Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Sema mi nilishusha tank likasafishwa about 3 weeks ago. Halikuwa na residue zozote. Ila sasa imezalisha tatizo jengine baya kweli. Gauge yangu inanipa false readings. Sijui hata ishu ni nini tena maana pump iko sawa ila toka iliporudishiwa wakati wanafunga tank ikawa inasoma empty kabisa hata baada ya kuweka full tank.

Nikaenda kwa fundi kufungua tena pump na kuigeuza pengine ilifungwa upande sio ikawa inasoma ila ilikuja kuniadhiri Jangwani pale sitasahau tena nikiwa na bibie. Ikabidi nitie triangle nipande fire na kidumu. Sasa sielewi sijui tatizo litakuwa nini kupelekea wrong readings
Mkuu ishu sensitive kama hiyo uwe unapeleka kwa mafundi wa uhakika, unaweza kuwa na nia nzuri ila jamaa wakakufanya ujute... Mm pia nawaza kusafisha tank ila natafuta hela niende toyota
 
Brevis engine yake ni inline 6! 1JZ Inaruhusu kufanya ma modes kibao tu sema uwe na hela tu. Ila kwa mwendo Brevis inanoga jamani, inachanganya effortlessly!
Shida ni hapo sheli lazma upewe membership card😂
Hapana mkuu,engine za brevis (1jz/2jz)-GE/FSE (Non-turbo)hazina modes zozote za maana,unazosemea wewe ni 1jz/2jz-GTE(Turbo) zilizoko kwny ma supra/Aristo ndio baba lao.
 
Mkuu ishu sensitive kama hiyo uwe unapeleka kwa mafundi wa uhakika, unaweza kuwa na nia nzuri ila jamaa wakakufanya ujute... Mm pia nawaza kusafisha tank ila natafuta hela niende toyota
Nimeamua nihamishe magoli tu kwa muda. Naweka mafuta ya kuzidi jiwe moja. Likishuka kufikia 1 najua ni time to refill. Mpaka ntakapoenda kwa mtu wa diagnosis.
 
Jamaa yangu we kiboko-Traffic anatumia taratibu gani kukuandikia?Anayestahili kupima ni nan? atapimaje ajali bila kufika tukio husika? jam inasababishwaje na aliyegongwa mpaka apigwe fain? kweli hamna namna [emoji1787][emoji1787]-Traffic alivyofika kituoni lazima alihadithia wengine encounter yako[emoji16][emoji16][emoji16]
Ndo mara yangu ya kwanza kupata ajali.

Lilikuwa wenge.

Baada ya ajali nikasubiri aje kupika. Nikaona anachorachora chini na kuhamia kwenye karatasi.

Baada ya hapo akaniambia niondoe gari tukamalizane na alienigonga. Nikamwambia hakuna kumalizana wakati ana bima. Mzigo ukalipwe na bima.

Akasema kitu kidogo mpaka msumbuane mahakamani? Nikamwambia kazi ya bima ni nini? Nikamwambia huyo jamaa hana uwezo wa kulipa matengenezo ya ile gari.

Yule jamaa akasema tumalizane. Nikamwambia kama kumalizana tunaenda garage, estimation zote utalipa kabisa ndo unaondoka.

Polisi akasema tuondoe magari yetu barabarani. Tukapeleka pale pembeni ya kibanda chao.

Kufika pale polisi ndo akanigeuka. Nimesababisha foleni.

Mabishano ndo yakahama toka kugongwa mpaka kusababisha foleni. Alienigonga akataka anipe 50K yaishe.

Kufupisha, tulibishana masaa mawili mazima. Akachukua leseni yangu akaingia kwenye kibanda chake akarudi na risiti ya fine. Sikuwaza tena kama nilimpa leseni. Sikumtafuta tena. Nikarenew baada ya kama miaka miwili hivi. Na ile fine sikuilipa mapaka dec 2020 walivyonikagua na vikamera vyao barabarani.

Yule jamaa ilibidi tupelekane garage. Akapewa estimation za matengenezo akalipa nusu na kuacha simu yake. Akaja kumalizia baada ya wiki hivi. Ambapo bima ingemlipia kirahisi sana.

Toka siku hiyo. Polisi nawaweka kundi moja na wanyama. Siwezi nikapata shida nikawapelekea polisi nitatatua mwenyewe.
 
50kph zone naenda 50kph....ikiisha natembea kweri kweri!
Kuna choko alinisimamisha kisa nimepiga honi kabla sijaifikia Zebra hapo nshaikacha 50 nimemwaga moto naitafuta 110kph. Ghafla mkono...Eti kwanini niwapigie wana kijiji honi ikiwa wanaelekea zebra.
Kanisumbua sumbua nikampa 10k nikaishia zangu.
 
Kuna choko alinisimamisha kisa nimepiga honi kabla sijaifikia Zebra hapo nshaikacha 50 nimemwaga moto naitafuta 110kph. Ghafla mkono...Eti kwanini niwapigie wana kijiji honi ikiwa wanaelekea zebra.
Kanisumbua sumbua nikampa 10k nikaishia zangu.
Duh hawa jamaa wana maswali ya ajabu. Mimi 50kph huwa napiga 50kph basi hapo kuna wanyonge wenye fujo wanakupita ikiisha 50kph dakika mbili nyingi naanza kutafuna mmoja mmoja
 
Back
Top Bottom