Wazee wa Tanga kusoma albadir kwa waliomuua Mzee Ali Mohamed Kibao

Hakuna kitu linaitwa Albadri ni usanii tuu kama KURJUANI ya Magoma.LYATONGA MREMA alisomewa za kutosha lakini alidunda mpaka alipofariki kwa uzee
 
Huwezi ukahukumiwa bila kosa aisee πŸ˜…
 
Hio dua lazma kwanza msomaji awe msafi kwelikweli, na iliwezekana sana enzi hizo kwa sasa labda waroge ila kukuta mtu msafi wa kukusomea albadili ikafanya kazi kwa sasa ngumu
Dua yenyewe ni uchafu itachaguaje msafi?
Albadiri ni dua chafu hivyo haichagui msomaji.
Ni mjuaji anayejua ndiye anayesoma albadir wala si usafi wa nafsi.
 
Kwa mujibu vitabu vyenu kusema hakuna Mungu ni kosa😊
Jino kwa jino sheria lazima ifuatwe. Hii ya albadiri hata kuna Jamaa yangu humu yupo anakusomea lakini uwe umefanya kosa sasa sio kuonea. Huyu mwamba ni hatari sana πŸ˜…
 
Jino kwa jino sheria lazima ifuatwe. Hii ya albadiri hata kuna Jamaa yangu humu yupo anakusomea lakini uwe umefanya kosa sasa sio kuonea. Huyu mwamba ni hatari sana πŸ˜…
Mimi nasema hakuna Mungu ni utapeli mtupu mwambie asome mkuu😊
 
Hakuna kitu linaitwa Albadri ni usanii tuu kama KURJUANI ya Magoma.LYATONGA MREMA alisomewa za kutosha lakini alidunda mpaka alipofariki kwa uzee
Lyatonga kaumwa sana sukari imemtesa,akababuka ngozi,akafiwa na mke,akafumaniwa,akaambukizwa ngomma,akafa na miaka si zaidi ya 77 ,,wakina malecela na msuya wana 90 +
Pili albadili hushika wenye kosa,labda hakuwa na makosa
 
Yule bibi 2025 itakuwaje
 
Mimi nasema hakuna Mungu ni utapeli mtupu mwambie asome mkuu😊
Kila mtu ana mtazamo wake kuhusu suala la imani hususa kwa nyakati tulizonazo. Nimezaliwa kwenye familia ya Wamishenari Babu zangu kuna Baba yangu ni Msaidizi wa Askofu huko Lake Zone na Shangazi yangu ni Mke wa Mchungaji lakini Mimi niliamua kua Muislam na nina enjoy sana.
 
Furahia mkuu
 
Mimi ni mkristo ,Naunga mkonk hoja

Tanzania nzima tuvisome hii albadili
 
Sina hakika kama zinafanya kazi, lasivyo vita vya mashariki ya kati vingewapoteza wengi watu wa magharibi (Ulaya & US)​
Albadri ni ushirikina wa kiarabu.
Na vita za mashariki ya kati ni za kidiplomasia sio za kidini.
Usichanganye madesa mkuu.
 
Hayo madude nishasomewa miaka kumi iliyo pita ili nife baada ya wiki ila naona nipo tuπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Hao walikutisha mkuu sio wasomaji.
Pia albadri haisomwi tu kiholela holela.
Pata mafundi uone balaa lake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…