Waziri Gwajima kukomesha ukatili baada ya video ya Mama akimshambulia mtoto kusambaa

Waziri Gwajima kukomesha ukatili baada ya video ya Mama akimshambulia mtoto kusambaa

Sasa Kwan Kuna shida gan hapo? Mbona ameadhibiwa Kawaida sana ? Yaan sku hizi taifa la kiherere sana !!! Wakiachwa mnaanza kua malezi mabaya Aya wakiadhibiwa umbeya Tena!!
Wewe ni bweg,e. Kwasababu umetoka kulelewa kwenye damilia ya makatili unaona ni sahihi mtoto mdogo kama huyo kupigwa namna hiyo.

Wapumbavu kama nyie ndiyo mnaufanya Uafrika uonekane sehemu isiyostahili kuishi viumbe.
 
Kweli nyakati zimebadilika wakati tunakuwa tumechezea kichapo kweli ingekuwa wakati zama hizi kumbe wazazi walikuwa wanaenda selo
Kweli Mimi kipigo Kama cha huyo mtoto nimechezea Sana na kuzidi.

Sasa zama zile kungekuwepo smartphone za kurekodi wazazi wetu wangeenda jela

Vipigo vilikuwa ni hasira zilizochanganikana na umasikini
 
Tukio la video ya mtoto akiadhibiwa vikali na mama yake, lililopostiwa na mwanahabari Tweve Devota kupitia mtandao wa X, limezua taharuki mtandaoni. Mama huyo, anayeishi Mbezi Mwisho, Dar es Salaam, anadaiwa kumtesa mtoto wake mara kwa mara.
Dkt. Gwajima D , Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, alijibu kwa haraka kupitia mtandao wa X, akiahidi kuchukua hatua mara moja. Alitoa mwaliko wa ushirikiano kutoka kwa mtoa taarifa ili timu yake ifike eneo hilo haraka na kumsaidia mtoto huyo.
Majibu ya Waziri Dorothy Gwajima yalionyesha uwajibikaji wa dhati wa ofisi yake, akisisitiza kwamba visa vya ukatili kwa watoto haviwezi kuvumiliwa na kwamba hatua stahiki lazima zichukuliwe kwa ushirikiano wa jamii.
Soma, Pia: Waziri Gwajima chukua hatua kwa ukatili huu aliofanywa mtoto shule ya Msingi Kitefu, Halmashauri ya Meru

Hawa wawe wanaripotiwa polisi. waziri Gwajima peke yake hataweza. Kuna wajinga wajinga wengi sana wamemzidi idadi
 
Ukweli ni kwamba umaskini ni chanzo kingine cha ukatili, Wanawake kazaneni kwenda shule, kazaneni kujishughulisha na biashara mpate vipato vyenu, hata mtu ukiachwa unaweza lea watoto bila hasira. Kuna single mothers wengi tu wanajiweza na wanalea watoto bila tabu.

Kama jamii ya kitanzania ile kampeni ya kumu-empower mwanamke bado iko kwenye 40% Bado sana…..
 
Ukweli ni kwamba umaskini ni chanzo kingine cha ukatili, Wanawake kazaneni kwenda shule, kazaneni kujishughulisha na biashara mpate vipato vyenu, hata mtu ukiachwa unaweza lea watoto bila hasira. Kuna single mothers wengi tu wanajiweza na wanalea watoto bila tabu.

Kama jamii ya kitanzania ile kampeni ya kumu-empower mwanamke bado iko kwenye 40% Bado sana…..
Ipi ni njia mbadala ya kumrekebisha mtoto anapokosea?
 
Wengine zamani tumepigwa zaidi ya hapo... maisha yanaenda kasi sana
Mi leo nimekubali kuwa mambo yanabadilika wazazi wa zamani walikuwa wanapiga aisee lakini ukifanya tathmini sio kwamba walikuwa hawatupendi ni kutufanya tuwe bora.

Tulikuwa tunapigwa lakini mahitaji yote muhimu yalikuwa yakipatikana kwa wakati.
 
Huko sio kupiga ni kautaka kuua hapo nguvu aliyotumia utafikir alikuwa anapigana na mwanamke mwenzake wanayelingana.

Ila sishangai wanawake wengi wenye miili kama hiyo Huwa wanakuwaga na roho mbaya, makatili pia ni single mothers.
 
Back
Top Bottom