhuni.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Mabwepande, DAR ES SALAAM
Mkishamaliza maliza kuhonga urithi mje kuanza kutusumbua tena tuwapokee na kuwachinjia kama mwana mpotevu, shubaamiti, if they can't make their own money they will waste yours!!!!!
 
hii thread ingependeza mzee wangu aisome[emoji23][emoji23][emoji23]..maana mzee kakaza fuvu hataki kuelewa.


alow mzee baba najua hayupo humu, lkn nitafanya kila njia hii mada imfikie, yaan nitaicopy na kwenda kuipaste kwa simu message inbox yake ilimladi tu aisome[emoji23].

yule mzee navyomjua hatoimaliza kuisoma ataifuta tu[emoji23][emoji23][emoji23]..
 
I couldn't agree more.

Kwa wanao amini maandiko Biblia inasema

Mit 13:22 SUV​

Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi; Na mali ya mkosaji huwa akiba kwa mwenye haki.

Ila hii miafrika huu mstari huwa inajidai haijauona. Wanakufanya mtoto ndo mtaji.

Makampuni makubwa yote kuanzia ndani hadi nje ya nchi ni generational companies walianzisha mababu sasa wajukuu wanaendeleza ila bongo unarithishwa uchawi na madeni tu. Bongo nyoso
 
ndo mana mimi sijawahi kuwa muumini wa kwamba kijana akikua eti akajitafutie wengine mpaka wanawafukuza nyumbani.. KIzazi cha sasa cha ajabu sana wazee wa zamani hata kijana akitaka kuoa wao ndo wanasimamia show nzima mahari na kila kitu unapewa shamba na ngombe ukaanza maisha na mkeo leo hamna hiyo kitu.

Tutafute mali kwa ajili ya watoto wetu kurithi wasome wakimaliza wanarudi kurithi mali zako na kuziendeleza ndo inatakiwa kuwa hivyo.
 
Hivi mzazi wako ana kipi cha ziada ili akurithishe? Au unataka a distributed poverty tu
Hahaaa! Nilisema kabla kwamba wazee wetu tusiwaingize kwenye mjadala huu maana waliamini kila anayesomeshwa atakuwa amerithishwa jambo la kipekee. Ni kweli kwa sasa tukiwadai tutakuwa tunatafuta distributed poverty.
Msisitizo ni kwamba kizazi cha sasa kisipoteze mihela mingi eti kinarithisha elimu bora wakati ajira hakuna.
 
WAZAZI ACHENI UHUNI NA VISINGIZIO VYA KIPUUZI. TOENI URITHI KWA WATOTO. ELIMU SIO URITHI

Anaandika Robert Heriel.
Yule shahidi kutoka Nyota ya Tibeli.

Andiko hili laweza waumiza wengi. Ikiwa unajihisi unamoyo dhaifu nakusihi usisome. Na ikiwa utasoma basi nisihusike na maumivu na madhara yatakayojitokeza nafsini mwako.

Niite Taikon wa Fasihi, Kuhani katika Hekalu jeusi.

Baba anamajukumu makuu matatu ndani ya familia, nayo ni;
1. Kuhakikisha ulinzi na usalama ndani ya familia(mke na watoto wake)
2. Kuihudumia familia( mke na watoto wake)
3. Kuzalisha Mali na kuandaa Urithi Kwa kizazi chake.

Hivyo Sisi Vijana tunapaswa tutambue mambo hayo matatu, mambo hayo hayana excuse nilazima yafanyike ili heshima ya Baba ilindwe.
Kabla hujaoa na kuzaa watoto lazima ujiulize, je unauwezo wa kumlinda na kumfanya Mkeo na watoto wawe salama?
Pili, unauwezo wankuwahudumia mke na watoto? Mwisho je mipango yako na uwezo wako ukoje katika kuzalisha na kuandaa Mali za Urithi Kwa watoto wako kulingana na nyakati na Zama watoto wako watakazoishi?

Siku za hivi karibuni kumezuka uhuni Fulani hivi Kwa wazazi hasa wababa kuleta visingizio vya kitoto kuhusiana na masuala ya kumuandaa mtoto na ulimwengu.

Wazazi acheni UHUNI, najua hampendi kuambiwa ukweli lakini hakuna jinsi acheni UHUNI. Najua wengine watakuja na maneno Yao ya kipumbavu na kutisha kuhusu laana lakini ukweli ni kuwa acheni uhuni. Hapa hakuna cha laana wala ndugu yake Radhi, huu ni ukweli, mnazingua.

Nawaambiaga Vijana kuwa kama Mzazi wako alishindwa kukupa Urithi usiondoke hapo nyumbani, kaa hapo hapo mpaka akupe kilichochako. Na Kama wazazi wako hawana makazi, muandame kokote mpaka kieleweke.
Vitisho vyao visikuogopeshe havina msingi wowote.

