Wazazi msipowafuatilia watoto wenu chuo mtajutia mwishoni

Wazazi msipowafuatilia watoto wenu chuo mtajutia mwishoni

Ww kama Mzazi omba akaunti yake ya chuo na password yake huko ndo utaona maendeleo ya mwanao chuoni
Hii Akaunti ya mwanafunzi haidanganyi yni akifanya test utaona tu
Anaweza akafanya vizuri mno darasani ila maisha ya mtaani akawa anazidi kupotea.Tulisoma na kijana alikuwa very bright class but alikuwa sio rizki,mwingine ni mdada ana akili sana ila yeye ni pombe wanaume na club.
 
Muda mwingine binti anakuwa hela ya kujimudu hana anaishia kujiuza chuo,mwingine anajilinganisha na watoto wa matajiri aliowakuta chuo anaishia kudanga afanane nao,pia company ya marafiki wa chuo unaweza kumlea mtoto wako vizuri ila akaja kuharibiwa na watoto wa watu wengine
 
Mzazi uwe na tamaduni za kufanya surprise check huko anaposoma mwanao. Utagundua ujinga mwingi tu. Watoto wa kike dunia inawaendesha sana. Kuna dogo mmoja nikamsifia kidogo tu anaanza kuniambia nimpe mimba anatamani mtoto.
Kuja kufuatilia kumbe kuna shost yake kazalishwa kawekwa geto. Wazazi wanatuma matumizi kumbe dogo kaahirisha masomo anasubiri mtoto akue.
 
Mm nadhani wazazi hawana uwezo wa kubadilisha lolote hasa walio mbali na vyuo, mfano mtu uko singida na mtoto wako anasomea chuo Dar hata ufanyeje huna uwezo wa kumdhibiti.

Mwenye uwezo wa kukomesha huu upuuzi ni serikali kwa kufuta huu upuuzi unao itwa uhuru ulio pitiliza vyuoni ,kwa sababu wenye busara walisha sema ya kuwa demokrasia ipo kwa ajili ya watu wenye akili na si kwa ajili ya wapumbavu.

Taasisi ya elimu ya juu ni taasisi nyeti sana ndani ya nchi ambayo inaandaa watu watakao amuwa msitakabili wa nchi lakini cha kushangaza serikali ni kama imefumba macho utadhani haioni kinacho endelea alafu kesho tukipata viongozi na watumishi wa hovyo tuanze kulalamika.

Tatizo waafrika tuna razimisha kuishi wa kufuata demokrasia ya kamagharibi hali ya kuwa sisi ni watu wawili tofauti kabisa, kuanzia upeo wa kiakili na mfumo wetu wa maisha
Mfano binti wa kijerumani mwenye umri wa 16 tiyari anakuwa amesha jiwekea malengo ya anahitaji kuwa nani na atafanya nn pale atapo maliza masomo, wakati binti wa kiafrika mwenye miaka 25 anacho waza ni kumiliki iPhone ili awalingishie mashoga zake na jinsi ya kuwapanga mabwana zake 10 anao tembea nao wasijuane, sasa watu wa namna hii huwezi ukawaongoza kwa mtindo mmoja ni lazima ufeli tu.

Huu upuuzi unao itwa uhuru vyuoni ukienda nchi nyingi za Asia na mashariki ya kati haupo na ndio maana wanazalisha wasomi wa maana wenye msaada kwa mataifa yao wakati huku Africa wanao jiita wasomi wamegeuka mizigo ndani ya matifa yao.
Comment bora kabisa hii.
 
Nilipomaliza chuo ndio nikaja shangaa ile lifestyle nilikuwa naishi. Sahivi naenda nawatazama vilevile wanavyofanya nashangaa ilikuwaje nilikuwa hivi. Unakuta vidada na jumpsuits vinatembea vimeshikana na boyfriends zao mitaani.

Niko na girlfriend nilipokuwa Advance yeye alikuwa O level yuko mkoa ila huwa anakuja tunakaa bila wasiwasi, muda anapigia mama au baba yake natulia bila kelele. Tunapanga safari, namtembelea ananitembelea tunazurua hadi mikoani. Akifunga anapitia kwangu na akifungua chuo anapitia kwangu.

Kitu kingine mzazi ogopa mfano wewe unaishi Moshi, mwanao anakwambia amepata field Mwanza wakati anasomea Dar, uongo mtupu.
Naunga mkono hoja naomba nipate lunch nije na Nondo za kutosha juu ya huu uzi
 
Miaka 18 ni mtu mzima wacha wajifunze maisha, kadri wanavyofanya makosa katika umri mdogo ndivyo wanavyopata experience ya maisha. Kila mtu anaweza kuharibikiwa ajirishi umri wake.
Utakuwa unawaza kwa kutumia tumbo lako
 
Ni kweli hivi vitoto hasa vya kike vimeharibika sana.Unaweza kuona kadogo.Ila ndio vinaharibu ndoa za watu,vinashindana kila siku jinsi ya kumridhisha mwanaume.Na vitundu haswa kitandani....
 
Wanafake sana maisha vyuoni, mbaya zaidi kuna mambo mengi wazazi hawayajui kuhusu maisha ya chuo hasa wale ambao hawakusoma.
 
Ni kweli unakuta kanapambana kuwa na mchumba wa ndani ya Chuo na nje ya Chuo angalau kipate vinguo na vipafyumu vya kuwalingishia wenzao.
mwisho wa siku ni maumivu, wanapelekeshwa sana na kuharibika. Wanatumika kuliko kawaida, birthday party zinawaponza pia
 
Kwa watoto wa kike hamna kwenda mbali sana, wewe tembelea madalali wa hizi pisi mjini humu, waombe wakutumie mikeka yao kama vile unachagua utashangaa kumuona binti unaemjua mule.

Dunia ya siku hizi inachekesha sana, watu wanatamaa za kupitiliza, hasa hawa mabinti kushindana na wenzao ndo inawacost
Oya wewe ni Isaya Bayi?
 
Rai kwa wazazi, kuna tabia ya kuwatambulisha watoto wanaoenda vyuo mikoani, wanatambulishwa kwa ndugu,jamaa, majirani n.k. ili asaidike, hii nayo ni threat nyingine kwa wanachuo hasa mabinti. Wanafanyiwa mambo ya hovyo sana na hawa watu japo sio wote.
 
Huko vyuo vikuu na vyuo vya kati hali inatisha kwa ngono. Niombe Serikali na mamlaka zinazohusika kuchukua hatua.

Tangu jana kuna meseji inatembea kwenye magrupu ya WhatsApp ikiwatahadharisha wazazi kufuatilia maisha ya watoto wao waliopo vyuoni.

Vyuo vinegeuka kuwa madanguro. Bila misingi imara ya elimu, taifa linaenda kuanguka hili.

Screenshot_20230220-122929.png
 
Back
Top Bottom