Wazazi kuweni makini na watoto wenu hasa wa kiume

Wazazi kuweni makini na watoto wenu hasa wa kiume

Expensive life

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2020
Posts
2,971
Reaction score
9,437
Inasikitisha sana kuona wazazi wanazaa tu kisha kuacha watoto wajilee wenyewe.

Dunia ya sasa imeharibika, hii imetokea juzi nikiwa nimelala zangu mchana majira ya saa saba, nikiwa kwenye usingizi mzito nasikia sauti ya mtoto mdogo akilalama aachiwe.

Sikutilia manani nikahisi huenda labda naota bahati nzuri wife alikuwa macho akaniamsha baba kuna mtoto hapa anafanyiwa kitu kibaya, ikanibidi niamke kweli nikasikia sauti ya mtoto mdogo wa kiume umri wake miaka minne akilalama.

Nikafungua pazia taratibu nakulikuta njemba likiwa limembania mtoto ukutani huku likiwa limemvua nguo, nikitoka kwa jazba kisha nikawajulisha majirani wengine wanusaidie tumkamate ni ajabu wamebaki tu wananishangaa.

Nikazunguka mwenyewe nyuma ya nyumba lile njemba lilipo niona likakurupuka na kumuachia mtoto kisha tukaanza kukimbiza huku nikiita mwizi, kwa kweli sikupata sapoti yeyote kutoka kwa raia wananitizana tu inaonekana huyu kijana anatoka mazingira yale wanamfahamu hivyo wameamua kumlinda.

Sikufanikiwa kumkamata hii kitu imeniuma sana, nilipeleka taarifa kwa wazazi wa mtoto wamejaribu kumuangali wanadai hakufanikiwa kumfanya chochote, nimewaachia wao hii kesi waifuatilie huyu kijana pale mtaani anafahamika.
 
Uswahilini ndio maana hata uhalifu hautokuja kuisha, watu wanawaogopa wahuni kwa kuogopa kufanyiziwa au kuchukiwa na mtaa sababu umemchoma mtoto wao kwa polisi.

Na hii hata mtu akifanya ubakaji, bila familia kusimama utashangaa wanapozwa kwa maneno matamu na visenti kiasi wananyamaza
 
Hali ni mbaya sana. Mkuu hongera kwa ulichofanya. Next time toka na silaha za jadi kama jiwe na panga. Hata akikuzidi mbio fyatua jiwe bayaaa kisogoni kwake.

Pia kama umeliona hilo ni vyema ukalofikisha kwenye serikali ya mtaa ili kikao kiitishwe na upate kuwaeleza wengine hali halisi.

Kuna ambao wataskia na watakaoshupaza shingo lakini muhimu ujumbe umefika
 
Uswahilini ndio maana hata uhalifu hautokuja kuisha, watu wanawaogopa wahuni kwa kuogopa kufanyiziwa au kuchukiwa na mtaa sababu umemchoma mtoto wao kwa polisi...
Na hii hata mtu akifanya ubakaji, bila familia kusimama utashangaa wanapozwa kwa maneno matamu na visenti kiasi wananyamaza
Wanalindana unakuta mtoto wa mkuu
 
Aiseee!! Hao jiran zako ni washenzi na wapumbavu
 
Mtoa mada ni maeneo gani hayo uliyojizuia kuyataja?.

Although haya mambo yapo sana na hawa jamaa disaini hiyo wapo wengi sana na baati mbaya siku hizi hakuna majirani, jirani yako ni yule mnayecheza naye vibubu na kuchangishana tu.

Nowadays NO UPENDO.
 
Inasikitisha sana kuona wazazi wanazaa tu kisha kuacha watoto wajilee wenyewe.

Dunia ya sasa imeharibika, hii imetokea juzi nikiwa nimelala zangu mchana majira ya saa saba, nikiwa kwenye usingizi mzito nasikia sauti ya mtoto mdogo akilalama aachiwe.

Sikutilia manani nikahisi huenda labda naota bahati nzuri wife alikuwa macho akaniamsha baba kuna mtoto hapa anafanyiwa kitu kibaya, ikanibidi niamke kweli nikasikia sauti ya mtoto mdogo wa kiume umri wake miaka minne akilalama.

Nikafungua pazia taratibu nakulikuta njemba likiwa limembania mtoto ukutani huku likiwa limemvua nguo, nikitoka kwa jazba kisha nikawajulisha majirani wengine wanusaidie tumkamate ni ajabu wamebaki tu wananishangaa.

Nikazunguka mwenyewe nyuma ya nyumba lile njemba lilipo niona likakurupuka na kumuachia mtoto kisha tukaanza kukimbiza huku nikiita mwizi, kwa kweli sikupata sapoti yeyote kutoka kwa raia wananitizana tu inaonekana huyu kijana anatoka mazingira yale wanamfahamu hivyo wameamua kumlinda.

Sikufanikiwa kumkamata hii kitu imeniuma sana, nilipeleka taarifa kwa wazazi wa mtoto wamejaribu kumuangali wanadai hakufanikiwa kumfanya chochote, nimewaachia wao hii kesi waifuatilie huyu kijana pale mtaani anafahamika.
Hama huo mtaa kama we ni mpangaji,
 
Haya mambo ni kuyasikitikia wote umtokea yeyeto na si ya kumcheka Mtu.

Muhimu ni kumuombea Mungu awalinde na kuwaombea kwa Mungu
 
Si ajabu hawakutoka sababu wanajua ni mtu fulani, ukifuatilia hata hayo matukio mara nyingi mtu akikamatwa utaskia "ndio tabia yake, kashazoea"
Wanashindwa kumdhibiti na kukubali mateso.

Mtu yeyeto ajifanyae mwamba zipo njia za kumdhibiti
 
Duuh kitoto cha miaka minne unakifanyia unyama huo na watu wapo kmya
 
Back
Top Bottom