gimmy's
JF-Expert Member
- Sep 22, 2011
- 3,312
- 3,345
Nakumbuka kisa cha yusuf.u wa bibilia kule misri ambapo mfalme aliota ndoto ile ambayo ilimshinda tafsiri,baada ya ndoto ile kujirudiarudia ndipo kukaonekana haja ya kumpata mtu atakae weza kuitafsiri.
Tafsiri ya yusuf.u ilibaini kwamba kutakuwa na miaka mitatu ya neema sana ambapo yusufu akatahadharisha kwamba wanapaswa kuhifadhi Chakula chakutosha.
Kadhalika yusuf.u akawatahadhirisha kwamba baada ya miaka mitatu ya neema yenye mavuno mengi,miaka mitatu inayofuatia itakua ni ukame na hakutakuwa na mavuno kabisa.
Hivyo yusuf.u akamwambia mfalme ya kwamba ahakikishe anahifadhi Chakula kitakachotosheleza mahitaji ya nchi kwa miaka sita jumla,yaani miaka mitatu ya neema+miaka mitatu ya ukame.Ndipo kwa hekima mfalme akamuachia Yusufu kazi yakuhifadhi Chakula kitakachoweza kuivusha nchi kipindi cha njaa.
Bashe wewe ndiye yusuf.u wa leo ambae mh raisi amekuamini lakini kwa bahati mbaya ni yusufu ulienyimwa maono.
Waziri TMA wanaendelea kutoa tahadhari juu ya mwenendo mbaya wa hali ya hewa lakini chaajabu bado umeendelea kushupaza shingo kwamba hatufungi mipaka nchi inaziada ya Chakula.
Kama mamlaka ya hali ya hewa wanatahadharisha msimu ujao kutakua na shida ya mvua,mwakani utakusanya wapi hio hifadhi ya taifa ya chakula?
Hii hifadhi ya Chakula hizi tani 150,000 unazojigamba nazo kwamba zinauwezo wakutosheleza nchi kwa miezi mitatu,hivi zinaweza fua dafu kwa nchi yenye watu 60 ml?
Waziri, tofautisha Mafuta ya kula na mahindi,mahindi ni Chakula watu wanateseka Sana kwa huu mfumuko wa bei kwa sasa.
Mafuta ya kula unaweza fanya hizi control zako ili ulinde wakulima na viwanda vya ndani kwani hili ni zao la biashara lakini kufanya haya kwenye mahindi ilihali TMA wanatahadharisha ukame kwenye msimu ujao,tambua unahatarisha usalama wa nchi.
Raisi muangalie huyu waziri usifuate kila anachoshauri ataligarimu taifa,kumbuka njaa haina mbadala.
Asante.
Tafsiri ya yusuf.u ilibaini kwamba kutakuwa na miaka mitatu ya neema sana ambapo yusufu akatahadharisha kwamba wanapaswa kuhifadhi Chakula chakutosha.
Kadhalika yusuf.u akawatahadhirisha kwamba baada ya miaka mitatu ya neema yenye mavuno mengi,miaka mitatu inayofuatia itakua ni ukame na hakutakuwa na mavuno kabisa.
Hivyo yusuf.u akamwambia mfalme ya kwamba ahakikishe anahifadhi Chakula kitakachotosheleza mahitaji ya nchi kwa miaka sita jumla,yaani miaka mitatu ya neema+miaka mitatu ya ukame.Ndipo kwa hekima mfalme akamuachia Yusufu kazi yakuhifadhi Chakula kitakachoweza kuivusha nchi kipindi cha njaa.
Bashe wewe ndiye yusuf.u wa leo ambae mh raisi amekuamini lakini kwa bahati mbaya ni yusufu ulienyimwa maono.
Waziri TMA wanaendelea kutoa tahadhari juu ya mwenendo mbaya wa hali ya hewa lakini chaajabu bado umeendelea kushupaza shingo kwamba hatufungi mipaka nchi inaziada ya Chakula.
Kama mamlaka ya hali ya hewa wanatahadharisha msimu ujao kutakua na shida ya mvua,mwakani utakusanya wapi hio hifadhi ya taifa ya chakula?
Hii hifadhi ya Chakula hizi tani 150,000 unazojigamba nazo kwamba zinauwezo wakutosheleza nchi kwa miezi mitatu,hivi zinaweza fua dafu kwa nchi yenye watu 60 ml?
Waziri, tofautisha Mafuta ya kula na mahindi,mahindi ni Chakula watu wanateseka Sana kwa huu mfumuko wa bei kwa sasa.
Mafuta ya kula unaweza fanya hizi control zako ili ulinde wakulima na viwanda vya ndani kwani hili ni zao la biashara lakini kufanya haya kwenye mahindi ilihali TMA wanatahadharisha ukame kwenye msimu ujao,tambua unahatarisha usalama wa nchi.
Raisi muangalie huyu waziri usifuate kila anachoshauri ataligarimu taifa,kumbuka njaa haina mbadala.
Asante.