KIJANA ATAONDOKA NYUMBANI KWA BABA NA MAMA YAKE IKIWA HAYA YATAFANYIKA
1. Atapewa Urithi wake,
Na Kama ni mzaliwa wa Kwanza au wamwisho ndiye anayepaswa kurithi Mali kulingana na utamaduni wa kabila Lenu basi huyo atabaki.

2. Endapo atajiweza hata bila kupewa Urithi.
Wapo Vijana ambao wamejaliwa uwezo wankupambana mara wanapokua wakubwa, kijana Kama unajiona unauwezo wa kuendesha maisha yako pasipo Urithi pia inaruhusiwa.

3. Atataka kuoa.
Kijana akitaka kuoa itampasa aondoke nyumbani kwao, wazazi wampe kilichochake, sehemu ya Urithi wake aondoke nao. Na huo Urithi uwe reasonable sio umpe Redio au Feni useme ndio Urithi, Urithi utakaomsaidia mtoto aendeshe maisha yake.
Mara nyingi Urithi wa wazazi Bora hujikita katika nyenzo za uzalishaji Kama vile mashamba, viwanja, visima vya maji au Nyumba, mifugo Kama NG'OMBE au Mbuzi, Miradi ya biashara Kama maduka, viwanda, n.k.
Sio umpe mtoto vitu havieleweki ndio uote Nimempa Urithi, huo ninauita UHUNI.

Siku hizi wazazi wamekuja na visingizio vya hovyo kabisa. Unakuta mzazi anasema, Mimi mwanangu Nimempa Elimu ndio Urithi wake. Pumbavu!
Elimu sio Urithi elimu ni basic need Kwa mwanadamu ambayo mzazi lazima umpe mwanao.

Ni ujinga na upumbavu kusema mtoto wangu namrithisha Elimu, Mimi nilipokuwa naambiwa hivyo nilikuwa nakataa katakata kuwa elimu niendayo kusoma sio Urithi isipokuwa ni sehemu ya basic need kwa binadamu.

Urithi lazima kiwe kitu unachokimiliki, sasa unakuta mzazi hata hajasoma anakuambia nimekupa elimu kuwa Urithi wako, ajabu hii! Elimu ambayo hauna?
Au unakuta mzazi anaelimu kubwa tuu labda ni Daktari, alafu anamuambia mtoto wake ambaye anaelimu ya sheria au Mwalimu, anamwambia, nimekurithisha elimu, sio kweli.

Unaposema Urithi unazungumzia Jambo ambalo unalomilikilulilonalo na unalompa mtu Kwa hiyari au pasipo hiyari. Mfano Mtoto anawezarithi Sura au maumbile ya wazazi wake, sauti, akili, miondoko, magonjwa miongoni mwa mambo mengine. Hiyo tunasema huo ni Urithi.

Elimu sio sehemu ya Urithi labda AKILI inaweza kurithiwa.

Elimu lazima mzazi Ampe mtoto mbali na Urithi ili kumfanya mtoto aweze kuyakabili Mazingira na Mali alizozirithi kutoka Kwa wazazi wake.

Mfano;
Mzazi WA kimasai au kisukuma kabla hajamrithisha mtoto Mali/mifugo ni lazima amfundishe/Ampe elimu ya mifugo na namna ya kuchunga NG'OMBE, Mbuzi na Kondoo. Mtoto akishakua mtu mzima Baba ndio humrithisha mtoto wake Sehemu ya mifugo Kama Urithi na Kwa vile mtoto anaelimu ya mifugo basi haitamsumbua.

Kumbuka mzazi hawezi sema nimekupa Urithi WA elimu ya kufaga NG'OMBE Bali atasema nimekupa Mali/mifugo Kama Urithi, Kwa vile unaelimu ya mifugo basi waweza kutenda Kwa Amani na Mungu akufanikishe.

Mfano wa pili,
Kwa familia za Wakulima,
Mtoto hufundishwa kulima, kutambua magonjwa ya mimea na namna ya kuhifadhi chakula. Kisha akishakua na kutaka kujitegemea Mtoto atapewa Urithi WA mashamba ambayo atayatumia kuendesha familia yake.

Sio umpe mtoto elimu ya kilimo alafu akatafute mwenyewe Shamba huo ni uhuni.
Ni Bora umpe Shamba alafu akatafute mwenyewe Elimu ya kilimo, hivyo ndivyo ilivyo.

Sasa wazazi wa kileo Kwa ujanja ujanja hujiingiza gharama zisizo na maana kumpa mtoto elimu ambayo kimsingi Kama hataajiriwa basi itakuwa haina kazi yoyote.

Unamsomesha mtoto Ada Kwa mwaka milioni mbili Kwa miaka minne mpaka sita alafu akimaliza shule anakosa chakufanya alafu unamuambia asikulaumu, wewe si kichaa tuu.

Mtoto anamaliza shule, humpi hata Urithi WA Shamba au hata kiwanja ambacho kimsingi ungeweza kumnunulia Kwa Ada Ileile aliyosomea.
Yaani umsomeshe mtoto Kwa Ada ya milioni mbili alafu ushindwe kumfurahisha mtoto hata Shamba la laki tano[emoji1787][emoji1787][emoji1787] wewe Kama sio mwendawazimu ni Nani.

