Wazazi wawezesheni watoto wenu kiuchumi

Wazazi wawezesheni watoto wenu kiuchumi

Raymanu KE

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2022
Posts
8,611
Reaction score
16,118
Siku hizi hali Ni Tete mtaani vyuma vimekaza kabisa hakuna michongo Wala nafasi za kutosha za ajira.

Vijana wengi wanahitimu vyuo wanarudi mtaani kutafuta ramani za maisha ila mambo hayaendi hawana CONNECTIONS kabisa.

Wengi wanakuwa ' liabilities' kwa wazazi wao licha ya kuwa na elimu ya juu.Utawakuta vijiweni kutwa nzima wanacheza bao mixer kubishana kwenye mambo ya Yanga na Simba.Inasikitisha Sana kuona vijana wetu wamekaa idol hawana lolote la maana wafanyalo.

Ni vibaya Sana kumuona mzazi anamshurutishwa mwanaye asepe nyumbani aende mjini kutafuta maisha.Je, ataendaje mjini wakati Hana connections Wala mchongo wa kueleweka.Wazazi wanatakiwa kuliangalia Hili suala kwa umakini Sana ili waweze kuwaokoa watoto kutoka kwenye Hali mbaya za kiuchumi.

Wazazi chukueni jukumu la kuwawezesha vijana wenu kiuchumi kwa kuwapa mitaji ya kuanzisha biashara ama kufanya kilimo kitakachowaingizia kipata wakati bado wanasikilizia michongo mingine.

Mwanao akishahitimu chuo tenga muda naye, mkae chini mzungumze umuulize Ni shughuli gani ambayo angependa kujihushisha nayo ya kumuingizia kipato.Akishakwambia Basi we mpe mtaji ama mfungulie hyo biashara aliyokupendekezea ili aweze kujiinua kiuchumi kuliko kukaa tu ku- idol mtaani.

Kwa mfano unaweza kumuwezesha mwanao kiuchumi kwa kumfungulia biashara ya duka la kuuza bidhaa mbali mbali, Banda la kuku, kupanda mimea Kama mboga na kadhalika. Naamini hi ndo njia pekee ambayo mzazi anaweza kumsaidia mwanaye baada ya kuhitimisha masomo.

Mwanao akiwa mwerevu Basi atajiongeza mwenyewe kwa kuikuza biashara uliyomuanzishia na kutengeneza faida kubwa.Na baada ya muda fulani atakuwa ameshapiga hatua kubwa ya kiuchumi na hakika wewe Kama mzazi utajivunia mwanao.
 
Ila kizazi hiki tuna tabu haswa. Mnasahau na sisi tuna wazazi wanaotutegemea kisha kuna hawa sasa wanataka tuwape mitaji alafu kuna wadogo zao ambao bado tunawasomesha na kuishi nao na mwisho kuna ndugu wengine wa kwangu na wa wife wananitegemea.

Mimi mwenyewe mwalimu wa Praimari
 
Wazazi wenyewe hohehahe, wanasubiri mabinti wao wahongwe ndipo wawaone mashujaa. Ufukara ukiingia kwenye ubongo ni hatari sana
**Zanzibar ndo mwendo huo,

1. Mabinti zao wengi wameolewa Arabuni (hasa Oman) na matajiri wenye visima vya mafuta wanatuma pesa kwa wazazi hapo Zanzibar maisha yanaenda.

*2. Vijana wa Ki-Zanzibari wanapambania kuoa Vibibi wa KITALIANO ambao wengi wamewekeza kwenye biashara ya utalii hapo Unguja. *

3. Mgao wa AJIRA na misaada toka bara (Tanganyika). umewapa ahueni wazanzibari kwenye ajira huko bara (majeshi na sekta mbalimbali za Muungano).

NB: Ndo maana m-Zanzibari haoni umuhimu wa kusoma, maana pesa ni rahisi mno
 
Ila kizazi hiki tuna tabu haswa. Mnasahau na sisi tuna wazazi wanaotutegemea kisha kuna hawa sasa wanataka tuwape mitaji alafu kuna wadogo zao ambao bado tunawasomesha na kuishi nao na mwisho kuna ndugu wengine wa kwangu na wa wife wananitegemea.

