Wazazi wengi huwaandikisha watoto shule za awali wakiwa na umri wa miaka mitano

Wazazi wengi huwaandikisha watoto shule za awali wakiwa na umri wa miaka mitano

uvivu wa kulea ndio kichocheo cha kukimbiza watoto shule,mtoto wa miaka 3 anaenda kusoma nini!!!!!
 
Inawezekana ni kukosa hela au sababu nyingine suala linalofanya wazazi wawapeleke watoto shule wakiwa na miaka mitano ili wakiwa na miaka sita waingia Darasa la kwanza. Hii ni sababu ambayo nimeitoa mimi kwa kuwa Shule za awali nyingi zinamilikiwa na serikali, i.e katika shule 18,554 zilizosajiliwa 89.48% zinamilikiwa na serikali. Hivyo sababu inaweza kuwa kweli wazazi wanapenda kukaa na watoto wao au hawataki kuwapeleka shule mapema ili wapate muda wa kuishi nao nyumbani
View attachment 2031596

Hii sio kusema kuwa walio chini ya miaka mitano au zaidi hawaandikishwi shule ya awali angalia graph hii


View attachment 2031599

Kwa Idadi hiyo utaona watoto wanaoandikishwa zaidi ni wenye miaka 5, ambao hukaa mwaka mmoja na kuingia darasa la kwanza wakiwa na miaka 6 wazazi wanaopeleka watoto wakiwa na miaka 3 ni wachache sana, huku wengine wengi wakiwapeleka watoto shule za awali wakiwa wamechelewa


Data zilizotumika ni kutoka TAMISEMI

Mtoto aache kucheza aende kubebeshwa mastress ya shule? Atasoma chekechea Umri huo wa miaka 5 au 6
 
Back
Top Bottom