Sisemi kuwakamia hapa, najaribu Kueleza na kuamsha akili zetu.

Elimu sio Urithi, Hilo mkae mkilijua.

Mimi pia ni mzazi, siwezi waambia watoto wangu ati nimewarithisha Elimu [emoji3][emoji3]
Kwa kweli waliniona Baba Yao ni mhuni sitawalaumu.

Mzazi Bora ni Yule anayeacha Urithi Kwa watoto wake.
Elimu sio Urithi.

Elimu inatabia ya kubadilika kulingana na wakati. Unamsomesha mtoto hiki Kwa vile wakati huu kinalipa akimaliza kitu hicho kimepitwa na wakati, nazungumzia thamani yake imeshuka, thamani ya elimu inashuka kutokana na kuwa siku hizi kila mtu anaouwezo wa kuipata.

Elimu ya sasa sio elimu ya baadaye.

Lakini ardhi ya sasa, au Shamba la sasa ni hilohilo hata miaka Mia ijayo, tena thamani yake ndio inaongezeka.

Rithisha mtoto viwanja, nyumba, mashamba, viwanda Kama unavyo, visima vya maji, migodi Kama unayo, hotel au lodge, Mifugo sio Sana kwani tabia ya nchi na Hali ya hewa haitabiriki.

Sio mzazi unakazi ya kusumbua watoto wakutumie pesa kisa uliwazaa na kuwasomesha, uliwasomesha vitu visivyoeleweka. Mrithishe mtoto Mradi Kama mashamba au Nyumba au viwanja, ndio umuombe akuhudumie.

Sasa mtoto hata Mradi wankumuingizia kipato Hana, kuishi kwenyewe anaishi Kama Ndege, Kodi inamsumbua, chakula kinamsumbua, bado na wewe umsumbue, Doooh!! Huo unaitwa uhuni hata Kama watoto wanashindwa kutuambia.

Nani asiyejua maisha magumu pasipo kuwa na chakuanzia, Urithi ndio starting point ya mtoto.
Vijana wa sasa wanahangaika kutokana na makosa ya Sisi wazazi. Alafu tunatishia na laana. Pumbavu hakuna laana za hivyo.

Mtoto awaze Kodi.
Mtoto awaze chakula
Mtoto awaze mavazi yake,
Mtoto awaze atapata wapi mahari, alafu unakuta mzazi anakuuliza mbona hauoi utafikiri alikupa mahari, pumbavu.
Mtoto awaze namna ya kwenda ukweni,
Mtoto awaze Harusi,
Mtoto awaze kumhudumia mzazi wake
Mtoto awaze serikali.
Hayo kisa kisingizio cha kumsomesha?

Urithi haupitwi na wakati kwani ni Jambo la miungu, Mungu ndio kaliweka.
Elimu Kwa vile ni man-made lazima ipitwe na wakati.
Ndio maana Kwa miaka ya 90 mtu mwenye elimu alikuwa keshatoboa lakini sio Kwa Zama za sasa.

Wazazi tuache UHUNI, turithishe watoto Mali za uhakika zitakazowasaidia kuzalisha Mali au kuendesha maisha yao.

Ulikuwa nami, Baba mhuni.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Mabwepande, DAR ES SALAAM
Umepewa elimu pambana kivyako unataka uandaliwe hadi mahari ya kuolea huo utakua uchoko sasa
 
Hangaika na mali yako Acha masuala ya urithi ndipo utaendelea
Utaendelea sawa ila angetoa urithi ingeleta bonding ya kizazi chake mpaka wajukuu wanakuwa na bonding kubwa kati yao maana wanajua nini babu yao alifanya katika familia ni kitu Mungu alitaka mzazi afanye kwa familia yake na ndo maana mtu akifa unasomwa wosia wa kizazi chake maana yake watu watataka kujua kizazi alichoacha kinamwelekeo gani? Au ameacha kizazi dhaifu duniani.
 
Hahaaa! Nilisema kabla kwamba wazee wetu tusiwaingize kwenye mjadala huu maana waliamini kila anayesomeshwa atakuwa amerithishwa jambo la kipekee. Ni kweli kwa sasa tukiwadai tutakuwa tunatafuta distributed poverty.
Msisitizo ni kwamba kizazi cha sasa kisipoteze mihela mingi eti kinarithisha elimu bora wakati ajira hakuna.
Hupewi elimu ili ukaajiriwe, la hasha. Unatafuta elimu ili uweze kupambana na maisha. Ukiona mtu anasema ameelimika ili akaajiriwe (utumwa) jua hajaelimika. Elimu inatengeneza hasslers kama anavyotamba Makamu wa Rais wa Kenya kwa kumpiga kijembe Kenyatta kuwa yeye alirithi lakini Rutto katafuta mwenyewe.
 
Back
Top Bottom