Mimi mwenyewe mwalimu wa Praimari
mpwayungu village
 
Ila kizazi hiki tuna tabu haswa. Mnasahau na sisi tuna wazazi wanaotutegemea kisha kuna hawa sasa wanataka tuwape mitaji alafu kuna wadogo zao ambao bado tunawasomesha na kuishi nao na mwisho kuna ndugu wengine wa kwangu na wa wife wananitegemea.

Mimi mwenyewe mwalimu wa Praimari
Hii coment jf iwekewe alama kila mtu aisome
 
Ila kizazi hiki tuna tabu haswa. Mnasahau na sisi tuna wazazi wanaotutegemea kisha kuna hawa sasa wanataka tuwape mitaji alafu kuna wadogo zao ambao bado tunawasomesha na kuishi nao na mwisho kuna ndugu wengine wa kwangu na wa wife wananitegemea.

Mimi mwenyewe mwalimu wa Praimari
Pole ticha pole sana nimekuonea huruma sana lazima uwahi kufa kwa hali hii

Kaka mpwayungu village njoo utoe pole za dhati kwa ndugu yetu mwalimu Kambaku
 
Mkuu ebu muwezeshe first born wako aliyehitimu chuo ili na yeye aje kuwaisaidia ndugu zake wadogo.
Ila kizazi hiki tuna tabu haswa. Mnasahau na sisi tuna wazazi wanaotutegemea kisha kuna hawa sasa wanataka tuwape mitaji alafu kuna wadogo zao ambao bado tunawasomesha na kuishi nao na mwisho kuna ndugu wengine wa kwangu na wa wife wananitegemea.

Mimi mwenyewe mwalimu wa Praimari
 
Kweli kabisa mkuu.Ila wazazi nao wanatakiwa wainuka kuwasaidia wanao mpaka pale watakapojimudu wenyewe.Na wakishaimarika kiuchumi hawataacha kurudisha mkono kwa wazazi.
Wazazi wenyewe hohehahe, wanasubiri mabinti wao wahongwe ndipo wawaone mashujaa. Ufukara ukiingia kwenye ubongo ni hatari sana
 
kuwezeshwa bila maarifa ya unachoenda kukifanya ni sawa na bure tu,me nazani msaada ni kutengeneza mindset za watoto wetu tangu wakiwa wadogo si kusubiri kuwawezesha mwishoni huko wakiwa wameshakomaa kiakili zikiwaza kuzunguka kwenye viti maofisini mfano mzuri wahindi kwenye biashara mtoto anaanza kwenda dukani angali mdogo wanarithishwa ujuzi/mbinu wangali wadogo
 
Unawazungumzia wananchi wa hii hii nchi ambayo mzazi anazaa ili mtoto aje kumsaidia akikua?....yaan mtoto anahudumia familia yake,wazazi wake na ndugu jamaa na marafk,lini utawezesha wanao?....
Ni upuuzi sana huu,tuzae Ili tuwasaidie na sie tukiwa wazee wao ndio watulee Kwa Mali tulizowapa.
 
Hapa ndipo wazazi wengi wa kiAfrica wanapofeli.Overdependancy Ni kitu kibaya Sana na huleta umaskini kwenye familia na jamii kwa ujumla.
Unawazungumzia wananchi wa hii hii nchi ambayo mzazi anazaa ili mtoto aje kumsaidia akikua?....yaan mtoto anahudumia familia yake,wazazi wake na ndugu jamaa na marafk,lini utawezesha wanao?....
 
Imagine mtu unapoanza 2 kupata kipato,hapohapo unaanza mgawanyo yaan unachakaa vibaya
Ni vibaya Sana mkuu.Afu bado hujasimama vizuri kiuchumi na tayari ushaanza kupigwa mizinga na familia ya kina mke.
 
Umeongea point nzuri Sana mkuu.
kuwezeshwa bila maarifa ya unachoenda kukifanya ni sawa na bure tu,me nazani msaada ni kutengeneza mindset za watoto wetu tangu wakiwa wadogo si kusubiri kuwawezesha mwishoni huko wakiwa wameshakomaa kiakili zikiwaza kuzunguka kwenye viti maofisini mfano mzuri wahindi kwenye biashara mtoto anaanza kwenda dukani angali mdogo wanarithishwa ujuzi/mbinu wangali wadogo
 
Back
Top Bottom