Waziri Bashe aache sifa apige marufuku Uuzaji wa Chakula nje

Waziri usikubali upuuzi huu wa kufukarisha wakulima Ili wazururaji wa mjini wanunue vitu Kwa bei ya chini wakati mkulima aliumia na mbolea kuwa juu..

Mtanunua tuu hata Bei ikiwa milioni madam tuna ziada ya Mazao mbalimbali
Mkulima amekuwa akionekana duni miaka yote na ndio sababu ya vijana wengi kuondoka vijijini na kuhamia mijini maana hawakuona faida yeyote ya kuendelea kubaki vijijini na kufanya kazi ambayo imekuwa haina tija yeyote kwa wazazi wao !! Sasa vita vya Urusi na Ukraine vinataka kubadili hali hiyo, muda sio mrefu kutoka sasa watu watajua umuhimu wa kilimo na mkulima !! Badala ya watu kujazana mijini watu wataanza kukimbilia mashambani !! Na kazi iendelee !!
 
Incentives ya kulima na kuona tija ni Bei ya Mazao na si vinginevyo..

Bashe na Serikali imesema kamwe haitafanya huo ujinga so long as tuna ziada ya chakula na chakula sio mahindi na mpunga tuu..👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220618-081021.png
    161.1 KB · Views: 6
  • Screenshot_20220612-131909.png
    108.3 KB · Views: 7
  • Screenshot_20220612-131709.png
    47.6 KB · Views: 6
  • Screenshot_20220609-225445.png
    158.8 KB · Views: 7
  • Screenshot_20220609-162050.png
    130 KB · Views: 5
Be honest, wakulima wenyewe wala hawamo humu JF......nyinyi mnaopiga zogo humu tunawajua ni walanguzi wa mazao mnaojiita wafanyabiashara ambao tunajua mnavyowalalia wakulima kupitia kubana mizani na kwa kutumia lumbesa na kangomba. Leo mnakuja kutafuta huruma humu JF ili mwendelee kutorosha mazao nje mkauze kwa bei ya juu bila kujali uhaba na bei kubwa za vyakula mnavyosababisha nchini. Nyie hamna tofauti na wahujumu uchumi....
 
Tena watoe mawazo wale wamo kwenye mavieite !! Wanaoogopa kukanyaga matope na majani na kupishana na nyoka huko mashambani !!
Aisee hii Nchi kiboko wapo kimya wakulima wakiuziwa mbolea bei juu kipindi cha mavuno wao ndio wanakuwa wa Kwanza kutoa mawazo wauze hapa hapa labda wangetoa wazo Serikali itangaze bei nzuri wanunue baadhi ya mazao wao sio mkulimz atunze harafu mtu atoke huko kupanga sehemu ya kuuza...
 
Kweli kabisa
 
Wewe mpuuzi Mkulima analima bila ruzuku halafu unataka kumzuia asiuze mazao yake
 
Mwaka huu tunanunua debe la mahindi elfu thelathini,huu ni mwezi wa sita tunanunua elfu kumi na nane
 
Hata yakiuzwa nje hakuna atakayekufa kwa njaa.Tena yapande tena watu wafidiye gharama ya pembejeo.
 
Who is going to protect farmers??

Mkuu nenda na wewe shambani kalime chakula chako mbona simple tuu.
We ni kiazi mlishwaji possible hujui hata bei ya unga na kinacho jadiliwa... nikuulize nawe nani atamlinda mlaji?
 
Kuna watu huwa wanaenda kulima wakitegemea mavuno mengi lakini wakishavuna wanapata mavuno lakini bei wanakuta iko chini na gharama za uzalihaji ziko juu. Utawasikia sitalima tena bora ninunue chakula.
Kwa mkulima wa Tanzania ukilima usipokutana na bei nzuri imekula kwako wanafaindi walaji. Kwa hiyo kwa Tanzania kufunga mipaka unamuumiza mkulima. Mwaka juzi mahindi kipindi Cha mavuno yalikua mia nne kwa kilo hadi mwaka mwingine wa mavuno. Mchele kilo kwa wastani ulisimamia 1000 kwa kilo mwaka mzima. Wakulima waliumia Sana kwa bei ndogo ambayo hata Fedha, muda na nguvu uliyoweka kwenye kilimo haifiki. Nguvu za soko ngoja zifanye kazi (Price mechanisms)mwaka ule serikali ilithibiti usafilishaji Nje ya nchi wakati mkulima analia.
Huu ni muda Sasa wenye mitaji kuwekeza kwenye kilimo Cha umwangiliaji ili uzalishaji ufanyike kwa mwaka mzima.
Serikali inatakiwa kuongeza ruzuku kwa zana za kilimo na pembejeo.
Serikali inanunua nafaka kidogo kwa ajili ya kuweka reserve kwa ajili ya price stabilization.
Serikali zilizoendea zinaweka stabilization fund kwa ajili ya kulinda mkulima na soko. Serikali inalinda mkulima na mlaji.
Mkulima wa Tanzania bei ikianguka mkulima ni kuanguka kabisa huku mlaji akichekelea. Bei Sasa zikipanda ili mkulima apate hata faida kidogo tunaishia kusema funga mipaka huku mkulima aumie.
Tulime zaidi tusifunge mipaka.
 
Kalime uone shuluba yake
 
Nilishaandika mara kadhaa hamchukulii serious,,sasa tusubiri tuone km serikali yetu haitaingia kwenye dhahama ya kutafuta chakula cha misaada, fanyeni upembuzi, uone faida ya kuuza na faida ya kununua baadae,km vp serikali inunue ihifadhi baadae wauze kwa bei ya serikali,,leo ruhusu watu wavute sigara, baadae dawa za kansa unanunua bei ya ajabu, faida iko wapi?? Mimi kunguru muoga
 
Mkulima amenuna🤣🤣🤣🤣
 
Mh Bashe Kuna mdau ameripoti Kutoka Mza, Kwa siku mbili hapakuwa na mahindi Wala Mihogo ktk masoko makubwa.

Stuka mapema mheshimiwa, Tunajua utendaji wako mzuri. Amen
 
Hv mnaosema chakula kizuiwe kuuzwa nje mnajielewa kweli ?? Mshawahi kulima kilimo cha biashara ili kujikwamua ? Vyakula vinarundika ndani soko hamna ,wakulima wanabaki maskini wa kutupwa alaf nyie watu wa mishahara mnaneemeka kazi kulilia nyongeza ya mishahara ,. Ni hvi Kila mmoja ashinde mechi yake , *****

Limeni na nyie ili mtunze mle ....!! Ninalima ili niuze , na sio kuwatunzia nyie wahuni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…