Uzuri wa gari isichokonolewa chokonolewa ( modification ).. kama unataka yenye 340 ni vyema ukajipanga ukachukua tu 😀😀😀. Gari zote tunazo hitaji zipo . Shida ni shekeli tuWale wanaofanya engine calibrate na tunings sio kwamba wanaongeza hizo kph ?
Sababu ulizotaka ndio zinanifanya niepuke safari za usiku.Usiku siwezi kukimbiza sana.
Naingiwa na woga tu. Halafu sioni mbali sana.
Mchana unaweza kuona hata 1Km kama ni tambarare kwahiyo unapimia kabisa.
Ila usiku maximum 500M. Ambayo ni ndogo sana kwa mimi kufanya sudden decision ukiwa above 150kph.
Ni kwasababu ushaendesha gari ingine stable zaidi. Kama mtu gari yake ni hio hio Carina anaamini hakuna gari stable kama yake.Nilishawahi drive Carina Ti 1500cc to 140km/hr gari ikawa inaanza kukosa stability,Swali nililojiuliza ni Je,itakuwaje kwa mtu anayeendesha Carina Ti 2200cc ambayo i think ni Turbo charged akaenda 180km/hr sijawah pata majibu.
RPM sizidishi 3000 nikiwa highway. Naiacha ichanganye yenyewe.Hahahah RPM unazingatiaga lakini au unabonyeza tu chuma itembee [emoji23][emoji23][emoji23]
Kuna siku nasafiri usiku, nikaona chombo mbele yangu kina taa moja, nikadhani ni pikipiki.Sababu ulizotaka ndio zinanifanya niepuke safari za usiku.
Sitakaa nimsahau yule trafiki.Duh hii kali!
Aisee-Huyu jamaa matraffic anaokutanaga nao nahisi ni wa aina yake ya kipekee 😁 😁 😁 🙌🙌🙌.Duh hii kali!
Jamaa yangu we kiboko-Traffic anatumia taratibu gani kukuandikia?Anayestahili kupima ni nan? atapimaje ajali bila kufika tukio husika? jam inasababishwaje na aliyegongwa mpaka apigwe fain? kweli hamna namna 🤣🤣-Traffic alivyofika kituoni lazima alihadithia wengine encounter yako😁😁😁Sitakaa nimsahau yule trafiki.
Na kwa wenge nikasahau hadi leseni yangu kwake.
Madalali ni makuzi sana basi tu.Ngoja niiende kwa mganga, abane hivyo hivyo hadi ishueke ifikie 6 million.. maana nao jamaa wale wajinga sana , ukiepeleka gari yako wanaanziaga 5 million hata kama gari ina vakue ya 15 million na huwa kama wanaitia mikosi yani, huto iuza sehemu ingine hadi uirudishe pale [emoji3][emoji3][emoji3].. na mie naenda kuwachomea .. [emoji2][emoji2][emoji2].. iwe ngoma draw.. bado nauchungu niliuza gari yangu 7 million.. na huku nilitakiwa niuze million 18 au 17.. ila sijui waliitia nuksi gani, alafu madalali wote wakaijua.. ikawa kama tangazo
Chuma gani hio uliiuza kwa pesa hio mkuu?Jamaa ndio mchezo wao pale, ujichanganye upeleke gari yako.. utalia chozi la kiutu uzima.. utauza gari huku unaumia.. bei zao kununua ndio hizo milion tano, nne, sita [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Ukiongeza HP(kutegemea ni stage gani unataka) then lazima modification ya Suspension&Brakes parts ihusike.Stability inapotea kwa ku tweak suspension parts sio horsepower na torque. Kama ni hivyo zile subaru zenye turbo zingekuwa zinaanguka maana sti zina kibati cha mpaka 280kph na haziyumbi.
Yule mhuni wa Arusha Speedometer yake ya Aristo ni 180km/h ila ikipigwa speedgun top speed inasoma 300km/h.Hivi najiuliza hamnaga namna ya ku calibrate speed na kufunga console mpya yenye gauges ya zaidi ya 180 kph! Maybe kufunga ile inayofika hata 300KPH?
It sucks kwa kweli gari ina mashine kubwa ila iko limited to 180KPH yan kiasi kwamba usiku mkali tokea round about ya Mlimani unajikuta umeshafuta 180kph kabla hata ya flyovers za Ubungo. Kile kipande huwa najiachiaga sana.
Mambo ya Gentleman Agreement hayo ndio yaliharibu mambo mkuu.Na kweli, engine yenye 8 cylinder na C.c 4300 kuwa na 180 ni makosa sana basi tu wajapana wanatunyanyapaa
Hii ya trekta isiyo na taa wala reflector nyuma nilikutana nayo mida ya saa moja usiku karibu na Nangurukuru, halafu upande wa pili naona taa za chuma inakuja. Siku ile nilikanyaga break nikaja kusimama kama mita 5 hivi kutoka kwenye trekta. Bahati nzuri nilikiwa just 100-120kph. Sipendi kabisa safari za usiku. Nasafiri usiku ikibidi tu na hapo speed mwisho 120.Kuna siku nasafiri usiku, nikaona chombo mbele yangu kina taa moja, nikadhani ni pikipiki.
Hamadi mita kama 50 naona ni gari ina mzigo.
Niliyumba siku ile sitasahau, sio kwa kumkwepa vile.
Siku nyingine maeneo ya mwanga, chombo hakina taa nyuma.
Nagundua ni trekta limebeba mazao nimeshafika mita kama 50 hivi. Nikamkwepa nikavaa tuta.
Nimetokea kuchukia sana kusafiri usiku. Hasa hizi barabara zetu huchelewi kukuta kundi la ng'ombe au mbuzi barabarani na upo zako 170kph.
Ndo utajua hujui.
Hapo ndipo ule msemo wa 'If it ain't broke don't fix it' unapo play part yake.Sema mi nilishusha tank likasafishwa about 3 weeks ago. Halikuwa na residue zozote. Ila sasa imezalisha tatizo jengine baya kweli. Gauge yangu inanipa false readings. Sijui hata ishu ni nini tena maana pump iko sawa ila toka iliporudishiwa wakati wanafunga tank ikawa inasoma empty kabisa hata baada ya kuweka full tank.
Nikaenda kwa fundi kufungua tena pump na kuigeuza pengine ilifungwa upande sio ikawa inasoma ila ilikuja kuniadhiri Jangwani pale sitasahau tena nikiwa na bibie. Ikabidi nitie triangle nipande fire na kidumu. Sasa sielewi sijui tatizo litakuwa nini kupelekea wrong readings
Yule ni mwamba,mbali na hiyo Aristo yenye 2gzte ana ile Chaser tourer nayo ni hatari,cha kushangaza kwa muonekano ni gari ya kawaida ila sokoni bei inagonga usd 20,000 bila cifYule mhuni wa Arusha Speedometer yake ya Aristo ni 180km/h ila ikipigwa speedgun top speed inasoma 300km/h.
Mambo ya modes hayo.
Kufika top speed ya 300km/h sio mchezo kabisa kabisa,hata hizi Germany machines nyingi zina speedometer ya 260km/-300km/h lkn unakuta top speed yake ya ukweli ni 240-250km/h hapo ndo mwisho.
Ina umiza sana.. sema ukikumbana na chuma kichovu unakitesa baraaaMambo ya Gentleman Agreement hayo ndio yaliharibu mambo mkuu.