Wazee wa Tanga kusoma albadir kwa waliomuua Mzee Ali Mohamed Kibao

Inasomwa lini? Na baada ya kusomwa inachukua muda gani kuanzia kuleta matunda yake??
 

Nawasisitiza wazee wa TANGA wasiache kusoma albadil ,kurujuan ,itikafu ili iwe fundisho kwa WAHUNI kama hao kufanya waliyoyafanya ,hao wahuni wakiwa wanaoza mwili huku wanajiona ndiyo watatia akili.

Nasisitiza wasiache kuwaonyesha show hao wahuni ,pia nawashauri wavuke maji hapo kutoka tanga kwenda Pemba ,napo wapo vizuri sana kwenye kuwapa somo WAHUNI kama hao.

Kitendo cha kumtoa uhai mtu asiye na shida na mtu ni makosa sana ,kuna askari kituo flani walikamata gari ya mpemba ambayo ilikuwa na mali ,wakampora pesa na baadhi ya biadhaa kuziharibu ,wale askari walioza huku wanajiona na mwingine nyama za miguu zilikuwa zinatoka inabakia mifupa tu,....Sasa Wazee wa TANGA msituangushe hao wahuni WAKIANZA KUOZA huku wanajiona nadhani matendo kama hayo yataisha.
 
Safi sana. Mungu atawasikiliza na karma itafanya kazi yake.
 
Kama kweli hao wazee watasoma hiyo dua basi tutegemee kuona watu wanatajana hovyo walioshiriki matukio haya na kupukutika mmoja baada ya mwingine.

Hii kitu unaweza usiiamini lakini kisomo kikipigwa ipasavyo aise haitachukia muda matokeo huanza kuonekana.

Uzuri wa dua hii inatafuta yeyote aliyeshiriki kwa namna moja ama nyingine na hata aliyekuwa anajua tu mpango mzima na akaamua kukaa kimya yumo kwenye mnyororo.

Unless kama ulijua lakini ukaficha kwa hofu ama vinginevyo hivyo kabla ya kisomo ukikiri kujua basi balaa hilo ataliepuka.
 
Yaani mtu msafi kwelikweli amuombee mtu ili mabaya yamkute?
Usafi sasa wa mtu huyo u wapi sasa?

Who can bring a clean thing out of an unclean?
Kikubwa awe upande wa haki.......wahehe wanaijua hii kitu
 
Masheikh wanajua hayo, dua yoyote ile lazima uwe msafi else unafanya kazi bure
Na labda wanaemsomea awe wa ukanda huohuo au imani hiohio....,,,,unaenda kumsomea mtu alishapikwa huko akazikwa na kufukuliwa tena ,ngoma inadunda
 
Na ninachowapendea Waislamu katika hii Dua yao huwa haitanii na taratibu naanza kuona huenda kuna Watu watapukutika kwa wingi ndani ya Wiki Mbili zijazo hadi Mwezi na si ajabu hata wengine nao Kampeni Ijayo wakawa si Wao kwakuwa watakuwa Wehu na Mburundi kupeperusha Bendera ya 2025 -2030.

Kudadadeki Shikamooni Wazee wa Mkoa wa Tanga. Naona kuanzia sasa Safari za Kisiwani Kuungama hazitopungua.
 
Hata mimi ningefanya ushirikina mzito sana ningekua mtu wa karibu wa huyo mzee au hata mtoto wake.. Aiseeh nisingewaacha hao jamaa! Mbinguni tutaenda kwa hesabu
Angedondoka kuanzia mzizi, shina mpaka matawi..kila aliyeshiriki.
Kuna mambo mengine yanafanyika yanatusababishia watu tuingie kwenye dhambi tu.

Hata kama mzee alikua na shida ndo mumuue mzee wa watu tayari Age Ago.!
 
Onyo Kali watalipata kabla ya kufanya hivyo
 
Kufa ni asili ya binadamu na kiumbe hai sio adhabu ,ila kwa hili nakemea vikali.
 
Nataamani niungane nao Wahenga hawa tafadhali wafanye haya kwa umakini mkubwa bila kukosea hata hatua moja, waanze kwa kufunga siku 7,kwanza, Aliyefahamu ushenzi huu akakaanao kimya ardhi imchukue, pasi huruma, na damu yake iwe nuru na kirutubisho bora kabisa kwa ardhi, NASHAURI WASOME ILE YA MKUNGU WA NDIZI NDIYO HUWA MARIDADI KABISA PASI NA SHAKA.
 
Hiyo ya mkungu ikoje hiyo..🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…